Zitto, Kwenye hili tayari umeshinda!

Zitto, Kwenye hili tayari umeshinda!

mbona kama hueleweki vile?. ulitaka kusema nini labda?.

Namaanisha chadema hawapotezi muda wapo busy na harakati za kuwakomboa watanzania.

Namaanisha Zitto wa leo siyo yule wa PM7. Labda kama una taarifa zaidi ya hii.

It is worst of time to discuss such craps like this one!
 
guys who against Zitto wanajificha sana hata utambuzi wa ID zao niwamashaka sana,lakini watetezi wa Zitto wako wazi kabisa na wanaongea bila uoga,hii nidhahiri sahiri Zitto kagusa maslahi ya maBig fish ndani ya CHADEMA..
Hata ya kwenye hoja ambayo inamgusa Lema,nakubaliana na mtoa mada kwa asilimia zote,yeye wakati anahaha kutafuta kichaka cha ujangiri,mwenzake anapigana kuisimamisha CHADEMA...Tanzania ina hitaji vijana wamfanano wa ZZK katika kuleta upinza wakweli nasio upinzani wa ki puppet kama uliopo sasa waviongozi kuwa wapigasoga wakisubiri ruzuku iliwaendeleze ujenzi wa makasri yao...

UPINZANI THABITI UTAJENGA CCM IMARA

lazima tuwaeleze ukweli mpaka ukweli uwaingie hata kama hawaupendi.
 
Namaanisha chadema hawapotezi muda wapo busy na harakati za kuwakomboa watanzania.

Namaanisha Zitto wa leo siyo yule wa PM7. Labda kama una taarifa zaidi ya hii.

It is worst of time to discuss such craps like this one!
waambie sasa WAGAZA wenzio waache kumchafua kwa majina bandia.
unajidai upo neutral kwa verified user ukiingia porini unamtukana.
lazima tubadilike
 
Mchange.

Hata wewe umeishawashida kwenze huu uzi hakuna wa kusimama na wewe.
 
Last edited by a moderator:
ulichoandika na unavotaka kutuaminisha ni vitu tofauti
mmetumwa nyie magamba kuharibu vyama vingine
kwa vile akili za magamba ni kuharibu badala ya kutekeleza ahadi hatuwashangai
mtajikuta mnapoteza muda na ikifika 2015 sijui mtaimba nyimbo gani tuwaelewe tena.
nakushauri ubadili avatar yako unajikashifu mwenyewe
ndio maana nachukia siasa,vijana wa Tanzania mnakubali kutumika badala ya kutumia akili zenu kuendeleza nchi.
CCM sio baba yako wala mama yako, nchi inahitaji sera na watekelezaji sio siasa za maji taka

kama kutumwa kuharibu vyama vya upinzania basi LEMA ndio mtumwa namba moja
 
Kusema zito ameijenga CDM sio sahihi...kusema zito ana mchango kwa CDM ilipo ni sahihi. CDM ilikuako kabla ya Zito Ipo na ataondoka ataiacha... Mwenye mchango kwa vuguvugu la mabadiliko ni mtu muhimu na akikengeuka anawekwa kando wengine wanaendelea..kanuni rahisi kabisa.
 
Mchange.

Hata wewe umeishawashida kwenze huu uzi hakuna wa kusimama na wewe.

hahahahahahahah. hakuna mwenye uwezo wa kupingana na ukweli.
sawa ya waongo wanaojificha na majina bandia ni kuwaumbua na kuwaambia ukweli tu.
 
Nahtaji mtu anitengenezee tisheti 2,moja nyeus na nyingne rangi ya chai ya maziwa yenye picha ya zitto kabwe na maneno #team zitto. Yeyote anayedeal na hzo mambo anipm. Hakika zitto ni mbarikiwa kama ronaldinho gaucho.
 
Kuna post naona imefutwa na MoDs ilikuwa inahusu Mutahaba amjibu Zitto sielewi kwa nini. Sema nimefanikiwa kuicopy.

Naomba kuuliza Muhataza ni nani??

Mutahaba ni nani hasa?? naomba nitumie hilo jibu la mutabaha kwenye inbox yngu ya fb,,,natumia jina la dotto rangimoto
 
Umeandika utumbo mwenyewe, utasoma mwenyewe ukishirikiana na masalia wenzako plus Lumumba project. Or else ni nani mwenye akili timamu atapoteza muda wake kusoma all this long rubbish?

nadhani umeandika huu utumbo wako baada ya kumaliza kusoma ANDIKO TAKATIFU TOKA KWA HABIBU MCHANGE..
duh!!! mnaomchukia ZZK mnaweza kuja kunywa sumu
 
unakijua unachokisema wewe?. ni kipindi gani ambacho chadema imekuwa kwa kasi na kwa nini?. acha kuongea ----- mkuu. lema hawezi kutumiwa kupambana na zitto, hawapo sawa hata kidogo

kumbe tatizo lako ni low reasoning capacity.
 
Theo Mutahaba amjibu Zitto

Ndg. Zitto
Nasikitishwa sana na hizi tabia zako za ajabu ajabu. Mimi nafanya kazi katika moja ya taasisi za ki usalama na nimeshirkia mara kadhaa kukupa fedha.

Nyendo zako hata na sisi tunazijua na nimeshangazwa na utoto wako wa kuandika waraka ambao umetoa vitisho ambayo inadaiwa kutoka kwa Andrea Codes. Ndugu napenda kukuonya kwamba umefanya mengi ambayo hata wana Chadema hawajui.

· Swala la Bomu Arusha ulishiriki na lengo ilikuwa ni kumuua mwenyekiti wa Chadema pamoja na
Ndg. Lema. Hii kitu ulipanga, wewe, mwigulu na vyombo vya usalama ·Zitto, rais Kikwete alipoenda Sudan ya Kusini uliambatana naye. Unakumbuka sababu ya wewe kuitwa? Nikukumbushie kwamba ilikuwa zawadi kwako ya kuihujumu chadema. CCM hawakupendi, bali wanapenda hujuma zako ndio maana walikudanganya kwamba watakusaidia kupata uenyekiti CDM ikiwepo kumuua Mbowe na kumdhoofisha Dr. Slaa

· Ndg. Zitto unadanganya umma kwamba unafuatilia fedha Uswisi wakati hii ni njama ambayo imesukwa na TISS kisha ukakabidhiwa ili CHADEMA isiibane sana serikali.

· Tueleze ni majina gani uliyoyapata. Na kama umeyapata, tunaomba kujua jina lako ni namba ngapi, kwa sababu na wewe una fedha nje ya nchi na ushahuidi tunao

· Umekuwa ukijenga mtandao wa kuwania uenyekiti na fedha ulizopewa na TISS pamoja na CCM ili kumn’goa Bw. Mbowe kwenye uenyekiti
wa CHADEMA ili 2015 CCM ishinde.

· Zitto, una ghorofa Dodoma karibu na St. Gasper Hotel. Fedha za kujenga lile jengo zimetoka wapi?

· Zitto, Barrick gold walikujenga shule pale jimboni kwako. Baada ya lile shule kujengwa na pia kupewa kitita cha fedha ulinyamaza kabisa

· Ndg. Zitto, wakuu wengi wa mashirika ya umma wameleta malalamiko TISS kuhusu unavyochukua
fedha kwao. Hilo unalijua kama ni ufisadi?


Ndg. Zitto, wewe ni kijana mdogo. Hizi tamaa zako za kifisadi zitaipeleka nchi pabaya. Tunakuangalia na kelele zako hasa fedha za uswisi. Usichezee na akili za watanzania. Wewe ni fisadi namba moja.

Umeficha fedha nje, ama nikukumbushe kwamba, majuzi ulipokuwa nje ya nchi ulitoa fedha kwenye benki Fulani. Ile account umefunguliwa na nani?

Badilika kijana. Kisiasa umeshajimaliza. Pengine nikukumbushie kwamba mawasiliano yako na Jack Nzoka, Mwigulu, Ridhiwani za kisaliti ndio chanzo cha kuanguka kwako. Ila hacha kuwadanganya watanzania na kiini macho cha Uswisi. Umeshajua mengi sana , usishangae kijana ukija kutoweka ghafla. TISS hawachezi na mtu. Na ni wao au CCM ndio watakao kumaliza sio CHADEMA.

Ule waraka unaosambaa ni mali ya TISS na imeratibiwa na CCM ambao ndio ndugu zako wakubwa Andrea, take care of your son. Get out of these Zitto corrupt acts. you know quite well that we wired you money and we have the evidence. Why would you waste your effort making noises? do you know the German government is investigating this matter? why would you fall for Zitto childish internet games of writing emails to the Chadema

leaders. So for your information, the document came from CCM and Tanzania Intelligence
Services Nakutakia kila la kheri kwenye kuhujumu Chadema.

mmmh!!! .......................this time tutayasikia mengi sana
hivi ni sababu ya uongozi tu ama kuna jingine khaa!
 
Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwa na mtindo wa kurushwa kwa shutuma mbali mbali kutoka kwa viongozi wajuu wa CHADEMA wakitumia majina bandia kumuelekezea ndugu zitto kabwe.

Kwa makusudi kabisa viongozi hao wakiongozwa na mwenyekiti, katibu mkuu na wakurugenzi kadhaa wamekuwa wakirusha kila aina ya shutuma humu mtandaoni lakini kwa hofu kubwa ndio maana wanajificha kwa kutumia akaunti bandia.

Jana na juzi nimepokea sms, emails na simu nyingi sana kuhusu hiki kinachoitwa ripoti ya siri ya SLAA, MBOWE NA WAGAZA WENGINE dhidi ya ZITTO zikisema namie nimetajwa humo kuwa ninashirikiana na Zitto kukihujumu CHADEMA.

Bahati mbaya sana, hakuna ripoti ama shutuma zozote anazopelekewa Zitto kutoka kwa hawa majamaa ambazo hazinitaji, na kwentye hii nayo nimeshuhudia nikitajwa mara nyingi kupokea pesa kutoka kwa Zitto kukihujumu chama.

Bahati mbaya zaidi ni kwamba wafadhili wa mkakati huu ''OPERESHENI ONDOA ZITTO KWENYE HOJA ZENYE MASLAHI YA TAIFA'' wamekosa njia sahihi ya kutumia, wamekuwa wakiwatumia watu wale wale ambao kwa zaidi ya miaka na miaka tumekuwa tukikitetea chama kuwa si cha namna hiyo.

kitendo cha MBOWE na SLAA kuwatumia JOSHUA NASSARY, GODBLESS LEMA, MAMUYA na wengine, kinauthibitishia umma wa watanzania kuwa sio kweli kwamba zitto ni tatizo kwenye CDM, kitendo hiki cha kuwatumia watu wanaolalamikiwa kuwa wanabebana kimisingi ya ASILI ya wanakotokea kinatuthibitishia watanzania kwamba CHADEMA ni chama cha watu wa eneo hilo.

lakini wamefeli zaidi kumtumia LEMA kuwa eti ni KAMANDA mwenye uchungu na CHADEMA kuliko ZITTO, hiki pia ni kielelezo cha upeo mdogo wa kufikiri kwa watu hawa.

ZITTO ni mjenzi wa NYUMBA inayoitwa CHADEMA, Zitto ameshiriki mpaka kuijenga CHADEMA tangu ikiwa nyumba ya nyasi, mpaka ikawa ya udongo, ikaja ikawa ya tofali za kuchoma na sasa CHADEMA ni nyumba ya VIGAE,

LEMA ni mpangaji tu kwenye hii nyumba CHADEMA, hakuna jinsi yoyote mpangaji akawa na uchungu na nyumba kuliko mwenye nyumba, hakuna na haitaka itokee.

LEMA ni mpita njia tu kwenye CHADEMA, Kamwe hawezi kuwa na uhalali wa kumsema na kumtukana mtu aliyekijenga chama kilichomsaidia kumfikisha hapo alipo.

Nani humu jukwaani alikuwa anamfahamu LEMA mwaka 2006, NANI?. nani alikuwa anafahamu lolote kuhusu lema 2007,2008,2009 mpaka 2010 kabla ya uchaguzi mkuu?.

Nani anayemfahamu Lema kipindi hicho kwenye CHADEMA?. LEMA ni TUNDA LA KAZI NZURI YA KISIASA ILIYOFANYWA NA ZITTO KABWE.

Wakati Zitto anahangaika kushirikiana na viongozi wenzake kuijenga CHADEMA, LEMA alikuwa ni KIBARAKA wa MZEE AUGUSTINO MREMA wa TLP.

Wakati Zitto anaibua hoja za msingi zenye maslahi kwa Taifa kama BUZWAGI na nyinginezo, LEMA bado alikuwa hata hajui chaguo lake la kisiasa katika nchi hii, yaani lema hakuwa akijua aende chama gani cha siasa.

Wanaokumbuka na wenye akili timamu watakubaliana nami kuwa ni zitto aliyekwenda Arusha kumnadi mgombea wa TLP wa udiwani wakati wa uchaguzi wa marudio 2008 huku lema akiwa mpiganaji kibaraka wa augustino mrema wa TLP.

wanachadema wanafahamu kuwa wakati tunafanya uchaguzi wa ndani ya chama mwaka 2009 LEMA ndio kwanza alikuwa ana siku 4 za uanachama wake ndani ya CHADEMA.

LEMA anapita tu njia CHADEMA kwa kuwa yeye ni msaka tonge tu kama wasaka tonge wengine, ndio maana alipita NCCR, ILIPOKUFA AKAKIMBIA, AKAPITA TLP ilipokufa akakimbia na sasa yupo CHADEMA nayo ikiyumba sidhani kama hataacha kukimbia. LEMA hana hadhi ya kukubali kutumiwa na kina MBOWE na GENGE lake kumshambulia ZITTO, hana hiyo moral authority. mpangaji hawezi kuwa na uchungu sawa na mwenye nyumba,

Leo CHADEMA ikipasuka, leo CHADEMA ikiyumba, ikitetereka atakayeumia ni ZITTO aliyeijenga na si LEMA aliyeidandia.

Nasisitiza hapa kuwa Hakuna namna yoyote ile inayoweza kumshusha Zitto kwenye heshima yake aliyojijengea kwa kusambaza uwongo wa namna hii, hakuna na hitakaa itokee.

Hakuna namna yoyote ile ya kumshusha zitto kwenye orodha ya wanasiasa bora na makini kwa kuwatumia watu kama kina lema na nassary ambao wakati wanaomba kura waliomba wakisema WATUMWE WAENDE BUNGENI WAKAWE KAMA ZITTO.

Again, ni rahisi sana kumshusha zitto kama kuna lolote baya amelifanya lisilo na maslahi kwa umma wa watanzania. ni Rahisi sana kumshusha na kumchafua zitto kama njia anazopita sio sahihi, LAKINI SIO KWA UWONGO WA KIPUUZI NAMNA HII.

Pamoja na kukiri kuwa Zitto ndiye mwanasiasa ninayemuamini na anayenivutia kuliko mwanasiasa yoyote Tanzania, na pamoja na ukweli kwamba zitto sio rafiki kwangu bali ni kaka yangu. Lakini sijawahi hata siku moja kupokea pesa kutoka kwake ama kwa MPESA au kwa TIGO PESA tangu nimefahamiana nae mpaka leo.

Ndio maana ninawapa pole MBOWE na vijakazi wake wanaotunga uwongo wa namna hii bila hata kujifikiria mara mbili mbili.

Uchaguzi mkuu wa ndani ya chama unawatia homa kundi la Mbowe na wagaza wenzake, uchaguzi huo unawafanya waweweseke kutwa kucha, mchana usiku.

Hakuna sababu ya kuhangaika na Zitto, wanachadema wapo na wataamua kwa yale mliyoyafanya, Zitto yeye ameshawaacha mile 2000 kwenye siasa zenye tija kwa Taifa.

Nimelazimika kuandika maneno haya baada ya kuona kuna huu ujinga unaofumbiwa macho na viongozi wa CDM kwa makusudi kabisa.
iliwahi kuandikwa humu mtandaoni kuwa ''Zitto ni maporomoko ya Nile, hayazuiliki kwa kifusi'' amewashinda na anaendelea kuwashinda.

Narudia tena kusema KWENYE HILI TAYARI ZITTO AMESHASHINDA.

1. Aliwashinda kwenye uwongo wenu mliokuwa mkiusambaza wa kupokea rushwa TANESCO lilipobumbuluka wakina mnyika, lissu na nassary wote waliufyata.

2. Aliwashinda mlipounda tume ya kumchunguza kuasisi migogoro ndani ya chama.

3. Alishinda kwenye hoja ya Buzwagi

4. Alishinda kwenye hoja ya kuwatimua mawaziri vilaza kwa kutoa hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu

5. Amewashinda kwenye hoja ya kuficha mali nje ya nchi (kama mabilioni ya uswisi) leo mnatapa tapa kwa kuwa bossi wenu anamiliki mali uarabuni.

Naomba niwakumbushe kuwa zitto ndiye mwanasiasa pekee wa upinzania anayeweza kuilazimisha serikali ikafanya maamuzi kutokana na hoja yake hata kama haipendi kufanya hivyo kwa wakati huo. Mfano ni hiyo hapo juu.

Naomba nihitimishe kwa kusema, ni kweli kwamba uwongo unapanda ghorofa kwa kutumia klifti, lakini hauwezi kubadilisha ukweli wa mambo daima dumu. uwongo utabaki kuwa uwongo tu na utaendelea kupuuzwa milele na milele.

Ndimi,
Habibu mchange
0762178678
mchangehabibu@yahoo.com

ni kweli kuwa wewe UMEFUKUZWA CHADEMA? Kama, ni kweli, kwanini ulifukuzwa? nikizingatia ile ripoti ya kwenye mitandao, ilikuwaje wewe ufukuzwe na kisha Zitto asifukuzwe?
 
Zitto anavyokuzwa as if kafanya jambo la maana sana katika siasa za nchi hii!

Wako watu wamefanya mambo makubwa sana lakini hawajikuzi namna hii na kutumia migogoro kupata sympathy!

Ni ujinga sana mtu kujikuza bila sababu za msingi, Mbunge kama Lissu ana miaka mitatu bungeni na amefanya mambo makubwa sana lakini sijawahi kumwona akijikweza katika mitandao ya kijamii usiku na mchana kutwa!

Wewe Mchange ulitegemea Zitto asisafishwe kwa rushwa za Tanesco wakati huyohuyo ni mshauri wa Nishati na Madini wa Mkono Advocates & Co. Hata kamsaidia yule mjinga mwenzenu kupata tempo kule.

Mnachokera ni kukuza migogoro mitandaoni, alisafishwa kwa rushwa kwa kuwa na yeye anakula hela ya Tanesco kupitia Mkono!

Kwa akili yako fupi umeshasikia Zitto akizungumza lolote kuhusu gas au nishati popote pale nje au ndani ya Bunge au mtandaoni anakokesha tangu Prof. Muhongo awaumbue yeye na Mkono bungeni!

Akili yako ya kuku haikuoneshi alvyohama hoja na kuamia kwenye pesa uswisi?

Kumlinganisha Mbowe na watu wenye njaa na masikini kama nyie ni upumbavu wa hali ya juu!
 
Last edited by a moderator:
Acha vitisho

Mnaandika tamko refu la kutaja majina ya watu.Hesabu idadi ya jina "Lema" kwenye hilo tamko.Utaweza kugundua kiwango cha hasira na upeo mdogo wa mwandishi.Hayuko sawa kisaikolojia

Nawewe umeamua kuipinga? Kweli maji yamezidi unga. Cc Yericko Nyerere
 
Last edited by a moderator:
Hii inaweza ikawa post yangu ya mwisho kwako, pengine utaelewa.

Hakuna anayedhani kwamba Mnyika au mwanaChadema yupo neutral bila upendeleo wowote. Na hilo siyo lengo langu na wala halipo katika asili ya binadamu. So, once more, inategemea na namna unavyopresent kutofautiana huko publically na pia nafasi yako kuproject hizo tofauti.

Huwezi kuona katika maandishi ya Mnyika akimpuuza Zitto kijinga kijinga kama wewe ulivyofanya kwa viongozi wako. Na hata kama Mnyika ikitokea ukahisi amefanya hivo, ana moral authority ya kufanya hayo. Anaweza kusimama akatetea mawazo yake kwamba "mimi ni Mbunge na kiongozi ndani ya chama, na nadhani fulani hauendi sawa".

Ona tofauti na wewe: "LEMA anapita tu njia CHADEMA kwa kuwa yeye ni msaka tonge tu kama wasaka tonge wengine"

Sasa, mwisho, ukiachilia mbali kwamba namna yako ya kuproject tofauti na waliokuwa wenzio haionyeshi humility kama mwanasiasa mchanga mwenye mwono wa kufika mbali kwenye chama, pia huna moral authority ya kumsema hivyo Lema. Na usidhani kwamba public itakupokea vizuri hata kama Lema amekosea (btw, ni mwanadamu). Na Mnyika wakati akiwa mchanga kwa level zako kisiasa, it would have been unthinkable for him to say such autrociously suicidal statements.

hakuna njia nzuri ya kuyasema maneno kuliko kuyataja kama yalivyo.
mwongo ataitwa mwongo, na mpita njia ataitwa mpita njia milele.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom