Ndo nakwambia tatizo sio la uislamu bali tatizo ni la hao waislamu(mashekhe)lau wangeliweka mfumo wa kukemea kila baya basi hata vijana wangekulia wakijua kwamba nguruwe na zinaa zote ni dhambi.
Nimekuelewa unachosema mkuu na hiyo hali naiona lakini ninachotaka kukikataa ni labda mtu atuambie kwamba uislamu haukukataza zinaa siriazi kama nguruwe,ndo mana nasema makatazo ya uislamu juu ys zinaa ni makubwa sana ukisoma maandiko.mfano tu kuna hadithi ya mtume inasema
من زنى بامرأة متزوجة عذب في قبره بنصف عذاب هذه الأمة
"atakayezini na mke wa mtu,basi akifa ataadhibiwa katika kaburi lake nusu ya adhabu ya umma huu"
Umeona makatzo ya uislamu juu ya zinaa hayo mkuu?
Sasa hapo kinachobakia ni waislamu kuzipaza sauti zao kukemea maovu pasi na kulibagua hili na lilie,jambo unalosema ni kweli udhaifu huo upo lakini ni udhaifu wa waislamu namna walivyolelewa labda wamelelewa katika mfumo wa kuidogosha zinaa japo wanajua ni dhambi na kuikuza nguruwe japo nayo ni dhambi.
Nakumbuka kisa kimoja
Jamaa alizini zanzibar akapata mtoto wa nje ya ndoa,wazanzibar wakaanza kumsema yule bwana kwamba anazini na kupata mtoto muislamu mzima eee hivi na vileee,sasa hao waliokuwa wanasema ni waajiriwa na wanamikopo ya riba.
Mimi kwa vile najuana nao nikawaambia mbona nyie mnamikopo ya riba na hamsemwi na wala hamtengwi? Au riba nayo siyo dhambi katika uislamu dhambi iwe zinaa tuu?
Au umeshajihalalishia riba tayari zinaa ndo mnaona kosa?
Jamaa wakakosa majibu ya maana nikajua kwamba mazingira aliyokulia mtu yanachangia kwa kiasi kikubwa kuikuza dhambi fulani na kuiwacha dhambi fulani.
Kama zanzibar dhambi ya ulawiti haipigiwi kelele kwa nguvu zote,lakini angalia machangudoa wanavyotiwa ambushi? Liwati na uchangudoa upi ni uovu mkubwa?sina maana uchangudoa uachwe lakini ilikuwa hii liwati ndo ikemewee mwanzo huku uchangudoa nao ukikomeshwa.
Nimeandika kwa kirefu kidogo utanivumilia.
Mantiki yangu ni kwamba huo wa kushadidia nguruwe na kuidogosha zinaa ni udhaifu wa waislamu na wala sio udhaifu wa uislamu.
Sijui umenipata kidogo mkuu?
Hoja yangu ni kwamba.kwanini itumike nguvu kubwa kwenye nguruwe na sio zinaa?dhambi ya zinaa imeelezwa kwenye vitabu vya dini na adhabu zake zipo wazi na kwa ukubwa wa adhabu ya zinaa inatosha kabisa kutuonyesha kwamba zinaa ni kosa kubwa sana.swali langu ni je kwanini masheikh wetu hawatumii nguvu kubwa kwenye makazo ya zinaa kama ambavyo wanatumia kwenye nguruwe?Leo hii wewe uonekane kwamba ni mzinifu na Mimi nionekane mla nguruwe walahi Mimi nitaonekana sifai kwenye uislam na wewe utaonekana huna kosa.
Sent using
Jamii Forums mobile app