Hii makala imenikumbusha mbali sana. Enzi hizo za mijadala; kupingana kwa hoja. Siku hizi vijana wanaogopa mijadala. Wanabebeshwa ya kuongea. They are socialised to defend people rather than principles! Nakumbuka baada ya maelezo yangu kijana wa swapo alikuwa mpole sana!
Mkubwa enzi za mijadala ya tija kulikuwa na viongozi wa ukweli sasa wale wote waliokuwa wanaifanya mijadala iwe huru na hawakuwa wanaogopa ukweli tayari wamejawa tamaa na wamehongwa na mafisadi. Tayari wale walioaminika wamekuwa wabomoaji. Tusilaumu hadhira tulaumu tuliowakweza mpaka juu wanatusaliti. Leo tumetushiwa kushughulikiwa na panya wa kwetu, viongozi wetu wanaacha taaluma wanakuwa wachawi kweli kuna kitu hapa.
Ni vigumu sana TZ yetu hii kumtofautisha msomi na asiye nashule kwani kunapokuja swala la data, ukweli, analysis watu wanaegemea kwenye maslahi. Vijana makini walikataa Richmond, Dowans ilipopenyezwa rupia wakaipigia makofi. Mhando alituhumiwa kwa rushwa mara akatetewa na wengi tunaoita wasafi na watetezi wa wanyone. Katiba inapigiwa debe ili mmoja awe raisi kwa kuuza vipengele vyote vya muhimu ndani ya mabadiliko ya katiba.
Sababu ya kutetea mali asili zetu zimekuwa binafsi. Ninyi viongozi ndio mnatubadilishia mada na wananchi wanaanza kutokuwaamini na kupoteza kabisa maana ya mijadala inayojenga.
Kiongozi makini akikimbia mstari uliomjenga anatupwa nje bila kujali mtaitaje mada za wananchi. Mandelea alipewa ahadi zote za maisha ya kifahari na makaburu akakataa, martin luther king, nk ndio maana wananchi walikuwa nyuma yao wakijenga hoja ambazo zilileta usawa na haki.
Leo niambie nani anaweza kuwa mfano, hatuaminiani kwani bakuli la fedha likiwapitia wengi wanageuka na kutuachia vita sisi wasakanyoka mtaani.
Kauli tata zinazotolewa na viongozi wa sasa na ushiriki haramu kwenye vita hii ambayo waathirika ni sisi tusio wabunge, madiwani, wala viongozi wa aina yeyote zaidi ya kusapoti yeyote mwenye nia njema ya kututoa msituni huku kwenye umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uhujumu, kuteswa na kuonea na sheria kama tupo ugenini hatuwezi kuonekana tuna tija.
Tunataka kuanzia sasa ninyi ambao tumewaamini muache kutulalamikia msafisehe closet zenu mtoke wasafi na kauli moja. Mkiona hamwezi kuelewana ndani ya uongozi wa juu anayeona haiwezekani ajiuzulu badala ya kuwa na makundi kama masalia, pm7 nk. Ni heshima sana kuona huwezi kufanya na kikosi kilichopo na kuachia ngazi ukasubiria kikosi kingine kuliko kuendelea kuwa mnafiki huku ukitamani kuchoma nyumba wote hata wasio na hatia waangue.
Vijana wa sasa hasa wa nchini kwetu (sio wote) wanakosa mwelekeo hawajui wanataka nini wala wanataka kwenda wapi, ndio maana ni rahisi sana kujizika kwa kibaba cha mchele.
DR ukiona mijadala imekuwa mikali na ukiisoma kwa undani utaona wazi vijana humu JF na site zote mtaani wamekatiswa sana tamaa na ushiriki wa vijana walio waamini kutaka kuiuwa CDM kwa tamaa zao au ugomvi wao binafsi au kununuliwa kwa vipande vya fedha. Waambie hao ndio sababu ya kuharibu mijadala.
Mijadala hii imekuwa kioo cha jamii, elimu, na makuzi mazuri sana kwa viongozi wa aina zote. Tumeshuhudia kashfa za aina zote kutoka kwenye nyumba za ibada, serikli, bungeni, jamii nk. Sasa kashfa zimneamia kwetu ndani ya nyumba tusiziogope tuonyeshe tupo tofauti na wao. Makundi hayajawahi kuservive popote duniani. Lazima mkubali kumeza mkaa wa moto watoswe majini wote watakaobainika kutvuruga sisi walalahoi waamka hoi.
Kujadili watu imeanzishwa na vinara wa siasa kwasababu zao binafsi za kutaka madaraka. Nimewasikia wengi, na nami ninaushahidi mkubwa kwa hilo, ni tabia ya tamaa na kiongozi kushindwa kabisa kufikiri. kwa nini usimshende mwenzekao kwa utendaji unataka kushindana kwamajungu na tuhuma. leo hii hapa JF viongozi wengi wengi wana ID zaidi ya tatu. Za kujisafisha, kuwaponda wenzao, kuanzisha majungu, na kuvuruga mijadala ili kulinda statue quo.
Vita vya madaraka vinaitafuna sana TZ na vyama vya siasa.
Ni maneno ya
Chief Mkwawa wa Kalenga. Kwa haki tutashinda