Zimbabwe: The turmoil, reconciliation, and the future!

Mukandara,

Yule mama ndiye aliyekuwa muandaaji wa mkutano ule kwa position yake kama secretary wa COMESA. Kwa hiyo alikuwa akiwalaki viongozi wote wa nchi za COMESA na kuwakaribisha ukumbini bila kujali uhasama wake nao. Kwa hiyo Mzee Mugabe akadhania kuwa "ameshapata" na kuanza kujitunisha kwa ajili ya photo opportunity.


Mzee yule ni hodari sana wa kusnatch photo op.
 
Kichuguu,

Naomba kufahamishwa zaidi swala hili maanake naanza kuchemsha!
Kwanza nimejaribu kutazama wanachama wa Comesa, Tanzania hatumo! hilo moja pili nimetazama secretary General wa Comesa inasema ni Erastus Mwencha ambaye ni Mzambia...Sasa nashindwa kuelewa nafasi ya Tibaijuka ktk Comesa na hapo Nairobi, Kenya.
Habari mbaya kuliko zote zinasema kwamba first lady wote wa nchi husika walikuwa na mkutano wao tarehe 23... Mugabe naona hakuingia na mkewe ila?!!!!!!!!

Tazama hapa:-
http://www.comesasummit.go.ke/docs/protocol.pdf

Na hapa http://www.comesasummit.go.ke/
 

Mkandara uko sahihi kabisa. Maelezo yangu ya awali yalikuwa yametokana na habari zilizokuwa kwenye lile gazeti la New Zimbabwe ambalo ni dhahiri lilipoti picha hizi vibaya. Ukweli ni kuwa mkutano ule wa COMESA ulifanyika kwenye ofisi za Makao Makuu ya UN pale Nairobi, ndiyo maana yule mama alikuwa akiwakaribisha wajumbe wa mkutano ule pale, siyo kuwa yeye ni secretary general wa COMESA.
 
Mimi nina njia ya mkato lakini sina uhakika itaibua changamoto gani nyingine endapo itatekelezwa. Kufanya yale ambayo tuna wataalamu wa kutosha kutekeleza....ondoa udhia....nadhani naeleweka.

Tanzanianjema

Kaka Mkandara bado sijapata njia nyingine murua zaidi ya hii ingawa bado najitahidi kufikiria

Tanzanianjema
 

Ama hii kama sio tooooooo late

Tanzanianjema
 
Tanzanianjema

Kwa taarifa yako tu huyu bwana amekwisha jijengea hekalu kule Malasyia ndiko atakakokimbilia kama akiwa hai, lets wait and see.
 
SA unions warn of 'dictatorship'


http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/5016024.stm

Mbeki aliwahi kusema hakuna AIDS (Ukimwi) mara alipoingia madarakani sasa anakuja huyu rapist - Kweli Afrika tuna kazi na ndio imeanza.
 
South Africa's unions want the government to ease poverty




http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/6690953.stm

No comment at this time.
 
Tanzanianjema,

Matatizo ya Zimbabwe hayaishii kwa Mugabe! nitarudia kuwa yeyote atakayeshika baada yake ni kuendeleza yale Mzee huyu atakuwa ameyaacha!.. ZANU-PF ni CCM ya Zimbabwe na kibaya zaidi hawana mtandao ndani uliogawanyika.
Hizi ndizo athari za vyama vilivyotafuta uhuru na kujijengea ngao kubwa ambayo leo hii wananchi wanashindwa kuvunja...
Na kibaya zaidi ni kwamba vyama vya upinzani vimeshindwa kujiendesha bila misaada toka nje jambo ambalo vyama hivi tawala wametumia kama mbinu ya kuwanyooshea kidole wapinzani!...Na kweli uhusiano wa vyama vyetu vya ndani na mataifa makubwa siku zote huna kuna walakini. Hatufahamu ktk urafiki huo wa misaada wameahidiana vitu gani!...

Hii imebaki puzzle kwa wananchi wote, hatufahamu kifanyike kitu gani zaidi ya kumwomba Mungu na labda kusubiri next generation ambao wanaweza kuungana na kuunda nguvu mpya kupata Uhuru wa mweli... still I doubt kuwa wataweza kuongoza nchi badala ya Kutawala wananchi!

Solution ya Zimbabwe imekaliwa na ZANU-PF (kurudisha baadhi ya hekta za mashamba) lakini sio rahisi wananchi kuikubali kwani wengi wanapinga kabisa. Kwa hiyo kuna uwezekano makundi haya yakaanza vita (wanaounga mkono dhidi ya wakle wanaopinga wazungu kurudishiwa mashamba. Na tukumbuke walioshika mashamba sasa hivi ni vigogo ambao walipigania uhuru na kupoteza ndugu zao, mali zao ktk vita ya kumuondoa mkoloni...

Kichuguu,
Mkutano umefanyika Kenyatta International Conference Centre na host na wahusika wote wametajwa tazama vizuri ndani ya site nilizokupa hapo juu!.. Huyu mama kaenda pale kama nani? ama ndio Wazimbabwe katika kupakaza wamechukua picha za mikutano mingine na kupachika story!
 
Tanzanianjema,

Matatizo ya Zimbabwe hayaishii kwa Mugabe! nitarudia kuwa yeyote atakayeshika baada yake ni kuendeleza yale Mzee huyu atakuwa ameyaacha!.. ZANU-PF ni CCM ya Zimbabwe na kibaya zaidi hawana mtandao ndani uliogawanyika.


Kaka nakubaliana na wewe lakini ni ukweli usiofichika kuwa endapo Kamarade Mugabe akiondoka atatoa nafasi ya rejuvination kwa mfumo wa kisiasa wa Zimbabwe na vilevile kuwapa nafasi hawa manyang'au wa magharibi kujirudi na strategy yao kushughulikia suala hilo.

Tatizo sasa si Ardhi tena maana hakuna kurudi nyuma tena lakini tatizo limekuwa MUGABE. Kila kinachoanendelea sasa ni lazima kiendane na MUGABE factor hivyo ni wazi akiondoka atatoa nafasi ya mwazo mapya haswa katika suala zima la njia gani zitumike kutekeleza mabadiliko ya sera ya Ardhi ambayo kama nilivyosema hapo mwanzo hakuna kurudi nyuma.

Hili pia litawasadia ZANU-PF kuendelea kuning'inia madarakani. Nashangaa kwa nini hawasomi busara hizi kwa walimu wao CCM.

Tanzanianjema
 
Tanzanianjema,

Nimeuliza vizuri Mugabe akiondoka leo nani atakamata nchi?... kama ni ZAPU-PF bado ni yale yale ya kumwondoa Mwinyi kumweka Mkapa!..nothing will change life of poor Zimbabweans.
Tazama dunia nzima tunavyo ingizwa magirini na hawa jamaa wa magharibi!.. Hiyo Afghanstan walisema waondoke Taliban, leo hii nchi ndio vita kuliko walivyokuwa na Mrusi!...Haya kule Lebanon walisema Syria iondoke mambo yaleyale tena mabaya zaidi, Iraq na Saadam, Palestine na Arafat yote haya ni matakwa ya hawa jamaa bila kuwepo na plan B inayowatazama wananchi ila maslahi ya nchi hizo.
Mimi nachosema tumwondoe Mugabe tukiwa na Plan B, plan ambayo tumeiweka sisi wenyewe ama Wazimbabwe kwa maslahi yao laa sivyo tutakuwa hatukuwasaidia kitu zaidi ya kuomba baba mshenzi afe watu wagawane mirathi!..
Nipe plan B nitakusikiliza na pengine kukubaliana na wewe lakini hili swala la Rejuvination mfumo wa kisiasa Zimbabwe ni ndoto. A theory ambayo haiwezi kabisa kuwasaidia ila kuongeza machafuko zaidi...
Ndio yaleyale nayozungumzia ya kumwondoa Habyalimana!
Siwezi kusimama hapa na kudai Kagame au M7 waondolewe madarakani Rwanda na Uganda bila kuwepo plan B... ni kutowatakia mema wananchi wa nchi hizo!
 
Zimbabwe police raid MDC office



Zimbabwean police have cracked down on MDC activities



http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/6695061.stm

Sasa Mugabe inabidi awaue wapinzani wote.
 

