Wimbo wa msanii Roma Mkatoliki, "Teremsha Bunduki" wafungiwa na BASATA kwa madai ya Kupotosha, Kuchochea Ghasia, pamoja na kuwa na maneno ya Uongo na Uchochezi kulingana na Kanuni za Baraza 25 (6) (b),(c),(d).
Katika wimbo huu, Roma amewataka polisi waache kupiga na kunyanyasa wananchi, waachie maandamano ya haki, akisisitiza kuwa bunduki si za kulinda mtawala anayeibia na kuteka wananchi.