Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,117
- 16,506
Kwani huku kufunga ni imani ya mtu au ndio kulazimishana kutokula mchana? Hizi imani zingine za shuruti hizi...zipewe polisi wasimamie basi
Atakuuzia nani hicho chakula?Mm nipo huku 2 months sasa nataka nishuhudie hiyo kitu
Mm sipelekeshwi na hao vilaza.
Sijui nyerere aliwaza nn kufanya muungano na haa watu..
Zanzibar ni nchi ya kiislamu ile sema watu wa bara ndio tunaibana... 99% muslimsSERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) imetoa onyo kwa wananchi watakaokula hadharani katika kipindi cha mchana wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma, Khamis Juma Maalim wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua serikali inatoa tahadhari gani kwa watu watakaobainika kula mchana wakati wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Alisema utamaduni wa wananchi wa Zanzibar ni kuheshimu kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa makundi yote ikiwemo wa dini tofauti. Alifahamisha kwamba utamaduni huo upo hata kabla ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964 wa dini tofauti kuheshimu dini za watu wengine.
Alisema kazi ya kutoa elimu kuhusu ujio wa mwezi mtukufu wa Ramadhani imeanza kutolewa na Ofisi ya mufti ambayo ndiyo yenye jukumu la kushughulikia masuala ya mambo ya dini ya Kiislamu.
Alisema kazi kama hiyo imeanza kutolewa na maimamu wakuu wa misikiti mbalimbali Unguja na Pemba ikiwemo katika sala za Ijumaa ambazo hukusanya idadi kubwa ya Waislamu kwa wakati mmoja.
Alikiri kuwepo vijana wengi wanaoacha kufunga katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na kula hovyo pamoja na kuvuta sigara. Maalim alisema zipo taarifa kwamba hoteli nyingi hufanya kazi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo wateja wake wakubwa ni vijana wa Kiislamu. Waislamu nchini wanatazamiwa kuanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wiki ijayo ambapo ibada ya funga ni moja ya nguzo tano za dini ya Kiislamu
Chanzo: Habari Leo
=====================================
Nataka kujua kipindi kwa kwaresma mbona hawakutoa tamko hili.
Kwaio wakristo wawe wanajificha wakati wa chakula cha mchana.
Hapana naona kuna harufu ya udini kuanza Zanzibar.
Nanunua mwezi huu then natia storeAtakuuzia nani hicho chakula?
Sasa ukiwataka ugomvi wapemba.pika chakula chako alafu ukalie barazani.Nanunua mwezi huu then natia store
unaona au uhalisia huo😵😵😵
more than 90% ni Muslims
Sawa. Lakini hao 1% au 10% wana gaki ya ku practise dini yao vyovyote wanavyotaka. Kama wanakula majumbani mwao mabarazani shida iko wapi? That is bigotry! [emoji57] [emoji57] [emoji57] [emoji57]unaona au uhalisia huo😵😵😵
more than 90% ni Muslims
Dini haiendeshwi kwa akili za MTU, kwamba Mimi nafikiri Bali ni sharia IPO katika vitabu vitukufu sisi ni kufuata tu. Hakuna andiko linalosema hivyo unavyofikiri Bali lipo linalosema anapata dhambi anaekula mchana Wa Ramadhani au kulisha bila dharura. Yule anaekula hadharani pia anapata dhambi kwa kumfanyia karaha mfungaji.Mi nafikiri ukiwa umefunga halafu mwenzio anabutua pilau mbele yako na ukaweza kuvumilia ndo imani hiyo maana umeshinda majaribu! Sasa iweje ufunge halafu hutaki kuona mwenzio anakula, hayo ni mambo ya kulazimishana kufunga, maana itaanza taratibu hivyo kwamba isiwe hadharani baadae watatoa amri kwamba hakuna anayeruhusiwa kupika mchana wakati wa mwezi mtukufu, tujifunze 'tolerance'
Kila mwaka iko hivyo ni utamaduni wa wazanzibari. Na wageni wala hawashangai naona ni nyie mnaotaka kuanzisha chokochoko.Hizi ndizo dalili za serikali kuwa na dini.
Ni bora ikatangazwa kimataifa ili wageni wasijisumbue kwenda zanzibar !!!
Kilalaheri mkuu usisahau kuleta mrejesho tuNanunua mwezi huu then natia store