Mishahara hewa yaizundua Serikali

Mishahara hewa yaizundua Serikali

Wafanye National pay day,waone majina ya watumishi hewa yatakavyo baki hayana wenyewe.Wakuu wa idara waje watoe maelezo hao waliokuwa wakiwalipa walikuwa wanafanyia kazi wapi?
 
Mpaka leo salary slip za kuanzia mwezi wa sita hazijafika kwa walengwa.Vitu kama hivi pia vinakwamisha kwa kiwango kikubwa maendeleo wafanyakazi waliotakiwa kukopa wanashindwa hivyo waache porojo hapo wapige kazi wananchi wanataka matokeo
 
Huyu mwigulu ni mtafuta sifa tu hana lolote anachosema hao wapeleke accounts zao hazina kwani hawawezi pia kupeleka accounts hewa? Kuna Freelancer kibao wanalazimisha kufungua accounts kwenye bank zao kwahiyo ni possible kwa hao wapigaji kuwafungulia accounts wote hewa na kuendelea kupiga pesa,wewe mwigulu kama mmegundua wizi huo wa zaidi ya 40b kwa mishahara hewa basi hao wezi lazima wakamatwe wafilisiwe na wafungwe hatutaki porojo mara sijui nimepeleka takukuru oh nimepeleka polisi na bla bla kibao mbona yule aliyekwepa kodi zaidi ya 7b ulimuweka hewani?

Cc: Tema Mate

Bro sisi wa TZ kuibiwa ni raisi sana, kAMa MWIGULU anasema tangu mwezi wa 7 wanalipa moja kwa moja kwenye akaunti na tayari wameokoa bilion40, wizara ya fedha ina hazina ndogo kila mkoa je wameshafatilia kujua taarifa ya ambao hawajapata mishahara tangu mwezi 7 ili wajue kila halmashaur ilikuwa inapokea kiasi gani cha mishahara hewa? na je kama waliweza kupata acount za wafanyakazi wote na wakawalipa mishahara kuanzia mwezi 7 inakuwaje washindwe kupata acount zingine chache zilizobakia hadi waombe wakurugenzi wawatumie wakati ndio watuhumiwa? wakitengeneza acount hewa atajuaje? usanii at work, mishahara hewa inaanzia TAMISEMI waanze GHASIA awaeleze aLichomeka wangapi, bila kumsahau KOMBANI nae atutajie wakwake alafu ndio waje kwa wakurugenzi HUU NI MTANDAO
 
Mwigulu usilete comedy fanya kazi hatutaki porojo mbonqa yule mwenye kiwanda mlimkata? Iweje hawa ulete porojo?

Cc: Tema Mate

Mafisiem kama wanataka kuzuia upotevu wa Pesa wachunguze kwanza Home Shoping Center wanavyosaidia wafanyabiashara kukwepa ushuru bandarini, Mandra Junior njoo hujibu hapa na fisiem yako
 
Mh!

Ni vigumu kwa taasisis kutengeneza mishahara hewa bila kuwa na ushirikiano na Utumishi na hazina. Bahati mbaya hao hao utumishi ndio wanaotumwa kwenye mataasisi kuja kukagua watumishi. Unategemea wataleta taarifa gani? Wakati mwingine wakija kwenye mataasisi wanampa incharge wa mishahara awape orodha ya watumishi.
 
Kazi nzuri,,lakini sijui tutafanikiwaje katika kudhibiti wizi huo ambao umeota mizizi. Mwigulu anajitahidi sana lakini kwa bahati mbaya yuko peke yake, siamini kama atapata msaada hata kutoka wizarani kwake kwa sababu bilioni karibu 40 kila mwezi haziwezi kuibiwa kirahisi bila msaada mkubwa kutoka wizarani kwake, na inawezekana hata huko alikopeleka majina ili hatua zichukuliwe na wenyewe wamo. Mwigulu asifanye mambo kimya kimya, hao ni wezi na wahalifu kama wahalifu wengine, kama ushahidi anao jambo ambalo sina shaka nalo awataje tuwajue ili hatua zichukuliwe bila kuoneana haya. Sh biliono 40 kwa mwezi ni sawa bilioni 480 kwa mwaka ni fedha nyingi ambazo zingeweza kumaliza kabisa tatizo la madawati kwa nchi nzima, ni kwa vipi wezi hao waonewe aibu. Mchemba sema usiogope sema, sisi wazalendo tuko nyuma yako na historia itakukumbuka daima dumu.
 
