Zanzibar: Ole wao watakaouza vyakula mchana

Zanzibar: Ole wao watakaouza vyakula mchana

Status
Not open for further replies.

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,933
Reaction score
11,863
Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi imesema itawachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wenye migahawa wanaouza vyakula mchana kwani tayari imeshapiga marufuku uuzaji wa vyakula kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.



My take :
Pamoja na kwamba Zanzibar ni nchi yenye waislamu wengi lakini hawapaswi kunyanyasa wengine hasa kipindi hiki cha mfungo, Zanzibar wanaenda watu wengi wa imani tofauti kuzuia hawa wenye migahawa kufungua biashara zao kutawafanya wageni na wasio waislamu kukosa sehemu za kula, lakini pia kufunga ni hiari ya mtu, na kufunga ni pamoja na kujizuia hasa pale unapomuona mwenzako anakula.
 
Ulale pema swahiba wangu Korongo,nakumbuka 2004 tulienda Znz ilikua kipindi cha Ramadhan basi swahiba wangu bila uoga kakamata chupa ya maji baridiiii mtaani acha wa Znz waanzishe zogo bahati nzuri swahiba utata ndio maisha yake tukaishia polisi ila bado swahiba yuko na maji yake anayanywa mbele ya polisi.
Baada ya siku 2 tukatwangwa barua kubadilishiwa kituo cha kazi ghafla tu tukatudi zetu bara pande za Moro ila mara ya mwisho kurudi Znz nilikua mtiifu na kufuata tamaduni zao ili tusikwazane.
 
Mgonjwa muislam anakula nyumbani si ana ndugu zake? Mgeni anakula anapofikia iwe ndani ya hoteli,lodge au gesti. Kula kula ovyo hadharani kwa ZANZIBAR marufuku.Na hiyo inafahamika miaka yote watu hawajaanza mfungo mwezi huu.
Sasa migahawa yote ya gesti, lodge na hotel imepigwa marufuku kuuza vyakula mchana, au hujasoma hiyo habari? Na huko Zanzibar wapo raia ambao si waislam, sasa kwa nini imani yako wewe imtie kifungoni raia mwingine wa tz na huku tz ikiwa haina dini? Who do you think you are?
 
Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi imesema itawachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wenye migahawa wanaouza vyakula mchana kwani tayari imeshapiga marufuku uuzaji wa vyakula kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

My take :
Pamoja na kwamba Zanzibar ni nchi yenye waislamu wengi lakini hawapaswi kunyanyasa wengine hasa kipindi hiki cha mfungo, Zanzibar wanaenda watu wengi wa imani tofauti kuzuia hawa wenye migahawa kufungua biashara zao kutawafanya wageni na wasio waislamu kukosa sehemu za kula, lakini pia kufunga ni hiari ya mtu, na kufunga ni pamoja na kujizuia hasa pale unapomuona mwenzako anakula.
Ngoja tusubiri waraka wa KKKT
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom