Ziara ya Waziri Kabudi yazaa matunda. Ni dhahiri Tanzania ina uhusiano mzuri na mataifa ya nje

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Zile tetesi kuwa Tanzania ina mahusiano mabaya na nchi za magharibi zimeonekana sio za kweli. Maana ziara aliyofanya waziri kabudi imezaa matunda.

Ziara hii pia imechochea kuanza kwa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta toka Hoima Uganda hadi Tanga nchini Tanzania.

Mradi ambao utazalisha ajira 4700 na kulipatia taifa la Tanzania mapato makubwa yatayotokana na kusafirisha mafuta kupitia bomba hilo.

Pia kampuni ya Total itajenga viwanda vya kusafishia Petrol . Mbali na haya waziri kabudi alionana na jumuia ya wafanya biashara ya Ufaransa-Medef. Alikutana pia na wadau wa utalii ambao watakuja kuwekeza hapa nchini.

Hivyo ni wazi kuwa Taifa letu bado lina mahusiano mazuri ya kidiplomasia tofauti na walivyodai baadhi ya wadau wa siasa hapa nchini.
 
Unadhani kuwaita watu Mabeberu kila kukicha ni Diplomasia. Ukakasi wowote wa mahusiano unaotokea / utakaotokea ni kukosa hekima / busara kwa viongozi wenyewe.

Pia kumbuka kwenye mambo ya biashara ni Quid Pro Quo, hata ukiwatukana watu in the end kama they have more to gain (dollarwise) who cares, ila wale ambao bottom line sio kutengeneza faida bali walfare ya watu duniani (utawapoteza)
 
Taarifa hii kwa kina iko wapi?

Maana tunavyojua sisi 'vibaraka wa mabeberu' ni kuwa bomba ni mali ya uganda na kuwa tutakachohusika nacho sisi ni tozo ya kuyapitisha hayo mafuta ardhi ya tz kama tuwatozavyo Rwanda malori yao. Sasa mazungumzo yapi tena wakati Museveni ndo' mwenye mradi?
 
Zile tetesi kuwa Tanzania ina mahusiano mabaya na nchi za magharibi zimeonekana sio za kweli. Maana ziara aliyofanya waziri kabudi imezaa matunda.

Ziara hii pia imechochea kuanza kwa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta toka Hoima Uganda hadi Tanga nchini Tanzania.

Mradi ambao utazalisha ajira 4700 na kulipatia taifa la Tanzania mapato makubwa yatayotokana na kusafirisha mafuta kupitia bomba hilo.

Pia kampuni ya Total itajenga viwanda vya kusafishia Petrol . Mbali na haya waziri kabudi alionana na jumuia ya wafanya biashara ya Ufaransa-Medef. Alikutana pia na wadau wa utalii ambao watakuja kuwekeza hapa nchini.

Hivyo ni wazi kuwa Taifa letu bado lina mahusiano mazuri ya kidiplomasia tofauti na walivyodai baadhi ya wadau wa siasa hapa nchini.
Ulikuwepo kwenye hiyo ziara au kabudi kakuambia?

Sent from my vivo 1904 using JamiiForums mobile app
 
Taarifa hii kwa kina iko wapi?

Maana tunavyojua sisi 'vibaraka wa mabeberu' ni kuwa bomba ni mali ya uganda na kuwa tutakachohusika nacho sisi ni tozo ya kuyapitisha hayo mafuta ardhi ya tz kama tuwatozavyo Rwanda malori yao.. sasa mazungumzo yapi tena wakati Museveni ndo' mwenye mradi?
Ha ha ha ! Eti Kabudi kaenda kufuatilia bomba la Uganda
 
Taarifa hii kwa kina iko wapi?

Maana tunavyojua sisi 'vibaraka wa mabeberu' ni kuwa bomba ni mali ya uganda na kuwa tutakachohusika nacho sisi ni tozo ya kuyapitisha hayo mafuta ardhi ya tz kama tuwatozavyo Rwanda malori yao.. sasa mazungumzo yapi tena wakati Museveni ndo' mwenye mradi?
Ziara ya Waziri Kabudi imetia chachu mradi kuanza.
 
Back
Top Bottom