Jamani majumbani kuna vituko msione watu wanapita wanacheka mkaona moyoni ni hivyihivyo.!! Rafiki yangu mpendwa ambaye anahali ya ulokole fulani hivi kapewa Live na Mkewe kuwa inabidi wasitishe shughuli zote za mapenzi kwa muda wa miezi mitatu. Nilipomuuliza sababu ya kusitishwa zoezi hilo amesema mkewe amesema kwa sasa anajipa likizo amechoka kuhangaishwa. Kimsingi jamaa ni wale wapole fulani hivi kwa kifupi hana mkwala. Nimemuahidi nitampa ushauri ili akabiliane na jambo hili. Najua mawazo ya wana jf yatakuwa msaada kwa huyu jamaa unadhani achukue hatua gani?