Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Mbunge mahiri na machachari kutoka chama makini Zitto Zuberi Kabwe ameweka wazi kuwa anautaka uraisi lakini akiwa atapata ridhaa kutoka kwa chama chake na wananchi kwa ujumla wao,




CHANZO: UDADISI: Rethinking in Action: ZITTO: "NDIO NATAKA KUWA RAIS"

Nafikiri Confedence ya kuongea kwenye forums sio tija ya kuwa Rais.Watanzania wanahitaji Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi.Zitto analalamikia sekta ya madini! Alikua miongoni mwa wabunge waliosimamia hoja hii 2005.Alinyoteuliwa kwenye kamati na mweshimiwa JK. Hajawambia wadau kilichojiri.

Zitto anahaki ya kikatiba kugombea urais ILA kwa maoni yangu naona asanii mwingi kwake. Uchaguzi uliopita jimboni kwake alipata upinzani mgumu na kuambulia asilimia inayoonyesha wanajimbo wameanza kumchoka.

Nafikiri Zuberi anajiweka kwenye daraja la super young politicians yeye mwenyewe.Kabla ya kuingia Bungeni alifanya wapi kazi?
 
Mwandishi na mleta mada inaonekana mna kinyongo na zitto!

Hana kinyongo bali huo ndiyo ukweli. CHEMA CHAJIUZA, KIBAYA CHAJITEMBEZA. Kama anazo sifa za kuwa rais wakati ukiwadia wana-wa-nchi watasema wenyewe. Mwl Nyerere alitahadharisha kuwa ikulu ni mahali patakatifu na mtu safi hawezi kupakimbilia, kwamba ukimwona mtu anakimbilia ikulu mwogope kama ukoma. Ikuku kuna biashara gani hata mtu akimbilie? Taasisi ya urais siyo chakula ambacho ukisikia njaa unataka shibe. Taasisi ya Urais siyo mzoga wa kugombania kama mafisi wenye njaa wafanyavyo. Matokeo ya "mimi nataka urais" ndiyo haya tunayoyaona leo ya maisha magumu kana kwamba Watanzania tunafanya mazoezi ya kuingia jahanam.
 
hakuna anaye mzuia zito haki yake ila, huwezi kusaema kitu wakati wowote mahalipopote na kwa watu wowote.huu sio wakati wa kuongea mambo ya urais,ni wakati wa kujenga chama na kutumikia wananchi, ikifika wakati wa uraisi kuna utaratibu wa kugombea na kuteuliwa ndanio ya chama bila kusababisha marumbano na mijadala wakati hu amba ndo kabisa tumetoka kwenye uchaguzi
 
nafikiri zitto anajiona sasa ameshafikia kilele cha safari yake kisiasa na itamcost,suala la yeye kuwa na ndoto ya kuwa raisi si tatizo,kwa stage aliyofikia naamini kabisa kama amekurupuka cha msingi ni yeye kuendelea kujijenga zaidi kisiasa ndani na nje ya chama ili na wafuasi wake pamoja na watanzania kwa ujumla tuendelea kuwa na imani nae hata hapo baadaye atakapo kuja sasa na tamko kama hili watu tumuamini,vinginevyo anampango wa kutuvuruga
 
The guy is good!! He can make some significant changes!

Tatizo lenu nyie wadanganyika ni kusahau mambo upesi upesi; huyu kijana hana intergrity ya kuwa Rais kwani hana maadili mema kama alivyoonesha wakati wa sakata la DOWANS!! Kijana anachukua milungula[ Rostama amehuhonga sana] na hata ccm wanamuhonga na wanamtumia kudestabilize Chadema otherwise why does he have to divert people's attention from concentrating on campaigning in Arumeru to his Presidential ambitions? Zitto is overrating himself!!
 
Hatimaye sasa nimejiridhisha pasipo na shaka ni kwa nini zitto Kabwe ni swahiba mkubwa wa Deputy Director wa Usalama wa Taifa ndugu Jacky Nzoka, Zitto aje hapa kuuelezea umma wa JF ni sababu zipi za msingi zilizokuwa zinamfanya awe na mawasiliano ya mara kwa mara wakati chama chake kiko katika uchaguzi mkuu na Idara ya usalama wa Taifa ndiyo ilikuwa inaihujumu CHADEMA? hapa sitalajii jibu rahisi kwa swali gumu.

Pili Ben Saanane nimekuwa nikifuatilia mabandiko yako kwa makini sana na kuna kipindi nilidhani huwa unaonewa, kumbe nilikuwa najidanganya, humu jamvini umejipambanuwa kwamba wewe ndio unayejuwa siasa na yeyote ambaye atakuwa kinyume na mtazamo wako basi wewe utambatiza kila aina ya jina mara mnafki mara hivi mara vile, kumbe sasa nimejiridhisha ni kweli chama chako kiliposema huna maadili hakuna walipokuwa wamekosea, kwa nini unatetea Alliance ndani ya chama? narudia kukwambia tena jifunze kwa John Mnyika, yule kijana anaaminika machoni pa watu kwa sababu he is humbled,......jiulize ni kwa nini kijana mmoja Mnyika alundikiwe vyeo na nyinyi wasomi mpo? endelea na Alliance. zako.

Kwa dhamira ya moyo wangu kabisa, SIAMINI KAMA ZITO ANAWEZA KUWA HATA WAZIRI MKUU ACHILIA MBALI KUWA RAIS. Namwona ni mtu anayependa sana madaraka, Umwenyekiti wa CHADEMA anataka yeye, uongozi wa kambi ya upinzani bungeni anataka yeye, kila nafasi kubwa ya kiuongozi anataka yeye. Watu wa namna hiyo ni wa kuwaogopa sana, watu wa namna hiyo wakiupata uongozi huwa ni ving'ang'anizi sana maana wakati wote hawapendi kuishi au kufanya kazi chini ya mtu mwingine. Zito anafanya mambo mengi mazuri lakini yenye msukumo wa hila wa nia ya kujijenga ili aweze kuyapata madaraka makubwa. Ninafahamu kuwa viongozi wa CHADEMA wanalijua hilo lakini ni wenye busara na wanamwacha mpaka siku ile ambapo Watanzania wengi watamjua Zito ni nani na ni mtu wa namna gani. Zito anasumbuliwa sana na fikra kuwa yeye ni mtu maarufu sana na anafahamu sana. Haiwezi kuingia akilini, mtu mwenye fikra zilizotulia anafikia kutaka kuacha jimbo lake eti akagombee ubunge jimbo la Geita au Kahama, kwa sababu gani? Na wananchi wa Kigoma walimtendea wema sana kumpa hizo kura kwa kitendo alichowafanyia, na ninaamini aliupata ushindi wa ubunge kwa vile JK alitaka ashinde, na ndiyo maana JK alienda majimbo yote ya Kigoma kupiga kampeni lakini hakwenda jimboni kwa Zito.
ZITO FOR PRESIDENCY, A BIG NO. Ana haki ya kugombea kama mtanzania mwingine yeyote lakini kupewa dhamana hiyo, siungi mkono. Ninaamini leo kama kukitokea chama chochote cha siasa, iwe CCM, CUF, TLP, PPT Maendeleo, n.k. ambacho kingeweza kumhakikishia Zito kuupata Urais, ni lazima angeenda huko. Kwake kilicho muhimu ni Urais wala siyo itikadi ya chama. Ni nia hii ya Zito ndiyo inayomfanya asitulie sana, mara yupo karibu na naibu mkurugenzi wa usalama wa Taifa, mara anafanya mikutano na akina RA, hii yote ni kwa sababu hajui ni nani na ni chama gani kitakachomhakikishia kuupata urais. WATU WA NAMNA HIYO NI WA KUWAOGOPA SANA KATIKA NAFASI KUBWA KAMA YA URAIS. Sina chuki wala ugomvi na Zito, nafurahia uwezo wake wa kujenga hoja na kufuatilia lakini sina imani na dhamira yake, na hii wakati fulani huwa ni hulka
 
Kwanza ni zamu ya Wakristo. So long as Zitto ni mjahidina asubiri mpaka 2025

mkuu umeona mbali, mimi binafsi sitaki tena kusikia mambo ya hawa jamaa wanaoitafuta ikulu kwa lengo la kuimarisha dini yao badala ya kutukwamua na umaskini.
 
nafikiri zitto anajiona sasa ameshafikia kilele cha safari yake kisiasa na itamcost,suala la yeye kuwa na ndoto ya kuwa raisi si tatizo,kwa stage aliyofikia naamini kabisa kama amekurupuka cha msingi ni yeye kuendelea kujijenga zaidi kisiasa ndani na nje ya chama ili na wafuasi wake pamoja na watanzania kwa ujumla tuendelea kuwa na imani nae hata hapo baadaye atakapo kuja sasa na tamko kama hili watu tumuamini,vinginevyo anampango wa kutuvuruga

Umenena ukweli rafiki!
 
huwezi kuamka asubuhi kabla hata hujapiga mswaki unaanza kupayuka..''mimi ni mpole''mimi ni mtu mwema sana, ninafaa.. nimekijenga chama toka nina miaka 16..mimi ndio nimekifikisha hapo kilipo ...ni mimi na mbowe tu ndio tuliokuwa tunakesha...nafaa jamani...wanaokuona ndio wanaweza kusema hivyo kama wewe ni mpole au mkali, jasiri au muoga......kama zitto anafaa hakuna haja ya kusimama kwenye kingo za barabara juu ya kilima alfajiri yote hii na kuanza kupayuka kuwa yeye ni mtu mwema na anafaa kuwa rais wa nchi......

hizi ni dalili za urafi ulipindukia...zitto hufai kuwa rais...take it or leave it
 
Holy c.r.a.p!!!!

He was saying his dreams!!! He even said if his party will ALLOW HIM!!! if not he will support any one endorsed by his party!! WHATS WRONG WITH THAT???

**** indeed... watu wanatafuta umaarufu kwa kutumia jina la Zitto sasa.

"ITS GOOD TO DREAM, BECAUSE THOSE WHO DON'T DREAM ACHIEVE LESS"
 
Naunga mkono hoja Zito hafai kuwa rais sifa zinamsumbua pia haaminiki kabisa huyu mtu kigeugeu sana
 
Ila watu wa kigoma sijui wakoje umaarufu kidogo tu wanataka kuongoza watu.kumbe ndomaana toka tupate uhuru hatujawai kuwa na mkuu wa majeshi kutoka kigoma watawala wanaogopa wasije pingunduliwa na this peoples.
 
Holy c.r.a.p!!!!

He was saying his dreams!!! He even said if his party will ALLOW HIM!!! if not he will support any one endorsed by his party!! WHATS WRONG WITH THAT???

my friend waberoya, i fully concur with you....there's nothing wrong at all.
however, we all as humans see these various dreams in life but simple wisdom tells us to keep our bowl shut about them.

say, that chick over there is some beauty and a dream of any man (i mean any man!).... now tell me - if you are married, will you speak your dream out to your wife? the answer to this is obvious and this is the sort of advice zitto's true friends are trying to extend to him.

am one of zitto's admirers - i will never hide this fact. i think he's a great leader and could make an excellent president in the long haul lakini inaelekea bila kujitambua anataka kukitia kitumbua chake mchanga kwa mikono yake mwenyewe!
 
Mimi sina tatizo na uhuru wa mawazo. Sina tatizo kabisa na kauli ya zito. Ni haki yake kikatiba na nina heshimu mawazo yake. TATIZO KUBWA NILILOKUWA NAO NI MUDA ZITTO ANAOTUMIA KUTOA MAWAZO YAKE. Chunguza utaliona hili. Zitto anapenda kutoa kauli zake kipindi ambacho chama chake kipo kwenye harakati fulani. ALIWAHI PIA KUTOA KAULI YA URAISI KWENYE JIMBO LAKE WAKATI BADO UCHAGUZI WA RAISI UNAENDELEA 2010. kwa hili watu wote wenye kupenda kuchambua na kuangalia vitu kwa undani si walaumi kwa KUMUITA HUYU JAMAA MNAFIKI. Angalia hata kampeni za uraisi 2010 alishiri kwa kiasi gani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom