samora10
JF-Expert Member
- Jul 21, 2010
- 7,594
- 4,798
We jamaa bana.. Moshi wanajielewa.. Yani mpaka umpigie mtu kura ndio akuletee maendeleo? maendeleo yanaletwa na kodi yako sio kura yako!Na Thadei Ole Mushi.
Watu wa Kilimanjaro sio wajinga kiasi hicho, watamchagua Rais Magufuli kwa Kura nyingi Sana kuliko wagombea wengine wa uraisi. Twende sawa na agenda zetu....
1. Kilimanjaro ina makabila mawili makubwa, Wachaga na wapare. Kwa silka ya makabila haya yapo profit oriented. Makabila haya haswa wachaga ni opportunist in nature.
Kuwa opportunist sio kosa au kitu kibaya kwa Kiingereza wanaelezewa watu wenye tabia hiyo kuwa huwa kila fursa inayojitokeza mahali huwa inatumika effectively ( *Opportunists are people who see a chance to gain some advantage from a situation,an opportunist seizes every opportunity to improve things for himself* )
Ndio maana wanakuambia kuwa ukiona mahali hayupo mchaga ondoka hakuna fursa Wala fedha.
Mwaka 2015 kwa jinsi Hali ya Mambo yakivyokuwa waliona kabisa kuwa Edward Lowassa atakuwa Rais, wakaamua kuside nao ili mambo yao yaende. Baada ya Uchaguzi hawakuamini kilichotokea.
2020 wanajua wazi kuwa uelekeo upo wapi leo kuanzia Mwanga Hadi Moshi mjini km 80.7 watu walisimama na majani ya Masale Kumpokea Rais Magufuli akitokea Same mkoani Kilimanjaro alikofanya mkutano Jana.
Kitendo hicho kimemgusa Sana Rais Magufuli na kwenye hotuba yake amerudia zaidi ya Mara 20 kuwa hakuwahi kupata Mapokezi makubwa kiasi hiki popote na haswa Mkoa wa Kilimanjaro.
Jani la *Isale* Lina maana nyingi lakini maana kubwa zaidi hutumika kumpokea mtu mwenye heshima na kuomba msamaha kwa watu waliokoseana. Kiutamaduni wa Kabila letu ukiombwa msamaha na Jani Hilo huna budi kuutoa msamaha huo. Rais Magufuli kalizungumzia Jani Hilo Mkoani hapa Kilimanjaro. Na amesema amesameheana na watu wa Kilimanjaro kwa makosa waliofanyiana mwaka 2015.
2. *Win win situation* nimeielezea Sana. Mara nyingi Rais Magufuli anasema kwenye Kampeni zake nichague nikuletee maendeleo. Hili halifichi huwa analisema hadharani. Mkoa wa Kilimanjaro una agenda nyingi ambazo zinatakiwa ziende ambazo zimekuwa haziendi.
Tuna Mambo makubwa matatu ambayo bila kura za kutosha tutaweza kuchelewa Sana kuvipata. Moja Moshi kupata hadhi ya Jiji. Hakuna mtu asiyejua faida za Jiji. Kihistoria Moshi ni mojawapo ya miji mikongwe Sana, kutanguliwa na Miji mingine kuwa Jiji ni aibu kubwa. Moshi ina Vigezo vyote kuwa Jiji. Watu wa kupush hili ni Mbunge anayeweza kufanya lobbying. Ni Dhahiri tukitaka huu mji uwe Jiji hata Kesho kutwa ni kuichagua CCM tu.
Jambo la Pili kubwa lipo Jimbo la Vunjo ambalo wanahitaji Sana kuwa na Halmashauri yao. Rais Magufuli kalizungunzia hili Sana. Hapa panahitaji political will yaani maamuzi ya kisiasa. Vunjo ikipata Halmashauri itarahisisha kujiletea maendeleo kwa haraka sana. Mji Mdogo wa njia panda unakua kwa haraka sana Kama Vunjo ikifanikiwa kujinasua Moshi Vijijini itaharakisha sana maendeleo ya eneo hili.
Jambo la tatu Kuna issue ya Barabara ambazo kwa muda mrefu wabunge wa Upinzani wameshindwa kufanya lobbying ya kukamilishwa kwake. Barabara zote za Old Moshi, Barabara ya Mabogini ambayo ni Kero Sana eneo hilo. Rais Magufuli kaizungumzia Barabara hii. Nani anayeweza kupishana na bahati hii?
3. Mkoa wa Kilimanjaro niliwahi kusema umebeba Mzigo wa Misumari. Gunia lenyewe ni kuwa Jamvi la Wapinzani. Yaani Wapinzani wamekuwa wakitaka kwenda Bungeni lazima wapitie Kilimanjaro. Kwangu Mimi ninavyoona Upinzani umedumaza Sana maendeleo ya Kilimanjaro.
Kudumaza maendeleo sio kwamba maendeleo hayapo Bali yapo Ila yaliletwa na watu wengine na sio Wapinzani. Tulipo tumesimama hatuendelei mbele matokeo yake tunaanza kupitwa kimaendeleo. Mkoa wa Kilimanjaro haupaswi kuwa Kama ulivyo. Hata Rais Magufuli kasema Mkoa wa Kilimanjaro unajichelewesha wenyewe. Kwa nature ya Wapinzani wa Taifa hili si watu wa round table si watu wa kufanya Lobbying ni watu wa kupinga kila kitu. Mkoa wa Kilimanjaro mwaka huu watajitua gunia hili la Misumari libebwe Tena na Singida au Mbeya. Hatuhitaji wabunge wakupinga tu, tunahitaji wabunge wanaoweza kufanya lobbying ya kumfuata rais Ikulu na kumuomba maendeleo ya maeneo yetu.
Wabunge wetu wamekuwa wakitumia nafasi zao za kibunge kujenga mahekalu ya nyumba nyumbani kwao huku wananchi wakibakia kupanua vidole tu. We need to change this kwa miaka Mitano tu.
4. Pamoja na Mambo Mengine leo Jambo la kufurahisha zaidi ni Askofu Mkuu KKKT kutokea kwenye Uwanja Leo na kufanya Sala ya kuombea Taifa.
Askofu Mkuu wa KKKT Dr Fredrick Shoo ni mojawapo ya watu wenye influence Sana kisiasa Mkoa Kilimanjaro.
Dr Shoo kwa namna Moja au nyingine amekuwa ana misimamo mikali Sana kuhusu Siasa za Tanzania Ila Kitendo Cha yeye kuwepo Kwenye mkutano leo wachambuzi wa Mambo ya kisiasa wamelitafsiri tofauti Sana na ni kiashiria Cha Rais Magufuli kukubalika na Makundi yote hata wale wenye msimamo mkali.
Rias bado anaendelea na Mikutano Mkoani Kilimanjaro. Tuendelee kulijadili Mkoa wetu na mustakabali wa maendeleo yetu. Kwa kichaga Kuna msemo usemao Mangi akikutembelea ndio wakati wa kumueleza shida za eneo husika. Kilimanjaro na Magufuli....
Ole Mushi
0712702602