Zimbabwe: The turmoil, reconciliation, and the future!

Zimbabwe: The turmoil, reconciliation, and the future!

Mkandara

Hapo tunakubaliana Mugabe nakumbuka alipochukua madaraka alimwambia Ian Smith 'utajiri huu wote sasa mimi ndio nauchukua kuongoza.'
 
Dua,
Hapo tunakubaliana Mugabe nakumbuka alipochukua madaraka alimwambia Ian Smith 'utajiri huu wote sasa mimi ndio nauchukua kuongoza.'

Hii ndio dhana inayonipa taabu sana kumkubali kiongozi ama chama chochote cha kisiasa nchini kama sii Afrika yote pamoja na kwamba wanajua sana kuhamasisha watu kwa hotuba na maandishi mazito na itikadi zao!
 
Mkandara,
1.tunachezewa akili tu hapa. swali zuri sana mkandara: Mugabe aliweza vipi kuendesha uchumi kwa miaka 20 aje kufurunda leo hii?

2.Haya mauaji ya 5th Brigade mbona yanaanza kupigiwa upatu leo? Mbona waliendelea kumpa silaha na misaada mara baada ya mauaji yale? Wanavyotoneka hilo jeraha ni kwa manufaa ya nani?

3.Lets be frank hapa: vikwazo vya uchumi vina athiri uchumi kiasi gani? sera mbaya za Mugabe zina athari zipi? Tupime tuone mzani unaelemea upande gani.

4.kwanini vita vya Msumbiji havikuathiri uchumi wa zimbabwe, lakini vita ya DRC vimeathiri uchumi wake?

5.Pamoja na vikwazo vya uchumi, njaa, ukame, na inflation, vyombo vya fedha vya magharibi bado vinamlazimisha Mugabe ku-service deni lake la nje. Naomba kuuliza kama hiyo siyo hujuma na mauaji.

6. Peter Ngumbulu[former PS wa Hazina] alipokuwa head wa Africa desk IMF alitamka wazi kwamba Zimbabwe inanyimwa fedha kwasababu za kisiasa, si kitu kingine.

7.Mugabe aondoke madarakani kwasababu kawatukana sana wazungu. Kwa kosa hilo wazungu hawawezi kumsamehe.
 
jokaKuu

1.) Unaongelea miaka ishirini ipi hiyo? Kama wewe ni mfuataji wa mambo ya Zimbabwe alipokufa mke wa kwanza wa Mugabe ambaye kwa asili alitoka Ghana miaka ya 1990 watu wengi walisema sasa uchumi wa Zimbabwe umekufa vile vile. Mugabe aliweza kuongoza vizuri kwa sababu Sally Mugabe (RIP) aliweza kumkataza kufanya mambo mengi ya kipumbavu aliyokuwa anafanya na mengine ambayo Mugabe alikuwa anaficha. Kutokana na kuzini kwake na secretary wake ambaye amekuja kumuoa na bado kijana anatumbua tu na hana lolote ajualo wazimbabwe wanamwita 'Graceland' alikuwa anajengewa nyumba karibu na Borrowdale subburb kwa wale waliofika kule kwa pesa ya walipa kodi chini ya Waziri Enock Chikowore ambaye alikuwa waziri wa Nyumba.

2.) Mauaji ya 5th brigade yalifanyiwa documentary miaka ya 1986 na waliokuwa Zimbabwe waliweza kuyaona, Kule Bulawayo ulikuwa unakwenda kwa kusindikizwa na polisi hadi walipokubaliana na Nkomo kupewa u-vice president kwa hiyo si kweli kwamba yanaongelewa leo. Hakuna mtu aliyempa silaha alikuwa na uchumi mzuri na aliweza kununua silaha. Vile vile safari za usiku na mapema sana zilikuwa marufuku kwa wengi waliokuwa kule kwani ndio magari ya hiyo brigade yalikuwa njiani kuwamaliza wale watarajiwa.

3.) Vikwazo vya uchumi vilikuwepo wakati wanapigania uhuru kwa hiyo hakuna tofauti.

4.) Musumbiji ni vita ipi hiyo? Kama ni RENAMO Zimbabwe walikuwa wanalinda the Railway corridor kwa bidhaa zao kwenda bandarini (Beira) na RENAMO walijua hilo hivyo walikuwa hawawezi kushindana nao.

5.) Hilo deni la nje walilipata miaka ipi? Na lilikuwa kiasi gani?

6.) Siwezi kusema hilo, lakini tupatie time frame mwaka gani?

7.) Mugabe aondoke madarakani kwa sababu mbili kuu za msingi moja ni kukaa madarakani kwa muda mrefu na kulewa madaraka na mbili kuharibu uchumi wa Zimbabwe.

Hakuna mwafrika yeyote ambaye hataki ardhi yake irudishwe lakini Mugabe hakuweza kulifanikisha hilo na anatumia hiyo sababu kupata support.
 
Dua,
Mara ya mwisho nilikuwa Zimbabwe na Botswana mwaka 1986 haya maneno sii kweli kabisa yameongezwa chunvi.
Wakati hawa jamaa wanapigania Uhuru ilikuwaje wawekewevikwazo vya kiuchumi wakati utawala ulikuwa chini ya Kaburu?...
Dua nilikuwepo Zimbabwe wakati wanapata Uhuru.. toka ukishuka airport yao ina wafanya kazi wazungu watupu (hata Mfagiaji) hadi waliposhika weusi sehemu zote! Ziimbabwe ilikuwa unapata kila kitu... shopping zetu tulizifanya huko hadi maswala ya Dubai yalipoingia..
Zimbabwe walijihusisha sana na vita ya Frelimo kuliko nchi nyingi na walipeleka majeshi yao kama tulivyofanya sisi....
Nadhani Jokakuu alimaana ya kwamba hawakuweza kuanguka wakati ule imekuwaje leo. Zimbabwe huru haijawahi kufungiwa ama kuwekewa vikwazo vya uchumi hadi hivi majuzi baada ya matatizo ya Ardhi.
Kwa hiyo tunahesabu toka 1982 hadi 2002 hiyo ni miaka 20 ambayo Zimbabwe dollar yake ilikuwa bado ina nguvu sana pamoja na matatizo yote. As a fact Tsh ilishuka haraka sana kuliko Zimbabwe dollar ktk kipindi cha toka 80's to 2000.
 
