Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,506
Zitto Kabwe ambaye ni Kiongozi mkuu wa ACT Tanzania usiku huu amefanya mkutano na wahariri wakuu wa vyombo vya habari Tanzania.
Mkutano na wahariri umeenda sambamba na chakula cha jioni katika hoteli moja katikati ya jiji.
Zitto ametumia nafasi hiyo kuwaomba wahariri wamsaidie kuitangaza ACT Tanzania ili kiwe chama kikuu cha upinzani na kilete mapinduzi ya kweli katika siasa za Tanzania
Katika mkutano huo Zitto aakiwa amefuatana na Prof Mkumbo na Mwenyekiti wa chama, amesema ACT itawashangaza wengi kuanzia Julai mara baada ya bunge kuvunjwa kwani makumi ya wabunge wa sasa watahamia ACT toka CCM, Chadema na Cuf. Amesema ACT itasajili wabunge wenye majina kama ya Messi na Yaya Toure na wala haitasajili vidagaa kwa maana ya wabunge wasio na makali.
Akaongeza kuwa ACT inaweza kuwa na mgombea urais mwaka hui tena mgombea tishio hasaaa lakini watu wasubiri wakati utakapofika. Zitto na Mwenyekiti wake wameahidi kuanza ziara ya mikoa kumi wiki hii kukitangaza chama katika awamu ya kwanza.
Nitawapa taarifa nyingine baadae katika thread mpya ya jambo lisilo la kawaida lililojitokeza baadae katika mkutano huo na kuleta mgawanyiko mkubwa kwa wahariri kupitia Jukwaa lao la Wahariri
Mkutano na wahariri umeenda sambamba na chakula cha jioni katika hoteli moja katikati ya jiji.
Zitto ametumia nafasi hiyo kuwaomba wahariri wamsaidie kuitangaza ACT Tanzania ili kiwe chama kikuu cha upinzani na kilete mapinduzi ya kweli katika siasa za Tanzania
Katika mkutano huo Zitto aakiwa amefuatana na Prof Mkumbo na Mwenyekiti wa chama, amesema ACT itawashangaza wengi kuanzia Julai mara baada ya bunge kuvunjwa kwani makumi ya wabunge wa sasa watahamia ACT toka CCM, Chadema na Cuf. Amesema ACT itasajili wabunge wenye majina kama ya Messi na Yaya Toure na wala haitasajili vidagaa kwa maana ya wabunge wasio na makali.
Akaongeza kuwa ACT inaweza kuwa na mgombea urais mwaka hui tena mgombea tishio hasaaa lakini watu wasubiri wakati utakapofika. Zitto na Mwenyekiti wake wameahidi kuanza ziara ya mikoa kumi wiki hii kukitangaza chama katika awamu ya kwanza.
Nitawapa taarifa nyingine baadae katika thread mpya ya jambo lisilo la kawaida lililojitokeza baadae katika mkutano huo na kuleta mgawanyiko mkubwa kwa wahariri kupitia Jukwaa lao la Wahariri