Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

CCM acheni tabia yenu ya kuficha ficha ugonjwa - ficha yote hapa duniani ruksha ila siyo maradhi - maana maradhi yana tabia ya kuumbua.

Watanzania hawa wanataka kujua:-

1. Je Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yupo wapi?
2. Na ana hali gani kiafya?

Msipotuambia tunampango wa kwenda mahakamani kuiomba ili watanzania wote kwa pamoja tuanze kumsaka popote alipo - maana yeye ndiye tulimchagua awe kiongozi wetu sasa kwa nini mumfiche?
Kwani ni nani aliesema Rais anaumwa? Hao waliosema anaumwa ndo wanatakiwa wathibitishe kauli zao.
 
Kwani ni nani aliesema Rais anaumwa? Hao waliosema anaumwa ndo wanatakiwa wathibitishe kauli zao.
kwa hiyo unataka kuwaambia nini umma wa watanzania wenye shauku ya kujua Rais wao aliko kwa hizi wiki mbili na ushee with no seen.
 
Watanzania tunakomeshwa tulivyozoea umbeya sijapata ona.Ebu tufanye kazi kwanza,Kama anaumwa tutajua tu huwa mwenyewe hanaga siri atatoka uko atatusema kwa kejeli mpaka basi yaani mpaka mfurahi .Muda ni jawabu la kila kitu ,wakitaka kumfisha mpaka 2025 sawa wakitaka kumchomoa sawa wakitaka kumficha sawa.Sisi tuangalie mambo yetu jamani kama hawataki kusema.Halafu shida ya yake ni kuwa hapendi kutangaziwa udhaifu ndio maana kila kitu lazima asifiwe so sio rahisi wakatangaza kitu chochote ambacho sio afya au sifa kwake.Mumzoeee tu mpaka mitano mingine iishe na sasa tunataka tumwongezee mingine saba.CCM oyeee ,yaani nao wanateseka kupata udaku kama wewe na mimi
 
Msipotuambia tunampango wa kwenda mahakamani kuiomba ili watanzania wote kwa pamoja tuanze kumsaka popote alipo - maana yeye ndiye tulimchagua awe kiongozi wetu sasa kwa nini mumfiche?

????????
 
Zitto kinachotokea hivi sasa kwa Rais wa Jamuhuri yetu ni kama marudio tu ya kilichomtokea Diwani wa Muhambwe Tumaini Bigilimana viti maalumu kupitia chama chako ACT Wazalendo. Mbona hukuwahi kuieleza familia chanzo cha kifo chake cha ghafla, na kwa nini hamkueleza alilazwa hospitali gani na kwa ugonjwa gani?

Wewe na ndugu yako Shaibu mliishia kutoa gari la kuusafirisha mwili kutoka Dar es salaam hadi kwenye kituo chake kuzika na hamkutoa taarifa zozote kuhusu kilichomuua Tumaini? Je wanafamilia nao waungane na kupaaza sauti dhidi yako na chama chako juu ya mpendwa wao aliyefia mikono mwako?. Zitto acha unafiki na ubabaishaji hasa kwa wasiojitambua na uache kusambaza chuki zako kwa wengine, ugomvi wako na Serikali usiutafutie koti la kujifunika kwa
jina la watanzania, hivi kweli ukiwa kwenye Serikali hii kupitia upande wa visiwani huwezi kupata taarifa sahihi za hali ya mkuu wa nchi kupitia viongozi wakuu unaowajua hadi uje humu kuhamasisha unoko? Hovyo kabisa wewe, mnafiki mkubwa.
 
Hii ni nchi ya ajabu sana..........

Eti mtu kuhoji tu hali ya afya ya Rais wetu kwa hivi sasa, anafunguliwa mashitaka ya jinai!

Wakati Katika ya nchi ipo wazi kabisa, katika ibara ya 18, inasema kila mwananchi anapaswa kupewa taarifa muhimu zinazohusu nchi yake
Tofautisha kuhoji na kutoa taarifa ambazo hazina uthibitisho
 
Wahuni tumewapuuza tu!

Hata wale wahuni wenzenu upande ule tumewapuuza!

Eti unaanza na mimi!

Usinitolee mimi mipovu yako humu sikukutuma uwe shabiki wa lile jitu kule kwa amsterdam.
Mimi siyo mpuuzi! Wala muhuni!! Ukipuuza hekima adimu hiyo ni wewe!! Hainihusu!!

Sijawahi kutoa povu sababu mimi siyo sabuni. Wala fafa.
Naona umeamua kuongea lugha yenu inayo eleweka kuzimu tu! Sasa mie siyo wa kuzimu.umekosea rudia tena...

Mimi siyo shabiki km unavyo dhania mashabiki. bali ni mwanafalsafa!!
 
Watanzania tunakomeshwa tulivyozoea umbeya sijapata ona.Ebu tufanye kazi kwanza,Kama anaumwa tutajua tu huwa mwenyewe hanaga siri atatoka uko atatusema kwa kejeli mpaka basi yaani mpaka mfurahi .Muda ni jawabu la kila kitu ,wakitaka kumfisha mpaka 2025 sawa wakitaka kumchomoa sawa wakitaka kumficha sawa.Sisi tuangalie mambo yetu jamani kama hawataki kusema.Halafu shida ya yake ni kuwa hapendi kutangaziwa udhaifu ndio maana kila kitu lazima asifiwe so sio rahisi wakatangaza kitu chochote ambacho sio afya au sifa kwake.Mumzoeee tu mpaka mitano mingine iishe na sasa tunataka tumwongezee mingine saba.CCM oyeee ,yaani nao wanateseka kupata udaku kama wewe na mimi
Kwa hiyo tukae tu wakati mtu haonekani? tunawaaminije wapambe wake? kama wamemdhuru ama wamemficha kwa sababu zao binafsi - watanzania sisi tukae kimya tu - Haiwezekani, huyu ni Rais wetu lazima tujue where the about zake - katiba yetu pia inaturuhusu kufanya hivyo.
 
Yani atoe afficial statement sababu ya maneno ya wahuni wachache huko Twitter?

Ulivyo kiazi sasa, waziri mkuu kasema, makamu rais kasema ila hutaki kuwaamini badala yake unawaamini wahuni toka ubelgiji.

Ujinga ujinga t
Hivi wewe una akili kweli? sio muhimu nani alianzisha hili suali, ukweli ni kuwa Tanzania yote kwa sasa inajadili suali hili, Magufuli ni rais wa Tanzania, na kama kuna uvumi kama huu ni wajibu wake kuwaweka sawa wananchi wake. huko nyuma kushatokea uvumi mara nyingi tu na magufuli hakuchelewa kuzimavumizi zote. sasa leo ni kwa nini anashindwa kufanya the same?

tuje kwenye point yako kuwa waziri mkuu na makamu wa rais wamesema na kwa nini hatutaki kuamini, hayo ni maneno tu kama alivyosema lissu. Anaeweza kumaliza suali hili ni magufuli na kila akikizidi kukaa kimya ndio taifa linazidi kuamini yaliyopo mitaani juu ya alipo rais wao.

Badala ya kukaa na kuwaita watu wahuni na wajinga, hebu funuwa macho yako na tumia akili uliyojaaliwa. Unaona mnyama analia myao myao na unabisha kuwa sio paka?
1. Hajaonekana hadharani wiki ya nne sasa (yuko busy na kazi)
2. Hajaonekana kanisani jumapili nne sasa (si kawaida yake kukosa misa nne mfululuzi)
3. Kashindwa kuhudhuria virtual meeting ya EAC leaders (labda hana access na computer au wifi)
4. Watu wanamzushia kafa au anaumwa, lakini anashindwa kukana hili (.....................)
 
Uhuni ni kusema rais anaumwa wakati huna hakuna popote imetangazwa anaumwa!

Uhuni zaidi ni kulazimisha mamlaka ziseme rais anaumwa sababu kuna mhuni mmoja yuko ubelegiji kasema rais anaumwa!

Kamwe uhuni wa hivyo hauwezi kuabududiwa na sekikali inayojitambua
hkn mahali walipotangaza Rais anaumwa.
Alah! Nimetambua Kuuuuumbe tunajibishana na mjinga.
Maskini amejiikalia zake kwenye bench lumumba anasubiri mgawo hajui kinacho endelea!!!!
Ahaaaaa!!! Yaani walishakuona kitambo huna maana wanakunyima taarifa muhimu. Watu wako mwenyewe!!!! Si uhame???? Uache upambe wa kijinga huo!!! Wanakuona zoba!aaaahggaaa!!!
 
Zitto bhana! Uambiwe na nani sasa hali ya Rais?

Waziri mkuu kasema yuko fiti
Makamu Rais kasema rais yuko fiti

Unataka uambiwe na nani sasa?

Huu upumbavu kumbe hadi kwa wasomi upo?
Wajinga mko wengi sana kwahiyo wee ukishaambiwa basi imetosha hutaki hata kusumbua akili yako kujilidhisha

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Jamani.. watu wamemumisi Sana JPM wanashindwa tu kusema.

Yaani Makamu wa Rais na PM wamesema hadharani lakini bado watu hawataki maneno hadi wamuone.

JPM you are so missed. They miss you so much.

May the Lord God bless you abundantly.
 
Kama Waziri Mkuu kasema rais ni mzima, anachapa kazi ofisini, nani tena atamkaimu wakati yupo ofisini? Aidha, tamko lingine rasmi la afya ya rais la nini tena ikiwa Waziri Mkuu katamka kuwa ni mzima wa afya? Utaratibu au mtindo wa rais wa namna ya kufanya kazi au kuwasiliana na wananchi ni wake binafsi, haupo kikatiba. Na sasa tujue kuwa ana mitindo mingi!

Kama tulizoea mtindo wake wa kuipigia simu hadhira au kusema na umma akiwa kanisani, basi sasa kasema kupitia kwa Waziri Mkuu. Si lazima apige simu tumsikie au aseme neno akiwa kanisani. Na mtindo huo si wa kikatiba!

Kwahiyo huu nao ni uvumi ambao Zitto Kabwe asingepaswa kuuandika asilani. Tuendelee kuamini tamko rasmi la Waziri Mkuu akiwa mkoani Njombe, basi!

Nimalizie kwa kuvishauri vyama vya siasa vijikite katika kujenga hoja za kulijenga taifa, kuleta sera na mawazo mbadala ya kuwasaidia wananchi. Viache kasumba ya kila siku kushupalia kusikia sauti ya rais au kuona sura yake. 2025 haiko mbali!
 
Back
Top Bottom