Boko haram
JF-Expert Member
- Nov 7, 2011
- 3,256
- 1,232
Nguruvi3,
punguza zogo jamvini japo kiduchu...kwani vipi msimamo wa Chadema kuhusu stakabali ya "Muungano"!?
....Teh! Teh!
Ahsanta.
Al akhy hapo pagumu na hata akijibu atajibu nyuma ya pazia!
Nguruvi3,
punguza zogo jamvini japo kiduchu...kwani vipi msimamo wa Chadema kuhusu stakabali ya "Muungano"!?
....Teh! Teh!
Ahsanta.
Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara
Na Sharon Sauwa, Mwananchi
Posted Jumanne,Novemba12 2013 saa 24:0 AM
KWA UFUPI
Inadaiwa haina mapato kujiendesha na kuchangia Muungano kama Srikali tatu zitapitishwa Katiba Mpya
Dodoma.Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Fedha na Uchumi ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Salimin Awadhi Salimin amesema Zanzibar haitakuwa na uwezo wa kuchangia uendeshaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kama muundo wake utakuwa wa Serikali Tatu.
Amesema Zanzibar haiwezi kuchangia hata kwa asilimia 10, hivyo kuukubali mfumo huo kunauweka Muungano katika hatihati ya kuvunjika. Katika utekelezaji wa utaratibu huo, Tanzania Bara na Zanzibar kila moja inatakiwa kuchangia asilimia 50 ya gharama za uendeshaji wa shughuli za Serikali ya Muungano.
Akizungumza katika semina ya Wabunge wa Muungano na Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar mjini Dodoma jana, Salimin alisema hali hiyo inatokana na udogo wa uchumi wa Zanzibar na kusisitiza kuwa mfumo wa sasa wa serikali mbili ndiyo unafaa.
Rasimu ya kwanza iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Julai mwaka huu ilikuwa inapendekeza kuundwa kwa Serikali Tatu; za Muungano, Tanzania Bara na ile ya Zanzibar.
Alisema wakati wa kujadili mfumo huo ni lazima kuangalia suala la kiuchumi katika Serikali mbili zilizopo, iwapo zina uwezo wa kugharimia uendeshaji wa Serikali ya Muungano.
Tunapokuwa na Serikali ya Tanganyika, tunapokuwa na Serikali ya Zanzibar, tunapokuwa na Serikali ya Muungano kwa vyovyote vile matumizi yatakuwa makubwa mno, alisema Salimin katika semina hiyo iliyoandaliwa
na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), kujadili Rasimu ya Katibu Mpya.
Alisema Serikali ya Muungano itatakiwa kuhudumiwa kwa mapato yanayotoka katika Serikali mbili zinazounda Muungano, jambo ambalo Serikali ya Zanzibar haiwezi.
Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya Zanzibar, nauangalia uchumi wangu wa mapato ya kila mwaka. Je, tunaweza kuchangia hata asilimia 10? alihoji.
Alisema mapato ya Zanzibar kwa mwaka 2013/2014 ni Sh240 bilioni tu na kutoa mfano wa Wizara za Mambo ya Ndani na ile ya Ulinzi ambazo ziko chini ya Muungano kuwa bajeti yake ni kiasi cha Sh1.3 trilioni kwa mwaka wa fedha wa 2013/14.
Alisema amepiga hesabu na kugundua kuwa gharama ya kuendesha wizara zote za Muungano inakadiriwa kuwa Sh3 trilioni.
Kama Sh3 trilioni zitahitajika katika kuendesha Serikali ya Muungano, sisi Zanzibar tukiambiwa tuchangie hata asilimia 10 tu ambayo ni sawa na Sh300 bilioni tutaweza? alihoji Salimin.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Tunaoiombea sana bendera hiyo na wimbo wa taifa. Tunawaombea mema sana. Tanganyika haina maumivu yooyote kwasababu haihitaji znz. Labda utueleze maumivu hayo ni yapi kama unayo japo moja.Tunaelewa Tanganyika inaumia sana zanzibar kudai mamlaka yake ndio mana mumechanganyikiwa kila mara munatumwa kuleta hii thread., kwa ufupi zanzibar ikawa na uwezo isiwe na uwezo sasaiv Wazanzibar wameamka, Zanzibar ya sasa siyo ile ya zamani na sasaiv Wazanzibari mpaka wahakikishe bendera yao ya zanzibar inapepea UN., pa pa pa pa.!,
@JokaKuu , hizo balozi na mambo mengine yote yanalipiwa na Tanganyika.
Utashangaa sana eti wanasema nafasi za ubalozi ziwe sawa. Hawa hawajui gharama wanajua vyeo na ajira baasi. Sheni kasema hilo wazi kama rais sasa wachumi uchwara wanataka tuamini 240 ndizo Tanganyika inazinyonya.
Kuhusu jeshi, hilo halimo katika bajeti ya SMZ tangu mwaka 1964.
Hilo hawalisemi wanachotaka ni misaada sawa sawa.
Tena walikwenda mbali na kuuliza eti kwanini hakuna mkuu wa majeshi aliyewahi kutoka znz, bila aibu wala haya.Hawajui gharama wanajua vyeo tu.
Mwenyekiti wa kamati kasema wao mapato yao bila kuondoa senti tano ni bilioni 240 ambazo zinatosha kuhudumia tume ya Warioba tu. Angalia moto wao wakati wanataka wajumbe wawe sawa, hawajui gharama wanajua nafasi za ajira na vyeo.
Leo wanasema muungano unawanyonya, tumewaambia wasije katika bunge la katiba ili kila kitu kiishe, hawataki.
Nimemsoma GHIBUU, kama walivyo wznz wengi wanataka mamlaka kamili halafu wanataka mkataba na Tanganyika.
Nimewauliza mkata uhusu mambo gani, hakuna jibu.
Hili swali hakuna anayeweza kulijibu kwasababu wanajua mkataba unahusu gharama za ulinzi, ajira, ardhi na soko la watu milioni 40.
Tanganyika haitafaidika na mkataba huo kwasababu kuna nini cha kushirikiana na znz the least to say.
Ndio maana umepiga stop Chumbe
Wanasema Tanganyika inawanyonya, nauliza katika mambo 22 yaliyokuwa ya muungano ni yapi Tanganyika ilifaidika kupitia mgongo wa znz.
Katika yale 15 yaliyoondolewa nani ameathirika zaidi. Tanganyika imepoteza nini kwa kuondoa 15.
Hawana jibu, kelele tu, namba hawataki kabisa kuzisikia.
Mkataba wanaosema ndio ukupe wenyewe kwa lugha laini. Maana yake msituache tubebeni kiaina.
Hawa jamaa muda wa kuwaone haya umekwisha ni kuwapa kavu kavu bila mchuzi.
Kama wanataka mkataba wafanye na Mohamed Dewji au Mengi ambao mapato yao yanalingana nao.
This time around hatutaki kubebana tena, njooni Dodoma na kitu mezani. Kama mna 240 semeni halafu mkae kimya mwenye kitu asema.
Mkija Dodoma mkubali kuwa muungano mnautaka na uwe mwisho wa kelele zenu.
Tumechoka, miaka 48 ya roba la karafuu sasa basi.
Tuacheni tupumue, nendeni mkaijenge znz ya neema. Tunawatakiwa heri sana. Hatuwahitaji mnatuhitaji
Nguruvi3, JJ(cert of std VII, member of village planning committee, ten cell leader)
The public enemy Number 1
Tunaoiombea sana bendera hiyo na wimbo wa taifa. Tunawaombea mema sana. Tanganyika haina maumivu yooyote kwasababu haihitaji znz. Labda utueleze maumivu hayo ni yapi kama unayo japo moja.
Pili, bendera na wimbo wa taifa havitoshi kama kuna jeshi la nchi jirani.
Tatu, sasa hivi mambo mzuri kabisa, kama mnataka bendera na wimbo wa taifa basi msije Dodoma.
Mwambie Ally Saleh na wajumbe wengine 14 wajitoe katika tume.
Kama wajumbe wa tume ya Warioba watafikisha rasimu ya mwisho katika bunge la katiba ambalo wznz watakuwepo, basi hapo bendera itapepea Chumbe na mwisho wa sauti ya wimbo wa taifa itakuwa mji mkongwe.
New york itakuwepo ile iliyopo, tena ikipepea na mungu ibariki Afrika.
Nimeulizahebu taumbieni ni misaada kiasi gani znz inakosa? Hebu weka namba.1. Wakati saiv Zanzibar ipo ktk harakati za kudai mamlaka kamili kama hapo awali tulivyougana na Tanganyika., nyinyi tanganyika mumeshindwa kuonyesha uzalendo pia kudai Tanganyika yenu, mumejivisha koti la Tanzania peke yenu ili benefit zote kutoka mataifa ziishie chumbe hazifiki zanzibar wakati neno Tanzania lilipatikana baada ya kuungana herufi 3 kutoka zanbar na 3 kutoka Tanganyika. maumivu yenu sasa yanakuja mutalikosa jina Tanzania na hamutaki jina lenu kuitwa Tanganyika, then Zanzibar ina vitega uchumi kibao ambavyo munatunyanyasa mtavikosa., kwani hujuwi? hilo 1.
2. Kwa sababu Tanganyika ilifanya hadaa na kuifanya zanzibar mkoa miaka yote hiyo ndio mana hata jeshi mumetuziba macho majeshi yote ni vichogo kutoka bara. tukiwa huru na mamlaka tutakuwa na jeshi letu hatuhitaji wakuria kutoka bara., kumbuka vita ya Idiamini ni majeshi ya zanzibar yaliyomkomesha idiamini dada
3. Kuja dodoma ndivyo mulipotugaragiza tena wazanzibar kwamba kila jambo liamuliwe dodoma zanzibar muliondoa hayo mamlaka miaka yote hiyo tokea babako wa taifa nyerere, sasa basi tutafanya maamuzi yetu kama nchi Zanzibar. Ally Saleh atakuja dodoma ili kuinasua zanzibar kwenye makucha ya Tanganyika na hapo ndio mwisho wa Dodoma., dodoma mtakutana nyinyi na chadema na NCCR mageuzi.,
4. Wimbo wa Taifa upo mjomba, Zanzibar ilipindua kwa mtutu wa bunduki tofauti na nyinyi Tanganyika nchi yenu mulipewa tu Zanzibar ilipigana kiume kutoka kwenye makucha ya wakoloni ndio tukapata uhuru wa zanzibar nenda katika historia usome., na bendera ya zanzibar ilikuwepo na inshaalah itarudi na itapepea UN kama kawaida.
''Siisi soteee tumeegombokaa kwa ndugu zeeetu walopotea, walio walio pigania nchi yetu makusudi makusudi ya kutugomba hatusaha hatusahau maisha yetu kwa roho kwa roho zao walozitoa ......................''
Nimeulizahebu taumbieni ni misaada kiasi gani znz inakosa? Hebu weka namba.
Je, bilioni 30 zilizopelekwa znz bila kujua ni za nini zilitoka nchi gani?
Je, ulinzi na usalama mnachangia kipi ambacho mnadhani ni zaidi ya misaada mnayopata?
Je, wizara ya mambo ya ndani, nje na ulinzi na usalama kama alivyosema Sheni hamchangii, ni uongo?
Je, wale wanafunzi wanaopewa mikopo wasiorudisha tofauti na wabara wanalipiwa na nani kutoka hazina Dar.
Je, mishahara inayotoka hazina Dar kwenda SMZ (Muulize komandoo na Aman) ipo katika fungu gani?
Hivi kupewa umeme uisolipia siyo msaada au lazima utoke ulaya
Je, 4.5 mnayopata kutoka pato la taifa ninyi mnachangia nini katika hulio pato?
2.Kwani wakati wa vita ya Amin Znz ilishiriki vipi ( Echolima).
Brigedia ngapi zilitoka znz na ilimwadabisha vipi Amin?Ziliharamiwa vipi. Hebu weka namba(samahani )
3.Mkishakuja Dodoma mumeshakubali kila kitu. Kwanini msigome kuja kabisa.
Mtafanya jambo gani ambalo mlishindwa kulifanya kwa kukubali tume ya Warioba.
4. Haa!!! leo imekuwa znz ilipindua kwa mtutu! si kila siku mnasema ni mamluki kutoka bara waliofanya mapinduzi.Wapi unasimamia wewe, mapinduzi daima! au mapinduzi zii.Zipo kambi mbili, wewe upo kambi ipi.
5.Tunataka sana bendera ipepee UNO lakini hilo halitokei kama hamtafanya maamuzi magumu.
Maamuzi magumu si kutia mguu Dodoma, maamuzi magumu ni kama yale mlioshindwa ya kura ya maoni, tume ya Warioba.
Mkataba ubaki Chumbe, njooni Tanganyika mrudi salama
Narudia tena na tena, Wazanzibar wakija Dodoma wamekubali muungano, period.Hizo porojo mtafute Salimn Awadh na balozi seif ali iddi akupe hizo hesabu za uongo ambazo Tanganyika inaisaidia Zanzibar., lakini mbona hukutaja trilioni ngapi zanzibar inaidai Tanganyika fedha zake taslim ilizochangia kuanzisha benki kuu? na hadi leo mapato mnabana huko?
Eti umeme bure, ivi wewe umekuwa mwehu kiasi gani hata usifahamu kwamba zanaibar inalipia umeme kutoka Tanganyika kama vile ambavyo tungeingia mkataba na nchi jirani au nyengine yeyote kupata huduma hiyo tena kwa nafuu zaidi?
Matrilioni mangapi munainyanyasa zanzibar kwenye mapato yanatoka zanizbar kwenda tanganyika kuanzia ushuru wa bandari hadi biashara ndogo ndogo zinazofanywa na wajasiria mali kutoka Zanzibar.
Mikataba yote ya kimataifa imeingia na serikali ya Tanganyika, Rais Dr. shein akija Tanganyika amekuwa kama mjumbe wa nyumba 10.,
kura ya maoni vipi? Zanzibar asilimia 66% walitaka mkataba uvunjwe muungano huu wa kidhalim
Naelewa mkuu ww ni shemegi yake Pinda., ila fahamu kwamba Zanzibar sasa imeamka na ukweli ni kwamba haturudi nyuma mamlaka ya Zanzibar yanakuja soon., izo serikali 3 zikiwepo na muungano ambao utakuwepo kuuvunjia kabisa ni dakika 5 tu., mumeingia kwenye mtego mtaumia sanaaa na ndio maana sasa munaenda mbio ili turudi kwenye serikali 2., haiwezekani ngooo!!
Thuluthi 2 iliyokubalika kwa upande wa Zanzibar na thuluthi 2 kutoka Tanganyika inatosha kuukata mzizi wa fitina kwenye Bunge la Katiba hakuna tena simple majority., utaenda ww na kibaka prof. kapuya kupiga makofi dodoma., shuwain
kumbe mumeumiaaa enn., na bado sasa ngoja maalim seif 2015 awe Rais wa Zanzibar hii ni rasha rasha tu mkuu, lo siento amiga.,
Lakini mkuu yote ya nini haya sisi tunataka nchi yetu tu. Kwa nini mnataka kunufaika kupitia mgongo wa Zanzibar., emu kama ni mzalendo dai Tanganyika yako usiwe mtumwa hadi kufa kwako., jikazeni hilo jina la Tanganyika ni lenu wenyewe.,
Narudia tena na tena, Wazanzibar wakija Dodoma wamekubali muungano, period.
Kama hawataki muungano wasije na bunge la katiba halitakuwepo.
Ukumbuke wametoa maoni tume ya Warioba ukiwa ni ushahidi kuwa wamo katika mchakato wa kuandika katiba.
Tuliwaambia wasusie tume wao wakaona idadi ya ajira 15 ni muhimu sana, wakamtanguliza Ally Salehe wa BBC ambaye sasa kakaa kimya anavuta mapesa. Hivyo mkija Dodoma kaaeni kimya muambie nini kifanyike.
Pili, hakuna kelele za madai ya kuanzisha benki kuu. Nadhani unajua katika 4.5 znz inayopata haichangii hata senti tano.
Tatu, tukianza kuweka hesbabu za ulinzi na usalam mtauza kisiwa.
Nne, usisaahu kuwa miaka 48 znz haijachangia chochote kwasababu mwaka 2013 wana bilioni 240 pungufu ya za Mzee Reginald Mengi.
lakini pia kama mnadai kitu vunjeni muungano msuluhishia atatafutwa mtapewa mnachokidai.
Wewe unadai asilimia 11 mwenzako asilimia 89.
Hata kama itakuja asilimia 90 ya wznz Dodoma, kitu wanachopaswa kuelewa ni kuwa wamekuja wenyewe.
Makao makuu yatakuwa Dodoma na watakuja Dodoma. Wakisha panda meli tu kuvuka bahari, kelele wanaacha chumbe, hesababu na mantiki zinatangulia.
Thisi time around hatusikii la udogo au wingi. Ukitaka usawa ni lazima uchangie sawa.
Haiwezekani uchangie kidogo halafu ule sawa. Hizo hesabu mwisho chumbe.
Na watakapokuwa wanakuja bendera ya taifa ndiyo itakuwa mbele, wimbo wa taifa ni mungu ibariki Tanzania.
Wakridui na kufika malindi wafungue vitambaa vyao na na nyimbo au kwaya.
Message ni kuwa as long as mtakuja Dodoma mkubali yaishe. Period.
Hoja ipo wapi, mimi sina ufundi wa matusi.pole sn mkuu, Zanzibar lazima ije dodoma kuzimaliza nguvu za Tanganyika kwa Zanzibar.,, kama umewahi kusikia Adui lazima huuliwa kwa silaha yake ndivyo ambavyo tutaikata mizizi CCM Dodoma.,,
Ivi ww huna macho? Warioba ndio mulimtegemea mbona amekuangusheni ameleta mfumo wa serikali 3 badala ya 2 muzlizokuwa munaziabudu? mbona munaenda mbio saivi hamlali serikali 3 hamzitakiiii? ivi ww upo dunia gani? waulize wenzako wametoka jasho hadi la meno.
ngoja nikutoe uchafu wa maskio sasa., nimewasikia wenzako wanalalamika kwa hofu wanasema serikali 3 zanzibar lazima itakuwa na mamlaka yk alafu huu muungano wakati wowote nutavunjika hautadumu., tunawacheka sana sisi ndio target yetu., period! Serikali 3 ndio mfumo uliokuwa kwenye ilani ya chama cha CUF., period!
chupi imewabana., we are comming dodoma to kill CCM for the last tym., period! ww kama mbabe toka kifua mbele udai Tanganyika yako usiwe mtumwa ndani ya nchi yk., Tanganyika ndio nchi yenu muliyopewa bila jasho na wakoloni, Zanzibar ilipigana kiume kutukomboa, period!
Lakini usjali ukiwa na passport yk au permit maalum utakuja zanzibar kutembea unywe kahawa na kashata na halua, jioni utaenda kula piza au urojo foro, muda wako ukiisha utasepa ndivyo watu wanavyoishi katika nchi za watu duniani.,
Sisi Waislam wa Tanganyika tunataka huu muungano uvunjike tupambane vizuri bungeni ukiangalia bunge letu lote sisi Waislam eti tunawakilishwa na Waislam wa Zanzibar ili aliwezekani, bunge letu asilimia 95 limejaa Wakirsto hiyo aslimia 5 ni kutoka Zanzibar bora huu muungano uvunjike tu tupiganie haki zetu.
GHIBUU,
..I am 100% with u.
..tushirikiane kupitia EAC au SADC.
..mambo yote kama ulinzi, biashara, etc etc yapo ktk mikataba ya vyombo hivyo.
..tena nchi mwanachama inaruhusa ya kuchagua kipengele gani isaini na kipi isisaini.
..haya malumbano ya Tgk vs Znz hayawezi kuisha ikiwa tutakuwa wawili peke yetu.
..kwasababu muungano wa sasa hivi umeingia ktk hali ya kutoaminiana, itasaidia sana tukiwa na wenzetu katika jumuiya kama ya SADC au EU kupunguza migogoro moja kwa moja baina ya wa-Tgk na wa-Znz.
cc gombesugu, Barubaru, Nguruvi3
Hoja ipo wapi, mimi sina ufundi wa matusi.
Kwa uchache ninaweza kutumia namba matsui nilidahfeli mtihani.
Ni hivi hata hizo 3 sifikirii ndio maana nawahimiza wznz wasije Dodoma kabisa.
Fuatilia rekodi utaona nilivyosaidia kutoa mawazo ya znz huru.
Tatizo znz ni woga hawapo tayari wakipewa fursa.Wkairudi malindi na vijibweni kelele sana.
Ni hivi kuja Dodoma ni kuja makao makuu ya nchi.