Zimbabwe ina matatizo matatu makubwa: la kwanza ni ukabila, la pili ni tamaa ya madaraka na incompetence ya Mugabe mwenye umri wa miaka 83, na la tatu ni ujinga wa raia wa vijini. Hapa nitaongelea hili la ukabila ambalo pia limesababishwa na zaidi na ubinafsi wa Mugabe ingawa linaonekana kuanza tangu wakati wa kugombea Uhuru hivyo kuwa na historia ndefu kidogo ikihusiha majina makuu ya uhuru wa Zimbabwe, kama akina Joshua Nkomo, Herbet Chitepo, James Chikerema, Joseph Msika, Abel Muzorewa, Ndabiningi Sithole, Maurice Nyagumbo, Josiah Tongogara, Edgar Tekere na Daniel Madzimbamuto. Ingawa wengi kati ya viongozi wa wapiganiaji uhuru walikuwa wakilenga kujenga taifa moja la Rhodesia (wakati huo) bila kujali makabila yao, baadhi yao (kutoka kabila la washona) walikuwa wakitaka wapate madaraka ya juu ya nchi kwa njia yoyote ile hasa kutokana na kabila lao. Tofauti hizi za malengo ya viongozi zilisababisha nguvu za upiganiaji uhuru kugawanyikagawanyika, na ndiyo maana chama cha ZAPU kilichoasisiwa na Joshua Nkomo na kuanzisha mapambao ya uhuru kilipata msukosuko wa kugawanyika mara nyingi sana na kutokea vyama kama ANC, FLORIZI, ZANU na ZANU-Ndonga.

Wakati Nyerere, Kaunda na Samora walipotoa msaada sana ya kugombea uhuru kule Zimbabwe, ZAPU walijichimbia Zambia ambapo ZANU wakajichimbia zaidi Msumbiji. Makundi haya mawili yaliongoza mapambao hadi kufikia uhuru chini ya banner ya Patriotic Front. Wakati huo lengo la Nyerere, Kaunda na Samora (Frontline States) lilikuwa ni kutoa misaada hadi Zimbabwe ikombolewe; walitegemea kuwa baada ya usinhindi wa pamoja, ZANU na ZAPU wataungana kama chama kiomoja cha Patriotic Front dhidi ya UANC cha Muzorewa (ambaye alikuwa akitambuliwa na Smith), ZANU-Ndonga cha Ndabaningi Sithole, na Rhodesian Front cha Smith. Hata hivyo ilipofika wakati wa uhuru, Mugabe aligeuka na wala hakutaka kuungana kabisa na Nkomo hasa kwa vile alijua kuwa wakati wa kura, yeye kama mshona angepata kura nyingi dhidi ya Nkomo ambaye alikuwa mndebele. Halafu baada ya uhuru Mugabe aliwatenga kabisa wafuasi wa ZAPU kwenye serikali isipokuwa Nkomo na watu wachache sana ambao walitumiwa bila kuwa na nguvu serikalini ili kuridhisha viongozi wa Frontline states. Hata hivyo matukio yaliyofuata baada ya uhuru kama yale ya mauaji ya wandebele yaliyofanywa jeshi la Mugabe la Fifth Brigade kule Gukurahundi baada ya kufundishwa na kupewa silaha na Korea Kaskazini, kuwindwa kwa Joshua Nkomo, na mambo mengine dhidi ya wandebele kwa jumla yalidhoofisha sana utaifa wa Zimbabwe, na huo ndio uliokuwa mwanzo wa Zimbabwe kuporomoka. Mugabe alijenga politics za nchi kwa msingi wa ukabila kutokana na tamaa yake ya madaraka. Ingawa leo hawaongei hivyo, ni vigumu kiongozi wa Zimbabwe kutoka kwenye kabila la Wandebele hata kama angekuwa na uwezo na busara kama nabii. Kutokana na ukabila huo huo, nafasi nyingi sana za juu kwenye taasisi mbalimbali za serikali zimepewa kwa watu kutokana na makabila yao bila kufuata uwezo wao wa kazi. Watu walio na nafasi za juu serikalini kutoka kabila la wandebele ni wachache sana na wamezipata kwa mbinde kiasi kuwa wanaimba wimbo wa YES SIR kwa Mugabe ili kutunza nafasi zao.

Kwa vile ukabila unachangia sana katika matatizo ya Zimbabwe, Mugabe akiondoka na kupatikana kiongozi mwingine ambaye hataabudu ukabila, itapunguza sana matatizo yaliyopo. Swala la plani B sidhani kuwa ni gumu sana kwa Zimbabwe, nitaliongelea huko mbeleni siku nyingine.

Mkandara,

Ule mkutano wa COMESA ulianza tarehe 11 May na kuisha tarehe 23 May; ulikuwa na jumla ya vikao 7 kama ilivyoorodheswa hapa kwenye ukurasa wa 3. Vyote hivi vilifanyika KICC isipokuwa kikao cha Mawaziri wa nchi za nje, Kikao cha Marais na Kikao cha wake za Marais. Venue kamili za vikao hivi vitatu haikutangazwa hadharani, kwenye pamphlet ya waandaaji ukurasa wa 4, wakisema "The Venue for the Heads of State Summit, Ministers of Foreign Affairs and the First Ladies Roundtable will be communicated in due course." Sasa kikao cha marais kilikujafanyika katika jengo la makao makuu ya UN-Habitat kitongoji cha Gigiri hapo Nairobi, Kenya. Angalia taarifa hii hapa. Ndiyo maana Mama Tibaijuka ambaye ni Director General wa UN-Habitat aliwakaribisha viongozi wale. Kwa bahati mbaya sana kuna magazeti mengi yaliyoripoti kimakosa kuwa mama Tibaijuka ni Secretary General wa COMESA badala ya kusema kuwa ni Director General wa UN-HABITAT ulipfanyikia mkutano ule.
 
Kichuguu,

Mugabe akiondoka na kupatikana kiongozi mwingine ambaye hataabudu ukabila, itapunguza sana matatizo yaliyopo. Swala la plani B sidhani kuwa ni gumu sana kwa Zimbabwe, nitaliongelea huko mbeleni siku nyingine.

Nitashukuru sana kama utaweza kunipa do ndoo za ufumbuzi wa swala la Zimbabwe!... kusema kweli akili yangu imekwama ktk kufikiria hali ya wananchi wa Zimbabwe bila kufikiria kwanza ufumbuzi wa swala la ardhi!..

Hata hivyo nipo tayari kusikiliza hiyo Plan B..na hasa huyo kiongozi ambaye atachukua madaraka!
 

Mkandara,

Samahani sikusoma hii mapema ningeweza kuandika leo hii, ila niliporudi kwenye computer nilitumia muda kujibu ile 911 consiprancy theory. Kwa vile maelezo haya ni marefu kidogo na mimi siyo mzuri wa kupiga mashine, ninahitaji muda kidogo. Uzee unanikosesha utamu. Nitaiandika labda kesho nikipata nafasi.
 
Ghana - Jerry Rawlings Clashes With Zimbabwean
25/05/2007 - Ghanaian Chronicle

FORMER President Jerry John Rawlings and Zimbabwe Minister of Justice, Legal and Parliamentary Affairs, Hon. Patrick Chinamasa, on Wednesday this week, vehemently opposed each other on current political issues in Zimbabwe.
The former Ghanaian Head of State suggested to the Zimbabwean Minister and his entourage to apologize to the people of Zimbabwe and others for troubles that have come up as a result of President Mugabe's land reform policy.
The ex-president was of the view that, in the land reforms, it was possible that toes were stepped on especially considering the manner in which the policy was implemented.
But Minister Patrick Chinamasa totally disagreed and stated that they owed no apology to anybody.
According to him, what the Zimbabwean government was seeking from the African Union Chairman, President J.A Kufuor and his team was a defence of African countries so that sanctions that have been imposed on Zimbabwe are lifted to enable them access credit from international markets.
"We are not apologizing for anything. If there had not been any resistance against us by going to European capitals, campaigning against us and lobbying the British not to own up to their commitment, that would not have happened," he said adding, "Clearly, they must realize the consequences of resisting; is not in their interest. So we have no apologies at all," he said.
The Minister made the observation when he led a team to pay a courtesy call on the former President, at his Ridge residence.
"Somehow, we are not making much ammunition from the fact that, this is one man, who has dealt with the most repugnant policy of the past as far as land acquisition issues are concerned. This is one man who has stood up and actually fought against imperialist policy. Admittedly, some aspects of it were a little bit too painful in terms of the manner in which it was approached. I believe that can be apologized for, for we all make mistakes," were the words of the former president.
Minister Chinamasa, who was accompanied by H.E. Ambassador Musaka, Zimbabwean Ambassador to Ghana; Mr. David Mangota, Secretary for Justice, Legal and Parliamentary Affairs; Mr. Water Tapjumaneyi, from the Ministry of Foreign Affairs; Mr. Wayne Vudzijena, Ministry of Home Affairs; Mrs. Monilla Kuhenee, Ministry of Justice and Mr. Jeremiah Mukota, Deputy ambassador, further explained to the ex-President why there was no need to render an apology to the people of his country but rather stressed the need for the lifting of sanctions.
According to him, the Zimbabwean government, remained a principled one and was prepared to accord everybody equal rights irrespective of where one came from.
He stated that it was unfortunate that people who had refused to apply for the re-allocation of lands were now crying all over.
Hon. Patrick Chinamasa who again disagreed with the ex-president over the latter's assertions that perhaps, the land reform policy could result in the whites leaving Zimbabwe with all their scientific competence, said sanctions should be lifted; "we don't need the largesse from the IMF or the World Bank. For the past 10years we have been operating on our own resources without any financial support, which demonstrates the resilience of our economy. We have been pummeled as far as we are concerned and all that we are asking for is the lifting of the sanctions".
The visit which afforded all the members the opportunity to openly discuss matters saw the Zimbabwean Minister advance his arguments. He said his government was battling seriously with the issues of de-colonisation and charged the AU under the chairmanship of President Kufuor to ensure that the liberation process, which was started some years back, would be completed.
Jerry Rawlings, after listening attentively to the explanations from the Minister whom he consistently referred to as "Chief", took a swipe at the Western Media for blacking out the other side of the story.
"Thank you. But the point is that some of these things are kept from some of us. Maybe, some of us are speaking from the perception of the Western Media who are against you. Or maybe, this is where a lot more effort had been made but I am saying that recently, the Zimbabwean government began to make some moves with regard to what they perceived as areas of rejection, as far as acquisition of land was concerned."
Before he proceeded, the Minister of Justice interjected and said, "What we are saying is that, the objective of the struggles must be realized. We did it by nationalizing our farm lands," adding that any Zimbabwean was eligible for allocation of land irrespective of whether the person is white or black. "If you are a black or white citizen you would all queue and make the application," he said.
Continuing, Flt. Lt. Rawlings who had with him, his wife, Nana Konadu Agyeman-Rawlings; Mr. James Victor Gbeho, former Foreign Minister and Mr. Emmanuel Victor Smith, his Special Assistant who is also the Managing Editor of Weekly Standard, said, "from what we are seeing under this unipolar exercise of power, the right of might under the leadership of some of these Western Powers is actually made to supercede the philosophy of the might of right."
Describing President Mugabe as a good leader for, "his sense of patriotism," he said perhaps some of the scenes that were captured by the Western media and broadcast were designed to demonize the policies of the Zimbabwean President.
After launching his usual attacks on British Prime Minister Tony Blair and U.S. President George W. Bush, he said, "what I want to say is that the fight against neo-colonialism appears to be a more Herculean task than the fight against colonialism. It appears we have got a long way to go."
He did not also mince words on what he thought was wrong on the part of the Pope and the outgoing Nigerian President, Olusegun Obasanjo.
 
Na hapa naona amejitahidi kweli kuwa diplomatic......

tanzanianjema
 
If there had not been any resistance against us by going to European capitals...


Yer to come to European capitals for shopping thats what they know.
 
UK denies imposing economic sanctions on Zimbabwe

2007-06-06 09:27:34
SOURCE: Guardian

Zimbabwe hawajawekewa economic sanctions kama vile baadhi ya wanabodi wanavyotaka tuamini. Waliozuiwa kusafiri kwenda europe kufanya shopping babu kubwa ni Mugabe na kundi lake kwa pesa ya walalahoi ndio wamepigwa stop na account zao kuwa Frozen. Hizi ndizo pesa ambazo wanalilia waendelee kuzitumia wakati wamekwiba.
 
Mugabe stripped of degree honour

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…