China inaheshimu haki za kujitafutia maendeleo za nchi zote zikiwemo zile zinazolengwa na nchi za magharibi

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111455273221.jpg


Kuwekwa vikwazo vya upande mmoja (unilateral sanctions), na kutumia majukwaa ya kimataifa kuweka vikwazo hivyo kumekuwa ni moja ya njia zinazotumiwa na baadhi ya nchi za magharibi, kuzibana nchi nyingine na viongozi wake, pale zinapoona kuwa nchi hizo hazifuati matakwa yao. Bahati mbaya ni kuwa wahanga wakubwa wa vikwazo hivi ni viongozi wa nchi zinazoendelea, iwe ni wale wa Amerika Kusini, Afrika na hata wa eneo la mashariki ya kati.



Kuwekwa vikwazo vya upande mmoja imekuwa ni njia ya muda mrefu inayotumiwa na nchi za magharibi, na mara nyingi nchi hizo zimekuwa zinaunda vikundi fulani vinavyofanya kila linalowezekana kuwabana viongozi wanaotofautiana nao mawazo kuhusu maswala ya uhuru, demokrasia na maendeleo. China kwa upande mwingine imekuwa ikiheshimu nchi na viongozi wa nchi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wale wa nchi za magharibi, kuwa na mawazo yao na kujiamulia mambo yao kama wanavyoona inawafaa.



Katika kutekeleza hilo kivitendo, China imekuwa wazi kwa viongozi na marais wote rafiki wa China ikiwa pamoja na wale waliowekewa vikwazo na nchi za magharibi, ambao imewakaribisha kufanya ziara China, iwe ni kufanya ziara za kiserikali au kushiriki kwenye mambo mengine. Baadhi ya viongozi walioitembelea China hivi karibuni ni pamoja na Rais Bashar Al Assad wa Syria, ambaye amefanya ziara ya kwanza nchini China tangu mwaka 2011 nchi yake ilipoingia kwenye mgogoro, na kuwekewa vikwazo na nchi mbalimbali za magharibi. Mwingine ni Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ambaye baada ya Marekani kushindwa kumwondoa madarakani na kuweka kibaraka wake, iliamua kumuwekea vikwazo.



Baadhi ya viongozi ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa hawaelewani na serikali ya Marekani, wamejikuta wakibanwa au hata kuwekwa nje ya jukwaa la kimataifa kutokana na shinikizo la serikali ya Marekani. Hali hii, mbali na kuzuia uhuru wa viongozi hao kushiriki kwenye majukwaa ya kisiasa ya kimataifa, pia imekuwa inakwamisha maendeleo ya nchi zao na hata kuziletea matatizo makubwa ya kiuchumi.



Mara nyingi nchi zinazoendelea zimekuwa zinalalamika kuwa nchi za magharibi zinatumia suala la vikwazo kama nyenzo ya kukwamisha maendeleo yao na kuzifanya ziendelee kuwa tegemezi kwa nchi za magharibi. Bahati mbaya ni kuwa kutokana na nguvu ya kiuchumi, kisiasa na hata kijeshi, malalamiko hayo yamekuwa yakipuuzwa na nchi hizo.



China kwa upande mwingine imekuwa ikisisitiza kuwa inaendesha sera yake ya mambo ya nje kwa kujitegemea, kwa hiyo vikwazo vinavyowekwa na nchi za magharibi dhidi ya nchi nyingine, kama havina idhini ya Umoja wa Mataifa basi haviizuii China kuwa na uhusiano na nchi hizo. Ziara za Rais Bashar Al Assad na Nicolas Maduro, ni mifano ya hivi karibuni tu ya China kuwa wazi kwa nchi yoyote rafiki kwake.



Hata hivyo ukweli utaendelea kubaki kuwa mfumo wa sasa wa kimataifa una dosari, kwani utaratibu wa kuwekwa vikwazo kwa upande mmoja bado upo na hakuna dalili kuwa utaondolewa hivi karibuni. Uzuri ni kama msemo wa waingereza unavyosema “when one door is closed, many more are open”, yaani mlango mmoja unapofungwa, kuna mingine mingi iko wazi.
 
Back
Top Bottom