Mkija Dodoma mlete kitu mezani si maneno , kudai vyaeo au ajira.
Halafu mkishatua Dodoma mumekubali yakaisha. BLW juzi walikuja Dodoma na habari ya kuomba znz isamehewe gharama kwasababu inachangia herufi tatu za muungano. Wakirudi Unguja utasikia kelele. No, this time tunasema wekeni kitu mezani.
Naona wewe ni mchanga sana
Tume ya Nyalali ili[endekeza serikali 3 wakati Seif wa CUF akiwa CCM na serikali mbili
Tume ya kisanga ilipendekeza serikali 3 wakati huo Seif yupo magereza
Tume ya mwanzo ya warioba *acha ya sasa* ilipendekeza serikali 3
Hivyo serikali 3 ni wazo lililokuwepo wakati Maalim wa CUF akiwa CCM na magereza.
Yeye hana lolote kuhusu hili. Siyo wazo la CUF
Lakini pia Maalim wa CUF amesema hataki serikali 3 akisadiwa na Ahmed Rajab na akina Jusa.
Lipumba ambaye ni mwenyekiti anasema serikali 3. Kwahiyo ni makosa kusema CUF ina msimamo juu ya hili.
Maalim Seif alishakana serikali 3 akisaidiana na Waarabu Ahmed Rajab, Jusa na Ally Salehe.
Wao wanataka mkataba ambao Tanganyika imesema haina sababu ya mkataba na znz ila znz inaweza kuwa na mkataba na Reginald Mengi wa Tanganyika.Ndio maana Maalim amebaki nao Chumbe na hautavuka.
Mkija Dodoma mumekubali kila kitu na mtakjuja tu kwasababu mnahitaji muungano kuliko tunavyowahitaji.
Mtakuja tu znz haiuzungushi mbele ya Tanganyika teh teh teh teh
Hoja ipo wapi, mimi sina ufundi wa matusi.
Kwa uchache ninaweza kutumia namba matsui nilidahfeli mtihani.
Ni hivi hata hizo 3 sifikirii ndio maana nawahimiza wznz wasije Dodoma kabisa.
Fuatilia rekodi utaona nilivyosaidia kutoa mawazo ya znz huru.
Tatizo znz ni woga hawapo tayari wakipewa fursa.Wkairudi malindi na vijibweni kelele sana.
Ni hivi kuja Dodoma ni kuja makao makuu ya nchi.
Mkija Dodoma mlete kitu mezani si maneno , kudai vyaeo au ajira.
Halafu mkishatua Dodoma mumekubali yakaisha. BLW juzi walikuja Dodoma na habari ya kuomba znz isamehewe gharama kwasababu inachangia herufi tatu za muungano. Wakirudi Unguja utasikia kelele. No, this time tunasema wekeni kitu mezani.
Naona wewe ni mchanga sana
Tume ya Nyalali ili[endekeza serikali 3 wakati Seif wa CUF akiwa CCM na serikali mbili
Tume ya kisanga ilipendekeza serikali 3 wakati huo Seif yupo magereza
Tume ya mwanzo ya warioba *acha ya sasa* ilipendekeza serikali 3
Hivyo serikali 3 ni wazo lililokuwepo wakati Maalim wa CUF akiwa CCM na magereza.
Yeye hana lolote kuhusu hili. Siyo wazo la CUF
Lakini pia Maalim wa CUF amesema hataki serikali 3 akisadiwa na Ahmed Rajab na akina Jusa.
Lipumba ambaye ni mwenyekiti anasema serikali 3. Kwahiyo ni makosa kusema CUF ina msimamo juu ya hili.
Maalim Seif alishakana serikali 3 akisaidiana na Waarabu Ahmed Rajab, Jusa na Ally Salehe.
Wao wanataka mkataba ambao Tanganyika imesema haina sababu ya mkataba na znz ila znz inaweza kuwa na mkataba na Reginald Mengi wa Tanganyika.Ndio maana Maalim amebaki nao Chumbe na hautavuka.
Mkija Dodoma mumekubali kila kitu na mtakjuja tu kwasababu mnahitaji muungano kuliko tunavyowahitaji.
Mtakuja tu znz haiuzungushi mbele ya Tanganyika teh teh teh teh