Mkandara

Mara ya mwisho nilikuwa Zimbabwe na Botswana mwaka 1986 haya maneno sii kweli kabisa yameongezwa chunvi.

Maneno gani yaliyoongezwa chumvi?

Zimbabwe walijihusisha sana na vita ya Frelimo kuliko nchi nyingi na walipeleka majeshi yao kama tulivyofanya sisi....
This is absolutely wrong.

Vikwazo aliwekewa Ian Smith sio Mugabe i.e. Zimbabwe walikuwa wana-trade na South Afrika under Pick Botha wengine wanamuita Peter William Botha. Zimbabwe walijihusisha vipi na vita ya FRELIMO NAONA UNACHANGANYA HAPA MOZAMBIQUE WALIPATA UHURU WAO 1975 KABLA YA ZIMBABWE what are you talking about na Zimbabwe 1980 vipi mzee naona unazeeka na data.

Nadhani Jokakuu alimaana ya kwamba hawakuweza kuanguka wakati ule imekuwaje leo. Zimbabwe huru haijawahi kufungiwa ama kuwekewa vikwazo vya uchumi hadi hivi majuzi baada ya matatizo ya Ardhi.
Kwa hiyo tunahesabu toka 1982 hadi 2002 hiyo ni miaka 20 ambayo Zimbabwe dollar yake ilikuwa bado ina nguvu sana pamoja na matatizo yote. As a fact Tsh ilishuka haraka sana kuliko Zimbabwe dollar ktk kipindi cha toka 80's to 2000.

Hivi vikwazo gani vya uchumi mnavyoongelea ninavyojua mimi vikwazo in place ni vya viongozi kwenda kutalii Europe na pesa walizoiba kuwa frozen i.e. account za Robert Mugabe and his cronies pamoja na WB na IMF lakini biashara kubwa ya Zimbabwe ya Tumbako na madini hakuna sanctions sasa sijui mnaongelea nini?
 
Mkandara,
1.Zimbabwe walikuwa na mkataba wa mafunzo ya kijeshi na Uingereza mpaka miaka ya 1998. Kwa msingi huo, wakati machafuko yanaendelea Ndembele, Uingereza ilikuwa ndiyo supplier mkuu wa silaha za Zimbabwe.

2.Ushirikiano wa kijeshi kati ya Zimbabwe na Uingereza ulikuwa mzito kiasi cha Special Forces[SAS] ya Uingereza kufundisha Paratroopers wa Zimbabwe. Wakati vita ya FRELIMO vs RENAMO imechachamaa majeshi ya Zimbabwe yaliweza hata kupata bunduki za Kiingereza ambazo ni mpya, na hazijasambazwa kwa vikosi vyote vya Uingereza.

3.Si kweli kwamba majeshi ya Zimbabwe yalikuwa yanalinda reli ya Beira na hayakushiriki katika vita dhidi ya FRELIMO vs RENAMO. There was so much defections in Frelimos army. Ilibidi Zimbabwe abebe mzigo mkubwa wa kuhakikisha Msumbiji haichukuliwi na Renamo. JWTZ ilikuja kutoa ushirikiano baada ya kifo cha Samora.

4.Vita ya FRELIMO vs RENAMO ilidumu kwa muda mrefu kuliko vita vya Congo. Sasa imekuwaje vita ya Congo iathiri uchumi wa Zimbabwe kuliko vita ya Msumbiji? Hiyo reli wanayodai Zimbabwe alikuwa akiilinda ilikuja haribika kabisa kwa hujuma za Renamo.

5.Ni nani alikuwa akiwasaidia RENAMO na UNITA kama siyo South Africa na Marekani?

6.Machafuko ya Ndebele yaliisha kwa Mugabe na Nkomo kusaini mkataba wa amani na kuunganisha vyama vyao mwaka 1987. Sasa kwanini miaka 20 down the road watu wanajaribu kutoneka makovu ya matatizo yale? Mugabe alishaomba radhi kutokana na mauaji yale. Inasikitisha sana kwamba BBC,UK,USA na MDC wamegeuza mauaji yale kuwa mtaji wa kisiasa wa kumuondoa Mugabe madarakani.

7.Zimbabwe imetumbikia ktk tatizo la madeni baada ya kukaribisha ushauri wa uchumi toka nchi za magharibi, IMF na WB. Tukubaliane kwamba hakuna aliyemshikia kiboko Mugabe kuchukua ushauri huo. Vilevile tukubaliane kwamba mpango wa Structural Adjustment Programme[SAP] ulikuwa na athari mbaya sana kwa uchumi wa Zimbabwe.

8.Hii MDC ilikuwa kama juwata ya Zanu-PF. Mwanzoni walikuwa wakipinga sana huu mpango wa SAP na athari zake kwa sekta ya viwanda Zimbabwe. Kitu kinachonishangaza ni jinsi walivyogeuka na kuwa pro-west.

9.Labda niulize swali dogo: Mugabe ametaifisha mashamba, sasa kwanini viwanda hata vile visivyotegemea mazao ya mashambani viathirike?

10.Bado naendelea kuuliza: Inakuwaje nchi yenye ukame, njaa, uhaba wa umeme, uhaba wa mafuta, inflation ya kutisha, ilazimishwe ku-service deni lake kwa vyombo vya fedha vya magharibi. Kwangu mimi hiyo ni hujuma na mauaji.

11. Peter Ngumbulu[Mtanzania] alikuwa Head wa Africa desk mpaka mwaka 2006. Wakati wake ndipo kura ya kuipa Zimbabwe budgetary support ilipigwa. Nchi zote zilipiga kura kwamba Zimbabwe ina-qualify, lakini fedha hizo hazikutolewa kwasababu ya veto ya UK na USA. Ndiyo maana Peter Ngumbulu akalalamika kwamba uamuzi wa kuinyima fedha Zimbabwe ulikuwa wa kisiasa.

12.IMF na WB wakikuwekea vikwazo basi huwezi kukopa popote pale ktk nchi za magharibi. Vilevile hizi kauli mbiu za BBC na Tony Blair zinafukuza wanaotaka kuwekeza Zimbabwe. Kwa kifupi, Tony "amemshika pabaya" Bob.

13.Waafrika tuna tabia ya kusahau kwa haraka sana. Miaka ya 60/70 Tanzania tulivunja uhusiano wetu na Uingereza kwasababu ya wao kukataa kumuwekea vikwazo vya uchumi na kijeshi Ian Smith.

14.Uingereza walimbwaga Ian Smith baada ya Nigeria/Obasanjo kutishia kutaifisha visima vya mafuta vya British Petrolium[BP] vilivyoko Nigeria. Bila hivyo, "mechi" kati ya Smith na Zanu/Mugabe ilikuwa imalizwe kwa mtutu wa bunduki, kama ilivyokuwa kwa Mreno kule Msumbiji.

15.Ili Mugabe aondoke kwa kutumia vikwazo vya Uchumi, UK na USA wanapaswa kumtishia Thabo Mbeki na vikwazo. That way, Mbeki atalazimika kumuondoa Mugabe pale, lakini kitakachotokea baadaye only GOD knows.

16.MDC hawataki uchaguzi mwaka 2008, lakini wanataka iundwe serikali ya mpito itakayojumuisha ZANU-PF na MDC. Hilo ndilo sharti kuu la MDC, na Mugabe hataki kulisikia.
 
Dua,
Kwanza nimpongeze Jokakuu kwa kuongoza maneno yangu. Maanake niliposema Frelimo basi mzee ukarudisha miaka nyuma hadi kabla ya Uhuru miaka ambayo hata wapigania uhuru wa Zimbabwe wenyewe Patriotic Front - PF hawajikusanya.
Mzee wangu tunazungumzia wakati wa uhuru wa Zimbabwe na sio nyuma ya hapo na hiuyo chunvi umeiweka ktk kifungu cha kwanza na cha pili kwa sababu ktk kipindi hicho nilikuwa nakwenda sana Zimbabwe karibu kila mwezi. na nimekaa sana mitaa ile miaka hiyo unayozungumzia.

Inaonyesha habari nyingi unazipata toka magazeti ya hao jamaa sasa nakuomba ipitie hii taarifa ambayo wengi wetu tunaikubalia kama ndo chimbuko la mgogoro wa Zimbabwe na nchi za Magharibi....
http://www.sum.uio.no/publications/pdf_fulltekst/WP2003_03_lee.pdf

Nitashukuru sana kama utanambia habari hii na maelezo yangu yanatofautiana vipi...
 
jokaKuu
1.Zimbabwe walikuwa na mkataba wa mafunzo ya kijeshi na Uingereza mpaka miaka ya 1998. Kwa msingi huo, wakati machafuko yanaendelea Ndembele, Uingereza ilikuwa ndiyo supplier mkuu wa silaha za Zimbabwe.


2.Ushirikiano wa kijeshi kati ya Zimbabwe na Uingereza ulikuwa mzito kiasi cha Special Forces[SAS] ya Uingereza kufundisha Paratroopers wa Zimbabwe. Wakati vita ya FRELIMO vs RENAMO imechachamaa majeshi ya Zimbabwe yaliweza hata kupata bunduki za Kiingereza ambazo ni mpya, na hazijasambazwa kwa vikosi vyote vya Uingereza.


3.Si kweli kwamba majeshi ya Zimbabwe yalikuwa yanalinda reli ya Beira na hayakushiriki katika vita dhidi ya FRELIMO vs RENAMO. There was so much defections in Frelimos army. Ilibidi Zimbabwe abebe mzigo mkubwa wa kuhakikisha Msumbiji haichukuliwi na Renamo. JWTZ ilikuja kutoa ushirikiano baada ya kifo cha Samora.


1. Zimbabwe hawakuwa na mkataba na UK sijui ulitiwa saini lini unaweza kufafanua hili? Kitu ambacho hakina ubishi ni wanajeshi wa Tanzania ambao walikuwa kule baada ya uhuru anbao walikaa hadi mwaka 1987 na kuanza kupunguzwa pamoja na wahandisi wa simu kutoka Tanzania.

2. Sio kweli kwamba waingereza walishirikiana kuwafundisha para wa kizimbabwe, Zimbabwe walikuwa wanalinda Beira Corridor na mara chache chache sana waliwafuata Renamo kwenye kambi zao na walikuwa wamepewa jukumu la kulinda bwawa la Kabora Basa ambalo ndio lilikuwa target kubwa ili kuikomoa Mozambique. Kama kweli wewe ulikuwa Zimbabwe wakati ule utakumbuka michango iliyokuwa inakusanywa kwenye supermarkets kwa ajili ya shughuli hiyo.

4.Vita ya FRELIMO vs RENAMO ilidumu kwa muda mrefu kuliko vita vya Congo. Sasa imekuwaje vita ya Congo iathiri uchumi wa Zimbabwe kuliko vita ya Msumbiji? Hiyo reli wanayodai Zimbabwe alikuwa akiilinda ilikuja haribika kabisa kwa hujuma za Renamo.


5.Ni nani alikuwa akiwasaidia RENAMO na UNITA kama siyo South Africa na Marekani?


6.Machafuko ya Ndebele yaliisha kwa Mugabe na Nkomo kusaini mkataba wa amani na kuunganisha vyama vyao mwaka 1987. Sasa kwanini miaka 20 down the road watu wanajaribu kutoneka makovu ya matatizo yale? Mugabe alishaomba radhi kutokana na mauaji yale. Inasikitisha sana kwamba BBC,UK,USA na MDC wamegeuza mauaji yale kuwa mtaji wa kisiasa wa kumuondoa Mugabe madarakani.


4. Kwanza hebu tupe miaka ya hizo vita halafu lazima ufahamu kwamba vita ya Mozambique ilikuwa rahisi kwa sababu wanapakana na ile ya Congo ilibidi wawe wana-airlift silaha pamoja na chakula sasa wewe piga hesabu hapo.

5. Kila mtu anafahamu hivyo.

6. Hayo makubaliano hayakuwa mwaka 1987 yalikuwa baada ya hapo. Wewe unampenda Mugabe je, unahabari ameua watu wangapi wasio na hatia? Kwa sababu Mugabe ni kipenzi chako lolote analofanya ni sawa tu. Ni sawa na Dito alivyoua wewe unaona ni sawa tu kwa sababu alikuwa mkuu wa mkoa lakini Klerlu alipouawa na Mwamwindi ilikuwa sawa Mwamwindi kunyongwa na kukaa jela miaka kadhaa.
Wazungu kusema sio hoja sio wazungu wote wenye roho ya korosho, mbona Sweeden waliendelea kuisaidia tanzania wakati IMF na WB walitususa?


7.Zimbabwe imetumbikia ktk tatizo la madeni baada ya kukaribisha ushauri wa uchumi toka nchi za magharibi, IMF na WB. Tukubaliane kwamba hakuna aliyemshikia kiboko Mugabe kuchukua ushauri huo. Vilevile tukubaliane kwamba mpango wa Structural Adjustment Programme[SAP] ulikuwa na athari mbaya sana kwa uchumi wa Zimbabwe.


8.Hii MDC ilikuwa kama juwata ya Zanu-PF. Mwanzoni walikuwa wakipinga sana huu mpango wa SAP na athari zake kwa sekta ya viwanda Zimbabwe. Kitu kinachonishangaza ni jinsi walivyogeuka na kuwa pro-west.


9.Labda niulize swali dogo: Mugabe ametaifisha mashamba, sasa kwanini viwanda hata vile visivyotegemea mazao ya mashambani viathirike?


10.Bado naendelea kuuliza: Inakuwaje nchi yenye ukame, njaa, uhaba wa umeme, uhaba wa mafuta, inflation ya kutisha, ilazimishwe ku-service deni lake kwa vyombo vya fedha vya magharibi. Kwangu mimi hiyo ni hujuma na mauaji.


11. Peter Ngumbulu[Mtanzania] alikuwa Head wa Africa desk mpaka mwaka 2006. Wakati wake ndipo kura ya kuipa Zimbabwe budgetary support ilipigwa. Nchi zote zilipiga kura kwamba Zimbabwe ina-qualify, lakini fedha hizo hazikutolewa kwasababu ya veto ya UK na USA. Ndiyo maana Peter Ngumbulu akalalamika kwamba uamuzi wa kuinyima fedha Zimbabwe ulikuwa wa kisiasa.


12.IMF na WB wakikuwekea vikwazo basi huwezi kukopa popote pale ktk nchi za magharibi. Vilevile hizi kauli mbiu za BBC na Tony Blair zinafukuza wanaotaka kuwekeza Zimbabwe. Kwa kifupi, Tony "amemshika pabaya" Bob.

7. SAP unayoongelea kwa Zimbabwe ni mwaka gani? Na hayo madeni nimeuliza ni ya katika kipindi kipi? Vile vile nani aliwatumbukiza kwenye hiyo kasheshe kama siyo huyu rafiki yako Mugabe?

8. MDC hawakuwa kama JUWATA (Jumuiya ya Wafanyakazi Tanzania) walikuwa ni ZCTU (Zimbabwe Congress of Trade Union) vitu viwili tofauti kabisa. Hawakuwa na uhusiano kama wa JUWATA na CCM. Acha uongo?

9. Uchumi wa Zimbabwe ulikuwa umeshikwa na Wazungu ambao ndio walikuwa wanalima na kufanya biashara zote i.e. Viwandani, kwenye machimbo ya migodi n.k. hawa ndio walikuwa wanadrive economy pamoja na kampuni kama Old Mutual ambayo inamiliki almost 70% ya majengo yote bora pale Harare na miji mingine, hawa ndio walikuwa wanunuzi wa shares kwenye Zimbabwe Stock Exchange ambayo ilikuwa ndio imeshika nafasi ya pili kwa kuwa good bourse in Afrika baada ya South Africa. Hawa ndio waajiri wakubwa Zimbabwe wanunuzi wa Tabaco walikuwa wankuja kununua moja kwa moja kwa mkulima na kukubaliana bei kwenye soko kila mwaka, uliza leo nani tena analima tumbako? Sasa hawa wakiweka silaha chini unakuwa huna kitu. Wengi wao wameacha kulima na kuishi kwenye nyumba zao za mijini na wengine kwenda Zambia na South Africa.

10. Hakuna anayewalazimisha kulipa deni kama hawalipi hawatapewa nyingine ndiyo sheria za kibenki Uki-default hawakupi tena ni uchaguzi wako hizo ni sheria zao waulize WB na IMF.

11. & 12. Unaongelea huyu jamaa 2006 hiki ni kichekesho uchumi wa Zimbabwe ulianza kuporomoka 1994 baada ya kuanza kwenda Congo, Tanzania ni nchi moja iliyowaonya lakini Mugabe alifikiri anafahamu zaidi yetu leo hii anapata umeme wa bure kutoka South Afrika pamoja na mafuta. Sasa UK na USA ndio wenye pesa ni lazima watoe kwa masharti yao sioni unalilia nini hapa, kwani wamekulazimisha kwenda kukopa? Zimbabwe kuna Gold nyingi tu uliza sasa mbona hawachimbi tena? tena wao walikuwa wanazitengeneza wenyewe kuziweka kwenye bullion pale pale Zimbabwe, unakwenda kuwauzia pale benki, walikuwa na kampuni yao ya uchunguzi wa madini yote kule Masasa njia ya kwenda Mutare. Hata WTZ wengi walikuwa wanakwenda kuuza Tanzanite in the 1990 na walikuwa wanalipwa USD 100 kwa carat na wanunuzi wakubwa walikuwa wako Borrodale kwenye kijiji cha SAM Levy karibu na race course.


13.Waafrika tuna tabia ya kusahau kwa haraka sana. Miaka ya 60/70 Tanzania tulivunja uhusiano wetu na Uingereza kwasababu ya wao kukataa kumuwekea vikwazo vya uchumi na kijeshi Ian Smith.
Tanzania hatukuvunja uhusiano na UK huu ni uongo siku zote Tanzania imekuwa ikionekana as bad boy kulinganisha na Kenya kwa sababu ya policies za JK Nyerere (RIP) na hilo sio kwa ajili ya ukombozi tu vile vile utaifishaji wa mashamba ya Mkonge, nyumba za msajili wa Majumba pamoja na Azimio la Arusha na mambo yote tuliyokuwa tunafanya kwa hiyo UK walikuwa hawatupendi na ndio kisa cha wao kuwasaidia zaidi Kenya na vile vile usisahau Tanzania haikuwa koloni la Mwingereza kwa hiyo ilikuwa vigumu wao kuwa na uhusiano mzuri ndio, mpaka leo UK wanaenda na kupendelea Kenya kuliko Tanzania (Bad boy).


14.Uingereza walimbwaga Ian Smith baada ya Nigeria/Obasanjo kutishia kutaifisha visima vya mafuta vya British Petrolium[BP] vilivyoko Nigeria. Bila hivyo, "mechi" kati ya Smith na Zanu/Mugabe ilikuwa imalizwe kwa mtutu wa bunduki, kama ilivyokuwa kwa Mreno kule Msumbiji.
jokaKuu acha uongo Ian Smith kama umesoma vitabu vyake na kuangalia all documentaries kuhusu mazungumzo ya uhuru wa Zimbabwe Lancaster break ilitokea baada ya kuwa na break kwenye ule mkutano na Tongogara (RIP) alipokuwa anaongea na Ian Smith Tongogaraakamwambia kuwa mama yake ndiye alikuwa house girl wa Ian Smith family wakati walikuwa wadogo na yeye Tongogara alikuwa bado mdogo na anamkumbuka, ndio ilipofikia hapo Ian Smith akaona kuwa kumbe anapigana na watu ambao wanamfahamu fika na kusoften msimamo wake lakini ndio jinsi Mugabe aliporudi Mozanbique alipoandaa mpango wa kumu-eliminate kwa njia ambazo aliendelea nazo hata alipokuwa rais (road carnage)



15.Ili Mugabe aondoke kwa kutumia vikwazo vya Uchumi, UK na USA wanapaswa kumtishia Thabo Mbeki na vikwazo. That way, Mbeki atalazimika kumuondoa Mugabe pale, lakini kitakachotokea baadaye only GOD knows.


16.MDC hawataki uchaguzi mwaka 2008, lakini wanataka iundwe serikali ya mpito itakayojumuisha ZANU-PF na MDC. Hilo ndilo sharti kuu la MDC, na Mugabe hataki kulisikia.


15. Sasa Mbeki yanamtokea puani yeye anafadhili mwizi ambaye hataki kukubaliana na wanacnhi wake sio MDC pekee ambao hawantaki hivi sasa natumaini umesikia hata hao ZANU PF wamemkatalia ule mpango wake wa kutawala hadi 2010 tayari kuna mpasuko huko na ataondoka tu hivi karibuni. Habari za uhakika umeme sasa ni kwa saa nne tu kila siku South Afrika yanawashinda!


16. mbona unageuza Mugabe ndio alikuwa hataki uchaguzi 2008 kwa kubadili constitution lakini amekataliwa unasoma udaku wake mzee?


Mkandara

Kwanza nimpongeze Jokakuu kwa kuongoza maneno yangu. Maanake niliposema Frelimo basi mzee ukarudisha miaka nyuma hadi kabla ya Uhuru miaka ambayo hata wapigania uhuru wa Zimbabwe wenyewe Patriotic Front - PF hawajikusanya.
Mzee wangu tunazungumzia wakati wa uhuru wa Zimbabwe na sio nyuma ya hapo na hiuyo chunvi umeiweka ktk kifungu cha kwanza na cha pili kwa sababu ktk kipindi hicho nilikuwa nakwenda sana Zimbabwe karibu kila mwezi. na nimekaa sana mitaa ile miaka hiyo unayozungumzia.

Inaonyesha habari nyingi unazipata toka magazeti ya hao jamaa sasa nakuomba ipitie hii taarifa ambayo wengi wetu tunaikubalia kama ndo chimbuko la mgogoro wa Zimbabwe na nchi za Magharibi....
http://www.sum.uio.no/publications/p...003_03_lee.pdf

Nitashukuru sana kama utanambia habari hii na maelezo yangu yanatofautiana vipi...
Wewe source yako ni wrong na huyu jokaKuu sioni sababu ya kumpongeza mbabaishaji sijarudisha miaka nyuma wewe unaongelea FRELIMO wakati unachanganya na RENAMO na miaka ya kupata uhuru hebu soma ulichoandika halafu uone mwenyewe jinsi ulivyojichanganya. Zimbabwe walikuwa kule kulinda Beira corridor tu muulize mtu yeyote yule kule Zimbabwe atakuambia hivyo, jokakuu nime-rebutt mambo yake mengi tu, Kama wewe kweli kipindi hicho ulikuwa Zimbabwe niambie mpambe wa Mugabe alikuwa anaitwa nani na alitoka nchi gani? Niwekee kwenye PM. Hii ni kukuonyesha tu kwamba hizi ni information kutoka jikoni sio kama wewe unavyofikiri.Hiyo pdf ni baada ya mwaka 2000 mimi nina original info.
 
Households in Zimbabwe are to be limited to four hours power supply a day in the latest setback to hit the country's struggling economy.

The measure, meaning electricity will only be available in homes between 1700 and 2100 local time, is likely to come into force immediately.

The move is designed to support the country's wheat farmers who need power to irrigate their crops.

Rampant inflation has led to widespread shortages of fuel and food.

The monthly rate of inflation rose to 2,200% in March, the highest in the world.

Farm priority

Critics accuse President Robert Mugabe of presiding over the destruction of the country's economy and society in an effort to hold onto power.

The longer period will drive prices for firewood and candles up
Francis Chakona, Newspaper vendor

But the government says Zimbabwe's economic problems are primarily due to foreign sanctions.

State-owned power firm Zesa Holdings said the restrictions would be in place for the next three months while demand for power is lower than at other times of the year.

Wheat farmers will be guaranteed power for 18 hours in an effort to boost the winter crop.

Zimbabwe is being forced to import maize after a poor harvest which the government blamed on drought conditions.

Power cuts have become a regular occurrence in Zimbabwe, where a shortage of foreign currency has prevented investment in the country's creaking infrastructure.

Key industries such as mining have been affected, putting further strain on the economy.

"This is no way a surprise," newspaper seller Francis Chakona told the Reuters news agency of the rationing move.

"But the longer period will drive prices for firewood and candles up and these items are already quite expensive."
 
Dua,

Niliandika hivi:-
Dua nilikuwepo Zimbabwe wakati wanapata Uhuru.. toka ukishuka airport yao ina wafanya kazi wazungu watupu (hata Mfagiaji) hadi waliposhika weusi sehemu zote! Ziimbabwe ilikuwa unapata kila kitu... shopping zetu tulizifanya huko hadi maswala ya Dubai yalipoingia..Zimbabwe walijihusisha sana na vita ya Frelimo kuliko nchi nyingi na walipeleka majeshi yao kama tulivyofanya sisi....
Sidhani kama hapa nazungumzia uhuru wa Msumbiji wa mwaka 1975 hali Zimbabwe wamepata uhuru 1980..ama naposema hawa jamaa waliwasaidia sana Frelimo ina maana nazungumzia wazungu akina Ian Smith bali Zimbabwe iliyokuwa huru.

Hilo swala la Mpambe sidhani kama ni dhihirisho la mimi kuwepo Zimbabwe kati ya miaka hiyo na sidhani kama wewe hapo unafahamu mpambe wa JK na anatoka nchi gani kiasi kwamba nisiamini kuwa wewe ni Mtanzania ama umeishi Tanzania ktk kipindi cha JK. Kifupi simjui na simjui kwa sababu sina taarifa hiyo wala haina umuhimu ktk mada hii kwa sababu huyo mpambe haongezi wala hapunguzi matukio tunayoyazungumzia. Mtu kama Shiri alikuwa akiogopwa sana Zimbabwe kuliko mpambe yeyote midomoni mwa watu.
Kisha unasema hiyo document ni baada ya 2000, sasa hapa tunazungumzia muda gani hasa?... kwa sababu Zimbabwe haikuwa na matatizo ya kiuchumi kama haya tunayoyaona leo nyuma ya 2000 toka wapate uhuru unless wewe unazungumzia mauaji.
Dua sio kwamba mimi nimesoma hiyo document tu ila nimesema nilikuwa nikienda sana Zimbabwe miaka ya 80's na hapakuwepo na matatizo kama tunayoyaona leo. Mambo mengi uliyozungumza hadi sasa ni tungo za tamthiria... Tanzanite caret 1 kwa dollar100? Old Mutual ku own 70% ya majumba makubwa ya mji wa Harare?... jamani hizi data mnazitoa wapi?
Mambo mengi yaliyoandikwa ktk pdf hiyo yamefanyiwa uchunguzi na wala sii mtu mmoja na kama wewe unadai unazo data za ndani zaidi basi nakuomba zimwage kisha watu wapime!
 
Western countries are concerned about the expected appointment of Zimbabwe to head a key UN body, the Commission on Sustainable Development.

Western diplomats said Zimbabwe, which is in the midst of an economic and political crisis, was hardly a good example of development.

The position traditionally rotates through the regions of the world, with Africa next in line.

Zimbabwe's candidacy is reported to have broad support within Africa.

Zimbabwe's Environment Minister Francis Nheme is being tipped by UN diplomats to be elected to the post on Friday.

However Erik Solheim, Norway's international development minister, said some countries still hoped to block the move.

"We do not find Zimbabwe the right country to head the CSD for the next period," he said.


A US state department spokesman, Tom Casey, has said: "We don't think that Zimbabwe would be a particularly effective leader of this body."

He said development there had "been going in only one direction - and it's backwards".

Power cut back

Zimbabwe is enduring the world's highest inflation, at more than 2000%, mass unemployment, and there are widespread accusations of civil rights abuses.

On Wednesday it was announced that households in Zimbabwe were to be limited to four hours' electricity a day, between 1700 and 2100 local time.

The measure, to ensure that wheat farmers are guaranteed the power needed to irrigate their crops, will be in place for the next three months, the state power provider said.
Story from BBC NEWS:
http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/6641271.stm

Published: 2007/05/10 01:21:40 GMT

© BBC MMVII

Maoni yangu, Naomba Zimbabwe wapate hiipost, na nataka kujua ni nchi ngapi za Africa zinazoisupport ZIM kwenye hili
 
Dua,
Mara ya mwisho nilikuwa Zimbabwe na Botswana mwaka 1986 haya maneno sii kweli kabisa yameongezwa chunvi.
Wakati hawa jamaa wanapigania Uhuru ilikuwaje wawekewevikwazo vya kiuchumi wakati utawala ulikuwa chini ya Kaburu?...
Dua nilikuwepo Zimbabwe wakati wanapata Uhuru.. toka ukishuka airport yao ina wafanya kazi wazungu watupu (hata Mfagiaji) hadi waliposhika weusi sehemu zote! Ziimbabwe ilikuwa unapata kila kitu... shopping zetu tulizifanya huko hadi maswala ya Dubai yalipoingia..
Zimbabwe walijihusisha sana na vita ya Frelimo kuliko nchi nyingi na walipeleka majeshi yao kama tulivyofanya sisi....
Nadhani Jokakuu alimaana ya kwamba hawakuweza kuanguka wakati ule imekuwaje leo. Zimbabwe huru haijawahi kufungiwa ama kuwekewa vikwazo vya uchumi hadi hivi majuzi baada ya matatizo ya Ardhi.
Kwa hiyo tunahesabu toka 1982 hadi 2002 hiyo ni miaka 20 ambayo Zimbabwe dollar yake ilikuwa bado ina nguvu sana pamoja na matatizo yote. As a fact Tsh ilishuka haraka sana kuliko Zimbabwe dollar ktk kipindi cha toka 80's to 2000.

Angalia ulivyoandika wewe mwenyewe. Sina ubishi zaidi ya hapa amini unavyoamini Norwegians waliofanya research ndio inayokubalika lakini wale ambao wako on the ground kwa sababu hawakuandika report hatuwezi kuwaamini.
 
Western countries are concerned about the expected appointment of Zimbabwe to head a key UN body, the Commission on Sustainable Development.

Western diplomats said Zimbabwe, which is in the midst of an economic and political crisis, was hardly a good example of development.

The position traditionally rotates through the regions of the world, with Africa next in line.

Zimbabwe's candidacy is reported to have broad support within Africa.

Zimbabwe's Environment Minister Francis Nheme is being tipped by UN diplomats to be elected to the post on Friday.

However Erik Solheim, Norway's international development minister, said some countries still hoped to block the move.

"We do not find Zimbabwe the right country to head the CSD for the next period," he said.


A US state department spokesman, Tom Casey, has said: "We don't think that Zimbabwe would be a particularly effective leader of this body."

He said development there had "been going in only one direction - and it's backwards".

Power cut back

Zimbabwe is enduring the world's highest inflation, at more than 2000%, mass unemployment, and there are widespread accusations of civil rights abuses.

On Wednesday it was announced that households in Zimbabwe were to be limited to four hours' electricity a day, between 1700 and 2100 local time.

The measure, to ensure that wheat farmers are guaranteed the power needed to irrigate their crops, will be in place for the next three months, the state power provider said.
Story from BBC NEWS:
http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/6641271.stm

Published: 2007/05/10 01:21:40 GMT

© BBC MMVII

Maoni yangu, Naomba Zimbabwe wapate hiipost, na nataka kujua ni nchi ngapi za Africa zinazoisupport ZIM kwenye hili


At last africa tunaonyesha tunasauti moja na kustick pamoja, for better or for worse, hiyo ni hatua ya kwanza, hayo ya kurekebisha uchumi yanaweza kufanyika, lakini I'm impressed kwamba for once tunaonyesha tuna uwezo wa kuungana.

West waache kuwa selfish, wapunguze matumizi yao, wanaimaliza dunia. Wanaact kama wapo peke yao. Nafikiri waafrika wameona hamna better country to voice that opinion loud enough now than z'bwe, they have nothing to lose. We should tell them this, and ask them, why it is they who consume the most of world resources, and it is they who affect the most of the world environment, but is is us, poor countries feeling the most of global warming? Is there a conspiracy? If Africa were to have the same level of production and consumption as them, the world will collapse in a very short time. So what does that tell us?
 
Dua,
Sasa Ondoa FRELIMO na weka hiyo RENAMO unayodai wewe tuone kama hii habari itakuwa na maana hata kidogo!... nitaonekana mpuuzi kusema hawa jamaa walisaidia Renamo wakati nazungumzia baada ya Uhuru, hata miaka nimeiweka kwa maandishi na kukuuliza wewe tunazungumzia wakati gani?.

Hata hivyo hakuna haja ya kubishana sana juu ya swala ambalo mimi na wewe kamwe hatuwezi kubadilisha kitu na kama alivyosema Keynez, bora sasa hivi viongozi wa Afrika wamekuwa na msimamo mmoja. Hii haina maana wanaunga mkono ama wanafurahia yale yanayotokea huko Zimbabwe. Bora kuukata mkono wa nje kisha tuta - deal na Mugabe sisi wenyewe!
 
Dua,
hakuna haja ya kuniita muongo, mbabaishaji, au msoma udaku. kama hukubaliani na yale niliyoandika basi yakanushe, au omba ufafanuzi. ukiniita majina unakuwa unanishambulia binafsi badala ya hoja zangu.

1.Umeniita MUONGO kutokana na madai yangu kuhusu mchango wa Nigeria ktk harakati za ukombozi Zimbabwe. Sasa sikuota ndoto kabla ya kuandika ktk forum hii. Hizi ni habari ambazo kila anayejisumbua kutafiti anaweza kuzipata. Here is one of the sources that supports what I wrote.

source:http://ekwuruke.tigblog.org/post/26146?setlangcookie=true

Massive material and financial aid from Nigeria were constantly channelled into and ultimately guaranteed the success of various liberation struggles. It is for this reason that Nigeria rightly earned the status of a "Frontline State." Also, in recognition of its stand against South Africa's apartheid, Nigeria was appointed to permanently chair the UN Anti-Apartheid Committee until the inhumane system was disbanded in 1994.

Nigeria did not hesitate to nationalise the British Petroleum Company in the late 1970s to force the hands of British colonialists and minority white settlers in granting independence to Zimbabwe.

Hapa pia wanazungumzia jambo hilo hilo.
source:http://www.thisdayonline.com/archive/2003/12/22/20031222com02.html
The final steps, which led to the process for independence, commenced at the Commonwealth Heads of Government meetings held in Zambia in April 1979. Putting pressure on Britain to act, Nigeria nationalized British Petroleum (BP). Though the British would have wished for someone else but Robert Mugabe (whom they thought was too Marxist in outlook) to win, Lord Soames, according to the late Hugo Young, the distinguished editor of the Times of London summed up that Mugabe's victory as the best thing for Zimbabwe, since Muzorewa was "useless" and Nkomo a Russian mole who would "have let the Russians in".


2.Umepinga maelezo kwamba hapakuwa na mkataba wa mafunzo ya kijeshi kati ya Uingereza na Zimbabwe. Ukweli ni kwamba Uingereza ndiyo waliowasaidia ku-demobilize wapigania uhuru toka Zanu na Zapu.

Vilevile, North Korean pamoja na kuwa ndiyo waanzilishi wa 5th Brigade, hawakudumu kwa muda mrefu kama Instructors wa kikosi hicho. Uingereza imetoa mchango mkubwa sana ktk ku-train jeshi la Zimbabwe, Jeshi la Anga, na zaidi Regiment ya makomando ya Zimbabwe.

source:
http://www.photius.com/countries/ko...tional_security_relations_with_the_t~177.html

In the 1980s, North Korea's highest profile military advisory activity was in Zimbabwe. Beginning in 1981, North Korea equipped and trained the Zimbabwean army's Fifth Brigade for counterinsurgency and internal security duties. P'yongyang provided almost all the equipment and about US$18 million worth of small arms and ammunition. The mission was not successful, however, and by 1986 the Zimbabwean government had the unit retrained by British military instructors

Mahusiano ya kijeshi kati ya Zimbabwe na Uingereza.
source:
http://www.regiments.org/regiments/africacentral/lists/cafrgts.htm

Fighting between the Shona and Ndebele (i.e. the ZANU and ZAPU factions) continued through the 1980s. In 1981-82 the government formed the 5th Infantry Brigade "Gukurahundi", composed solely of ZANLA troops, and used exclusively for internal control. This controversial formation soon terrorized the country and sought retribution from old tribal enemies. Its North Korean advisors were dismissed in 1983, and British assumed the training role. The state of emergency, declared in 1965, was ended in July 1990.


3.Majeshi ya Zimbabwe yalikwenda Msumbiji kulinda reli na mitambo ya umeme Cabora Bassa. Lakini hali ya usalama ilivyozidi kuwa mbaya ilibidi Zimbabwe waingilie kati na kupigana bega kwa bega kuwasaidia Frelimo.

Nina hakika vita ya Msumbiji ilidumu kwa muda mrefu kuliko ile ya DRC. Unaweza kudai kwamba DRC ni mbali na hiyo inaongeza gharama, lakini vilevile usisahau kwamba vita ya Msumbiji lasted longer, and that increased the costs too.

source:http://ccrweb.ccr.uct.ac.za/archive/defencedigest/defdigest03.html

In the process of protecting their trade routes, the ZDF literally joined the Mozambican civil war on the side of the Mozambican Government and ended up involving at least 30 000 Zimbabwean troops. They conducted military operations against Renamo throughout the length and breath of Mozambique. Sometimes these operations were conducted jointly with the FAM, but in most cases the Zimbabweans acted on their own. More than 40 FireForce and StrikeForce operations were conducted including the twice recapturing of the Renamo Headquarters at Cassa Banana in the Gorongossa Mountains in 1985 and 1986.

These operations stretched the ZDF's capabilities to the limit, literally halting all other military activities in Zimbabwe including training. The ZDF put in all available equipment and manpower.
 
jokaKuu

8.Hii MDC ilikuwa kama juwata ya Zanu-PF. Mwanzoni walikuwa wakipinga sana huu mpango wa SAP na athari zake kwa sekta ya viwanda Zimbabwe. Kitu kinachonishangaza ni jinsi walivyogeuka na kuwa pro-west.

Sasa hebu niambie haya maneno ambayo ni yako ni ya kweli? No. Ndio sababu nimesema mbabaishaji. Kwa sababu hata kipofu ukimwambia maana ya JUWATA na ZCTU ataona tofauti kama nilivyoandika.

14.Uingereza walimbwaga Ian Smith baada ya Nigeria/Obasanjo kutishia kutaifisha visima vya mafuta vya British Petrolium[BP] vilivyoko Nigeria. Bila hivyo, "mechi" kati ya Smith na Zanu/Mugabe ilikuwa imalizwe kwa mtutu wa bunduki, kama ilivyokuwa kwa Mreno kule Msumbiji.

Haya ndio maneno yako ya kwanza na sasa unasema hivi:

Massive material and financial aid from Nigeria were constantly channelled into and ultimately guaranteed the success of various liberation struggles. It is for this reason that Nigeria rightly earned the status of a “Frontline State.” Also, in recognition of its stand against South Africa’s apartheid, Nigeria was appointed to permanently chair the UN Anti-Apartheid Committee until the inhumane system was disbanded in 1994.

Nigeria did not hesitate to nationalise the British Petroleum Company in the late 1970s to force the hands of British colonialists and minority white settlers in granting independence to Zimbabwe.

Statement yako ya kwanza umesema Nigeria kutishia lakini hii ya pili ambayo ndio source Nigeria walitaifisha visima tayari in late 1970 sasa unaongea nini? Huu ndio ubabaishaki wenyewe na wala sio tusi. Ukisoma waliokuwa kwenye ule mkutano walivyosema ndivyo mimi nimeandika.

Basis za Zimbabwe kwenda Mozambique ilikuwa ni kwa sababu ya Beira corridor na cabora Basa sasa unarudia yale niliyosema mwanzo na vile vile deal ya uhusiano ambao unausema na UK ulikuwa ni mdogo sana wa few Instructors sio kama vile ilivyo kwenye ushirikiano kama vile Kenya n.k. na vile vile nimekwambia fafanua namna hii: Zimbabwe hawakuwa na mkataba na UK sijui ulitiwa saini lini unaweza kufafanua hili?

Soma between the lines jinsi nilivyofafanua na sio kukurupuka na kusema kitu ambacho sijasema.

Anyway amini unavyoamini lakini mimi siwezi kum-support killer kama Dito kwa kuua watu wasio na hatia.


Mkandara

Ubishi wangu umekwisha ndugu yangu tuendelee na mapya kama yapo, sina sababu ya kum-convice member yeyote abadili msimamo wake.
 
jokaKuu

13.Waafrika tuna tabia ya kusahau kwa haraka sana. Miaka ya 60/70 Tanzania tulivunja uhusiano wetu na Uingereza kwasababu ya wao kukataa kumuwekea vikwazo vya uchumi na kijeshi Ian Smith.

Huu niliita ni uongo sasa hebu tuambie ni lini Tanzania tulivunja uhusiano na UK. Na kama hatukuvunja je, huu sio uongo?

Habari ya wewe kusoma udaku naona unaweka chumvi mimi sijasema hilo.
 
Dua,
Wala usinielewe vibaya.. mimi nakubali sana baadhi ya maelezo yako isipokuwa tatizo ni pale mtu anaposimamia kitu na kutoa hukumu hali habari hizi zote zimetengenezwa na binadamu... tena basi kwa kulipwa na taasisi fulani ambayo pia inawez kuwa na interest zake. Kifupi dunia hii ni bora sana kuitazama kwa darubini na vizuri kuwana na mguu ndani maanake Leo hii news ni biashara!

Tofauti kubwa niliyokuwa nayo na wewe ni pale unapotafuta kosa ndani ya maandishi ya mtu na kuyatumia hayo kama hoja. Mathlan hili la JUWATA na ZCTU, sioni kabisa ugonvi uko wapi ikiwa mtu kasema katumia neno KAMA...Muhimu zaidi nadhani ni kuwepo kwa facts..
Nikisema Paka ni kama chui nadhani ni muhimu tuangalie undani wa hilo neno KAMA na limetumika kwa malengo yapi.
Otherwise mshikaji nipo nawe sehemu kibao (mada) ... isipokuwa hii ndugu yangu naungana mkono kabisa Jokakuu na jitihada za serikali yetu kusimama kuitetea Zimbabwe!..as country hawa jamaa hawawezi kuiadhibu nchi nzima kwa sababu ya kiongozi mmoja ambaye dawa yake ilikuwa jikoni ikipikwa.. wao wakaiopoa na kulisha sumu nchi nzima.
 
Mkandara

Point taken problem inapokuja unapofananisha jumiya ya wafanyakazi iliyo under CCM umbrella na trade congress ambayo haina uhusiano na chama tawala. Ukweli huu ndio ninaousuta. Kitu kingine ambacho sikubaliani nacho ni kuwakashifu western countries kwa kusema ukweli, hakuna hata nchi moja iliyolazimishwa kukopa WB au IMF na ndio masharti haya haya ambayo Mwalimu (RIP) aliyakataa na tulikuwa tunasaidiwa na Sweeden na nchi nyingine za scandinavia.

Botswana walikuwa wana barabara moja tuu kuu hadi miaka ya 1990 lakini kwa sababu wametumia resource zao vizuri leo hii wako mbali sisi tumekalia kuwakumbatia wezi na kushabikia wauaji hilo sikubaliani nalo.

Kweli hatuwezi kuwauza Zimbabwe na ni lazima tu-wasupport lakini huyu killer ni lazima aambiwe. Huwezi kuua watu kama inzi halafu watu wakuheshimu.
 
Back
Top Bottom