Zitto Kabwe, Meles Zenawi Role Model Politician

Status
Not open for further replies.
Ritz baada ya kuishiwa hoja za kupost sasa umeanza kupiga ramli.
Sisi ni wacha Mungu hatuogopi wala kutishwa na ramli za waganga njaa wa ccm.

Mkuu Mwita umenikosha hizi ni Ramli kama za Sheikh Yahya.Amechemsha..Mkuu nasikia Jumamosi kuna M4C Mzambarauni na Mnyika ataunguruma...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco
Ritz ni Mtu ambaye anaeleweka hapa JF na wala hamtishi mti kwa Propaganda zake. Ritz hana tofauti na Martin Shigela. Ritz ni kijana asiyejiamini kwa kila anachokipost hapa ndio maana mara nyingi akipost hapa JF watu wakimjibu anamwita chama aje kumsaidi ila naona siku hizi chama amegundua kutetea Propaganda za Ritz ni kujishushia Thamani

Nilishamwalika katika Mnakasha Ulioanzishwa na Mwana CCM mwenzake Mchambuzi lakini Ritz hakutokea nikathibisha Maneno ya Mchambuzi kwamba CCM inakosa Mvuto kwa sababu ya Vijana kama akina Ritz

Nani alikuwambia Ritz ni CCM yaani nyie Pro-Chadema JF mtu yeyote hakiwa against Chadema basi ni CCM.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ritz,

nyie ndio mnazidi kumharibia Zitto. Kwanini wana CCM ndio mnaoongoza kumtetea? Wewe ni kada wa CCM sasa unataka Zitto awe rais kuliko unavyotaka kwa mgombea wa CCM? Hizi siasa mngewaachia wale wazee na nyie mjikite kusafisha chama chenu kiuzike kwa watanzania 2015 maana at that time hata Jeshi halitaweza kuwasaidia kubaki ktk Dola!!!

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html
 
Zenawi alisimama na chama chake cha EPRDF

Zitto husimama mwenyewe au kama m/kiti wa kamati ya Bunge

asilani kuuvaa unaibu katibu wa chama,achilia mbali ushiriki kwenye operesheni Sangara na M4C
 
Nani alikuwambia Ritz ni CCM yaani nyie Pro-Chadema JF mtu yeyote hakiwa against Chadema basi ni CCM.

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html
 
Last edited by a moderator:
Ikumbukwe mwaka 2009 Zitto alichukuwa fomu ya kugombea ya uenyekiti wa Chadema, akimpinga Mbowe ambaye tayari alikuwa amechukuwa fomu ya kugombea kipindi kingine cha pili hali iliyoleta kizazaa kikubwa ndani ya chama hicho, kabla ya wazee kuingilia kati na kushauri Zitto aondoe jina lake.

Wafuasi wa kambi ya Zitto safari hii wamesema wamejipanga kimkakati kuhakisha kwamba Zitto anagombea uenyekiti.

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html
 
kabla hajafikia kuwa Meles atakuwa ameshakimbizwa CDM.Washauri wake mmemshauri atafute urais kwenye facebook
na twitter
Zito Kagwe ni Mwanasiasa Mzuri lakini hana sifa ya kuwa Raisi.Si kila mtu ambaye ana mvuto kwa wananchi anafaa kuwa Rais.Angalia mheshimiwa BEN MKAPA nani alikuwa anamfahamu kwamba angekuwa Raisi.Mkapa pamoja na kutokuwa na washabiki na kutojulikana kabla ya kuchaguliwa Raisi, lakini baada ya kuchaguliwa Raisi alipiga kazi na alikuwa makini kwenye uongozi wake na wote mnaona matunda ya Mheshimiwa Ben Mkapa.Kila kinachoshabikiwa na wengi baadaye kinakuja kuwa na Kasoro na madhara huko mbeleni.Huu ni mtazamo wangu.
 
www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html
Hiyo thread sina uhakika kama ritz alishawahi kutoa comment yake. Na akama alitoa comment atakuwa hajaipitia muda mrefu sana hata kabla hajaanzisha huu uzi wake wa ramli.
 
Hiyo thread sina uhakika kama ritz alishawahi kutoa comment yake. Na akama alitoa comment atakuwa hajaipitia muda mrefu sana hata kabla hajaanzisha huu uzi wake wa ramli.

Mkuu wangu gongo za mchana ni mbaya sana,anadhani watanzania wa leo ni wajinga tena.Mkuu vipi maandalizi ya Jumamosi mzambarauni? PoliCCM wametoa kibali?
 
Mkuu Mwita umenikosha hizi ni Ramli kama za Sheikh Yahya.Amechemsha..Mkuu nasikia Jumamosi kuna M4C Mzambarauni na Mnyika ataunguruma...


Ni kweli mkuu Bavicha wanakinukisha jumamosi pale mzambarauni, bila shaka utatia timu!
 
Mkuu wangu gongo za mchana ni mbaya sana,anadhani watanzania wa leo ni wajinga tena.Mkuu vipi maandalizi ya Jumamosi mzambarauni? PoliCCM wametoa kibali?

Ha ha haa. Kizazi cha chang'aa hiki cha hovyo sana.
Sina uhakika sana kama policcm wameshajibu notice ya mkutano huo, ingawa natambua katibu wa jimbo alikuwa anashughulikia hiyo kitu. Nitakufahamisha baadae bado ninamtafuta mwenyekiti wa jimbo kupata uhakika.
 
www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html

Hii unaita kura ya maoni? Au ni mawazo ya wanachama wa JF? Is it open, reachable and fair? Unaweza kutumia vigezo vya kisayansi kuthibitisha matokeo yake? Kwa facts zote, hii si kura ya maoni. Sababu ni kwa ajili ya watu fulani wachache katika jamii, wenye malengo maalum kwa sababu maalum. Kifupi kura yako hii unayoita ya maoni, mtu mmoja mwenye kupaswa kuwa na kura moja, aweza kuwa na kura elfu moja kwa kutumia computer moja. All you need ni User names tofauti tofauti basi. So wapenzi wa ZZK kwa mfano wanaweza kuwa 100 tu kwenye forum lakini wakawaout number wapenzi wa Dr. WS, hata kama wako 200, simply user names.
 
Hii unaita kura ya maoni? Au ni mawazo ya wanachama wa JF? Is it open, reachable and fair? Unaweza kutumia vigezo vya kisayansi kuthibitisha matokeo yake? Kwa facts zote, hii si kura ya maoni. Sababu ni kwa ajili ya watu fulani wachache katika jamii, wenye malengo maalum kwa sababu maalum. Kifupi kura yako hii unayoita ya maoni, mtu mmoja mwenye kupaswa kuwa na kura moja, aweza kuwa na kura elfu moja kwa kutumia computer moja. All you need ni User names tofauti tofauti basi. So wapenzi wa ZZK kwa mfano wanaweza kuwa 100 tu kwenye forum lakini wakawaout number wapenzi wa Dr. WS, hata kama wako 200, simply user names.

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-29.html
 
Zitto ukiona mpaka unashabiikiwa na huyu mwenye sura chafu ritz ujue umekwisha na cdm tunakuli timing tu.......tamaa,sifa na uroho ndio vimekufikisha hapo..........

Mie sio mshabiki wa Zitto naelezea hali halisi tu mkuu.
 
Mkuu Mvaa Tai, the motive behind ni nia dhalimu iliyofichika ya mleta mada ili kutengeneza reaction fulani kwa mada yake!.

Hebu msome hapa!.

"Kwa mujibu watu wa karibu wa Zitto Kabwe", yupo tayari kuishi na kufa akiwa kwenye mapambano " Huu ni uzushi tuu, hakuna watu wowote wa karibu na ZZK, bali ameisoma makala ya ZZK kuhusu Zenawi na sasa anaitumia kumjengea chuki ZZK ili kuwatia hofu wana Chadema kuwa ZZK yuko tayari kupambana hadi kufa ili kuwa mgombea wa Chadema!.

"Wafuasi wa Zitto Kabwe wametoa onyo kwa Mbowe" Huu pia ni uzushi, hakuna mfuasi yoyote aliyetoa onyo lolote kwa yeyote!.

"mkakati wowote mchafu wa kutaka kumkwamisha Zitto kugombea urais" - Huu pia ni uzushi ili kuonyesha kuna mkakati wa kutaka kumkwamisha ZZK kugombea!

" ZZK ndiye anayekubalika" Hakuna survey yoyote iliofanyika kuthibitisha kuwa ZZK ndiye anayekubalika!

"wafuasi wa Zitto ambao wengi ni kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kigoma, Dar es Salaam, Morogoro, Kagera, Tanga, Mtwara, Lindi, Singida, Pwani, Ruvuma" Huu pia ni uzushi kwa lengo la kuwaaminisha watu kuwa ni kweli Chadema kina ukabila, hivyo kujenga dhana kuwa ukiondoa kanda ya Kaskazini, wafuasi wengine wote wa Chadema wa mikoa yote hiyo ni wafuasi wa ZZK!.

"mkakati wa Mbowe na Dr Slaa kutaka kumzuia ZZK" huu pia ni uzushi, hakuna mkakati wowote wa kiongozi yoyote wa Chadema kumzua mwanachama yoyote kugombea nafasi yoyote!.

"endapo watathubutu kumzuia basi watamuua kuwapigia kura wagombea wa vyama vingine lakini si Chadema" huu pia ni uzushi wa tisha toto ili kujenga hoja kuwa ushindi kwa Chadema 2015 ni kupitia kwa ZZK pekee, bila ZZK hakuna ushindi kwa Chadema!

"Zitto Kabwe inasemekana ndiye ambaye anaungwa mkono na karibu vijana wote wa nchi hii walioko ndani na nje ya Chadema, na hasa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini," huu pia ni uzushi wenye lengo la kumjengea chuki ZZK!.

Itakumbukwa mwaka 2010 wakati wa kampeni za ubunge jimboni kwake Zitto Kabwe aliwaambia wapiga kura wake wampe muhula wa mwisho mwaka 2015 hatagombea tena ubunge" Ni kweli ZZK aliomba mhula wa mwisho ila sio kweli aliaga ili akagombee urais bali alipanga kuingia kwenye a totally diferent venture away from politics!.

Lengo ni "ill motives"!.

Pasco.

NB: Pasco wa jf, sio mwanachama, mfuasi au mshabiki wa Chadema, bali kama mwanahabari, ninayo direct access kwa top leadership ya Chadema, kama ilivyo kwa CCM, CUF na vyama vingine vyote, na nimeiunga mkono presidential bid ya ZZK kupitia Chadema, kwa CCM naiunga mkono presidential bid ya EL, kwa CUF, Prof. Lipumba ndie mgombea urais wa kudumu wa CUF bara na Maalim kule Zanzibar ila naunga mkono bid ya Jussa kumpokea Maalim, 2020!.

Nimekuelewa!! Umezidi kuniweka katika mtazamo wangu wa siku zote dhidi ya Ritz.
 
Wanabodi,

Zitto Kabwe mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Chadema na Naibu Katibu Mkuu (Bara), Naibu Kiongozi Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

Kwa mujibu watu wa karibu wa Zitto Kabwe, yupo tayari kuishi na kufa akiwa kwenye mapambano kama ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi, ambaye ni kipenzi chake alianza mapambano na aliyekuwa Mfalme wa Ethiopia Haile Mariamu, akiwa na umri wa miaka 19 na hatimaye kufanikisha mapambano yake ya kuingia Ikulu akiwa na umri wa miaka 36.

Wafuasi wa Zitto Kabwe wametoa onyo kwa Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho kuwa mkakati wowote mchafu wa kutaka kumkwamisha Zitto kugombea urais wakati ndiye anayekubalika utakigharimu chama hicho kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 wafuasi wa Zitto ambao wengi ni kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kigoma, Dar es Salaam, Morogoro, Kagera, Tanga, Mtwara, Lindi, Singida, Pwani, Ruvuma, wanapinga mkakati wa Mbowe na Dr Slaa kutaka kumzuia endapo watathubutu kumzuia basi wataamua kuwapigia kura wagombea wa vyama vingine lakini si Chadema.

Zitto Kabwe inasemekana ndiye ambaye anaungwa mkono na karibu vijana wote wa nchi hii walioko ndani na nje ya Chadema, na hasa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, Itakumbukwa mwaka 2010 wakati wa kampeni za ubunge jimboni kwake Zitto Kabwe aliwaambia wapiga kura wake wampe muhula wa mwisho mwaka 2015 hatagombea tena ubunge bali atagombea urais ili aweze kuwatumikia Watanzania wote kwa ujumla wao.


Kumbe ni wafuasi wa Zitto!!! Sio wa Chadema!
 
Hii unaita kura ya maoni? Au ni mawazo ya wanachama wa JF? Is it open, reachable and fair? Unaweza kutumia vigezo vya kisayansi kuthibitisha matokeo yake? Kwa facts zote, hii si kura ya maoni. Sababu ni kwa ajili ya watu fulani wachache katika jamii, wenye malengo maalum kwa sababu maalum. Kifupi kura yako hii unayoita ya maoni, mtu mmoja mwenye kupaswa kuwa na kura moja, aweza kuwa na kura elfu moja kwa kutumia computer moja. All you need ni User names tofauti tofauti basi. So wapenzi wa ZZK kwa mfano wanaweza kuwa 100 tu kwenye forum lakini wakawaout number wapenzi wa Dr. WS, hata kama wako 200, simply user names.

Kwa tafsiri yako kura ya maoni lazima ishirikishe wananchi wote sio? hata uchaguzi mkuu hawashiriki watu wote itakuwa hii ya maoni?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom