Mauaji ya Kutisha Tarime

Mauaji ya Kutisha Tarime

Kuna mtu (muuaji) ameibuka wilayani Tarime, hadi sasa ameshaua watu kumi ktk kijiji cha Mogabiri kwa kuwadungua na risasi na leo asubuhi amewaua watoto wawili wakati wanaenda shuleni, lakini kamanda Kamugisha kanda maalumu amekaa kimya! !!.
 
Nchi hii mbaya!!! usalama wa raia unalindwa na Police, Je police wameshindwa kazi zao?
 
Tata Hata kama angekuwa mmoja bado ana haki ya kuishi. P'se be serious. Usicheze na maisha ya watu.
 
Bado kuna mauaji pamoja kuwa kanda maalumu, pamoja na operesheni Kimbuga kupita, kuna haja ya Waziri wa Ulinzi na JKT kutafakari upya hatua sahihi.
 
Nimetoka asubuhi tarime kuja huku nyamongo nimepata taarifa kuwa wamemkamata huyo muuaji yaani inatisha

RIP mwasi matiko(mhandisi) ila nawe kama hujatubu jehamu inakusubiri maana mwaka juzi ulidakwa na kamera za cctv ukiwanga katikati ya mgodi wa north mara
 
RIP mwasi matiko(mhandisi) ila nawe kama hujatubu jehamu inakusubiri maana mwaka juzi ulidakwa na kamera za cctv ukiwanga katikati ya mgodi wa north mara

Hoya mbona una quote alafu unamsema mtu mwengine watu watadhani mimi northmara yenyewe huwa nakuja na kuondoka same day. kama hapa namaliza mzigo nasepa Rocky city.
 
habari zilizonifikia kuwa ndani ya masaa 72 watu tisa wameuwawa katika wilaya ya tarime mauwaji hayo ni kiholela hadi sasa hajafahamika muaji ni nani na atakaye uwawa ni yupi hofu kubwa imetandaa
 
Wananchi wenyehasira kali hawapo? kumbe kazi yao kuua wezi wa kuku tu? mbona hawaonyeshi hasira zao kwa huyo muuaji mpaka police wa muue!
 
Mtu mmoja asiyefahamika anatafutwa kwa tuhuma za mauaji Mjini Tarime, mtu huyo ambaye anafanya matukio ya ajabu ya mauaji leo majira saa nne asubuhi amewaua watu wanne katika Kijiji cha Kemakorere. Anafanya mauaji hayo kwa kutumia Bunduki, inasemekana mtu huyo akishaua hachukui kitu chochote bali huua na kutokomea kusikojulikana.

Mtu huyo haijajulikana kama ni mwanamke ama mwanaume kwa kuwa hajapatikana mpaka sasa.

Kamanda wa Polisi Mjini Tarime amethibitisha uwepo wa muuaji na mauaji hayo ambapo watu takriban saba wameshauwawa mpaka sasa.

Mji wa Tarime umejaa taharuki watu hawana amani...

Jeshi la Polisi linahaha mpaka sasa, kwani linafanya msako wa kufa na kupona kumpata mtu huyo....

Source: Morning Star Radio
 
Mmmm Tanzania nako wanaiga Marekani kulenga shabaha kwa binadamu mwenzio? Maisha ya watu saba ni wengi sana tuombe msaada wa teknologia ya kupata picha yake kama lile tukio la padri kule Zanzibar
 
habari zilizotufikia mpaka muda huu idadi ya watu wanane 8 wamefariki.
Wameuawa na mtu /watu wasiojulikana .
Yaani baadhi ya miili imekutwa na majeraha ya risasi.
Wahusika ni kama vile snipper.balaa balaa balaa.
 
wana jf, tarime kuna janga la kitaifa, kila siku tunapoteza watu.wawili hadi.watatu kwa kupigwa risasi. jana wananchi walitaka kuandamana kwenda kwenye ofisi ya RPC kuhoji kwanini watu wanauwa bila wauwaji kukamatwa.wakati magari ya patrol ya polis wa kanda maalum yanaonekana yakilandalanda ovyo mitaani. Juzi ameuawaa askari mstaafu mtoto wa kwanza wa marehem Major Gen. Marwa kwa risasi moja tu. Inaonesha muuaji na sniper kwani huua kwa risasi moja tu. Hali ni tete... you may never know who is next
 
Mpaka sasa hv takribani watu kumi wamethibitishwa kuuwawa na mtu asiyejulikana.
Mauaji hayo yamefanywa na mtu huyo ktk sehemu tofauti tofauti kwa kutumia bastola. Mtu huyo ambaye mpaka ss hajakamatwa/kujulikana amekuwa akifanya mauaji usiku, anamimina risasi za kutosha tu kwa mtu mmmoja hana hata chembe ya huruma hata kidogo.
Swala la kujiuliza n kwamba, kwann serikali hajatoa taarifa rasmi kuhusu mauaji hayo? Au Rais atangaze rasmi Amri ya kutotembea usiku.
 
Back
Top Bottom