Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
MADAKTARI wa Hospitali ya Apollo India, wamefanikiwa kumfanyia operesheni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe ambaye alipelekwa huko wiki iliyopita kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya kipanda uso.
Kaka wa Mbunge huyo, Salum Mohammed aliliambia gazeti hili jana kuwa operesheni hiyo iliyotumia muda wa saa nne, ilifanyika salama na hali yake inaendelea vizuri. "Walianza kumfanyia operesheni saa 4:00 asubuhi na ilikamilika kwenye saa 8:00 mchana. Kwa sasa (Zitto) anaendelea vizuri.
Tayari amezinduka, amekunywa juisi na sasa (jana) amepumzika," alisema Mohammed. Alisema operesheni ilifanywa na jopo la madaktari lililoongozwa na Dk Sunil Narayan Dutt ambaye ni mtaalamu wa magonjwa ya kinywa, njia ya kupumua na kichwa na pia ndiye mkuu wa kitengo cha upasuaji katika Hospitali ya Appolo. Mohammed alisema madaktari hao walieleza kwamba aina ya operesheni hiyo huwa haihusishi upasuaji wa fuvu.
"Walichokifanya ni kuingiza chombo maalumu puani na kwa kutumia kompyuta, waliweza kuona kila kitu na ndipo wakaanza kufanya operesheni kwa kuona kupitia kompyuta," alisema Mohammed.
Alisema operesheni ilifanyika kikamilifu na Naibu Katibu Mkuu huyo wa Chadema anaendelea vizuri na hakuna tatizo lolote ambalo linamsibu kutokana na upasuaji huo.
"Hadi sasa anaendelea vizuri na hakuna tatizo lolote ambalo limempata kutokana na upasuaji huo. Mheshimiwa Zitto anaendelea vizuri ingawa anaonekana kuchoka kutokana na shughuli hiyo," alisema Mohammed.
Zitto alipelekwa India kwa matibabu baada ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyokuwa ikimpatia matibabu kupendekeza rufaa hiyo.
Alipelekwa MNH akitokea katika Hospitali ya Aga Khan ya Dar es Salaam akitibiwa ugonjwa wa malaria.
Kaka wa Mbunge huyo, Salum Mohammed aliliambia gazeti hili jana kuwa operesheni hiyo iliyotumia muda wa saa nne, ilifanyika salama na hali yake inaendelea vizuri. "Walianza kumfanyia operesheni saa 4:00 asubuhi na ilikamilika kwenye saa 8:00 mchana. Kwa sasa (Zitto) anaendelea vizuri.
Tayari amezinduka, amekunywa juisi na sasa (jana) amepumzika," alisema Mohammed. Alisema operesheni ilifanywa na jopo la madaktari lililoongozwa na Dk Sunil Narayan Dutt ambaye ni mtaalamu wa magonjwa ya kinywa, njia ya kupumua na kichwa na pia ndiye mkuu wa kitengo cha upasuaji katika Hospitali ya Appolo. Mohammed alisema madaktari hao walieleza kwamba aina ya operesheni hiyo huwa haihusishi upasuaji wa fuvu.
"Walichokifanya ni kuingiza chombo maalumu puani na kwa kutumia kompyuta, waliweza kuona kila kitu na ndipo wakaanza kufanya operesheni kwa kuona kupitia kompyuta," alisema Mohammed.
Alisema operesheni ilifanyika kikamilifu na Naibu Katibu Mkuu huyo wa Chadema anaendelea vizuri na hakuna tatizo lolote ambalo linamsibu kutokana na upasuaji huo.
"Hadi sasa anaendelea vizuri na hakuna tatizo lolote ambalo limempata kutokana na upasuaji huo. Mheshimiwa Zitto anaendelea vizuri ingawa anaonekana kuchoka kutokana na shughuli hiyo," alisema Mohammed.
Zitto alipelekwa India kwa matibabu baada ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyokuwa ikimpatia matibabu kupendekeza rufaa hiyo.
Alipelekwa MNH akitokea katika Hospitali ya Aga Khan ya Dar es Salaam akitibiwa ugonjwa wa malaria.