Ex Spy
JF-Expert Member
- Jan 15, 2007
- 333
- 2,838
Disemba 10, 2025
Kanada inapitia upya msaada wake wa muda mrefu kwa Tanzania baada ya ukandamizaji wa kikatili uliofanywa na Polisi na Wanajeshi, ambao unaripotiwa kuua mamia ya raia waliokuwa wakiandamana kupinga uchaguzi wenye utata.
Ottawa imetoa msaada wa kimataifa wa Dola Milioni 3.4 kwa Tanzania tangu uhuru wake, ikiiona nchi hiyo ya Afrika Mashariki kama mshirika imara na mwenye amani – hadhi ambayo sasa ipo mashakani huku kukamatwa na kufungwa kwa watu kukiendelea.
Serikali ya Tanzania ilikusanya idadi kubwa ya Polisi na Wanajeshi kuzuia Maandamano ya kitaifa yaliyopangwa kufanyika Jumanne, Disemba 9, 2025. Mitaa mingi ilikuwa kimya sana, huku Watanzania wengi wakiogopa kutoka nje kwa hofu ya kukamatwa. Maandamano madogo yaliyotawanyika yaliripotiwa katika maeneo machache.
Tanzania imekuwa mpokeaji mkuu wa msaada wa Kanada kwa miongo kadhaa, ikiwemo mwaka 2023-24 ilipopokea msaada wa dola milioni 141, kulingana na Global Affairs Canada.
"Kutokana na matukio ya hivi karibuni, Kanada inafanya mapitio ya kina ya msaada wake wa kimataifa kwa Tanzania ili kuhakikisha ufanisi na uadilifu endelevu wa programu zake," msemaji Alexandre Fournier aliliambia gazeti la The Globe and Mail siku ya Jumanne wakati akijibu maswali.
Alisema Kanada itaelekeza msaada wake kwenye afya, elimu na programu za ukuaji jumuishi kwa jamii maskini na zilizo hatarini zaidi nchini Tanzania.
Kanada inapitia upya msaada wake wa muda mrefu kwa Tanzania baada ya ukandamizaji wa kikatili uliofanywa na Polisi na Wanajeshi, ambao unaripotiwa kuua mamia ya raia waliokuwa wakiandamana kupinga uchaguzi wenye utata.
Ottawa imetoa msaada wa kimataifa wa Dola Milioni 3.4 kwa Tanzania tangu uhuru wake, ikiiona nchi hiyo ya Afrika Mashariki kama mshirika imara na mwenye amani – hadhi ambayo sasa ipo mashakani huku kukamatwa na kufungwa kwa watu kukiendelea.
Serikali ya Tanzania ilikusanya idadi kubwa ya Polisi na Wanajeshi kuzuia Maandamano ya kitaifa yaliyopangwa kufanyika Jumanne, Disemba 9, 2025. Mitaa mingi ilikuwa kimya sana, huku Watanzania wengi wakiogopa kutoka nje kwa hofu ya kukamatwa. Maandamano madogo yaliyotawanyika yaliripotiwa katika maeneo machache.
Tanzania imekuwa mpokeaji mkuu wa msaada wa Kanada kwa miongo kadhaa, ikiwemo mwaka 2023-24 ilipopokea msaada wa dola milioni 141, kulingana na Global Affairs Canada.
"Kutokana na matukio ya hivi karibuni, Kanada inafanya mapitio ya kina ya msaada wake wa kimataifa kwa Tanzania ili kuhakikisha ufanisi na uadilifu endelevu wa programu zake," msemaji Alexandre Fournier aliliambia gazeti la The Globe and Mail siku ya Jumanne wakati akijibu maswali.
Alisema Kanada itaelekeza msaada wake kwenye afya, elimu na programu za ukuaji jumuishi kwa jamii maskini na zilizo hatarini zaidi nchini Tanzania.