Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Status
Not open for further replies.
Hahahahaaaaa,nina mpango wa kufungua bucha ya kitimoto zanzibar maana nasikia biashara hiyo inalipa sana huko!Yaani mzigo haukai!
kafiri kupangishwa nyumba yenyewe ni kazi !
 
Huyo ni kafiri mwenzio japo hilo ni jina tukufu!

''Do not judge, or you too will be judged. For in the same way you judge others, you will be judged, and with the measure you use, it will be measured to you''
 
Mkuu umeeleza tu asili ya Mfungo au Ramadhani lakini hujaeleza maudhui ya mtu mwingine asiye muislamu kukatazwa kula hadharani.Kama ulivyoeleza vizuri kuwa maudhui ya ninyi kujifutarisha hadharani katika makundi ni njia mojawapo ya promotion ya Uislamu ndivyo naomba pia utueleze maudhui ya watu wengine wasiohusika na mfungo kukatazwa kula hadharani.
Wana uhuru wa kula ila wasile hadharani, kwa hadhara itapunguza shibe yao !?
 
Wewe unahitaji kula ukidhi njaa yako au unata kula hadharani !? ...ni wazi unataka kufanya karaha tu kwa wafungaji !

Kwa hiyo kumbe maudhui ya katazo la watu kujilia popote wanapoona inafaa ni kuepusha ninyi kuwa-disturbed na harufu ya Chakula? Kwa hiyo watu wazima wanaweza kupelekeshwa na Harufu za vyakula?
 
Sio 90% ndo waislam sema 99% ni waislam hizo amri zipo kabla ya Muungano lamsingi hao wenye itikadi nyingine wanatakiwa kutii tu.ni masiku machache lakini yana kheri nyingi sana na ndani yake kuna makumi matatu.
sawa mkuu kunguru nimekusoma
 
Sijaelewa ulichokisema hapa! Sababu ya kutoruhusiwa watu hao kula hadharani ni nini?
Mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwezi wa ibada ya kujuzuia kula mchana kwa waislaam, ingawa wapo waislaam walioruhusiwa kula bali nao wasile hadharani !
 
Kwa hiyo kumbe maudhui ya katazo la watu kujilia popote wanapoona inafaa ni kuepusha ninyi kuwa-disturbed na harufu ya Chakula? Kwa hiyo watu wazima wanaweza kupelekeshwa na Harufu za vyakula?
kwahiyo na wewe umepania kuihinikiza anga kwa harufu ya chakula !?
 
Zanzibar ni nchi ya waislam .unataka kipindi cha kwaresma wamtangazie nani?
Zanzibar ni nchi ya waislam .unataka kipindi cha kwaresma wamtangazie nani?
Kwa hiyo kwa akili yako hawa wachache hawatakiwi kulindwa na sheria? Mbona kwenye nchi zenye wakristo wengi haki za waislamu na minority wengine wanalindwa kwa sheria? Au ustaarabu upande huu hakuna?
 
Kama kuna sheria inayoruhusu watu wasile mchana mwezi mtukufu wa Ramadhani na ifanye kazi yake.Kama haipo hiyo sheria watu wale tu watakavyo,lakini ulaji wao usiwabugudhi wale waliofunga.
Mambo ya Amani ni vigumu sana kuyajadili kisiasa,vinginevyo sheria itamke kufanya hivyo.
 
Mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwezi wa ibada ya kujuzuia kula mchana kwa waislaam, ingawa wapo waislaam walioruhusiwa kula bali nao wasile hadharani !

Huwezi tu kuzuia jambo bila sababu maalamu.Tuambie watu wakila hadharani kuna athari gani?
 
Watu hawana imani za kushinda majaribu,kwamba akiona mtu mwingine anakula basi atamezea mate!Unatakiwa uyashinde majaribu na sio kukimbia!
Mtu mwenye imani hasa na ibada ya mfungo hawezi tetereka kwa kumuona mtu akila!
Kujilinda kote huko kwa kuzuia wengine wasiohusika na ibada hiyo kuishi kwa utaratibu wao wa kila siku ni ishara ya udhaifu wa kiimani!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom