Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

JokaKuu,

Nimekusoma,khabar za siku tele ndugu yangu.

Binafsi nisingalipenda kuchambua kwa kina hapa,maana ni kweli usemavyo yakuwa haya majambo yameshajadaliwa mno humu Jf,tena kwa nyakati mbalimbali bila ya kupata usuluhishi/ufumbuzi!?


Hata hivyo nimependa yakuwa kama dasturi yako,unajitahidi mno kutumia lugha ya kiungwana.

Kuhusu huo mfano wako kiduchu ulotoa hapo mwisho wa hiyo bayana yako;ati Zanzibar imejifaragua kuongeza majimbo ya uchaguzi ili "ifanane" na Tanganyika/Bara!? Yaani imenilazim kucheka kiduchu....

Kwani hiyo population ya Zanzibar kwa sehemu mbalimbali visiwani mle ndo ile ile tangia ile 1964!?...haijawahi kuongezeka japo kiduchu!?

Sasa kama kuna mabadiliko/ongezeke la population kwenye maeneo/majimbo mbalimbali visiwani humo,sasa huoni yakuwa hali hiyo ndo ilofanza wao kukidhi haja ya kuongezeka kwa majimbo ya uchaguzi,badala tu ya kudai ati wamefanza/wanafanza hivyo kwa kutaka "kujifananisha" na hiyo Tanganyika!?

Nimefurahika
tumezungumza japo kiduchu,nami tajitahidi kufuatilia huu mnakasha kwa utuvu.

Ahsanta.
gombesugu,

..niwie radhi kwa uchechefu wangu.

..naomba niweke wazi kwamba sikuwa na nia ya kuwafunjia heshma wa-Znz ktk bandiko langu la mwanzo.

..nakubaliana na wewe kwamba population ya Znz imeongezeka tangu tuingie ktk muungano.

..lakini sidhani kama hiyo ni justification ya kuwa na wanasiasa[wawakilishi na wabunge] wengi kiasi tunachoona sasa hivi.

..pia sidhani kama ongezeko hilo la wawakilishi na wabunge ni kwa ajili ya kukidhi matakwa na mahitaji ya wananchi, bali ni kwa ajili ya kukidhi matakwa ya MUUNGANO.

..kwa mtizamo wangu huu "utitiri" wa wanasiasa[wawakilishi na wabunge] ni mzigo wa gharama kwa wananchi wa Znz. sasa ili muutue mzigo huo inabidi mtoke ktk muungano, na muunde serikali ndogo, inayosimamiwa na baraza la wawakilishi dogo kuliko hili lililoko sasa hivi.
 
Last edited by a moderator:
He he hee! Misaada!


Je umewahi kupitia bajeti yoyote ya Tanganyika au Tanzania ukaona inajitosheleza? Bila kutegemea misaada na mikopo kutoka nje?

Skuli muhimu sana ahali yangu hususan unapotaka kuzungumzia mas'ala ya kiuchumi.

Pole sana.
 
labda nikuulize Je huo mvungano wenu mtachangia kwa ratio ya watu, eneo au madaraka.

Je kwa Uoni wako Znz wanaweza shindwa wapi kama itaachwa huru kiuchumi na maamuzi?

Kumbuka kuwa Mvungano ni kama KOTI. kama utaona linakubana au kukutia joto si unalivua tu. Je kuna ubaya hapo?

sasa Povu zote za nini kuleta mitazamo ya kisiasa katika mambo ya kiuchumi hususan kwa Znz?

Pole sana

Barubaru,

..muungano kati ya Tgk na Znz ni impossible kutokana na tofauti ya ukubwa wa eneo na idadi ya watu baina ya mataifa yetu.

..tofauti baina ya Tgk na Znz ni kubwa mno kiasi kwamba siku zote kutakuwa na malalamiko baina yetu.

..Znz ikitumia vizuri rasilimali zake, pamoja na kuwa na mahusiano mazuri ya kiuchumi na majirani zake, inaweza kabisa kusimama yenyewe nje ya muungano.
 
Last edited by a moderator:
Si kweli, hakuna mzanzibar anayethubutu kudai nchi yake.
Wote wanaongea chumbani na uvunguni mwa vitanda, tena wanabweka wakiwa na wamefunga taulo mbela ya ahali zao. Wakitoka nje kimyaa! nitakueleza

1. Tuliwaambia kura ya maoni kuhusu mustakabali wa znz, mkagoma na kujiminya minya
2. Tukaawambia acheni msishiriki tume ya Warioba, mkudai wajumbe sawa hata kama hamjui wanalipwa na nani
3. Tukawaambia nyote mkatae serikali 1.2.3 kilichofuata ni muungano wa mkataba.
Mkagoma kuchomoa mnataka kujificha na kusetiri dhiki zenu kwa mgongo wa mkataba
4. Tukawaambia msichague wajumbe wa bunge la katiba, akili zenu zikwatuma mdai wajumbe zaidi
5. Juzi Wajumbe wa BLW walikuwa Dodoma wanakula msasa na posho, hawakugoma kuja.

Hakuna mzanzibar mwenye nyodo ya kukataa muungano. Tumeshathibitisha na tunasema wazi hakuna!
Ninyi mkae kimya tu mpate mafaio ya sasa na uzeeni. Mnapata mafao kuanzia mnasoma bura hadi kazi na uzeeni. Hakuna anayedai nchi, ni wapiga kelele tu wamejaa

Nguruvi3.

Hapo ndio ninapoona mnajidanganya.

Ni wapi na lini mliwaambia wazanzibar hayo unayonena. Mliwaambia katika chombo gani rasmi cha habari au ndani ya Bunge au mdaharo gani wa wazi au hata katika Gazeti gani? naomba utufafanulie hapo.


Lakin pia kumbuka nchi yenu badi ni tegemezi na mara nyingi sana kunakuwa na njaa maeneo mbalimbali mpaka kufikia watu kula mizizi na hata wanyama kufa kwa njaa na ukame. Je umewahi kusikia Znz watu wanakufa njaa? Kwanini msiwatosheleze watu wenu kabla kuwapa jirani zenu Znz? Je ni akili hiyo?

Lakin kwanini muwaambie Znz wafanye na NYINYI MNAOGOPA NINI KUFANYA? Au ndo mnaogopa vivuli vyenu na fadhwila mnazopata kutokana na kuidhulumu Znz?

Lakin kwa kudhibitisha kuwa mna walakin. hebu fikiria Tanganyika ni ji nchi likuuumba kwenda kuungana na Znz yenye ukubwa wa idadi ya watu sawa na wilaya ya Ilala , tena muungano wa pasu kwa pasu. Je ni akili hiyo?

Mimi naona ni dhambi tu ya kunung'unika inawasumbua wakti wanzenu Znz wanalalamika mchana kweupeeee bila kumwogopa mtu wala nini.

Poleni sana .

 
hahahaaaaa huu uzi nimeupenda sana. Binafsi nilishaliwaza hilo siku nyingi baada ya rasimu ya katiba kutolewa. kama hawana uwezo kuna haja gani ya kuwa na malalamiko kila siku kumbe hata kusimama kwa miguu yao tuu ni shida. hao wapewe option mbili tuu tuwe na serikali tatu ambayo watatakiwa kuchangia uendeshaji wa serikli ya muungano au kuwe na serikali moja tuu toka kigoma mpaka mtwara hadi pemba.
 
Barubaru,

..muungano kati ya Tgk na Znz ni impossible kutokana na tofauti ya ukubwa wa eneo na idadi ya watu baina ya mataifa yetu.

..tofauti baina ya Tgk na Znz ni kubwa mno kiasi kwamba siku zote kutakuwa na malalamiko baina yetu.

..Znz ikitumia vizuri rasilimali zake, pamoja na kuwa na mahusiano mazuri ya kiuchumi na majirani zake, inaweza kabisa kusimama yenyewe nje ya muungano.

Joka Kuu.

Mimi kama mtaalamu wa uchumi nasema Znz nje ya Muungano uchumi wake utakuwa kwa kasi sana na haya nilipambanua vizuri sana katika Uzi wa NINI FAIDA YA MUUNGANO KWA ZNZ.

Na kwa mtu yoyote mwenye akili timamu kabisa hawezi kukubali nchi yenye watu zaidi ya 45 Milioni ikaungane PASU KWA PASU na nchi yenye watu Milioni moja na nusu. Je inaingia akilini kweli?

Tena kwa muungano ambao ni HARAMU usiofata sharia za kimataifa ya kuunganisha nchi huru mbili huku nchi kubwa ikilazimisha huo Muungano. Je huoni kama Tanganyika kuna vitu wananufaika hapo? na manufaiko hayo kwa kutumia hiyo nchi ndogo yanafikiwa mpaka kuvimbiwa na kutaka kuifanya kama koloni lao.

ndio hao wanaoleta propaganda za kisiasa kusema Znz haiwezi simama pekee yake bila kutoa sababu za kiuchumi bali kuleta porojo za uzandiki pasi na kujua kuwa UCHUMI sio porojo ni taaluma inayojitosheleza

Free Znz.

 
Nguruvi3.

Hapo ndio ninapoona mnajidanganya.

Ni wapi na lini mliwaambia wazanzibar hayo unayonena. Mliwaambia katika chombo gani rasmi cha habari au ndani ya Bunge au mdaharo gani wa wazi au hata katika Gazeti gani? naomba utufafanulie hapo.


Lakin pia kumbuka nchi yenu badi ni tegemezi na mara nyingi sana kunakuwa na njaa maeneo mbalimbali mpaka kufikia watu kula mizizi na hata wanyama kufa kwa njaa na ukame. Je umewahi kusikia Znz watu wanakufa njaa? Kwanini msiwatosheleze watu wenu kabla kuwapa jirani zenu Znz? Je ni akili hiyo?

Lakin kwanini muwaambie Znz wafanye na NYINYI MNAOGOPA NINI KUFANYA? Au ndo mnaogopa vivuli vyenu na fadhwila mnazopata kutokana na kuidhulumu Znz?

Lakin kwa kudhibitisha kuwa mna walakin. hebu fikiria Tanganyika ni ji nchi likuuumba kwenda kuungana na Znz yenye ukubwa wa idadi ya watu sawa na wilaya ya Ilala , tena muungano wa pasu kwa pasu. Je ni akili hiyo?

Mimi naona ni dhambi tu ya kunung'unika inawasumbua wakti wanzenu Znz wanalalamika mchana kweupeeee bila kumwogopa mtu wala nini.Poleni sana .
Tumewaambia katika midahalo makaongamano n.k. Hata maneno ya mwenyekiti wa kamati ya fedha yametoka maeneo kama JF, unajua amebeba kila kitu tulichosema. Unataka tuvute uzi kwa ushahidi?

Kuhusu njaa, ndugu yangu nenda Pemba na Unguja uone. Lakini hilo si muhimu sana kwasababu njaa ipo kila mahali duniani.

Hakuna pasi pasu kaika muungano uliopo. Kilichpo ni sisi kubeba watu milioni 1. Labda unifahamishe hiyo pasu pasu ni kwa jambo gani. Hakuna kitu kama hicho, kilichopo ni kubebwa mgongoni hata mwenyekiti wa kamati ya fedha amesema.
Hivi unawezaje kuwa na pasu pasu ukiwa na mshirika asiyeweza hata kupia umeme.

Mwenyekiti wa kamati ya fedha kasema hamjawahi kutoa chochote kwa miaka 50 kwasababu ya uchumi. Kasema mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLW wakiwemo waliberali. Sasa kuna pasu pasu gani.

Tume ya warioba hamjui inagharamiwa na nani, pasu ipo wapi. Gharama za bunge la katiba ni zaidi ya bilioni 200. Pasu itoke wapi

Tunasema hivi kama mkija katika bunge la katiba mkubali yaishe.Kaa kimya hakuna kelele
BLW wakiwemo waliberali juzi walikuwa Dodoma raha mstarehe, hakuna aliyesimama na kudai znz! wamechukua posho wanaishia! wakiwa baharini wakali kweli kweli wakishatua Tanganyika kimyaa. Jusa alikuwepo pia.
 
Mkuu Ngongo
Hao wanajinadi ni waongo Zanzibar haina uwezo huo muungano ni lulu; Barubaru sio mtanzania ni mtu Oman anaishi Qatar mambo ya muungano hayamuuhusu!


Yana nikhusu sana kumbuka Kitovu changu nilipozaliwa kilizikwa kule Kyanga, Mwera.

Itakuuma sana lakin ukweli laazima tutasema. Na waZnz wamestuka huo unyonyaji wanaofanyiwa na majirani zao.

Pole san
a
 
Joka Kuu.

Mimi kama mtaalamu wa uchumi nasema Znz nje ya Muungano uchumi wake utakuwa kwa kasi sana na haya nilipambanua vizuri sana katika Uzi wa NINI FAIDA YA MUUNGANO KWA ZNZ.

Na kwa mtu yoyote mwenye akili timamu kabisa hawezi kukubali nchi yenye watu zaidi ya 45 Milioni ikaungane PASU KWA PASU na nchi yenye watu Milioni moja na nusu. Je inaingia akilini kweli?

Tena kwa muungano ambao ni HARAMU usiofata sharia za kimataifa ya kuunganisha nchi huru mbili huku nchi kubwa ikilazimisha huo Muungano. Je huoni kama Tanganyika kuna vitu wananufaika hapo? na manufaiko hayo kwa kutumia hiyo nchi ndogo yanafikiwa mpaka kuvimbiwa na kutaka kuifanya kama koloni lao.

ndio hao wanaoleta propaganda za kisiasa kusema Znz haiwezi simama pekee yake bila kutoa sababu za kiuchumi bali kuleta porojo za uzandiki pasi na kujua kuwa UCHUMI sio porojo ni taaluma inayojitosheleza

Free Znz.

Wenzako walikuwa Dodoma juzi hawakusema hayo, walichukua posho wakapanda meli.
Tunataka mpate znz yenye neema ili muendelee zaidi ndio maana tunasema susieni bunge la katiba ili mambo yaishe.
Mkija tu mumekubali kila kitu.

Nendenei mkajenge Dubai yenu hakuna wa kuwazuia tena tunawatakiwa heri muwe kama Luxenbourd au Emirate.
Hakuna anayewakatalia hilo, lakini basi onyesheni nia. Siyo kelele na posho.
Kung'ang'ania vyeo na ajira bila kujua zinatengenezwaje ni ukupe.

Miaka 50 mgongoni tumechoka, tuacheni tupumue
 
Tumewaambia katika midahalo makaongamano n.k. Hata maneno ya mwenyekiti wa kamati ya fedha yametoka maeneo kama JF, unajua amebeba kila kitu tulichosema. Unataka tuvute uzi kwa ushahidi?

Kuhusu njaa, ndugu yangu nenda Pemba na Unguja uone. Lakini hilo si muhimu sana kwasababu njaa ipo kila mahali duniani.

Hakuna pasi pasu kaika muungano uliopo. Kilichpo ni sisi kubeba watu milioni 1. Labda unifahamishe hiyo pasu pasu ni kwa jambo gani. Hakuna kitu kama hicho, kilichopo ni kubebwa mgongoni hata mwenyekiti wa kamati ya fedha amesema.
Hivi unawezaje kuwa na pasu pasu ukiwa na mshirika asiyeweza hata kupia umeme.

Mwenyekiti wa kamati ya fedha kasema hamjawahi kutoa chochote kwa miaka 50 kwasababu ya uchumi. Kasema mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLW wakiwemo waliberali. Sasa kuna pasu pasu gani.

Tume ya warioba hamjui inagharamiwa na nani, pasu ipo wapi. Gharama za bunge la katiba ni zaidi ya bilioni 200. Pasu itoke wapi

Tunasema hivi kama mkija katika bunge la katiba mkubali yaishe.Kaa kimya hakuna kelele
BLW wakiwemo waliberali juzi walikuwa Dodoma raha mstarehe, hakuna aliyesimama na kudai znz! wamechukua posho wanaishia! wakiwa baharini wakali kweli kweli wakishatua Tanganyika kimyaa. Jusa alikuwepo pia.

Nguruvi3.

sasa tujaalie unachosema ni kweli.

sasa kwanini hamuwatosi waZnz kama mnaona wanawanyonya na kila wakti wakilalamika kudai mafao zaidi?

Je kuna Siri gani hapo kwa Tanganyika?

Mbona hiyo hiyo Tanganyika tena chini ya Nyerere huyo mmoja wa waasisi wa mvungano wenu aliweza kutumia mbinu zote na kuhakikisha anavunja EAC na kwanini mnashindwa huo mvungano na Znz?

Je mpo sawa kweli kichwani? mbona mnapita na kunung'unika kila pahala badala ya kuchukua maamuzi magumu?

 
Joka Kuu.

Mimi kama mtaalamu wa uchumi nasema Znz nje ya Muungano uchumi wake utakuwa kwa kasi sana na haya nilipambanua vizuri sana katika Uzi wa NINI FAIDA YA MUUNGANO KWA ZNZ.

Na kwa mtu yoyote mwenye akili timamu kabisa hawezi kukubali nchi yenye watu zaidi ya 45 Milioni ikaungane PASU KWA PASU na nchi yenye watu Milioni moja na nusu. Je inaingia akilini kweli?

Tena kwa muungano ambao ni HARAMU usiofata sharia za kimataifa ya kuunganisha nchi huru mbili huku nchi kubwa ikilazimisha huo Muungano. Je huoni kama Tanganyika kuna vitu wananufaika hapo? na manufaiko hayo kwa kutumia hiyo nchi ndogo yanafikiwa mpaka kuvimbiwa na kutaka kuifanya kama koloni lao.

ndio hao wanaoleta propaganda za kisiasa kusema Znz haiwezi simama pekee yake bila kutoa sababu za kiuchumi bali kuleta porojo za uzandiki pasi na kujua kuwa UCHUMI sio porojo ni taaluma inayojitosheleza

Free Znz.

Barubaru,

..nakubaliana na wewe 100% kwamba uchumi wa Znz unaweza kupaa.

..lakini hilo litategemea kama mtajipanga vyema na kutumia rasilimali zenu vizuri.

..pamoja na hayo,nasimama ktk hoja yangu kwamba muungano hauwezekani kutokana na tofauti kubwa ya kieneo na population baina ya Tanganyika na Zanzibar.

NB:

..Mwakilishi hajasema kwamba Znz haiwezi kusimama peke yake na kupaa kiuchumi, bali amesema Znz haina uwezo wa kuchangia 50/50 masuala ya muungano. He also defended his views with data.

cc gombesugu, Nguruvi3
 
Yana nikhusu sana kumbuka Kitovu changu nilipozaliwa kilizikwa kule Kyanga, Mwera.

Itakuuma sana lakin ukweli laazima tutasema. Na waZnz wamestuka huo unyonyaji wanaofanyiwa na majirani zao.

Pole san
a
wa mapato ya bilioni 240! kidogo kuliko ya manispaa ya Ilala.
Kusomeshwa watoto bure ndio kunyonywa. Kulala usingizi na kuwasha taa hadi asubuhi bila bili ndio unnyonyaji
Kusubiri mishahara ya hazina ndio unyonyaji

Kwa bilioni 240 nani akanyonye. Hata TBL wana mapato makubwa zaidi ya hayo nani akanyonye ndama
 
Wenzako walikuwa Dodoma juzi hawakusema hayo, walichukua posho wakapanda meli.
Tunataka mpate znz yenye neema ili muendelee zaidi ndio maana tunasema susieni bunge la katiba ili mambo yaishe.
Mkija tu mumekubali kila kitu.

Nendenei mkajenge Dubai yenu hakuna wa kuwazuia tena tunawatakiwa heri muwe kama Luxenbourd au Emirate.
Hakuna anayewakatalia hilo, lakini basi onyesheni nia. Siyo kelele na posho.
Kung'ang'ania vyeo na ajira bila kujua zinatengenezwaje ni ukupe.

Miaka 50 mgongoni tumechoka, tuacheni tupumue

Nguruvi3.

Ndio maana siku zote nasema Tanganyika ni nchi ya watu wa KUNUNG"UNIKA. Na kumbuka hakuna dhambi mbaya kuliko dhambi ya Kunung'unika na hiyo ndio inayowatafuna.

Znz wao wa kulalamika tena wanalalamika mchana kweupee kila mtu anasikia.

Kumbuka nyie ndio wenye MPINI kwa maana JESHI, POLISI, Zana zote za kivita na maamuzi sasa mnacho khofia ni nini kuvunja muungano mpaka muwasubiri Znz ambayo haina jeshi wala polisi?

Kwani msiwatose wa Znz mkawa huru kujenga vatican yenu kwa utulivu zaidi?

Je mpo sawa kweli nyie au ndo yale yale kunung'unika na kuogopa vivuli vyenu wenyewe?

Poleni sana.

 
Barubaru,

..nakubaliana na wewe 100% kwamba uchumi wa Znz unaweza kupaa.

..lakini hilo litategemea kama mtajipanga vyema na kutumia rasilimali zenu vizuri.

..pamoja nasimama ktk hoja yangu kwamba muungano hauwezekani kutokana na tofauti kubwa ya kieneo na population baina ya Tanganyika na Zanzibar.

NB:

..Mwakilishi hajasema kwamba Znz haiwezi kusimama peke yake na kupaa kiuchumi, bali amesema Znz haina uwezo wa kuchangia 50/50 masuala ya muungano. He also defended his views with data.

cc gombesugu, Nguruvi3
Na sisi tunasema tunawatakia heri wakapae na uchumi wao.
Tusichokitaka ni kelele za uongo. Mwenyekiti kasema katika serikali 3 hawawezi kuchangia hata asilimia 10. Maana yake ni kuwa zigo hilo alibebe Mtanganyika, haina shida kwasababu tumebeba miaka 50. Shida ni pale wenzetu wanapokaa katika mikutano ya mabara ya taasisi zao kama BAKUZA, UAMSHO, BAZAZI n.k. wakipanga nafasi za uwaziri na vyeo, ajira na fursa sawa. Hakuna hata siku moja utwasikia wakitoa hesababu. Sasa kama huwezi kuchangia unapata wapi ushujaa wa kutaka vyeo na ajira.

Mfano, eti rais wa muungano awe kwa zamu. Kwamba, rais anayetoka walikochangia 0 awe na kauli kwa mali za watu.
Mawaziri na ajira sawa kwasababu ni nchi mbili, tukiweka hesabu za malipo yao wenzetu wanakimbia wanasema sisi wadogo, sisi wachache n.k. Sawa kama ni wachache hoja ya nchi mbili sawa inatoka wapi?

Akili za wznz ni katika vyeo na ajira baasi, hakuna kingine cha ziada. Ndio matunda ya kubebwa kila siku mtu anadhani ana haki ya kukaa mgongoni. Miaka 50 inatosha tumechoka

Tuacheni tupumue
 
wa mapato ya bilioni 240! kidogo kuliko ya manispaa ya Ilala.
Kusomeshwa watoto bure ndio kunyonywa. Kulala usingizi na kuwasha taa hadi asubuhi bila bili ndio unnyonyaji
Kusubiri mishahara ya hazina ndio unyonyaji

Kwa bilioni 240 nani akanyonye. Hata TBL wana mapato makubwa zaidi ya hayo nani akanyonye ndama

Hapo ndipo ninapokushangaa. kama yote hayo ni kweli KWANINI HAMVUNJI MUUNGANO? pasi na shaka kuna mengi ya faida mnapata kutokana na kuwa Znz.

Mbona kwenye EAC mpo makini sana katika mas'ala ya Ardhwi, Ajira na mengine. sasa kwanini msiyaangalie hayo pia kwa Znz ili mvunje kwa amani mbaki kama majirani?

Acha kunung'unika CHUKUA MAAMUZI MAGUMU kwani huna udugu wa kuzaliwa na Znz. Kila mtu abebe msalaba wake kwanini wewe umbebee Znz? Je mpo wasa kweli nyie? au ndo yale yale kunung'unika ndio jadi yenu.

 
Barubaru,

..muungano kati ya Tgk na Znz ni impossible kutokana na tofauti ya ukubwa wa eneo na idadi ya watu baina ya mataifa yetu.

..tofauti baina ya Tgk na Znz ni kubwa mno kiasi kwamba siku zote kutakuwa na malalamiko baina yetu.

..Znz ikitumia vizuri rasilimali zake, pamoja na kuwa na mahusiano mazuri ya kiuchumi na majirani zake, inaweza kabisa kusimama yenyewe nje ya muungano.
Inaweza kabisa kusimama hakuna shaka. Ni nchi iliyokuwepo hakuna shaka juu ya hilo.
Kinachokataliwa hapa ni wao kuwalaumu Watanganyika kwa kuwanyonya ili hali wao wametumbukiza mirija yao wanafyonza tu. Hawana mtima wa aibu au haya. Nani akaibe 240 bilioni!
Ndio maana tunasema wao wakazane nasi tutawasiaida waondoke katika dhiki ya muungano.

LAKINI kama wanakuja kuchukua posho na kupiga kelele wakiwa baharini huo ni ufisadi.
BLW juzi wlaikuwa Dodoma na Jusa alikuwepo, kimyaa! subiri warudi minazini usikie matusi yao.

Nendeni mkaijenge znz ya Dubai hakuna anayewakataza, tusichotaka kusikia ni Tanganyika kunyonya ndama asisye na kiwele! uongo sasa basi tafuteni suluhu ya matatizo yenu si Tanganyika.

Juzi tumejua ZECO wamefisadi mapesa ya umeme lakini bill analipa Mtanganyika, halafu matusi anapokea Mtanganyika.
 
Na sisi tunasema tunawatakia heri wakapae na uchumi wao.
Tusichokitaka ni kelele za uongo. Mwenyekiti kasema katika serikali 3 hawawezi kuchangia hata asilimia 10. Maana yake ni kuwa zigo hilo alibebe Mtanganyika, haina shida kwasababu tumebeba miaka 50. Shida ni pale wenzetu wanapokaa katika mikutano ya mabara ya taasisi zao kama BAKUZA, UAMSHO, BAZAZI n.k. wakipanga nafasi za uwaziri na vyeo, ajira na fursa sawa. Hakuna hata siku moja utwasikia wakitoa hesababu. Sasa kama huwezi kuchangia unapata wapi ushujaa wa kutaka vyeo na ajira.

Mfano, eti rais wa muungano awe kwa zamu. Kwamba, rais anayetoka walikochangia 0 awe na kauli kwa mali za watu.
Mawaziri na ajira sawa kwasababu ni nchi mbili, tukiweka hesabu za malipo yao wenzetu wanakimbia wanasema sisi wadogo, sisi wachache n.k. Sawa kama ni wachache hoja ya nchi mbili sawa inatoka wapi?

Akili za wznz ni katika vyeo na ajira baasi, hakuna kingine cha ziada. Ndio matunda ya kubebwa kila siku mtu anadhani ana haki ya kukaa mgongoni. Miaka 50 inatosha tumechoka

Tuacheni tupumue

Nguruvi3

Kisebusebu na kiroho papo.

Utanung'unika huku unaumia tu na Znz wanafaidi kupitia mgongo wako. CHUKUA MAAMUZI MAGUMU KUVUNHJA MUUNGANO.
 
Tatizo tunakua na viongozi ambao ni kama vile hawana exposure. Hiyo ya kila serikali (yani ya Tanganyika na Zanzibar) kuchangia serikali kuu ni mfumo mmoja tu. Mfumo mwingine ni ule wa Marekani ambapo majimbo ya Marekani haya "changii" bajeti ya serikali kuu bali serikali kuu ina mamlaka ya kutoza kodi zake na serikali za majimbo zina mamlaka ya kutoza kodi zake.

Tukichukulia mfano wa Marekani ina maana serikali ya muungano itaweza kutoza kodi ya kujiendesha kama inavyo jiendesha sasa na serikali ya Tanganyika kuwa na mamlaka ya kuwa toza kodi wakazi wa Tanganyika (nasisitiza wakazi sio lazima "raia") na serikali ya Zanzibar kuwa na mamlaka ya kutoza kodi wakazi wa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom