Zitto kuwa m/kiti wa CHADEMA taifa?

Zitto kuwa m/kiti wa CHADEMA taifa?

Heee, hiyo mikakati inatishia uhai wa CHADEMA manake kusema ukweli tuhuma hizo za ukasikazini na udini zipo masikioni mwa watu. Nadhani kuna watu wanzisambaza kwa makusudi. Kwa kutumia hiyo mikakati naona kuna hatari ya Zitto kushinda, amejipanga. Hivi unakumbuka JK alipochukua form ya kuomba ridhaa ndani ya CCM ili achaguliwe kuwa mgombea wao mwaka 2005 pale Kibaha, aliulizwa je ukishindwa, akasema hapa hakuna kushindwa na kweli alishinda. Tusubiri tuone ya Zitto.
 
Wanachadema wakikubaliana, hilo ni jambo dogo na linalowezekana. Awe na msimamo wa kukitetea chama tu, hoja zinajengeka, na anaweza kukubalika.
 
Unafahamu kutunga Uongo, endeleza Propaganda za kisiasa, ni haki yako pia kutoa maoni ila nikwambie kitu;

Katika Chadema hakuna kupokezana kuongoza, bali mtu huchaguliwa kwa uwezo wake na kama Zitto ataonekana kuweza kuongoza atachaguliwa na wanachadema.

Katika Chadema hakuna makundi ya sisi Vijana wale wazee, hao wote ni wamoja na lengo lao ni kuona Chama kinashamiri.

Kwa sasa Viongozi wakuu wa Chadema ni Mbowe na Dr wa ukweli Slaa, sisi ndio tunaowasikiliza na si kelele nyingine za milango.

Uzushi, Unafiki na Uchonganishi wako Vishindwe kabisa. wewe ni fungu la kukosa kwa hii mada yako lete nyingine.
 
Zito anahaki ya kuwa mwenyekiti,cha msingi ni demokrasia ichukue mkondo wake.na pia achunguzwe nia yake ni ya dhati ya kuwakomboa wananchi ama ana nia nyngne
 
Rafiki yako hakukueleza ukweli nilichosikia mimi ni kwamba Zitto anaandaliwa kuwa mufti wa waislamu Tanzania kutokana na kuwa na elimu ya kuridhisha, kwani huyu mufti wa sasa hivi akikaa kikao meza moja na maaskofu hawezi kuwa napointi ya kuongea kwa sababu ni darasa la saba, huo ndio mkakati uliopo kwa sasa kwani licha ya swala la umri wake kuwa mdogo, imethibitishwa kwamba hakuna umri maalum wa kuwa mufti, na kuhusu kitakuwaje awe mufti wakati zitto haswali sala tano, hoja hiyo ilipanguliwa kwamba kuna viongozi wengi tu wa Bakwata ambao ni wakristo na wengine ni masheikh lakini wanamiliki bar za kuuza pombe, na wengine wameoa wanawake wakristo lakini hawajafunga ndoa za kiislamu. nitaendelea kuwapa update hizi kwa kadili ninavyozipokea.
 
Zitto Ameshaharibu yeye abaki tu kula hela za mafisadi amabzo zina malip yake. Zito hana tofauti na tambwe hiza kwa sasa!
 
Zito anahaki ya kuwa mwenyekiti,cha msingi ni demokrasia ichukue mkondo wake.na pia achunguzwe nia yake ni ya dhati ya kuwakomboa wananchi ama ana nia nyngne

Nadhani ana uwezo pia....lakini kama alivyoambiwa JK na Mwalimu 1995 (japo hakupenda hata leo)....mimi naona bado kidogo...akue
 
Siku zitto akipewa uenyekiti wa Chadema, wa kwanza mie naihama CCM na nnahamia Chadema.

Lakini, nnavyojuwa Chadema wanarithishana kutoka Baba Mkwe mpaka Mkaziamwana.
 
Siku zitto akipewa uenyekiti wa Chadema, wa kwanza mie naihama CCM na nnahamia Chadema.

Lakini, nnavyojuwa Chadema wanarithishana kutoka Baba Mkwe mpaka Mkaziamwana.

Yasokuhusu katu hutuyaweza..........
 
Umetumwa na CCM wewe.

Eti zitto hatapata kura nyingi kwa wachagga? Sijui hapa unataka kusema nini.

kwahiyo tuamini CDM ni chama cha wachagga, au Cha watu wa kaskazini?

Mbona unataka kutugawa wewe? Pole, kwangu umengonga mwamba.

Eti umeambiwa na rafiki! Sihitaji kuwa na Degree kujua hii umeitunga.
 
Zitto kabwe hana hoja ya msingi amebaki kuwa wakala wa mafisadi. Hizo hoja anazozisema za uchaga na ukristu hazina tija kama na yeye anaamini katika propaganda hizo ya ukabila na udini ni bora akakaa pembeni aiache chadema na wafuasi wake. Zitto ameshapoteza mvuto kwenye chama na katika jamii ya watanzania. Watu wamepoteza imani naye. Zitto ambaye ningeweza kumuunga mkono kwa asilimia mia kugombea nafasi hiyo nyeti katika chama ni zitto wa mwaka 2007 sio huyu zitto wa sasa aliyechakachuliwa akachakachulika. Suala la zitto kupigiwa chepuo kuwa mwenyekiti wa chadema ni mkakati unaopangwa na mafisadi na wabaya wa chadema ili kukimaliza chama kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.. Nina amini hata kama zitto akigombea na mbowe bila kutumika mbinu chafu zitto hatakuwa na ubavu wa kumshinda kamanda mbowe.
 
icon1.png
Re: Zitto kuwa mkiti wa chadema taifa?


Rafiki yako hakukueleza ukweli nilichosikia mimi ni kwamba Zitto anaandaliwa kuwa mufti wa waislamu Tanzania kutokana na kuwa na elimu ya kuridhisha, kwani huyu mufti wa sasa hivi akikaa kikao meza moja na maaskofu hawezi kuwa napointi ya kuongea kwa sababu ni darasa la saba, huo ndio mkakati uliopo kwa sasa kwani licha ya swala la umri wake kuwa mdogo, imethibitishwa kwamba hakuna umri maalum wa kuwa mufti, na kuhusu kitakuwaje awe mufti wakati zitto haswali sala tano, hoja hiyo ilipanguliwa kwamba kuna viongozi wengi tu wa Bakwata ambao ni wakristo na wengine ni masheikh lakini wanamiliki bar za kuuza pombe, na wengine wameoa wanawake wakristo lakini hawajafunga ndoa za kiislamu. nitaendelea kuwapa update hizi kwa kadili ninavyozipokea.​
 
CCM huwa wananipa raha sana, wanafikiri siasa za uzushi zinaweza kuwaokoa kutoka motoni. Kwa sasa watatumia mbinu zao za zamani zitashindwa, watakufa kama KANU. Tuendako CCM itapasuka vipande viwili au vitatu, JK atabakiwa na kipisi akisaidiwa na baadhi ya mafisadi, mafisadi wataondoka na kipisi chao, mandondocha ambao hawajui mtumbwi unapokwenda watabaki wanashangaa, CCM waadilifu wataachwa kwa sababu hawana uwezo wowote wa kukemea, wala kuzuia.

Swala la nani atakuwa mwenyekiti wa CDM sio ishu, anaweza kuwa yeyote, katiba ndio muhimili mkuu wa chama chochote cha siasa. Katiba inaweza kumfanya fisadi akaacha ufisadi wake pale inapoweka wazi kuwa ukiharibu inakutoa na kukushitaki.

Swala la chadema lazima liwe gumzo kwani ****** hana kitanda, anaiona segerea yeye na Rizone 2017.

Chadema katu fisadi hata penya kwenda juu.
 
icon1.png
Re: Zitto kuwa mkiti wa chadema taifa?


Rafiki yako hakukueleza ukweli nilichosikia mimi ni kwamba Zitto anaandaliwa kuwa mufti wa waislamu Tanzania kutokana na kuwa na elimu ya kuridhisha, kwani huyu mufti wa sasa hivi akikaa kikao meza moja na maaskofu hawezi kuwa napointi ya kuongea

Mh! diversion. JF beware of this post.
:focus:
 
usipokuwa makini kwa hizi siasa unaweza kuchanganyikiwa!,mimi yangu macho ila nachoamini chadema ina watu wengi makini si rahisi kununuliwa kirahisi hivyo,si nec ya akina khadija kopa.
 
Wakuu,
Kuna habari za kuaminika kuwa Mh Zitto Kabwe ameanza harakati za kutaka kuukwaa uenyekiti wa Chadema Taifa. Nimeziita habari hizi tetesi kwa sababau sijui degree ya ukaribu kati ya Zitto na rafiki yake niliyeongea naye.
Mikakati ya kuusaka uenyekiti huo zimeshaanza na tayari ameanza kupanga safu ya uongozi hasa kwa ngazi ya Kitaifa.
Hoja ambazo ameaza kuisambaza chini kwa chini, kisiri siri sana na kwa umakini wa Hali ya juu ni kama zifuatazo;
HOJA ZA ZITTO ZUBERI KABWE kwa wapiga kura wake.
A) Uchaguzi uliopita alimpisha Mbowe kwa Ushauri wa Wazee kwa unyenyekevu wote, kwa hiyo safari ndugu yetu naye atawaomba wazee kuwa hii ni zamu yangu nami naomba nigombee na/au ikiwezekana nipite bila kupingwa kama Mbowe. Atawaomba wazee hivyo.
B) Hoja ya pili Chadema ni Chama kinachoungwa mkono sana na vijana hivyo, Dr Slaa siyo Chaguo bora kwa CDM kwa sasa kuwa mkiti ILA yeye ndiye Chaguo bora. Dr Slaa ni Mzee, Mbowe aachie kwa hiari hata kama katiba inamruhusu kwa kuwa ameongoza miaka 9 mpaka 2013 uchaguzi utakapofanyika.
C) Tatu, Chama chetu kinonekana au kinatuhumiwa kuwa chama cha Wachagga . Hivyo mimi nitamaliza hoja hiyo ili tushinde 2015. Ndani ya mkakati huu anategemewa kuchota kura toka mikoa yote isipokuwa wachaga. Wanategema kutumia fitina ikibidi hasa kama mbowe atagombea tena. Ikionekana Mbowe ana nguvu watamlazimisha kwa kashfa iwe iwavyo.
D) Mbowe na Slaa wote wawmetoka kaskazini, SASA ni muda muafaka na kanda zingine nazo ziongoze CHADEMA kama tumekomaa na tunataka kuingia ikulu.Hoja hii nayo inategewa kuwapa nguvu mikoa mingine. Tayari wapambe wako kazini isipokuwa kanda ya kaskazini.
E) Kete kubwa kuliko zote ni kuwa, kwa kuwa Chadema inatuhumiwa kwa udini na waislamu, mimi ndiye suluhisho pekee. Hapa tayari kuna watu wamesambazwa kwa wajumbe ambao ni waislamu ndani CDM ili wamwuunge hasa wale wanaoonekana kuwa wataweza kumaintain nafasi zao na kuwashawishi potetial leaders to be. Kumbuka uchaguzi wa taifa utafanyika baada ya chaguzi za ngazi ya chin kuisha kote nchini.

MIKAKATI
A) Viongozi ambao ni washabiki wake nchi nzima wamepewa fedha za kutosha kuhakikisha kuwa wale wanaomwuunga mkono wanashinda nafasi za kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa na Baraza kuu ili kumpitisha yeye mwaka 2013.
Kinachoshangaza kwa taarifa nilizo nazo toka moja wa marafiki zangu ambaye ni mtandao wake na asiyejua msimamo wangu ni kuwa fedha si tatizo katika kundi hili.
B) Washabiki wake ambao ni wanachadema na wasiowanachedema wanamchangia fedha nyingi sana. Wanakadiria kukusanya sh Bil moja. Hizi fedha nazo zilinipa mshangao nikizingatia kuwa alikuwa na confidence kupita kiasi.

NB; Alikana kabisa kuhusu watuhumiwa wa UFISADI kuwafadhili wao. Pia alikana kuwapo kwa mkakati wa kuhama Chadema ambao umekuwa ukirushwa katika jamiiforum ila alikiri kuwa bosi wao zitto anajua kila kitu katika JF kuhusu yeye. Ameamua kutojibu baadhi ya tuhuma huko JF na magazetini. Alisema, sasa tunampango wa kutumia sehemu ya fedha kusafisha majeraha ya mwahalisi, JF na magazeti mengine kwa mbinu yo yote. Sikuelewa maana ya Mbinu yo yote.
Kilichonishangaza kuliko zote.
Nilimwuuliza, je mkishindwa mko tayari kukubali matokeo? Alikataa kata kata kuwa kunakushindwa katika mikakati yao, piga ua gara gaza hakuna kushindwa. Iwe iwavyo lazima tutashinda.
Binafsi nilishindwa kumwelewa, nijuavyo, katika siasa kuna kushinda na kushindwa pia.
Wakubwa,
Humbly I submit.
Umefanikiwa utunzi ila tumekugundua umetumwa wewe,CDM si NCCR, TLP au CUF hainunuliki na ZITTO anajiko kwa JK na kwa MAFISADI kuganga njaa na hana uwezo wa kuiongoza CDM sanasana anatumiwa na wanaotaka urais 2015 lakini atashindwa vibaya.
 
Ukweli kwa sasa ni kuwa hata huko Kigoma, wameshasema kama ataendeleza undumilakuwili wake, hata Ubunge hapati.

Unakuja kusema awe Mwenyekiti? Mtu ambaye ALIKIKIMBIA Chama chake Bungeni baada ya kushindwa hoja kwa kura?

Sasa akiwa Mwenyekiti, bado ataendelea kukimbia?

Hapo ndipo alipofanya Makosa makubwa sana ambayo milele yatam-cost.

Alitakiwa kuwa na chama chake hata kama yeye HATAKI kwa sababu tu, alishindwa kuwaridhisha wanachama wa Chadema wasitoke bungeni siku Kikwete alihutubia.

Ananikumbusha wimbo wa Chidumule wa MV Mapenzi Namba 2.
 
Back
Top Bottom