Featured content

Sirari: Wananchi wampambania mwenzao asitekwe!
Ni baada ya mwananchi mmoja kudaiwa amechukuliwa na "wasiojulikana" ambapo baada ya wananchi kufunga njia zote watu hao 'wasiojulikana' walikimbilia Polisi
Fahamu jinsi ya kutumia Pressure Cooker kwa usahihi ili kuepuka mlipuko
Pressure cooker ni kifaa muhimu jikoni kinachopunguza muda na kuokoa nishati kwenye baadhi ya mapishi ambayo huchukua muda mrefu kuiva. Siku za hivi karibuni matukio ya kifaa hiki kulipuka yamekuwa yakiongezeka kwa kasi huku sababu mbalimbali zikitajwa kusababisha hilo. Fahamu matumizi sahihi ya Pressure Cooker ili kuwa salama wakati wote unapoandaa mapishi yako.
Mzazi: Nilipigiwa simu kuwa mwanangu amechukuliwa na watu wasiojulikana...
Ashura Simba, mama wa Mickdady (21), anayeishi Tabata Chang'ombe, alieleza kuwa alipigiwa simu kuwa mwanaye amechukuliwa na watu wasiojulikana. Licha ya jitihada zake kumtafuta, hakufanikiwa hadi alipopokea taarifa za kupatikana kwa miili ya vijana hao wanne eneo la Mapinga, mkoani Pwani.
Heche akamatwa na kuzuiliwa Sirari akielekea Kenya kumzika Odinga
Pamoja na kumuweka kizuizini, Mamlaka ya Uhamiaji Tanzania imemnyang'anya hati yake ya kusafiria (Passport) bila kueleza kwanini wamechukua uamuzi huo.
Madagascar: Kanali Randrianirina aapishwa kuwa Rais, awashukuru waandamanaji
Randrianirina, ambaye alikuwa kamanda wa kikosi maalum cha jeshi, aliapishwa katika Ukumbi Mkuu wa Mahakama ya Katiba ya Juu, hatua iliyotamatisha mchakato wa haraka wa kuichukua madaraka ya nchi yenye wakazi takribani milioni 30 iliyoko katika Bahari ya Hindi, upande wa mashariki mwa Afrika
Cameroon: Raia waandamana, wachoma baadhi ya Majengo ya Serikali wakidai hawamtaki Rais
Wananchi wengi wamejitokeza barabarani wakipinga kile wanachokiita “uchaguzi wa wizi” na wakitaka Rais Paul Biya aondoke madarakani, wakimtaka Issa Tchiroma Bakari kutangazwa mshindi halali
Wasira: Kuna maswali kuhusu Polepole, alisema ametelekezwa Cuba halafu ghafla ikawa ametekwa Tanzania!
Wassira: Sitaki kuzungumza sana mambo ya Polepole kwasababu sasa hivi yanachunguzwa na Polisi, lakini yako maswali vilevile juu ya Polepole kwasababu, Polisi haohao walimwandikia wito aende akaandikishe kwao mambo anayo yazungumza kupitia mtandao ili wayachunguze Polepole akawaambia yeye yuko nje ya nchi...ametelekezwa Cuba alafu ghafla ametekwa Tanzania
Wamiliki wa "Online TV" zilizorusha maudhui ya Polepole wakamatwa na Polisi
Wakuu, Watu wanne waliokuwa wanamiliki akaunti za mtandao wa Youtube za Wispoti TV, T.Media Two na Costa Tv wamekamatwa kwa madai ya kuendesha akaunti hizo bila ya kuwa na leseni. Akaunti hizo ni kati ya zile zilikokuwa zikirusha press za Polepole kila alipokuwa akizitoa. Kumbuka Polepole alishawahi kusema kuwa media zimelipwa huku nyingine zikitishwa kutorusha maudhui yake. Hili limethibitika sasa, maana waliokuwa wakiendelea kurusha maudhui hayo ndio kama hawa ambao kama walishindwa...
Raila Odinga afariki dunia nchini India kwa mshtuko wa moyo
Raila Odinga (RAO) afariki dunia huko India. Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80. R.I.P Papa. Utangulizi Raila Amolo Odinga ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri zaidi katika historia ya Kenya na Bara la Afrika kwa ujumla. Kwa zaidi ya nusu karne, amekuwa nembo ya mapambano ya demokrasia, mageuzi ya kisiasa, na haki za kijamii. Safari yake imejawa na changamoto, mafanikio na matukio makubwa ambayo yameunda sura ya siasa za Kenya. Maisha ya Awali na Elimu Raila alizaliwa tarehe 7 Januari...
Madagascar: Kikosi maalum cha Kijeshi chamwondoa Madarakani Rais Andry Rajoelina
Kikosi maalum cha Kijeshi nchini Madagascar cha 'CAPSAT' kimetangaza kuchukua madaraka, kikimwondoa madarakani Rais Andry Rajoelina, baada ya Wabunge katika Bunge la kitaifa kupiga kura ya kumwondoa, licha ya Rais Rajoelina kutangaza kulivunja kabla ya kura kupigwa.
Madagascar: Rais akimbia nchi ili kulinda maisha yake kufuatia maandamano makubwa ya kitaifa
Rais Rajoelina alitarajiwa kutoa hotuba ya televisheni Jumatatu jioni, lakini hotuba hiyo iliahirishwa baada ya “kikundi cha majeshi yenye silaha kutishia kuchukua udhibiti wa vyombo vya habari vya umma,” kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi yake kupitia Facebook.
TCRA yazuia maudhui ya Mange Kimambi kuonekana Tanzania. Waamuru Meta kufuta post zake!
Mafisadi yamejipanga Kwa njia zote. Leo wameamuru meta ambao ni wamiliki wa Instagram kushusha post zote za kuhusu ufisadi wa serikali Kwamba serikali haitaki kuona post za watoto wa fisadi Seleman Momba ambaye ndo mkurugenzi wa usalama wa Taifa wakichezea mamilion ya USD nyumbani huku wananchi wakikosa hata nafasi katika mwendokasi Serikali haitaki kuona magari ya kifahari ya Abduli Serikali haitaki kuona apartments za Abdul Haitaki wananchi waone manunuzi ya ovyo Mange anahamasisha...
Fanya hivi ili uweze kuperuzi mitandao iliyozuiwa (blocked) bila ya kudownload VPN kwenye Kompyuta yako
Ni wazi kuwa matumizi ya mtandao yameminywa sana Tanzania kwa sababu za kisiasa zinazowekwa kwenye mtazamo wa kiusalamaua na kimaadili, tumefikia kipindi mtu anahitaji kutafuta mbinu za kuweza kupata taarifa kutoka kwenye majukwaa muhimu ya habari kama X na hata sasa Baada ya kusitishwa kwa muda kwa leseni JamiiForums hasa kwa watumiaji wa Tanzania. Mamlaka zimeendambali zaidi hadi kufikia hatua ya kuzuia kuperuzi tovuti za kudownload huduma za VPN. Kwasasa Matumizi ya VPN Tanzania...
Ezekiel Wenje ajiondoa CHADEMA na kujiunga rasmi na CCM
Nilijua huyu baba awezi kujishikilia muda wote CHADEMA, na hivi alitajwa sana na Lissu kwenye hela za Duli basi ilikuwa ni suala la muda tu😂 =========== Mbunge wa zamani wa Nyamagana na mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya ziwa Victoria Ezekiel Wenje leo amatengaza rasmi kuhamia CCM na kukikacha CHADEMA baada ya kukitumikia kwa miaka kadhaa. Kazi ambayo imefanya CCM tangu tumepata uhuru ni jambo kubwa sana ni suala la nchi kuwa na amani na utulivu, amani na maendelea ni mapacha nchi ikiwa na...
Zimbabwe: Kamanda wa Jeshi aungana na Wananchi dhidi ya Rais Mnangagwa; asema nchi sio ya wahalifu (kina Chivayo)
Veterani wa vita aliyekimbizwa na mamlaka, Blessed Runesu Geza, anayejulikana pia kama “Cde Bombshell”, amewaomba Wazimbabwe waamke dhidi ya kile anachodai kuwa ni kunyakuliwa kwa dola na wizi wa rasilimali za taifa na Rais Emmerson Mnangagwa na wadanganyifu wake.
Mchungaji Victoria: Tutapata wapi sadaka mkiandamana? Sisi tunaishi kwa kula sadaka
"Sisi Tunakula Sadaka, Maisha Yetu ni Sadaka” Mtumishi wa Mungu Mchungaji Victoria Joseph wa Life Center International Bible College pamoja na wengine wamesema kuwa wao kama viongozi wa dini, endapo amani itatoweka kutokana na kelele za mitandaoni, watakosa sadaka. Wakizungumza na waandishi wa habari, viongozi hao wamewahimiza Watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025 kwa maslahi mapana ya nchi, huku wakikemea vikali wale wote wanaotaka kuvuruga amani kwa sababu zao...
Kwanini Mwalimu Nyerere alisusia Uchaguzi wa Wakoloni mwaka 1958?
Wengi humkumbuka Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kama Baba wa Taifa, lakini wachache wanakumbuka kuwa aliwahi kususia uchaguzi ulioandaliwa na wakoloni mwaka 1958. Hili si jambo la kawaida, kwa kuwa viongozi wengi huona uchaguzi wowote kama nafasi ya kuingia madarakani. Lakini kwa Nyerere, misingi ilikuwa muhimu kuliko kushinda kura. Kilichotokea Mwaka 1958, serikali ya kikoloni ya Kiingereza ilitangaza uchaguzi wa Baraza la Kutunga Sheria (Legislative Council). Lakini mfumo wa uchaguzi...
Humphrey Polepole adaiwa kutekwa usiku wa kuamkia Oktoba 6
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange ameandika.... "Hi guys nimetumiwa hii ni mtu ana insist ni ndugu yake na Polepole. I don’t know what to think, Mimi nilidhani Polepole hayuko TZ. I’m posting ili Polepole mwenyewe ku confirm kama yuko Okay, Ila mimi kama sijui niipe uzito gani hii taarifa. . Dada habari za asubuhi.mimi ni ndugu wa karibu na familia ya Humphrey polepole. Asubuhi ya kuamkia leo wamevunja nyumba aliokuwa ana kaa nakumchukua. Wamemteka Polepole, naomba uwaarifu...
Sisi ni Mabingwa wa Kuharibu? Toka Mabasi 140 hadi 30
Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa kampuni ya UDART (mwendokasi) ilianza ikiwa na mabasi 140 lakini hadi kufikia hiyo juzi yalibakia mabasi 30! Yaani wameshindwa kutengeneza mabasi zaidi ya 110!
Back
Top Bottom