Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Huwa sishangai zitto kutoa maneno ya namna hiyo na mara aote nimekuwa niandika na kuwatzhadharisha sana watz kuhusu zitto.........ni rahisi sana kumfananisha zitto na akina augustine mrema........nitaendelea kusema kuanzia pale nilipokosa imani moja kwa moja na zitto ni pale alipokubali kununuliwa na rostam na lowasa ili atumie umaarufu wake kidogo kuwashawishi watz mitambo ile chakavu inunuliwe mpaka akatofautiana na viongozi wake na pia wana ccm wenye mapenzi mema na nchi hii.............tangu hapo ndipoi nilipoona jinsi kijana huyo anavyoweza kuwa msaliti hapo baadaye.................hakuna asuyeijua ccm walivyowanafiki kwa kuwanunu watu kwa bei rahisi na zitto yumo ndani japo yupo mguu mmoja ndani mwingine nje
 
ninachokumbuka wakati wa serikali ya mkapa tulukuwa tunashanga ,bei ya 1ltr ya maji ya kilamanjaro ilikuwa ni kubwa kuliko 1ltr ya petrol


Wala CCM na propaganda zao wasitughilibu na 'quotes' zao.

Serikali ya Mkapa siyo sawa na ya huyu 'mzee wa msuli'.

Kama amesifu CCM ya Mkapa anaweza kuwa na hoja.
 
Ni kweli Zitto amelewa kwa kuleweshwa na CCM walimfunga kinywa pale alipopewa seta ya Madini maana Tangu apewe pale hajaweza tena Kutapika na Kuharisha Uovu uliokuwa unafanywa na CCM, Jamani Kijana mwenzetu Kabwe kakabwa Tumtafutie dawa asije akawa kichaa, kwanza nataka nimrekebishe kwa kusema serikali ya CCM imeimarisha Uchumi wa Nchi si kweli na anatakiwa akemewe na apewe adhabu kali na kufukuzwa Chama Chadema kwani ingekuwa kama CCm imeimarisha uchumi watu walio wengi wangelala njaa na hata watu kukosa Ajira na wengine wana PhD, Degree, lakini Kazi hamna na Ingekuwa Uchumi wa nchi ni mzuri hata hakuna haja ya watu kama Dr slaa kuwafichua walikula na kujiwekea hela ya watanzania, au Ingekuwa si njaa kikwete angeenda kuomba omba kama mtu aliyefiwa na wazazi na aziyejiweza huo ndio uchumi imara? you Zito Think Before you speak and remember that you are not talking to the Blinds or Viziwi na Viwete wala Vipofu bali unaongea na watu tuojawa n ahuzuni na uchungu kwa ajili ya Tanzania Yenye kila kitu lakini kutokna na sera Mbovu ya CCm nchi imeoza kwa kufanywa dampo la vitu kutoka Ulaya na omba omba wanazidi wakati nchi ingeweza kujilisha na kutotukanwa na kunyimwa misaada na nchi za wazungu kwa kile wanachodai kuwa Watanzania ni Wachafu na hawajui kutumia misaada vizuri ndio maana wale wadhamini walisitisha kiwango cha misaada, lakini leo tukimpa kikwete tena atazidi kufanya starehe zake chavu na kuiacha nchi katika hali mbaya mbaya zaidi, lakini Ashukuriwe Mungu ametuletea Mkombozi wa Watanzania Dr W slaa ili apate kwenda Ikulu na kungoa Mizizi yote ya Uovu na Uaribifu na Kutupa njia ya kuingia tena katika uchumi zuri na wenye faida kwa watu wote si kama CCm walivyotufanya ni Bora tungekuwa tunatawaliwa na wazungu mpaka sasa kuliko walivyotawala CCM Mungu Uwapoteze wote Viongozi wa CCM wasziweze kuiba kura Bali wawe Vipofu na utupe kiongozi kama Dr slaa na Umlinde na Mabaya na Makombora ya CCM na Umpe DR Slaa Hekima na Ujuzi kama Ulivyomuongoza Musa ndivyo Utakavyomuongoza SLaa na watanzania . Amen
 
