Nikizifikiria mateso vifo ,mateso waliyofanyiwa wananchi wa Zanzibar hususan Pemba,ukimuangalia Jusa wamempa kilema,ukimtazama yule mzee wa Histroria wamempoteza na mauaji kibao katika uchaguzi uliopita,msifikiri dua zao zimebuma,Dua za aliedhulumiwa hazirudi zinajibiwa tu,
Haya sijui tuseme sasa ni mateso kwa wahusika au kwa nchi nzima,CCM inabidi mtubu ,mnaona kama mnapuyanga kwa raha zenu,kumbukeni tu adhabu ya Mwenyezi Mungu ina rangi nyingi.
Husein Mwinyi itasha mkutano Unguja na Pemba kwa siku mbali mbali uwaombe radhi WaZanzibar na uwaombe msamaha wa dhati kabisa.kweli Maalim Seif ameridhia makubaliano na kutaka umoja,ila dua zilikwisha ombwa ,hivyo wahi kabla hujachelewa kuwaomba waZanzibar au hata humo misikitini unamopita pita,watu bado wanamajonzi makuu,wanacheka wanafurahi lakini moyoni mawazo huwajia na kusononeka.
Usione shida watakufahamu Waombe radhi WaZanzibari ,umeuona mapokezi ya Msiba wa Maalim Seif, WaZanzibari karibia wote walijawa na majonzi makubwa sana sana,sio wa misikitini wala wa makanisani. Kwa maana hio CCM Zanzibar haikuwepo na haitakuwepo. Mkabili Mwenyezi Mungu umueleze unataka kuwaomba radhi waZzanzibar ,uzidi kubarikiwa.