Zitto: Namsubiri Mbowe Mahakamani

Zitto: Namsubiri Mbowe Mahakamani

Status
Not open for further replies.
Mwana CCM yeyote mwenye kushadadia issue ya ZITTO na CHADEMA ni malaya wa Kisiasa.
By Cyril Chami

Kwani huyo Cyril Chami ni nani mpaka umnukuu, mbona mitazamo inapishana siolazima tuamini maneno yake, twambie wewe mtazamo wako ni upi
 
Last edited by a moderator:
Mbunge wa kigoma kaskazini zitto Kabwe (Chadema), amesema anamsubiri mwenyekiti wa chama hicho, Freema mbowe mahakamani.
Zitto ametoa kauli hiyo baada mbowe kutangaza kumburuza mahakamani kutokana na kile kinachodaiwa kumzushia tuhuma za uongo
Nasema sitaki malumbano na kiongozi yoyote, nachotambua masuala ya mahakama yanajibiwa mahakamani na si vinginevyo" alisema zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya MTANZANIA kutaka kujua msimamo wake kutokana na kauli ya Mbowe kukududia kumshitaki, kutokana na madai ya kusema uongo dhidi yake. Zitto ambaye yupo nchini Nigeria anakohudhuria vikao vya kamati za Bunge za serikali kwa nchi za Afrika, alisema pamoja na Hali hiyo mahakama ndio njia pekee ambayo haki ya mtu inaweza kupatikana.
Alisema kwa msingi huo, hivi sasa hayuko tayari kuruhusu malumbano ambayo Hayana tija kwa Taifa.

" nipo Nigeria na bahati mbaya ninaumwa sana, ila hivi Leo ninamshukuru Mungu nimepata nafuu kidogo. Kama nilivyosema mwanzo sitaki Malumbano na mtu. Pamoja na kusema anaumwa, hakuwa tayari kufafanua ni ugonjwa gani unaomsumbua.

" huu muda nahitaji kutafakari maisha yangu kisiasa na kwa vyovyote vile masuala ya mahakamani yatajibiwa mahakamani", alisisitiza zitto
Wapi Ben Saa 8
 
Mbowe anazuga tu, hawezi peleka pua yake mahakamani kwani anafahamu atakavyoumbuliwa. Ugumu wa kesi za kashfa unatakiwa kuthibitisha usafi wake, na unaowashitaki wanathibitisjha uchafu wako!!!

Hii mbinu tu ya kufifisha mjadala wa usanii wanaoufanya, kuwaaminisha Watanzania kwamba wao ni wasafi na kuwaonyesha wachafu na maadui wa Watanzania huku wao nyuma ya pazia wakiwapigia magoti hao hao wanaowaita wezi wa rasilimali za Watanzania kuwaomba fedha.

CHADEMA waendelee tu kumwamini Lissu, ila wajiu atawamaliza, hata kama JK hatumpendi bali kauli yake kuhusu huyo mwanasheria ndio ukweli wenyewe!
 
Mbunge wa kigoma kaskazini zitto Kabwe (Chadema), amesema anamsubiri mwenyekiti wa chama hicho, Freema mbowe mahakamani.
Zitto ametoa kauli hiyo baada mbowe kutangaza kumburuza mahakamani kutokana na kile kinachodaiwa kumzushia tuhuma za uongo
Nasema sitaki malumbano na kiongozi yoyote, nachotambua masuala ya mahakama yanajibiwa mahakamani na si vinginevyo" alisema zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya MTANZANIA kutaka kujua msimamo wake kutokana na kauli ya Mbowe kukududia kumshitaki, kutokana na madai ya kusema uongo dhidi yake. Zitto ambaye yupo nchini Nigeria anakohudhuria vikao vya kamati za Bunge za serikali kwa nchi za Afrika, alisema pamoja na Hali hiyo mahakama ndio njia pekee ambayo haki ya mtu inaweza kupatikana.
Alisema kwa msingi huo, hivi sasa hayuko tayari kuruhusu malumbano ambayo Hayana tija kwa Taifa.

" nipo Nigeria na bahati mbaya ninaumwa sana, ila hivi Leo ninamshukuru Mungu nimepata nafuu kidogo. Kama nilivyosema mwanzo sitaki Malumbano na mtu. Pamoja na kusema anaumwa, hakuwa tayari kufafanua ni ugonjwa gani unaomsumbua.