Naona wanazikusanya za Uchaguzi mwakani..... Ukweli utadhihirika tu.... Leo ndio wameshtuka....
 
Hii ni porojo tu kama zilivyo porojo nyingine.....badala ya kumkamata mwizi eti mtu anakamata kidhibiti na kumwachia mwizi halafu anapiga kelele...another comedy episode
 
kwa akili yako unadhani akipelekewa acount ndiyo ataishia hapo tatizo hujamsikiliza unakukurupuka bawacha bana.[/QUOT

Ebu acha utani na kutafuta sifa: Naibu waziri anapaswa awakamate awapeleke mahakamani... ni wahujumu uchumi!!! Kuna polisi wa kutosha, kamata hao watu... ita waadishi wa habari wawapige picha kama waharifu wengine... umma uwaone... sharia ichukue mkondo wake...Tofauti na hapo tutasema hizo 40 bil wanagawana wengi.... akiwemo huyo mheshimiwa!!
 
Tatizo ni watumishi hapo hazina wakishirikiana na utumishi na wahasibu kutoka halmashauri ma idara za serikali
 
Bro sisi wa TZ kuibiwa ni raisi sana, kAMa MWIGULU anasema tangu mwezi wa 7 wanalipa moja kwa moja kwenye akaunti na tayari wameokoa bilion40, wizara ya fedha ina hazina ndogo kila mkoa je wameshafatilia kujua taarifa ya ambao hawajapata mishahara tangu mwezi 7 ili wajue kila halmashaur ilikuwa inapokea kiasi gani cha mishahara hewa? na je kama waliweza kupata acount za wafanyakazi wote na wakawalipa mishahara kuanzia mwezi 7 inakuwaje washindwe kupata acount zingine chache zilizobakia hadi waombe wakurugenzi wawatumie wakati ndio watuhumiwa? wakitengeneza acount hewa atajuaje? usanii at work, mishahara hewa inaanzia TAMISEMI waanze GHASIA awaeleze aLichomeka wangapi, bila kumsahau KOMBANI nae atutajie wakwake alafu ndio waje kwa wakurugenzi HUU NI MTANDAO

Umeongea vya maana sana!! Mwigulu chukua huu ushauri kama una nia kweli ya dhati maana naona unaleta bla bla nyingi.
 
Mafisiem kama wanataka kuzuia upotevu wa Pesa wachunguze kwanza Home Shoping Center wanavyosaidia wafanyabiashara kukwepa ushuru bandarini, Mandra Junior njoo hujibu hapa na fisiem yako

Huyo Jamaa ni noma yupo imara sana ana yard ya kufa mtu china ambapo wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi ndio wanamtumia maana yeye anachaji kidogo sana! Mwigulu anza na huyu kama uwaziri haujaota mbawa!
 
Kuna hatua mbili za kuwachukulia wale wote waliojihusisha na mishahara hewa.
  1. Kuwachukulia hatu za kinidhamu
  2. Kuwachukulia hatua za kisheria

Hatua ya kwanza haihitaji TAKUKURU wala mahakama. Kama kweli ana niya ya dhati angeanza na hatua ya kwanza wakati tukisubiri hatua ya pili ambao ni mlolongo mrefu
 
Swali la kizushi; hivi watu tumeanza kusikia stori za mishahara hewa lini..? Kwa upande wa wananchi naamini hili ni swala lililotegemewa sana.. Ila afadhali limeshughulikiwa, ingawa natamani wawe wamemaliza mianya yote ya mishahara na malipo mengine hewa..
 
punguzeni sifa wahaya,! Huo msemo ni wa kihaya??
Mrembo punguza hasira utakuja kuzeeka haraka hivi uwe nungayembe, hiyo mimi niliisikia kwenye harusi moja wapo am,bapo MC mmoja alisema hivyo hivyo nilivyo - quote.
 
Huyo Jamaa ni noma yupo imara sana ana yard ya kufa mtu china ambapo wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi ndio wanamtumia maana yeye anachaji kidogo sana! Mwigulu anza na huyu kama uwaziri haujaota mbawa!

Yaani kawasababishia wafanyabiashara kariakoo kufilisika baada ya kugundua njama zake za kuwaingiza mkenge
 
Back
Top Bottom