Zitto, Kitila na Mwigamba wajisalimisha CHADEMA

Zitto, Kitila na Mwigamba wajisalimisha CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Zitto na Kitila hawawezi kuomba msamaha hizi ni porojo za kawaida kutoka Bavicha.

Kuomba msamaha ni ushara ya uungwana. Nilitarajia ungempongeza Zitto angalau kwa kujitutumua kuomba radhi badala ya kumkejeli na kuikejeli chadema. Zitto ameshapia kina cha maji. Anajua nje ya chadema Zitto ni galasa. Anajua pamoja na matamko ya wahuni bado watanzania wana imani na chadema.
Zitto anatambua kuwa wengi waliokua wanamuunga mkono hawapo naye. Anajua hata wana ccm wameanza kumkimbia. Anapoutazama mwisho wake anaona handaki zito la kisiasa mbele yake. Ni kichaa tu atakayeacha kuomba radhi...Waliompa kiburi wamemtelekeza kama walivyotelekezwa madiwani wa Arusha.
Zitto kwisha habari yake....!
 
Kwa matamshi yako hapa inaonyesha unaweza zaidi mchezo wa cheusi chekundu,ubishi na ugomvi wa Baa zaidi.
hili suala ni la kamati kuu wewe huna mamlaka ku decide watu wafikirie nini au kujaribu kuwa convince dude
 
Wawekwe under probation kwa mwaka mmoja. Katika kipindi hicho wasiruhusiwe kugombea nafasi yeyote ndani ya chama, kuitisha wala kushiriki mkutano wowote wa ndani wa chama, au mkutano wowote unaowahusu wanachadema. Halikadhalika wamtaje MM2 ni nani, na wawataje washiriki wengine wa ule mtandao, ambao nao eventually watawekwa kwenye probation ya mwaka mmoja endapo wataomba radhi...
 
Watu wajinga sana,Swala Dennis Msaki na Lwakatare,Liko wazi hata ukiiangalia ile Video youtube CDM inapanga Ugaidi,Watu wanasubiri mwakani wapewe FBI wathibitishe video ya kweli,ili muchinjiwe Baharini,ili USA na ULAYA wajue CDM Magaidi.kwa kuwa WATZ wamewajuwa na miishio yao CDM Mwakani.

hahaha ccm na FBI ya kichina, ccm mliuwa watu kanisa la Arusha ili kugombanisha waiskamu na wakristo, mkauwa watu mkutano wa chadema ili wstu waamini ni ugaidi masikini hamkujua kulikuwa na cctv, chadema ikawaumbua mpaka leo hamja thubutu kuleta FBI wala Facebook..hiyo video hata mwenye elimu ya video edit ya siku mbili anaweza kugundua hilo kuwa ni fake...
 
Mh Mbowe , wasipofukuzwa hawa , usituombe usitulaumu wana chadema baadae kidogo.
 
Unafiki wa chadema kwa hiyo kila kitu mnakiweka hadharani?
Hivi akina Zitto wakiamua kuweka kila jambo uchi mtabaki salama?

Kama kungekuwa na jambo baya,nina uhakika 100% zzk angeliweka hadharani ili CDM izidi kuumia.Lakini kwa sasa lolote baya nitakalosikia juu ya CDM najua ni uzushi tu kama ambao wamekuwa wakiwazushia baadhi ya makamanda kuwa ni magaidi.Mtu kama huyu anayefanya kila aina ya hujuma hastahili kusamehewa kamwe

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
hili suala ni la kamati kuu wewe huna mamlaka ku decide watu wafikirie nini au kujaribu kuwa convince dude

Ngumu kumeza eeh!..... Naona unatokwa povu kama umemeza mche wa mshindi, pole weye
 
Chadema bhana baada ya kuona jahazi linazama maridhiano halafu vifaranga wao wamewahi huku kuja kujisafisha huku ili waonekane wameshinda
 
Wawekwe under probation kwa mwaka mmoja. Katika kipindi hicho wasiruhusiwe kugombea nafasi yeyote ndani ya chama, kuitisha wala kushiriki mkutano wowote wa ndani wa chama, au mkutano wowote unaowahusu wanachadema. Halikadhalika wamtaje MM2 ni nani, na wawataje washiriki wengine wa ule mtandao, ambao nao eventually watawekwa kwenye probation ya mwaka mmoja endapo wataomba radhi...

Mkuu Tuko, zitto na wahuni wenzie ni wa kufukuza..hizo zingine ulizozisema ni kujifurahisha. Zitto afukuzwe uanachama!
 
Last edited by a moderator:
Kama kweli wanataka msamaha ni vizuri wakasema ukweli wote jinsi CCM ilivyowatumia! Wawe wazi bila kuficha neno!!! Kusema tu wana mapenzi na CDM haitoshi!! Hayo ni mazingaombwe ya mchana kweupe! Wajieleze kwanza kwa umma! Baada ya hapo nguvu ya umma ndiyo itakayowahukumu!!

danganya toto hiyo wangekuwa na mapenzi na chama wasingekubali kuwa vibaraka wa maccm,umeona wapi mwanamke au mwanaume akasema ana mapenzi na nyumba yake halafu analala kwa jirani?hao kazi ni moja wafukuzwe ili iwe fundisho hawakuona madiwani wa hapa arusha kitu walichofanyiwa na chama kinapeta ile mbaya hapa Arusha na tukawarudisha madiwani kata zote nne na bado kuna moja ya sombetini tunaenda kuichukua january labda waogope kuitisha uchaguzi,nasema tena timua hao wasaliti waende kwa waliowatuma.
 
Hawa wametukosea adabu sana, inabidi waite press conference na kukanusha mazagaza yote waliokuwa wakituchafua. ujue ninawamind sana hawa jamaa. Wasirudishwe kirahisi tu.
 
Kuomba msamaha ni ushara ya uungwana. Nilitarajia ungempongeza Zitto angalau kwa kujitutumua kuomba radhi badala ya kumkejeli na kuikejeli chadema. Zitto ameshapia kina cha maji. Anajua nje ya chadema Zitto ni galasa. Anajua pamoja na matamko ya wahuni bado watanzania wana imani na chadema.
Zitto anatambua kuwa wengi waliokua wanamuunga mkono hawapo naye. Anajua hata wana ccm wameanza kumkimbia. Anapoutazama mwisho wake anaona handaki zito la kisiasa mbele yake. Ni kichaa tu atakayeacha kuomba radhi...Waliompa kiburi wamemtelekeza kama walivyotelekezwa madiwani wa Arusha.
Zitto kwisha habari yake....!
Ni kweli kuomba msamaha ni kitendo cha ungwana upo wapi huo msamaha?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom