Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Niko Zanzibar hali si shwari nimeamua kuachana na mikutano yangu na kurudi bara. Kila kona mabomu, pia maduka yamefungwa na vyakula naona ni ghali ghafla.
Muda huu naandika niko kwenye boti hakuna abiria na maduka yanafungwa .Ukaguzi ama upekuzi ni mkali hapa bandarini na boti hazina abiria si kutoka Dar kuja Unguja wala Unguja Dar.
Kila mtu analaani na matamshi yanaelekezwa kwa KAFU huku mitaani lakini kwenye sirikali wameamua ku deal na hawa wahuni kinamna.
Mahakama imewapa dhamana ila naambiwa wengi wameshindwa masharti na sasa kila kona mtaani kuna askari na njia zimezibwa na askari ni wa kumwaga.
Nimeona wanajeshi wa JWTZ mtaani na hata magareza wakiwa na silaha kwenye maeneo mengi ya makutano ya barabara nk.
Haya niko chomboni nakula maji sasa kuja bara .
Muda huu naandika niko kwenye boti hakuna abiria na maduka yanafungwa .Ukaguzi ama upekuzi ni mkali hapa bandarini na boti hazina abiria si kutoka Dar kuja Unguja wala Unguja Dar.
Kila mtu analaani na matamshi yanaelekezwa kwa KAFU huku mitaani lakini kwenye sirikali wameamua ku deal na hawa wahuni kinamna.
Mahakama imewapa dhamana ila naambiwa wengi wameshindwa masharti na sasa kila kona mtaani kuna askari na njia zimezibwa na askari ni wa kumwaga.
Nimeona wanajeshi wa JWTZ mtaani na hata magareza wakiwa na silaha kwenye maeneo mengi ya makutano ya barabara nk.
Haya niko chomboni nakula maji sasa kuja bara .