Zitto, natanguliza pole kwa yatakayofuata kwenye thread hii.

hahahaaaa umenichekesha sana ndugu yangu..unajua nilikuja sijacheka kwa muda mrefu thanks very much

Kuhusu zito mie naona ana haki ya kuzungumza anachokiamini zaidi kuliko kuzungumzia desturi na ngonjera za itikadi....
mix with yours
 
Lakini wanajamvi kujenga barabara au kuleta umeme ni wajibu wa serekali kwa sababu tunalipa kodi,hivi kwa nini tuwasifu kwa kutekeleza wajibu wao? Tatizo hapa ni je kwa kiasi gani serakali inawajibika ndio shida ya CCM maana serekali yoyote inayotoza kodi raia wake ni wajibu wake kuwapatia huduma kwa kiwango kinachoridhisha.
 
Hii stori imeandikwa na gazeti la CCM kifitna fitna...halafu imechakachuliwa.
 
Zitto atakuwa mnafiki nae,kama aliweza kuisifia serikali ya mkapa kasahau vipi kuiponda serikali ya JK kwa kuharibu uchumi ?
 
Jamani, tuwe waangalifu... hivi mnadhani zitto aliishia hapo kwenye hiyo hotuba??? Mbona tunakurupuka sana siku hizi

Ili kukamilisha hotuba na pia kuwa na mawazo wazi we must read the whole speech

Kumbukeni hata kwenye changamoto na hasa kwenye siasa huwa tunaanza na pongezi na baadae ndio tunaweka changamoto.... Lets not be like simba na yanga jamani, politics ni kwa faida ya watanzania na si chadema, kafu au ccm

msimamo mkali haujawahi kuleta maendeleo popote pale

Was it really necessary to issue such a statement? Wapo akina sie ambao hatutaweza kuchambua mambo kama alivyodhamiria yeye na kuchukulia kwamba hafai kuwa kwenye kundi la 'wapinzani' kwa kuwa ameakifagilia chama tawala! Hivi kweli hiyo ni kazi yake Zitto kufagilia chama tawala katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ambapo watu wanapigana kufa na kupona ili kukiondoa madarakani chama hiki kikongwe kilichopoteza dira na chenye kutoa ahadi za uongo za ghilba kwa wananchi?

Nadhani Zitto atakuwa ameelemewa kwenye jimbo lake ndio maana anajaribu kujiweka sawa mbele ya nyuso za wana CCM ili labda wamkumbuke kwenye ballot box!
 
al sahaf-makamba anajua hii mbinu ya kusifiana. kwa lugha nyingine kamkata kilimilimi dr. bilal
 
Mimi nilisha waambia hawa chadema ni nguvu za soda!! Mmoja baada ya mwingine atajitokeza na kuonyesha unafiki walionao kudai wana uchungu na nchi hii kuliko wa tz wengine!!! Sasa yako wapi? Ikiwa mtu kama zito kashaongea hayo aliyosema sasa anangoja nini si atangaze rasmi amejiunga na ccm!! Asione haya kwani wako wengi waliomtangulia kama vile masumbuko lamwai, na wengine wengi tu, hata mabere marando kuna wakati alikuwa anabebwa na ccm kama mtakumbuka wakati ule alipopigiwa kura nyingi toka ccm na akawa mbunge wa afrika mashariki! Tangu hapo marando alikuwa hathubutu kuinyoshea kidole ccm!!

Jamani ati leo marando ndio mpiga debe mkubwa wa chadema!! Hawa watu wanataka kutufanya sisi wa tz kuwa ni majuha siyo!!! Sasa tutawaamini vipi leo tukiwapa madaraka hawa si ndio wataiuza nchi yote pamoja na sisi tuliomo ndani?? Ikiwa watu wenyewe ndio hawa wenye kutangatanga utafikiri kuku anaetaka kutaga mayai!! Kweli wataweza kuongoza taifa lenye watu zaidi ya milioni 40?

Mtu kama padri wilberd slaa akiwa ni mbunge ananyakuwa mke wa mtu na kesi yake iko mahakamani, jee, akipewa urais si ndio wake zetu watakuwa hatarini kuchukuliwa kila mara atakapotembelea mikoani kwa shughuli za kiserikali?? Wa tz tuacheni ushabiki wenye hamasa tutajuta baadae! Mimi nashauri tufikie uamuzi wa kuirudisha ccm madarakani kwani hawa ndio tunaowafahamu vizuri na kikwete hana madaraka yoyote ya kuwashuulikia mafisadi kwani mahakama ndiyo yenye jukumu la kuendesha kesi hivyo tuwe na subira kesi si ziko mahakamani? Mbona tuna pupa? Hata hussein obama amemsifia kikwete kuwa ni kiongozi bora anaeongoza kwa kufuata utawala wa sheria!! Sasa si nyie wana chadema mumemuita dr.slaa kuwa ni obama wa tz ktk mkutano wake wa juzi huko moshi!! Sasa mbona huyo obama mwenyewe anamsifia kikwete?? Sasa obama wa tz ni slaa au ni kikwete???
 
Zitto ameshanunuliwa huyu, ukifuatilia kauli zake toka kipindi kile ambacho mama yake mzazi pia alihusika katika kale ka "mgogoro" Chadema na kuwa anabwabwaja hovyo utaanza kupata picha Zitto amekuwa ni mtu wa namna gani. Nafahamu kwamba ana mashabiki wake wengi tu humu ndani na mimi nilikuwa mmoja wao ila kijana wameshamharibu huyu kwa sasa. Mfano mwingine halisia ni siku ile alivyozindua kampeni zake jimboni kwake na moja kwa moja kuanza kuongelea habari ya yeye kugombea urais 2015 bila hata ya kuulizwa.

JF bana, yaani mtu akipost tu kitu hapa tunakurupuka kuchangia hata kama akisema source ni wapi. Kuna mwenye gazeti hilo la uhuru aweke scnanned copy hapa? Hiyo habari imeandikwa na aliyepost na sio kuwa ameichukua na akacopy kutoka kwenye gazeti moja kwa moja. Kabla sijaweza kufikia hatua ya kusema kuwa zitto keshanunuliwa, kwanza ningependa kuiona hiyo nakala ili nijue maudhui yote ya hiyo habari

Pili, kama Zito amenunuliwa, basi nadhani price atakayopewa ni ndogo sana, because market yake na umuhimu wake viko at the bottom right now. Chadema kwa sasa ipo beyond positiion iliyokuwepo NCCR, wakati ule. Kuna kipindi Zito angeweza kuidamage chadema, kipindi amechukua fomu ya kuomba Uenyekiti, wazee wa chadema kwa busara zao wakamsimamisha, that was a very material time
This time Chadema hawana muda wa ugomvi, wana kazi moja tu kuichukua nchi, hata Zito leo atoke Chadema na kuingia CCM hatakuwa na damage yeyote kwa sababu no body will care for that, sana sana watamtukana na kuendelea mbele, moto unawaka vibaya sana wajamani, tone moja la Zitto haliwezi kuzima huu moto.

CCM wenyewe wamenywea jinsi public ilivyorespond kuhusu suala la mjinga yule Mshumbushu, ndio maana hawaliongelei tena, kwa kuwa liliwadamage wao kuliko lilivyo idamage chadema. So pay no attention na huu ujinga wa sijui zito kafanyaje, yeye ana kibarua cha kutetea jimbo lake kule Kigoma. akishindwa, bei yake itazidi kuporomoka, so he is very carefully na anachokiongea. Bottom line siamini hii habari kama kweli imetolewa kwenye gazeti kama ilivyoandikwa!!!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom