Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

Pia tumeambiwa nchi imeshindwa kujiendesha mpaka tung'ang'anie kujua alipo mtawala kama vile kuna jambo limekwama?
Hawa wanaumbuka....! Walishawajaza wafuasi wao kuwa ooh! nchi inaendeshwa kwa 'one man show' mara nini sijui! Sasa, uongo wao ndiyo unawatesa, wala hawana lolote zaidi.
 
So contradictory!

Zitto unasema Viongozi wa juu wako kimya, wakati huo huo unasem PM ametoa kauli, pia VP ametoa kauli. Sasa hapo issue ni ukimya wa viongozi, au huwaamini?

Pia unataka serikali itoe maelezo. Nani tena atoe maelezo ikiwa Mkuu wa shughuli za serikali ameshatoa kauli?

Usizunguke mbuyu, issue uitakayo ni rais kujitokeza hadharani.
Tokea waziri mkuu atoe tamko sasa ni siku kadhaa zimepita
 
Waache wafiche tu atakapokufa ndo watanyosha maelezo vizuri.Biblia inasema Mwovu akifa watu hupiga kelele.
Awamu ya tano wamesha zowea kuvunja katiba. Hii nchi imekuwa kama danguro kule Buzaa. Yaani kila kiongozi analo taka kuongea ndilo hilo ataongea. There is no rule of law.
 
Kwa hiyo kuna tetesi kuna "watu" kwa kofia ya mamlaka ya Rais washaanza kwapua hazina za nchi huko BOT!!!

Nafikiri kila kitu kiko documented, hata hizi tetesi zikiwa kweli watasakwa tu, na ikiwa kweli Mzee wetu mpendwa ni mgonjwa basi siku akirejea ofisini watazitapika.

Magenge kwa sasa ktk Tanzania yetu hayafugiki, haijalishi ni nani na kwa uhusiano gani!
 
Zito bwana, unataka kuiingiza mkenge serikali iseme anaumwa probably Korona then mje na dhihaka zenu.!
Binadamu aisee ukimsikiliza utadhan Anakusud jema kumbe anakutegea tu uingie mtegon mwake.!
 
Tena anafaida ya kuongea na Makamu wa kwanza wa Rais, au hata yeye hajui alipo mwenzake?
Makamu wakwanza wa rais Zanzibar majukumu yake nikushauri rais wa zanzibar tu.hanakazi nyingine vilevile wanaweza kumbania kumpa taarifa
 
Zito bwana, unataka kuiingiza mkenge serikali iseme anaumwa probably Korona then mje na dhihaka zenu.!
Binadamu aisee ukimsikiliza utadhan Anakusud jema kumbe anakutegea tu uingie mtegon mwake.!
Kazi ya upinzani ni kuikosoa Serikali saa 24 kila siku ndiyo maana hawaachi chochote kiwe kikubwa kidogo wao wanapita navyo vyote
 
Zitto ana haki ya kuhoji...tetesi zikiwapo ni vema kutatuliwa. Serikali imekuwa ikitoa matamko kukanusha tetesi na taarifa za uongo, hivyo andiko la Zitto ni njia mojawapo ya kuclear tetesi
 
-Afya ya Rais, kwa umuhimu wake, ni jambo lililowekewa utaratibu wa kushughulika nalo inapotetereka. Tunatambua pasi na shaka kwamba Rais anaumwa, tunashangazwa na ukimya unaoendelea kutamalaki katika suala hili. Ni kwa kiasi gani ugonjwa wa Rais unasababisha ashindwe kutekeleza majukumu yake ni suala lililo katika utaratibu wazi wa kikatiba.
 
Zitto na Lissu mmewaelimisha wa TZ na serikali vya kutosha. Ila ninawasiwasi kuwa mnapigia mbuzi gitaa.
 
Kwa kutokujua nafasi yetu kama "RAIA" wa taifa hili, viongozi wamechagua kutufanya watakavyo. Hiyo ndiyo faida ya ujinga. Tungelijua nafasi yetu, suala la wahusika kutueleza aliko Rais lisingekuwa hisani, bali wajibu.

Bahati mbaya sana, wengi wetu tumempa Rais hadhi ya kuwa "naibu mungu" kiasi kwamba tunaona kuwa kuhoji chochote kuhusu hali yake na vitendo vyake ni sawa na dhambi ipasayo mauti.

INASIKITISHA SANA.
Tudai katiba mpya inayokataza mambo ya hovyo ikiwemo Usiri usio na tija kwa Taifa
 
Zitto bhana! Uambiwe na nani sasa hali ya Rais?

Waziri mkuu kasema yuko fiti
Makamu Rais kasema rais yuko fiti

Unataka uambiwe na nani sasa?

Huu upumbavu kumbe hadi kwa wasomi upo?
Yuko wapi Raisi wetu?!
 
Sio wote waendao njia moja wamenia mamoja.

Hata ikiwa Zitto ana mambo yake, ila asipuuzwe. Huenda hayuko njia moja watu wenye nia ovu.

KATIBA KATIBA KATIBA ni MUHIMU sana
 
Nikizifikiria mateso vifo ,mateso waliyofanyiwa wananchi wa Zanzibar hususan Pemba,ukimuangalia Jusa wamempa kilema,ukimtazama yule mzee wa Histroria wamempoteza na mauaji kibao katika uchaguzi uliopita,msifikiri dua zao zimebuma,Dua za aliedhulumiwa hazirudi zinajibiwa tu,
Haya sijui tuseme sasa ni mateso kwa wahusika au kwa nchi nzima,CCM inabidi mtubu ,mnaona kama mnapuyanga kwa raha zenu,kumbukeni tu adhabu ya Mwenyezi Mungu ina rangi nyingi.
Husein Mwinyi itasha mkutano Unguja na Pemba kwa siku mbali mbali uwaombe radhi WaZanzibar na uwaombe msamaha wa dhati kabisa.kweli Maalim Seif ameridhia makubaliano na kutaka umoja,ila dua zilikwisha ombwa ,hivyo wahi kabla hujachelewa kuwaomba waZanzibar au hata humo misikitini unamopita pita,watu bado wanamajonzi makuu,wanacheka wanafurahi lakini moyoni mawazo huwajia na kusononeka.
Usione shida watakufahamu Waombe radhi WaZanzibari ,umeuona mapokezi ya Msiba wa Maalim Seif, WaZanzibari karibia wote walijawa na majonzi makubwa sana sana,sio wa misikitini wala wa makanisani. Kwa maana hio CCM Zanzibar haikuwepo na haitakuwepo. Mkabili Mwenyezi Mungu umueleze unataka kuwaomba radhi waZzanzibar ,uzidi kubarikiwa.
 
Kikwete akiwa raisi aliwahi kwenda Uk kufanyiwa upasuaji wa tezi dume na taarufatulikuwa tunapatiwa. mbona la huyu linakuwa gumu?
 
Back
Top Bottom