Hao "wananchi" anaowasemea ni wangapi, alikutana nao lini, na ni kweli kama walimpa hoja hizo alizozijadili, au ni ubunifu wake binafsi au unawakilisha foreign interests za watu wa nje wanaomtumia?
Kama dhamira zake/zao zinawatuma kuamini kama anaumwa, basi uwasilishaji wa hoja zake zinakiuka uungwana, utamaduni na malezi ya Watanzania. Nilitarajia aonyeshe angalau chembe ya huruma na simamzi, badala yake kinachojionyesha ni kibri, kukosa utu na kufurahia madhira ya wengine!
Utamaduni huu ni mgeni kwetu na wale tusiufumbate! Na kwa vile chama chake kina wabunge...awatumie kupata taarifa sahihi kwa kile anachokitilia shaka!
Kunyamaza pia ni uungwana!