Ziara za viongozi wa nchi kubwa za magharibi zaonesha umuhimu wa China katika jukwaa la kimataifa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111430975690.jpg


Katika siku za hivi karibuni viongozi wa nchi za magharibi wamekuwa wakifanya ziara kadhaa nchini China, wakitafuta njia mbalimbali za kuhimiza ushirikiano kati ya nchi zao na China. Mwishoni mwa mwaka 2022 Chansela wa Ujerumani Olaf Scholz aliongoza ujumbe mkubwa kwenye ziara yake ya kwanza nchini China akiwa chansela, na baadaye Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alifanya ziara kama hiyo, ambayo ilifanyika kwa pamoja na ziara ya mwenyekiti wa kamisheni ya Ulaya Bibi Ursla von der Leyen.

Hizi ni ziara za mwanzo za viongozi waandamizi wa nchi kubwa duniani, ambao wamekuja China kuthibitisha utayari wao wa kuendelea na ushirikiano na China kwa manufaa ya nchi zao pamoja na manufaa ya dunia nzima.

Ziara hizi zimefanyika wakati hali ya kiuchumi na usalama barani Ulaya sio shwari, hasa kutokana na mgogoro wa Ukraine. China imeonekana kuwa ni chaguo sahihi kwa nchi hizo kuangalia fursa za kibiashara na kiuchumi zilizoko China. Lakini pia kutokana na mgogoro kati ya Russia na Ukraine, viongozi wa nchi nyingi za magharibi hawana mawasiliano mazuri na Russia, na wanaamini kuwa ukaribu uliopo kati ya China na Russia, na hasa kati ya Rais Xi Jinping na Rais Putin, unaweza kuwa ni sehemu ya utatuzi wa mgogoro huo. Kwa hiyo kwa baadhi ya viongozi wanaopenda kuona utatuzi wa amani wa mgogoro wa Ukraine, China inaonekana kuwa moja ya machaguo muhimu

Pamoja na kuwa Umoja wa Ulaya, Ujerumani na Ufaransa ni nchi za magharibi, ukweli ni kuwa kwenye baadhi ya mambo haya yanayohusiana na uchumi zimekuwa zinaonesha kupendelea kuwa na sera ya mambo ya nje inayojitegemea na inayozingatia hali halisi. Hii ni tofauti ilivyo kwa baadhi ya nchi ambazo zinalazimika au kulazimishwa kufuata sera ya mambo ya nje inayoshinikizwa na Marekani, ambayo kutokana na matumizi ya mabavu inaziathiri nchi hizo kuliko hata inavyoiathiri Marekani.

Kilichooneshwa na Ujerumani, Ufaransa na Umoja wa Ulaya, ni kuwa ushirikiano kati ya China, unaamuliwa na wao kwa maslahi ya nchi zao, na sio kushinikizwa na Marekani. Mfano mzuri ulioonekana kwenye maslahi haya ni kuwa China imeweka oda ya ndege 160 aina ya Airbus, biashara ambayo sio tu itainufaisha Ufaransa, bali pia itazinufaisha nchi mbalimbali za Umoja wa Ulaya zenye matawi ya kiwanda cha ndege za Airbus. Wakati huo huo Ufaransa pia imeagiza meli kubwa 16 za mizigo kutoka kwa China, na kwa kufanya hivyo sio tu imelinda ajira za wafanyakazi wa viwanda vya meli kubwa vya China, bali pia imehimiza ukaribu uliopo kati yake na China.

Uzuri ni kwamba nchi za Afrika zimekuwa na msimamo linapokuja suala la mahusiano kati yake na nchi nyingine duniani. Licha ya kelele nyingi ambazo zimekuwa zikiendelea kwa muda mrefu kuupaka matope uhusiano kati ya China na nchi za Afrika, msimamo wa nchi karibu zote za Afrika kuhusu ushirikiano wake na China, ni kwamba ni ushirikiano wa kunufaishana. Lakini kuna hali ya ajabu ambayo inapaswa kutazamwa. Kama uhusiano kati ya China na Umoja wa Ulaya, au China na nchi yoyote ya Ulaya ni jambo zuri, kwanini baadhi ya wachambuzi wa magharibi wanaupaka matope ushirikiano kati ya China na Umoja wa Afrika, au ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika? Sababu inaweza kuwa ni ubaguzi wa kisiasa tu au sababu ya ushindani wa kiuchumi. Lakini kilichooneshwa na viongozi wa nchi za Ulaya, kinatwambia kuwa wanachoongea na wanachotenda ni tofauti kabisa.
 
Ulaya wako tayari sana kushirikiana na China katika masuala ya kibiashara tatizo ni yule mume wao Marekani anataka awafanyie maamuzi
 
Back
Top Bottom