Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

Zitto ni tatizo, hasa inapokuja swala la njaa.
 
Yaani mungu ni wa Ajabu sana. Anaweza kuumba watu wenye sura Mbili tofauti sana kama Zitto. huyu jamaa ili aiponde serikali, anasubiri yeye "personally" ndio a-be "challenged". laa sivyo, mambo ni shwari sana kwake. Ila nikukumbushe ZITTO kwamba pesa za Uswizi na Epa bado hatuzijui zilikokwenda , na JK bado Mungu huyuhuyu wa Ajabu anampa uhai (sijui mpaka lini); leo wewe unamsifia wakati hatuna majibu. Kumbuka Utumbo wa Mwangosi ulitoka nje sio kisa ni mkubwa ila kwasababu alitumbuliwa kwa maksudi na polisi kwa maagizo ya RPC. Wewe unang'ata na kupuliza..... Utakula kwenzi la Huyuhuyu Mungu wa ajabu kweli na apa.
 
jk anaweza kubeazwa kwa upole wake na uhuru aliowapa watanzania ndiyo uhuru huo wanautumia vibaya mpaka wanatukana.lakini wakati wake ndo huo unayoyoma naamini atakapo staafu umuhimu wake mtautambua tu hata mnaombeza.

uhuru upi aliotupa jk wakati hayo ni matakwa ya kikatiba na kisheria?ni lazima kuheshimu uhuru wa mtu kutoa maoni yake bila kubugudhiwa,sasa mbona sioni kitu jk alichotupa?watu wanajua haki zao na namna ya kuzitumia halafu wewe unasema jamaa ndio katoa kama hisani?ingekuwa ni uwezo wake angetuziba mdomo lakini ndio hivyo hawezi ata iweje.
 
Ben saanane anamsfia membe.....zito anamsifia jk...cdm kina mnyka kuweni makini bundi kaingia kwenye chamam chenu njaa mbaya
 
Ben saanane anamsfia membe.....zito anamsifia jk...cdm kina mnyka kuweni makini bundi kaingia kwenye chama chenu njaa mbaya
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

“Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa,” alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

“Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu,” alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung’oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

“Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu,” alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

“Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa,” alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.

Mmhhh!! Naanza kupata wasiwasi
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

"Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

"Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa," alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

"Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu," alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung'oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

"Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu," alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

"Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa," alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.
UNAFIKI ninaouchukia mno! ni wa huyu kiongozi wangu ZZK!! Hebu eleza uhusiano wa Rais na TISS. Uhusiano wa TISS na watoa kucha na watoboa macho wa watanzania wema. Kama JK ana uhusiano na TISS basi ana uhusiano na watoa kucha na macho kwa wapinzani wa mlengo wa CCM. Halafu ZZK anauita UHURU wa maoni! Watu wanaoagiza nyuma pazia kushughulikiwa wanahabari hao ni akina nani? JK ni mtu asiyetaka lawama! mtu anayeficha upande mweusi wote! Alipokataa kutokumjua mwenye DOWANS aliniacha kinywa wazi!!
 
Katiba mpya inaandikwa chini ya UONGOZI wa Jakaya. Hili halijawahi kufanyika tangu mwaka 1977. Jakaya ataiacha TANZANIA nyingine kabisa mwaka 2015. Jakaya anaweza kuwa "ameshindwa" hayo mengine mnayosema lakini hili la KATIBA anaelekea kuliweza.

Kwa wenye uwezo mkubwa wa fikra, mjitahidi kufikiri vyema. Jakaya anaiunda upya TANZANIA.
 
Zitto anaongea nini?

Anaongelea mabilioni yaliyifichwa uswis,Aliipa muda serikali iwataje na isipofanya hivyo atawataja,sasa sijui ule muda bado tu au tayari?au ndio anampongeza Bwana Mkubwa ili amwambie Lukuvi au Wassira wataje.
 
-Kwenye Sera za Mambo ya Nje hatuangalii matukio ya kutembelewa.Sera yetu ya Mambo ya Nje ambayo tenets zake ni za tangu enzi za Mwl.Nyerere zinatakiwa kufanyiwa overhaul.

Leo hii unashindwa kumtofautisha Rais na Waziri wa Mambo ya Nje.

Ikiwa unawezesha Marais 2 wa Mataifa makubwa ambayo yana ambitions za kuchota raslimali(Ambition za kibeberu) huku mikataba ikiwa ya Siri na huthubutu kuweka wazi ili watanzania wajue kama tumenufaika ama la,does it make you a vibrant leader? Huo ni udhaifu

Hatuwezi kujivunia kutembelewa na Mabeberu ikiwa hatujui na wala hatushirikishwi katika mikataba iliyosainiwa.Hapo wananchi tutakua tumemsaidia Chifu Mangungo.

2:Economic Diplomacy:Hadi sasa sera zetu za mambo ya nje zimeshindwa kwenda kasi na trend ya Dunia.Kenya wamelichukulua hili kwa umakini.Wizara imeshindwa ku-intergrate wizara ya Fedha na uchumi,viwanda na Biashara,Kilimo,Mali asili na Utalii na wizara ya Uwezeshaji.Tumekomalia uzururaji wa Rais kama nguzo kuu ya sera za Mambo ya nje.Tunatekeleza Sera ya Kuomba na Kushukuru

Membe ni msomi mzuri kwenye International Relations na ana uwezo lakini Rais hawezi kukwepa lawama za kuingilia Foreign Affairs.

Katika mamia ya Ziara za Rais nje ya nchi isije kuonekana kuwa ndiyo utekelezaji wa Sera za Mambo ya nje.Hapana!

Kukiwa na Sera imara kila jambo linaenda vizuri badala ya kutegemea kipaji cha kutembea cha Rais.Sera ni institutional Mechanism.Taasisi imara na sio watu imara wa kukata mbuga halafu wanarejea na matunda mwitu yenye sumu na kuiangamiza familia pole pole kwa miaka mingi ijayo.

Ni nini sera yetu kwa Afrika?Nini sera yetu specific kwa EU?Ni nini sera yetu kwa Middle East?Ni nini Sera Yetu kwa SADC.Ni ipi sera yetu kwa Latin America?Ni utashi na kipaji cha Rais kuweza kuweka pozi la Picha na wakuu wa nchi hizo tu?Uimara wa Rais hapa Siuoni zaidi ya kipaji chake tu cha kutembea na kuimarisha Album

Actually Rais asingekua na njia nyingine ya kuficha udhaifu wake zaidi ya kutoa uhuru wa maoni ambao ni constitutional Right.Siyo Hisani.

Nimezikubali hizi comentS.
 
“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi
kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama
rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi
kwamba nchi ingekuwa katika machafuko
makubwa,” alibainisha Zitto.


Hivi ndugu Zitto wakati anatoa matamshi hayo sijui kama alifikiria tukio la kuogofya kama la mwanahabari David Mwangosi...
Sijui kama alifikiria vitisho wavipatavyo wale wote wanaothubutu kuweka bayana kadhia za Serikali hadharani...
Serikali ya sasa ni kama panya tu, inang'ata na kupuliza ili ionekane ni njema mbele ya wananchi wake...
Na sijui kama huwa anamsikiliza Nchimbi.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

“Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa,” alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

“Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu,” alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung’oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

“Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu,” alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

“Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa,” alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.

Nilianza kumchukia zzitto lakini mwishoni nikakuta sosi na jamboleo roho ikatulia uhhhhh
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

"Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

"Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa," alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

"Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu," alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung'oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

"Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu," alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

"Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa," alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.

Maajabu ya serikali ya Mhe Kikwete
1. WEZI WA MABILIONI YA FEDHA KUTOKA ACCOUNT YA EPA WAOMBWA WARUDISHE FEDHA WALIYOKWAPUA KWA HIARI YAO. SIJASIKIA MPAKA LEO NANI ALIRUDISHA NANI ALIKATAA KURUDISHA NA AMBAYE HAKURUDISHA ALICHUKULIWA HATUA GANI..? Hosea alipotaka kuchukua hatua akambiwa achaa.. Mtaani kwetu ukiiba suruali tuu hukumu yako ni kifo chaa moto wa petrol na tairi kiunoni....
Matokeo yake rushwa imeota mizizi na kwenye taasisi kama polisi ambayo ndio mkono wa kuwakamata na kufikisha mbele ya sheria wahalifu umekuwa ndio mkono mkuu wa kupokelea rushwa. TOOO BAD
2. Ni kipindi cha kikwete ambapo wanafunzi walioandamana ili wapate haki yao ya kusoma au flied walipigwa mabomu na virungu kama magaidi. Hili moja kati ya ajabu
3. Wafanyakazi waliokuwa wanadai ongezeko la mishahara kukidhi ugumu wa maisha waliitwa mbayu wayu.. Sijui maana yake ni nini? Ila hili nalo ni ajabu
4. Mauaji ya viongozi na wanaharakati wa kijamii. Mtu kapigwa kangolewa meno, macho utumbo. Haya yote ni makosa ya jinai illa kwa sababu walikuwa against kikwete wote kesi zao hazina mbele wala nyuma. ni sawa na kesi ya mbwa aliyegongwa na gari.. HILII NALO NI AJABU JINGINE
5. vURUGU ZA KIDINI. kukiri kwa Profesa lipumba kushirikia na mkuu kueneza propaganda za udini. Hili nalo ni ajabu jingine.
6. Ni rais ambaye amesafiri sana katika historia ya tanzania. Mpaka sasa katumia zaidi ya mwaka mzima nje ya nchi kwa gharama za walipa kodi. HILI NALO NI AJABU JINGINE. NDIO MAANA ANAJULIKANA MNO HUKO NJE KWA SABABU NDIO ANAKOISHI MUDA MREFU. SITASHANGAA SIKU OBAMA AKISEMA KIKWETE NI FAMILY FRIEND NA JIRANI YAKE KULE MAREKANI. MAANA HUO MUDA WOTE ALIOKAA NJE YA ANAKIDHI VIGEZO VYA BAADHI YA NCHI VYA KUPATA URAIA.
7. Ni katika kipindi chake kama mwenyekiti wa chama ambapo ukiwa mahiri wa matusi na bingwa wa kutunga propaganda za kuua upinzani unapandishwa cheo na unakuwa right hand man. So tusishangae hawa vijani walivyohama kwenye misingi ya CCM na kuwa mapingwa wa kuimba na kulink kila tatizo linaloikumba serikali ya tanzania na chadema. Lolote baya litakalotokea nchii mkuu hataki kusikia habari yoyote kama haitigusa chadema. Uchumi kujumba ni vurugu za chadema, mtwara kudai wasisahauliwe chadema hao, wanafunzi kufeli chadema ipo hapo.. Kiufupi ni kipindi ambacho rais ana washauri ambao wanamshauri kile anachotaka kusikia.


YAPO MENGIII SANA YA MTUKUFU RAIS WETUU.. MI NINACHOKUOMBEA UMALIZE KWA AMANI BROO, KWA KIZAZI HIKI CHA SASA KAZI NI NGUMU MNO KWAKO, NA HONGERA KWA PALE ULIPOFIKIA.


NI KWELI RAIS WETU KIKWETE NI MTU WA MAAJABU MNO.
 
Zito huwa ni kigeugeu siku zote, Rais kama waziri wa mambo ya nje kila kukicha safarini hata hoa jamaa wa usalama nao sijui huwa wanafanya kazi gani labda kwasababu hakuna kikundi wala mtu anayetishia uhai wake kama marais wengine kama Obama.
 
duh,huyu zito ni ndumila kuwili,tatizo naye anasaka madaraka kwa pande zote mbili,leo pamoja na elimu yake anamsifia rais kwa ujio wa rais wa china na marekani?halafu naye anasema anataka kulitumikia taifa,kiukweri nji ya zito inaonekana ileeeeeeeeeeeeeee nyeupe.
 
Mboe kamsifia JK ,Selasini kamsifia JK,Sasa Zitto akifanya inakuwa nangwa???au kwasababu hatoki kanda yenu!!!
 
Hekima za Kikwete zitaanza kuthaminiwa akitoka madarakani.
Ni kweli kabisa mkuu, siku zote aliyeko madarakani huwa hasifiwi. Ni mpaka atoke, aje kichaa ambaye atawapelekesha watu ndo hekima, busara na umakini wake huy bwn utakapokumbukwa. Ni kama mtu akishakuwa marehemu ndo utaona anapambwa kwa sifa kibao na ambazo hata hakuwa nazo
 
Back
Top Bottom