Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi
kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama
rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi
kwamba nchi ingekuwa katika machafuko
makubwa,” alibainisha Zitto.


Hivi ndugu Zitto wakati anatoa matamshi hayo sijui kama alifikiria tukio la kuogofya kama la mwanahabari David Mwangosi...
Sijui kama alifikiria vitisho wavipatavyo wale wote wanaothubutu kuweka bayana kadhia za Serikali hadharani...
Serikali ya sasa ni kama panya tu, inang'ata na kupuliza ili ionekane ni njema mbele ya wananchi wake...

Kuna siku wananchi watamshukuru rais wao kuwaacha wavute hewa, mali ya serikali. What's freedom, and its limits?
 
Mkuu hapo umesema kweli tupu, na hapo ndo hoja ya msingi ya kumfanya awe DHAIFU, yaani kutolerate yanayo liangamiza taifa alailo apa kwalo!

Zitto wakati mwingine huwa anashangaza, siamini kwamba akili yake hailijui hili analo jaribu kulitetea!

Zitto ni mchumia tumbo, pia ni lazima amsifie kimpwete, kuhusu huo uhuru wa kuongea anaouzingumzia huyu zito kabwe, hiyo ni haki ya mwananchi yoyote yule.ni haki ya kikatiba...hiyo hiyo katiba mbovu ya mkoloni inaruhusu.sasa anapomsifia kikwete hatumuelewi.
 
uvumilivu au udhaifu mkuu hawez kuwepa moja kati ya haya
 
Mchumia tumbo maskini huyu mtoto, amezoea vya kunyonga hivi kweli zitto unaweza kufikiri tutakubali kurudishwa nyuma na njaa zako? unajifanya mental kwa njaa? hivini kwa nini usitoke tu Chadema mwenyewe mpaka uharibu nguvu na matumaini ya watanzania? hatutakubali kamwe upumbavu huu, okay JK wa ajabu so? cheap staff halafu eti unataka uenyekiti wa chama cha watu wenye akili nenka huko kwa waha wenzio uzuri unajua kwenye mpango wetu haupo, shenzi kabisa hili toto laanakum kujikomba mpaka basi kabisa
 
hahahahahahaha
acha nicheke.

hivi uhuru wetu wa maoni ni hisani ya rais?
yani zitto anataka kutwambia kuwa angekuwa yeye ni rais leo hii tusingepata fursa ya kumkosoa?

Ina maana zitto angekuwa kwenye kiti cha jk ange funga na kuuwa wengi maana angechukia sana?

Yani zitto anataka hata haki yetu tuipigie magoti? uhuru wa kutoa maoni ni haki yetu hata angekuwa nani. Ina maana kipindi cha mkapa watu hawakutoa maoni?

HETI HUWA NA CHUKIA MTU AKIMUITA RAIS DHAIFU. hivi zitto ni kweli jk hana udhaifu kwenye utendaji? mbona utaki kumwambia ukweli unampanba?

zitto wewe si ndio ulipiga marufuku wabunge kuisifia serikali ya ccm? au sio wewe?

zitto ni kweli maendeleo yanapimwa kwa kutembelewa na wageni wengi?

Inaelekea ukiwa rais siku ukiitwa dhaifu huyo mtu kesho yake lazima aage dunia.

zitto ni kweli hakuna sababu ya jk kuitwa dahifu? hivi ni kweli haya matatizo yote uliyo yasema hakuna linalotokana na udhaifu wake kataika utendaji?

hii tabia ya ukigeugeu si nzuri kabisa nadhani hata yeye ana kushangaa kabisa.

Mkuu huyu jamaa ni kinyonga.
 
Kwa mujibu wajibu na uwezo nilionao kutokana na katiba ile ile ya mwaka1977. Ninauwezo wa kusema lolote pasi na kukiuka masharti sheria ama uhuru wa mwingine sasa nasema "TUACHE KUSEMA TUSIYOYAFAHAMU"
 
academic enrollment, barabara kuu za kwenda mikoani, wilayan, mijin, madaraja_afya, mishahara etc_sidhan kama kuna rais anayemgusa_sema anachafuliwa kama strategy ya kupeleka madaraka kasikazini_wasiowajua watawafuata_nilikuwa huko nikawaona hamna dira
 
UDOM, KATIBA MPYA, SONGWE AIRPoRT in Mbeya, DARAJA KIGAMBONI, DARAJA MALAGARASI, barabara zilizofunguka kitaifa na impact yake kwenye national economy_sema wengi hum ndo hivyo mpo hum hum dar scope yenu ndo hiyo hamuwez kuona aliyofanya huyu jamaa
 
Hapa ndo utofauti wetu kama wana jf na binadamu wakawaida unapoingia. Kinachonipa taabu sana ni pale baadhi yetu tunapowezakushindwa kuona udhaifu wa serikali hii chini ya jk.
 
Kasheshe,

..PCCB iko chini ya Ofisi ya Raisi.

..PCCB wamemshtaki Mramba kwa matumizi mabaya ya madaraka yake.

..kwa maana nyingine Ofisi ya Raisi wanaamini kwamba Mramba amefanya makosa hayo.

..wangekuwa hawaamini wasingemburuza mahakamani.

..sasa kitendo kile cha Raisi kumpigia kampeni Mramba huoni kwamba ni kukinzana na maamuzi ya chombo anachokiongoza mwenyewe??

..zaidi, ukizingatia kwamba Raisi pia anateua majaji, huoni kwamba kitendo cha yeye kumpigia kampeni mtu mwenye kesi mahakamani ni kunajenga picha ya kuingilia utaratibu mzima wa kesi hiyo??

..hivi umeona wapi kwengine ambapo Raisi anawafanyia kampeni za kisiasa washtakiwa wa ufisadi??


Joka juu, you are very right kama Rais hajaicha PCCB ifanye kazi freely.... kama ameiacha PCCB ifanye kazi free then you are wrong.
 
Integrity is doing things, even if no one is waching.
Sijui anachokiona zitto ni yapi?
 
Hapa ndo utofauti wetu kama wana jf na binadamu wakawaida unapoingia. Kinachonipa taabu sana ni pale baadhi yetu tunapowezakushindwa kuona udhaifu wa serikali hii chini ya jk.

ni lini hatukuwahi kuwa na Serikali dhaifu Tanzania tangu kuanzishwa kwake?
 
-Tayari tunaye Rais anayehukumu watuhumiwa.Aliwahukumu wezi wa EPA akawaamuru Warudishe

-Tunaye Rais anayetoa hukumu kwa kumuita mtuhumiwa Basil Mramba kuwa ni Panga la Zamani lisiloisha Makali

-Tayari tunaye Rais anayemsifia mtuhumiwa wa RICHMOND kuwa umaarufu wake unatosha kukipa chama ushindi huko Makuyuni

Katika tuhuma kuna pande mbili,ni aidha wapo Innocent ama Guilty.Kwa mtuhumiwa yeyote haitakiwi Rais mwenye busara kufanya pre-judgement!
Kasheshe,Come correctly!


"Everybody is considered Innocent until Proven Guilty",

That what president is demonstrating to you people who want to become parliament, judiciary and executive at same time... I know babu hawezi hii!!!

Brother Ben Sa8 please engage your brain, things are easy and no-brainer to understand...
 
Waafrika tuna mawazo ya kitumwa sana na huwa tunafikiria kiongozi kama rais ni mungu wa nchi na ana uwezo wa kufanya chochote kwa yeyote muda wowote anaoamua. Imefika stage tunaona rais ambaye hajaua na kufunga wananchi wanaomkosoa ni ''mtu wa ajabu''. Rais akitembelewa na marais wa nchi nyingine wanaofukuzia kupata malighafi eti ni ''rais wa ajabu''. Sasa huyo Zitto si ndio wengine wanamnadi ni mtu mwenye upeo na anafaa kuwa rais?
 
kwani huyu sie yule aliyepiga marufuku viongozi wa CDM kusifu viongozi wa ccm?
Namna anavyomfagilia kikwete anamshinda Nape!
Zitto CCM-B (II)
 
Back
Top Bottom