Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Mwiba, gombesugu,

..Zanzibar ni ndogo kieneo na kiuchumi.

..kuitia ktk muungano na Tanganyika ni kutafutana ubaya na lawama.

..haya mambo tumekuwa tukiyasema kwa muda mrefu sana hapa JF.

..tunaposema hayo wengine mnafikiria tumeamua kuwavunjia heshima lakini huyo mwakilishi kasema ukweli.

..labda nikupeni mfano mdogo: kabla ya mapinduzi Znz majimbo ya uchaguzi yalikuwa hayazidi 30. sasa hebu angalia wakati huu tuna muungano Znz ina majimbo mangapi ya uchaguzi? majimbo yameongezwa Znz ifanane-fanane na Tanganyika.

cc Nguruvi3, Barubaru
 
Last edited by a moderator:
weli hatutaki muungano na mafuta yetu hivi hamjui? au mnataka kuendelea kutunyonya? na kutuibia rasilmali zetu za mafutana bahari kuu?

Mafuta yetu Pemba sio yenu Unguja ila ni mali tu ya serikali ya Zanzibar kimaandishi si munaona karafuu tunazalisha sisi angalia ofisi Unguja ya ZSTC ilivo angalia na Pemba na mafuta kule Tundaua munayataka sio
 
Hizi ndizo hoja zinazotakiwa kwenye Muungano. Kwa maana nyingine, serikali ya Zanzibar haitaki serikali tatu wakati pia wanadai serikali mbili zinawanyonya!. Hoja iliyojificha hapa ni kuwa, Wazanzibar hawataki muungano. Finito.

Siyo jambo la kushangaza kusikia hoja kama hii kisiasa kwa sababu serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaongozwa kwa kiasi kikubwa na sera za CCM ambapo serikali mbili ndiyo sera yake na pia Salimin Awadhi Salimin ni mwakilishi kupitia tiketi ya CCM.

Hakuna haja ya kuwa na muungano kama hakuna manufaa endelevu kwa wananchi wake. Swala la kuwa kwenye muungano ambapo msingi wake mkuu ni siasa halina mashiko hata kidogo katika dunia ya sasa inayonyambulishwa kiuchumi zaidi.

Bila kujali anachokisema ni sera ya CCM, fact always fact hasa katika uhalisia wa jambo ambalo linahusisha uchumi. Watanganyika lazima tuuangalie muungano kiuchumi zaidi na katika uchumi ndipo tunapata gharama za serikali tatu halafu vile vile kuna kuchangia gharama za EAC achilia mbali regional economic, political and security cooperation schemes with other nation. Hizi ni gharama kubwa sana na sidhani kama Watanzania wanapata value for their tax money.

Kwa nini tusiachane na Zanzibar na tukakutana nao katika SADC kama member nation kitu ambacho ni political and economic sense kuliko kung'ang'ania kuwa na nchi ambayo haiwezi hata kulipa 10% ya gharama za Muungano.

Kiuchumi Tanzania itanufaika sana kuwa mwanachama wa SADC zaidi ya kuwa na muungano na Zanzibar na hasa iwapo watanzania watatumia ipasavyo nafasi hii kwa sababu ukiangalia total population and GDP kwa kila nchi inakupa wastani wa per capital $2,080.

Huwezi kula keki ukabaki nayo. Ninaamiini unapohitimisha kwa kutamka Tanzania una maana ya Tanganyika? Mawazo yangu ni kuwa huyu Bw Salmini anatetea sera ya Chama chake bila kuangalia mengine au anatuthibitishia kuwa wakati wote Tanganyika ilkuwa 'inaumia'. Pengine mapato yao yamefunikwa kwa kuwa ndani ya mfumo wa serikali mbili. Lakini pamoja na hayo kwa muundo wowote ule utatengenezwa utaratibu wa kugharamia uendeshaji wa serikali na vyombo vyote vya dola.
 


Ngongo,

Achana na hayo mambo ya wana siasa. Jitahidi utazame hilo katika lugha nyepesi kabisa.hebu jiulize Znz ina watu wangapi? Je ina eneo la ukubwa gani? na tazama majirani zao tanganyika wako wangapi? na eneo lao kiasi gani?

Jiulize kama Znz itachwa iwe huru kabisa kiuchumi yaani kupata misaada na hata kukopa bila kusahau mapato yao ya ndani watashindwaje kulipa gharama za Muungano?

Na kama watashindwa si watakuwa huru Kujitoa kwani lazima kuwe na Muungano wa nchi hizo.

lakin kwa sisi wachumi tunasema Nje ya Muungano, Znz uchumi wake utapaa kwa kasi kubwa sana na hili nililibainisha wazi kwa mapana na marefu kwenye uzi uliosema Nini faida za Muungano kwa Znz. Pitia huko utajifunza mengi.

Waachwe Znz wapumue. Miaka 50 imetosha.

Inatakiwa Znz huru kiuchumi na kifikra na kimaamuzi.

Cc. Nguruvi3, Joka kuu
 
Mwiba, gombesugu,

..Zanzibar ni ndogo kieneo na kiuchumi.

..kuitia ktk muungano na Tanganyika ni kutafutana ubaya na lawama.

..haya mambo tumekuwa tukiyasema kwa muda mrefu sana hapa JF.

..tunaposema hayo wengine mnafikiria tumeamua kuwavunjia heshima lakini huyo mwakilishi kasema ukweli.

..labda nikupeni mfano mdogo: kabla ya mapinduzi Znz majimbo ya uchaguzi yalikuwa hayazidi 30. sasa hebu angalia wakati huu tuna muungano Znz ina majimbo mangapi ya uchaguzi? majimbo yameongezwa Znz ifanane-fanane na Tanganyika.

cc Nguruvi3, Barubaru

labda nikuulize Je huo mvungano wenu mtachangia kwa ratio ya watu, eneo au madaraka.

Je kwa Uoni wako Znz wanaweza shindwa wapi kama itaachwa huru kiuchumi na maamuzi?

Kumbuka kuwa Mvungano ni kama KOTI. kama utaona linakubana au kukutia joto si unalivua tu. Je kuna ubaya hapo?

sasa Povu zote za nini kuleta mitazamo ya kisiasa katika mambo ya kiuchumi hususan kwa Znz?

Pole sana

 
Mimi nafikiri waZnz wapo wazzi kabisa na wame table hadhwarani mchana kweupeeeeeeeeeeee bila woga wala khofu ndani ya barza la wawakilishi na kwenye viriri vyote vya siasa. WANATAKA MUUNGANO WA MKATABA, NJE YA HAPO KILA MTU ACHUKUE CHAKE.

Sijapata kusikia msimamo wa tanganyika iwe bungeni au popote zaidi ya ku discuss misimamo ya Znz huru.
 
Kweli Zanzibar ni ndogo kieneo ila kiuchumi sidhani kama ilikuwa hivyo ila baada ya huu Muungano ndio mmetutilia ufukara na kutufanya tuwe watu duni sana ,mnataka tuwe tunategemea kila kitu kutoka huko Tanganyika na ndio kama inavyoonekana katika hoja zenu ,nyie nchi ndogo sijui uchumi wenu mdogo ,hebu ulizia na katafute historia ya Zanzibar ,Zanzibar wakati kabla ya Muungano ilikuwa vipi na ilitoa msaada kumsaidia nani ? Yakhe huu Muungano ukifa leo basi nakuhakikishieni machogo ,hautapita muda mrefu tutawasaidia tena tutawasaidia kwa ari na mori na moyo wa jeuri ,huko Tanganyika hamna kitu mmekalia kuti kavu. lazima mtapigana mapanga tu !
 
Ngongo,

Sina hakika kwa undani zaidi na hayo matamshi ya huyo Bwana Kiongozi kama alivyonukuliwa na hilo jarida.

Insha Allah,tunafuatilia hizi khabar kwa utuvu...lakini nakhis yakuwa hayo ni mazungumzo tu ya kisiasa,kwa maana nyingine ni coded words za sisi kukwambiani nyinyi Watanganyika yakuwa huo Muungano hatuutaki tena,ushitushinda kwa mangi ya ulaghai na dhuluma!?

Hicho ni kipimo changu tu binafsi kiduchu kwa kuanzia,lakini tarejea tena hapa barzan kadri mnakasha utakavyoendelea.

Labda Mufti Barubaru,atakapopata fursa ya kujongelea hapa barzan yawezakuwa ana mangi ya kutujuza...maana yeye ni mbobefu wa mahisabu na takwimu hizo za fedha za kuendesha huo "Muungano".

Lakini pia tujikumbushe japo kiduchu,yakuwa kabla ya hizo Serikali tatu,italazim pia turejee nyuma kiduchu na kujikumbusha madeni ya Serikali ya Muungano/JMT,ambayo inadaiwa na Serikali ya Zanzibar!?

Sijawahi hata siku moja kuona member/s yeyote au hata thread yeyote humu JF,ikikumbushia zile "enzi za Mwalimu"; wakti Tanganyika na Serikali ya Muungano vikiwa taabani kiuchumi,na zikitegemea pita kiasi senti/akiba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar-SMZ ili kujikimu na kujiendesha!?

Mnakumbuka yakuwa wakti ule wa ile vita ya Nyerere dhidi ya Uganda,SMZ iligharamia kwa kiasi kikubwa mno ile vita ambayo binafsi Wananachi wa Zanzibar wala Serikali yao haikushirikishwa kikamilifu kwenye yale maamuzi dhaifu ya Nyerere kungia vitani baada ya kumchokoza kwa makusudi yule mpuuzi Idd Amin kwa miaka kadhaa!?

Mnakumbuka pia,SMZ ililazimishwa na Nyerere kutumia akiba yake takriban yoote kugharamia yale yaliyoitwa ati "mapambano ya ukombozi wa nchi za Afrika"!?

Niwia radhi Mkuu,hapa silalamiki asilan,lakini ni muhimu pia kiduchu kujikumbusha fadhila,ihsan na madeni mangi mno dhidi ya hiyo Tanganyika aka JMT...ambayo(madeni dhidi ya JMT) mpaka kesho hayajawahi kuzungumziwa hata na Viongozi wowote wa ngazi za juu,na hatujui sababu ni ipi!?...labda woga,ubinafsi,uchu wa madaraka,vitisho au upumbavu wa fikra!?

Ahsanta.

Sijakusoma Mkuu,
Ina maana Zanzibar inaidai Tanganyika?
 
wanataka nafasi za sawa za wabunge hizo tuwape ila tukija kwenye uchangiaji iwe 50 kwa 50 hawawezi watoke
Kila nchi ikusanye ushuru wake na pia kila nchi iweke viwango vyake vya kodi nyama,nyanya na mazao yote yanayotoka bara kwenda zanzibar yatozwe kodi sio wanakuja huku nakuchukua mazao halafu wanatufanya watu watanganyika bei inapanda
bidhaa watakazoingiza huku zitozwe kodi nchi yetu sio jalala wawe na mamlaka yao ya mapato na sisi tuwe na yetu tuone kama wataweza hata kujilipa mishahara ukifikiria juzijuzi jengo lao la baraza la wawakilishi limejengwa kwa fedha za muungano wanashindwa hata kujenga jengo la chombo chao kinachotumika kutunga sheria
Kila nchi iwe na shirika lake la umeme na walipe na pia kwa sababu kila nchi ina mamlaka yake ya kusimamia usafiri wa majini kila nchi ilipe kodi zake
kila mtu asiruhusiwe kumiliki ardhi kwenye nchi isiyo yake wala kumiliki majengo
baada ya hapo ndio tutajua nani anamnyonya mwenzake anayetaka kurudi inabidi aombe kwa kukubali masharti atakayopewa
 
Wataongea tu, hakuna namna.

Kwa sasa tuna serikali mbili, serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Muungano -ambayo kimsingi inahusika na mambo ya Tanganyika na yale ya Muungano. Kama mwenyekiti anasema kuwa Zanzibar haina uwezo wa kuchangia Serikali ya Muungano endapo kutakuwa na serakali tatu, maana yake amekiri kuwa hata sasa hivi Tanganyika ndio inalipa 'bills' zote. Sasa huo unyonyaji aoimba Maalim Seif unatoka wapi?

Na siku zote tumekuwa tunasema hapa, madai ya pasu kwa pasu yasishie kwenye kuepeana nafasi za kazi peke yake, kila upande wa Muungano uwalipe watu wake.

Wasipokuwa makini hii inakula kwao, maana Tanganyika wamechoka kuitwa wakoloni, sasa watadai serikali moja au tatu.
Ndugu yangu ukiongelea muungano hutasikia mzanzibar akiongelea gharama hata siku moja.
Kitu cha kwanza ni kutafuta nafasi za ajira na vyeo baasi. Hilo ndilo muungano kwa znz

Kama ulivyosema siku zote tumewasikia wakisema wana nyonywa , sasa hesabu zimewekwa mezani wanaanza kusingizia mambo ya udogo. Katika tume walikomaa wawe na wajumbe sawa wakisema wao ni nchi mbia, sasa hivi ubia umeshapotea baada ya kuambiwa waweke kitu mezani.

Wamekomalia wajumbe sawa wa bunge la katiba, wakiambiwa gharama wanasema wao ni wadogo.

Kama wanakubali udogo wakubali kila kitu.

Tumesema zaidi ya miaka 5 kuwa hawa weznetu wanafundishwa kusema lakini hawana tafakuri.
Leo wanakimbia kimbia hovyo wakati wamepewa mamlaka kamili. Mamalaka wanataka kuchangia hawataki

Umesema vema sana kuwa huu ni ushahidi kuwa tunalipia serikali ya muungano wakati wao kazi yao kubwa ni kulala, kupiga domo, kudai vyeo na nafasi.

Eti wanasema rais wa muungano uwe wa kupokezana sasa huyo rais anayetoka mahali pasipotoa hata 10% anakuja kutuongoza kwa lipi. Hawa weznetu tatizo lao si muungano ni zaidi ya hapo........

Ushahidi unajitokeza kuwa hatuwahitaji maana hata ulinzi na usalama wanaosema hawana wanalipiwa na mtanganyika achilia mbali mambo mengine.
 
wanataka nafasi za sawa za wabunge hizo tuwape ila tukija kwenye uchangiaji iwe 50 kwa 50 hawawezi watoke
Kila nchi ikusanye ushuru wake na pia kila nchi iweke viwango vyake vya kodi nyama,nyanya na mazao yote yanayotoka bara kwenda zanzibar yatozwe kodi sio wanakuja huku nakuchukua mazao halafu wanatufanya watu watanganyika bei inapanda
bidhaa watakazoingiza huku zitozwe kodi nchi yetu sio jalala wawe na mamlaka yao ya mapato na sisi tuwe na yetu tuone kama wataweza hata kujilipa mishahara ukifikiria juzijuzi jengo lao la baraza la wawakilishi limejengwa kwa fedha za muungano wanashindwa hata kujenga jengo la chombo chao kinachotumika kutunga sheria
Kila nchi iwe na shirika lake la umeme na walipe na pia kwa sababu kila nchi ina mamlaka yake ya kusimamia usafiri wa majini kila nchi ilipe kodi zake
kila mtu asiruhusiwe kumiliki ardhi kwenye nchi isiyo yake wala kumiliki majengo
baada ya hapo ndio tutajua nani anamnyonya mwenzake anayetaka kurudi inabidi aombe kwa kukubali masharti atakayopewa

Yakhe mwenye fedha hununua ,sasa hamuoni kana kwamba ninyi machogo ni wakulima na sisi wavisiwani ni wanunuzi ,kuna ubaya gani hapo ,mtatutembezea bidhaa zenu tuna hiari yetu kuzinunua tena kama bado hazija expire,halafu hamna wa kumuuzia zaidi ya Zanzibar yaani sisi ndio wanunuzi wakubwa ,tukiwacha kuzinunua zitawaozea na mtakosa hela ! mtapigana mapanga !
 
Huwezi kula keki ukabaki nayo. Ninaamiini unapohitimisha kwa kutamka Tanzania una maana ya Tanganyika?
Yes, nilikuwa nina maana hiyo na nimebadilisha. Thanks kwa dokezo.

Mawazo yangu ni kuwa huyu Bw Salmini anatetea sera ya Chama chake bila kuangalia mengine au anatuthibitishia kuwa wakati wote Tanganyika ilkuwa 'inaumia'. Pengine mapato yao yamefunikwa kwa kuwa ndani ya mfumo wa serikali mbili. Lakini pamoja na hayo kwa muundo wowote ule utatengenezwa utaratibu wa kugharamia uendeshaji wa serikali na vyombo vyote vya dola.
Ninakubaliana na point yako lakini huoni kuwa kuna matatizo mbele kwa sababu kama wameishasema hawawezi hata kulipia 10% ya mchango wa muungano ina maana hakuna faida ya kuwa na muungano kwa Tanganyika.

Kama anasema ili kutetea kisiasa hoja ya Serikali mbili basi hajui kuwa angalizo lake linatufanya tuhoji mchango wa Zanzibar katika muungano huu uliopo na faida ya Tanganyika kuwepo ndani ya huu muungano ambao bila hata kuchunguza kwa undani ni ukweli kuwa Tanganyika inabeba gharama za Tanganyika na pia muungano achilia mbali utumishi ambao unawanufaisha Wazanzibar kwenye 50-50 wakati idadi yao yote ni kama mkoa mmoja wa Tanganyika.

Mimi nilishasema muda mrefu kuwa hatuhitaji Muungano kwa sasa. Ni bora kila nchi ibebe mzigo wake na tukutane kwenye mashirikisho kama SADC, EAC, COMESA, AU n.k.
 
Hakuna haki bila wajibu. Mtu yeyote aliyefika na kukaa Zanzibar na Pemba bila shaka atakuwa na maswali mengi kuhusu hawa watu. Wavivu.maneno kibaao.fitna ndo usiseme wanajifanya waarabu wakati wao ni waswahili wasio na hata kikombe cha mafuta. Hapa gharama ni pasu-pasu. Ndo watapata akili. Usiwaone wakijitapa hapa Dar. Pemba hawajafanya lolote. Ndugu zao wanaishi porini.
 
KWahiyo kubalini kwamba bila Bara, Zanzibar inakufa! Nina maana hii, kumbe siku zote hizi sisi ndio tunaowalea sio?
 
wadau hoja ya huyu mwenyekiti, ni kwamba serikal 3 ndio zitawafanya smz kushindwa kulipa, sasa swali ni jee kwenye serikal 2 wanalipa asilimia ngapi?
Kama serikal 3 hawawezi kulipa sasa Maalim Seif na chama chenu kwann muje na option ya serikal 3?
Wazanzibar kubalin serikal 2 tu lakin mupunguze mambo ya Muungano badala ya 30 yawe 9 au chini ya hapo, otherwise mnajichanganya wenyewe.
 
Kweli Zanzibar ni ndogo kieneo ila kiuchumi sidhani kama ilikuwa hivyo ila baada ya huu Muungano ndio mmetutilia ufukara na kutufanya tuwe watu duni sana ,mnataka tuwe tunategemea kila kitu kutoka huko Tanganyika na ndio kama inavyoonekana katika hoja zenu ,nyie nchi ndogo sijui uchumi wenu mdogo ,hebu ulizia na katafute historia ya Zanzibar ,Zanzibar wakati kabla ya Muungano ilikuwa vipi na ilitoa msaada kumsaidia nani ? Yakhe huu Muungano ukifa leo basi nakuhakikishieni machogo ,hautapita muda mrefu tutawasaidia tena tutawasaidia kwa ari na mori na moyo wa jeuri ,huko Tanganyika hamna kitu mmekalia kuti kavu. lazima mtapigana mapanga tu !
Tulieni! kasemea mwenzenu kuwa bajeti ya ulinzi na usalama ni trilion 1.3 ninyi bajeti ni 240bilioni. Lini Tanganyika itaitegemea znz. Leo tuna ushahidi kuwa kwa miaka 50 tumekuwa tunawalipia gharama halafu mnadai vyeo na nafasi za kazi.

Tume ya warioba znz 0 haikutoa hata senti tano. Mchango wa znz ni kukimbilia wajumbe sawa. Aly Salehe kapata ajira kimya. Bunge la katiba gharama zake hamuwezi kuchangia hata 1/8, mchango wenu vyeo na nafasi za ajira.

Hatuwahitaji, msije katika bunge la katiba,period. Tumechaoka kuwabeba mkicheza mdumange.
 
Huyu Salimin Awadhi anachokiongea ata hakijuwi ni mbumbumbu wa kutupwa kabisa., kwani zanzibar hapo awali ilipoungana na Tanganyika zikawa nchi 2 huru lini ulisikia Zanzibar ina madeni inadaiwa na tanganyika kwenye Muungano zaidi ya kwamba sasa Tanganyika ndio inadaiwa hela nyingi sana na Zanzibar? fedha za benki kuu hadi leo.,

Kama Zanzibar hawawezi kuchangia serikali ya Muungano njia nyengine basi ni kuvunjwa Muungano ili Zanzibar iwe huru hayo madeni ya michango yaweze kuepukika kabisa.,

Milioni mbili kwa mwezi ndio zinamsumbua huyu Salmin Awadh.,
 
Huyu Salimin Awadhi anachokiongea ata hakijuwi ni mbumbumbu wa kutupwa kabisa., kwani zanzibar hapo awali ilipoungana na Tanganyika zikawa nchi 2 huru lini ulisikia Zanzibar ina madeni inadaiwa na tanganyika kwenye Muungano zaidi ya kwamba sasa Tanganyika ndio inadaiwa hela nyingi sana na Zanzibar? fedha za benki kuu hadi leo.,

Kama Zanzibar hawawezi kuchangia serikali ya Muungano njia nyengine basi ni kuvunjwa Muungano ili Zanzibar iwe huru hayo madeni ya michango yaweze kuepukika kabisa.,

Milioni mbili kwa mwezi ndio zinamsumbua huyu Salmin Awadh.,
Hakuna pesa Tanganyika inadaiwa.
Ninyi hamjui kuhusu mgao mnaoupata kila mwezi. Hamjui huduma ambazo mumezipata kwa miaka 50 na leo watu wenu wanaweka wazi kabisa kuwa muungano uliendeshwa na kodi za Watanganyika.

Vunjeni muungano mdai machodhani kama hamtajikuta mnauza kisiwa chote.

Tumewaambi siku nyingi kuhusu gharama za muungano. Leo maji yamewafika shingoni mnalalamika kuhusu udogo.

By the way ninyi vijana wa Tanganyika mliokosa mikopo iulizeni serikali yenu kwanini mkose mikopo ili hali pesa za kodi za baba zenu zinakwenda ZNZ kwa mikopo ya wananfunzi wa 1) Kusoma bila kurudisha mikopo 2) Kupewa hata nafasi zenu kwasababu tu ya uzanzibar..
Eto hawataki muungano wakati wapo Dodoma! thubutu nani asiyependa sh ya Tanganyika!

Wanajiandaa kuongeza wajumbe waje kwenye bunge la katiba badala ya kuwakataza, huku uvunguni mwa vitanda wanapiga domo hawataki muungano.

Tumechoka kusikia kelele zenu tuna mambo mengi ya muhimu. Hatuwezi kuishi kwa kuwabeba mkicheza msewe halafu mnataka vyeo na ajira. This time around pasu pasu kama hamtaki njiaa nyeupee bandarini rudini mkaijenge znz ya pembe za ndovu na watumwa. Znz iliyokuwa inagawa sambusa barabarani na mapilau katika vituo vya mabasi, znz yenye neema.

Tuwabebe halafu mtukane! ebo! leo mnasema bila haya hamjiwezi! mkiondoka hapo mumechukua posho mnaelekea bandarini na matusi. Posho za Mtanganyika! tumechoka kelele na midomo yenu.
Tatizo leni si muungano ni jingine linalohitaji kampeni ya Lowasa.
 
Back
Top Bottom