Zitto amburuza Kilewo polisi

Zitto amburuza Kilewo polisi

Status
Not open for further replies.
Mbakaji Kapuya hao hao polisi wanamtetea na kumlinda
 
Chadema ina mwakili wengi kuliko wanachama

Mambo ya Chadema yanakuhusu nini??? Ukiulizwa Pili pili usiyoila inakuwashia nini??, Mmeshaumia hakuna jipya tena, sisi tunaendelea kuwafundisha na kuwapa elimu watanzania ni jinsi gani ya kukabiliana na Mamluki kama nyinyi na wote wenye nia ovu kwa mabadiliko.

Kama wewe ni mzalendo kwani unang'angania nchi za watu, au nyiye ndiyo vipandikizi.
 
Nawajua hawa:
  1. Tundu Lissu
  2. Prof. Abdallah Safari
  3. Mabere Nyaucho Marando
  4. Nyaronyo Mwita Kicheere
  5. ....
  6. ......
Kuna jembe lingine Edson Mbogoro, huyu aliikamata kesi ya Mnyika pale jimbo la Ubungo
 
Mambo ya Chadema yanakuhusu nini??? Ukiulizwa Pili pili usiyoila inakuwashia nini??, Mmeshaumia hakuna jipya tena, sisi tunaendelea kuwafundisha na kuwapa elimu watanzania ni jinsi gani ya kukabiliana na Mamluki kama nyinyi na wote wenye nia ovu kwa mabadiliko.

Kama wewe ni mzalendo kwani unang'angania nchi za watu, au nyiye ndiyo vipandikizi.

Mkiambiwa ukweli mnakuwa mbogo,punguza povu kwanza
 
Nchi ya Wakristo.....

Ukiisoma Historia ya Uislaam utakuta kuwa, Waislaam walipokuwa wakiteswa na ndugu zao walioupinga Uislaam hapo Makkah wakati alipoanza Mtume Muhammad SAW kuhubiri Uislaam, aliwaambia ili kuepuka mateso basi waende Habashi, na huko ilikuwa nchi ya Wakristo na Mfalme Mkristo. Tatizo ni nini?
 
hivi zito anataka kufanya madudu halafu watu wamwangalie tu, hizi ni enzi zingine. Yeye akitaka awe msafi
 
Mkiambiwa ukweli mnakuwa mbogo,punguza povu kwanza

Tulia wewe. haya maji marefu yeyote aliye na roho ya ubinafsi, usaliti na mwenye hofu asiye na ujasiri hawezi kuwa katika mstari wa mbele kwenye mapambano haya.

Ni bora ukafanye mambo yako ya kifamilia na siyo siasa maana huziwezi.
 
Naona unaandika nakuanza kutoa majibu mwenyewe duh kweli wewe wenge.unasadifu jina lako.

umeona jamaa yako Zitto anaonewa? Kazi nzuri sana, manaibu wawili wote washamleta 'abdala kichwa wazi' nawe ukawapa 'mwajuma binti maringo' kwa furahaaaaa!
 
umenena,halaf huyu jamaa ana damu ya kunguni sidhan kama kwenye hili atachomoka,maana inasemekana ushaidi upo

Zito Mbona mwoga hivyo ! alishindwa kumchana live kwenye Vikao Kama wao walivyofanya wakati wa kumvua vyeo Mbona wao hawakwenda polisi? Kushitakiana wenyewe kwa wenyewe hiyo na dalili ya Zito kumwogopa kileo ! Zito nenda kashauriane na Deus Malya kabla ya kuendelea na mashitaka
 
Kufuatia madai yaliyotolewa na Zitto Kabwe yakuwa ametishiwa kuuawa,Mapema leo Jeshi la polisi limemhoji Henry Kilewo kuhusiana na tishio hilo.Maelezo haya ni kwa mujibu wa fecebook wall ya Kilewo mwenyewe muda mfupi uliopita.

========== Aachiwa Huru =========

Jeshi la Polisi limemwachilia Katibu wa Chadema DSM Kamanda Henry Kilewo kwa kujidhamini mwenyewe tena bila ya Masharti yoyote.

Kilewo aliwasilimakao makuu ya jeshi hilo leo kuitikia wito.Alipofika alikuta anapaswa kuhojiwa kuhusiana na kumtishia maisha Naibu katibu mkuu wa Chadema aliyefukuzwa Zitto Kabwe.

Kulitokea mabishano makali ya zaidi ya saa moja na baada ya hapo alihojiwa kwa saa moja.

Inadaiwa Kilewo alilitaka jeshi hilo kushughulika na mambo ya msingi yanayowasumbua wananchi na kuachana na wanasiasa waliofilisika kisiasa na sasa wanatafuta pa kujishikiza.

Kamanda Kilewo anatetewa na Wakili Msomi Peter Kibatala ambaye ameteuliwa hivi karibuni na Kamati Kuu kuwa mkurugenzi wa sheria na haki za binadamu wa Chadema.
 
[h=5]Henry Kilewo[/h]57 minutes ago via Mobile


Ndiyo nimetoka kuhojiwa na jeshi la polisi mahojiano yaliyochukua takribani lisaa limoja na mabishano yaliyochukua lisaa limoja kabla ya kuanza maelezo.


Cha msingi ni kuwa mtu mmoja aitwaye zitto kabwe ametishiwa kuuwawa, lakini maelezo yangu kwa jeshi la polisi leo ni kuwa waangalie mambo ya msingi ya mnchi hii kuliko kukimbilia upuuzi wa wanasiasa uchwara waliyoporomoka kisiasa na sasa wanatafuta kicki ya kurudia.

Jeshi la polisi limeniachia kwa kujidhamini mwenyewe bila mashariti yeyote yale...

Ahsanteni na mungu awabariki... we shall overcome,never say never
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom