Muhimbili yaja na mpango wa dharura kuwahudumia Wanachama wa NHIF

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,565
Kutokana na baadhi ya hospitali binafsi kusitisha huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuanzia leo Machi mosi, 2024, uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) umekuja na mpango wa dharura wa kuwahudumia.

Hatua hiyo inalenga kuwawezesha wawe na mwendelezo wa huduma. Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Mohamed Janabi amesema hayo leo kupitia mtandao wa Instagram wa hospitali hiyo.

Amesema MNH imeongeza muda wa kuona wagonjwa katika kliniki zote za Upanga kupitia vyumba 75 vya kuona wagonjwa na vyumba vya kuona wagonjwa 59 viliyopo Mloganzila.

Profesa Janabi amesema huduma inaanza saa tatu asubuhi hadi saa nne usiku au mpaka mgonjwa wa mwisho atakapomaliza kuonwa na daktari.
 
Watu wanaikimbia Muhimbili kwa sababu ya foleni ndefu, yaani unaweza kukaa masaa nane kwenye foleni. Madaktari ni wazuri sana.

Serikali haina uwezo wa kutibu wagonjwa wote kwenye hospitali za serikali. Iache kufanya siasa na maisha ya watu.
 
Watawala wanauliza .."Vipi huko hali ya usalama? Vyombo vya usalama vinajibu...Nchi ipo salama.

Watawala wanagonga mvinyo na kuchovya mapaja ya kuku kwenye mayonize ....huku wakijadili kupata chanzo kipya cha mapato kutoka kwenye mifuko ya Raia.
 
Aisee Janabi ameanza kufanya comedy no wonder see him like comedian now….!
Hivi wana dawa za kutosha?
Wana wafanyakazi wakutosha?
Ummy na Janabi punguzeni kufanya mizaha kwenye afya za watu
 
Back
Top Bottom