" huu muda nahitaji kutafakari maisha yangu kisiasa na kwa vyovyote vile masuala ya mahakamani yatajibiwa mahakamani", alisisitiza zitto
.

Msomi utamjua tu, MBOWE aende tu mahakamani, vyombo vya habari siyo mahakama.
 
Uwezo wa zitto ni zaidi ya viongozi wote wa makao makuu wa chadema hutaki unaacha ila huo ndiyo ukweli.

Taifa hili limepata hasara kubwa coz uwezo wenu wa kufikiri na kuchambua mambo ni mdogo sana. Hii ni hatari sana na poleni sana
 
Watu wa kigoma kwa kupenda kujitutumua!!Yaani hapo anataka amwonyeshe mwenyekiti wa chama nani mbabe Kati ya mwanachama na mwenyekiti au!?

Mie najiuliza hivi Zitto hizi jeuri za kubishana na mwenyekiti wa chama kazitoa wapi?

Hivi Mwigulu Nchemba au Nape Nnauye anaweza akabishana na J.K kweli?Hata kama ni kupigania demokrasia?Demokrasia gani inatafutwa kwa kutukana viongozi wako wa chama kwenye mitandao ya kijamii huku ukihubiri kuwa unakipenda chama hichohicho wanachokiongoza?

Zitto hafai hata kwa Limao!

Wajinga tu na wachumia tumbo ndo huwaabudu wenyeviti wa vyama,Anakosolewa Mungu sembuse huyo P-mbi.
 
Ndugu mtoa mada nashukuru kwa mada yako ila umnikera tu kwa hitimisho lako hata nikaona hatamada yako haina maana tena,tutahubiri ukabila mpaka lini?mtanzania wa leo unazungumzia ukabila nani atkaye kuelewa juu ya hilo zaidi ya kujua ni ushabiki wa kisiasa zaidi jamani tubadilike.
 
Hili gazeti mhariri wake ni Absalom Kibanda aliyekuwa mhariri wa Tanzania Daima zamani.

Absalom Kibanda huwa anajinasibu kwamba yeye na Zitto ni marafiki sana.

Gazeti la Mtanzania mmiliki wake ni Rostitamu ambaye ametajwa mara kadhaa kuwa na mawasiliano ya karibu na Zitto. Pia katajwa na Zitto eti alimuhonga Mbowe kipindi cha uchaguzi.

Kwa sababu hizo hapo juu zageti hili haliaminikina kamwe haliwezi kuaminiwa kwa habari inayowahusisha watajwa hapo juu.

Kwa vyovyote litaandika udaku tu

kwani mbona Rostam amewahi kuwa na mawasiliano na Mbowe? Au hilo hulijui
 
mnampamba kwa ujinga,huku akifa na kusahaulika kisiasa.CDM tulishampiga stop kutumia majukwaa yetu kufanya harakati zake.kwetu huu ni wakati wa kupanga na kutekeleza mikikati ya ushindi ktk chaguzi za serikali za mitaa na si kurumbana na marehemu mtarajiwa kisiasa,story zake c muda mrefu zitafutika na magazeti kama mtanzania yatakosa cha kuandika.
 
Huyu dogo Zitto alishakuwa kama wema sepetu kwa kupenda attention ya watu.

Kama anaumwa si yupo Nigeria, basi aje aende Kwa TB Joshua aombewe mapepo ya mwandiga yamtoke.
 
Last edited by a moderator:
Wapuuzi bongo lala ndio mtabaki kumsifia zitto! ! Ana uwezo gani huyo mwandiga marehemu??? Labda kwenu nyie chama chakavu maccm
 
...mh. Mbowe twende taratibu na hicho kirusi kinatekeleza azma yake ya kupoteza muelekeo wa chama baada ya juhudi za kukiua kugonga pua. Akija mahakamani aje na majibu ya mkwanja aliokuwa anavuta pale kwenye ofisi za MOTeL...
 
Ninacho ona watanzania tunakuza mambo kishabiki, kama wewe ni mpenzi wa zitto au chadema kwa nini msiandamane tujue mmechukinzwa? Kila sitto zitto, chadema chadema nini? Mnatuchosha, tuna maswala ya katiba mpya, uchaguzi unakuja badala tufikirie maendeleo tufikiri migogro oooo uchaga udini naona hamna cha maana hapa badilikeni kuna mambo ya msingi kwenye hii miaka miwili.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom