Somoche
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 6,148
- 7,002
Jamani kumejitokeza Mtu/ kikundi cha watu Wilayani Tarime kinachoua watu katika hali ya kusshtua na kushangaza sana, mimi binafsi nina taarifa za watu wawili waliouwawa jana na hao wauaji, jambo la kustikitisha ni kwamba wauaji hao tangu wameanza kuua yapata wiki moja sasa bado hawajakamatwa na hivyo kuwafanya wananchi kuwa na hofu kubwa na usalama wao.
Ni wito wangu kwa Jeshi la polisi kuongeza nguvu ya askari wenye utaalamu na Ujasiri kwasababu hali hii sasa inatisha kweli kweli..Polisi wa kanda maalum inaonekana bado hawajaweza kupata ufumbuzi wa mauaji haya...
Ni wito wangu kwa Jeshi la polisi kuongeza nguvu ya askari wenye utaalamu na Ujasiri kwasababu hali hii sasa inatisha kweli kweli..Polisi wa kanda maalum inaonekana bado hawajaweza kupata ufumbuzi wa mauaji haya...
Mtu mmoja asiyefahamika anatafutwa kwa tuhuma za mauaji Mjini Tarime, mtu huyo ambaye anafanya matukio ya ajabu ya mauaji leo majira saa nne asubuhi amewaua watu wanne katika Kijiji cha Kemakorere. Anafanya mauaji hayo kwa kutumia Bunduki, inasemekana mtu huyo akishaua hachukui kitu chochote bali huua na kutokomea kusikojulikana.
Mtu huyo haijajulikana kama ni mwanamke ama mwanaume kwa kuwa hajapatikana mpaka sasa.
Kamanda wa Polisi Mjini Tarime amethibitisha uwepo wa muuaji na mauaji hayo ambapo watu takriban saba wameshauwawa mpaka sasa.
Mji wa Tarime umejaa taharuki watu hawana amani...
Jeshi la Polisi linahaha mpaka sasa, kwani linafanya msako wa kufa na kupona kumpata mtu huyo....
Source: Morning Star Radio