Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la usambazaji wa nukuu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii zinazodaiwa kutolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Mojawapo ya nukuu hizo, iliyochapishwa kwenye mtandao wa Facebook, inamdai Rais Samia amesema: "Natamani muda wangu uishe."
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa kupitia vyanzo mbalimbali vya mtandaoni umebaini kuwa hakuna ushahidi wowote unaoonyesha kuwa Rais Samia aliwahi kutoa kauli hiyo, iwe katika hotuba, mahojiano, taarifa rasmi au kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.
Aidha, ukaguzi wa hotuba na taarifa rasmi zinazochapishwa kupitia kurasa za mawasiliano za Ikulu ya Tanzania haukubaini sehemu yoyote ambayo Rais Samia amesema...