Maswali ambayo nimekuwa nauliza na hakuna Mzanzibar aliyewahi kunijibu ni kuwa
1. Tanganyika itapoteza nini kwa Zanzibar kujitenga?
2. Kwanini Wazanzibar wasiondoke kwanza bara wakadai nchi yao wakiwa kwao?
3. Wazanzibar 400,000 wanafanya nini bara Vs Wabara 1000 walioko visiwani
4. Wazanzibar zaidi ya 50 wanafanya nini latika bunge la bara? mbona hawasusii bunge na kurudi kwenye baraza lao la uwakilishi.
5. Kwa uchumi wa bilioni 500, wabara wanafaidika nini kutoka Zanzibar? Hii ni sawa na bajeti ya wizara ya akina mama na watoto au mapato ya soko la kariakoo.
6. Zanzibar inachangia kiasi gani kuendesha serikali ya muungano.
Tujadiliane kwa haya