Zitto apewa majukumu ya Kimataifa

Mheshimiwa Zitto,

kwanza hongera sana kwa kuteuliwa kwako. Hii ni dalili kwamba kazi zako kama mbunge zinathaminiwa na watu wengi hata nje ya nchi yetu.

Ila tu mimi pia nina ushauri, pamoja na kushiriki kwenye tume mbalimbali, weka juhudi zako kubwa kwenye kuendeleza jimbo lako la Kigoma. Mafanikio yako kama mbunge yatakuwa judged na juhudi zako za kuwakomboa wana jimbo lako kuliko kitu kingine chochote.

Ukianza kushiriki hizi tume na kamati mbalimbali ni rahisi mno kujisahau na kukuta jimbo linabaki pale pale.

Mafanikio mema katika shughuli zako.

Zitto Hongera.
Naungana na Mheshimiwa 'Mtanzania' kumtahadharisha Zitto, na kuongeza kwamba mara nyingi hizi posts za kimataifa huwa zinalevya! Tanzania ilivyo sasa inahitaji kwa asilimia mia nguvu za vijana kama Zitto wenye uchungu wa kweli na taifa hili.

Zitto, usije ukawa kama akina wengine ambao wamepata uwakilishi Bunge la Afrika Mashariki tu na hatuwasikii tena wakivalia njuga ama kujihusisha ipasavyo na masuala ya ndani ya nchi kama ilivyokuwa huko nyuma.
 
Mheshimiwa Zitto, hongera.

Ukienda kwenye mikutano yenu huko Ubelgiji nahakika kazi ya kuiwakilisha na kuiremba remba Tanzania utamwachia Balozi. In fact, keep your distance from the balozi's and them, wala nyumbani kwake usiuweke saaana, much less kulala. Ndio CCM hao hao. Nahakika utakuwa independent.
 
Majukumu haya ni BORA SANA kuliko yale ya JK ya ZIMBABWE...God Bless Hon Zitto na WE WANT ONE AFRIKA...Naomba uweke msisitizo kwenye maslahi ya AFRIKA.
Once again tuko pamoja.
 
Hureeeeeii Zitto

Hongera sana. Ama kweli Tanzania sasa tunapasua mawimbi kupitia CHADEMA.
 
Hongera zana kwa Mh. Zitto; ni kweli ana uwezo wa juu sana kushughulikia conflict prevention and human security. Je kuna mbunge mwingine zaidi ya Zitto kutoka Tanzania aliyeteuliwa kwenye hiyo body?
 
Hongera Zito kwa kazi mpya, nakutakia ufanisi bora na uzidi kuliuza jina la TANZANIA. BRAVO.
 
Zitto,
Hongera sana na kama walivyosema jamaa huko nyuma kuwa makini na tahadhali sana lugha za hawa jamaa.. Unaweza kuwa targeted kukubadilisha kwa kipande cha nyama..
Rememberr this - Mbwa mbwekaji sana mtupie kpande cha nyama! hii ndio michongo yao!
Ni heshima kubwa umepata lakini kuwa makini sana na tunakutakia kila la kheri..
Wanaweza kukubeba sana wakikuchoka tu watakutua mahala usipotegemea!
 
hongera sana mheshimiwa zitto.
ila nitalichukua suala la mwanakijiji kama alivyoliwakilisha hapa ...kwa faida yangu na wengine ....
mheshimiwa zitto hebu tuambie umesaidia vipi jimbo lako hadi sasa? ....
natanguliza shukurani
 
Zitto,

Hongera kwa kukaribiashwa katika kamati hii. Kwa kuangalia wajumbe wake ni watu mashuhuri sana. Nenda kama mwanafunzi mzuri, jifunze kazi na kuyatumia utakayojifunza kwa Taifa letu na hasa jimbo lako.

Ni nafasi ya pekee, uliyoipata, Umshukuru Mungu. Uwe mnyenyekevu asiye na kiburi au majivuno.

Tunakusubiri 2020!
 
Zitto,
Hongera kwa majukumu unayoongezewa. Tumia nafasi hizi nzuri kwa kujifunza zaidi wenzetu walikofikia kwenye demokrasia kuliko mengineyo.

Halafu fanya juu chini ujiunge na either Georgetown, Havard au Columbia University kabla ya kumaliza nngwe yako hii ili uanze shule baada tu ya 2010, whether ukishinda uchaguzi au la. Unahitaji angalau Masters na kuachana na general degree. Huko utapanua sana uelewa wa siasa na mengineyo. Congratulations and good lucky.
 
Congratulations Comrade Zitto.
"To whom much is given,much is expected from him." We as members of this forum and loyal citizens of our nation are expecting much from you. You have proved to be a champion of the poor and a fearless soldier a country has ever had.
 
Mhe Zitto, tunakutakia mafanikio mengi sana!! Kumbuka kuna waTz zaidi ya milioni 35 nyuma yako wakikuunga mkono na kukuombea dua utuwakilishe vyema!!
 
Hongera kwa kuonekana unaweza Brother, sisi pia tunaamini unaweza na tunakuombea Mola akushike mkono ili pia utumegee elimu uipatayo huko.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto, ameteuliwa kuungana na Mtandao wa Wabunge Duniani, wanaoshiriki kuzuia na kulinda usalama wa wananchi.

Saafi sana, hivi ile kazi aliyopewa na Kiongozi wa Germany wakati fulani iliisha au bado anaendelea nayo kwa wanaofahamu?
 
HONGERA KWA NAFASI HII ,POLE KWA KUONGEZEWA MAJUKUMU.MAANA KUTIMIZA YOTE KIKAMILI NA KIFANISI NI KAZI NA YOTE NI MUHIMU.

Takecare care brother and enjoy.
 
Back
Top Bottom