Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Wacheni hivi mnapapasa au mnajua kilichopo ,hivi Mungano wa Ulaya una nchi ngapi ? Katika nchi hizo hakuna zilizo ndogo na ambazo nyingine bora Zanzibar kwa Utajiri ,Hapa kwenye huu Muungano tunaojing'ang'aniza wa EAC hivi nchi zote ni tajiri ?

Tatizo lipo wapi au kwa huyo memba wa Chama Cha Mashetani (CCM) ambae anajivutia huko upande wa pili yakhe kama tutakuwa hatuna uwezo hapana jipya eti ,si tutagawana mbao tu ! Aafu tutajiunga na Kenya na Uganda na Rwanda ,tutapeleka maombi huko ,ila kwenu kwa vile tutakuwa hatuna uwezo tutawasamehe ,halafu nyie wazito sana hamubebeki ,ndio maana akina Kenya wamewatenga kiaina ,mnaonekana mumo lakini hamumo ,kiukweli mpo outside mpo kama outsider tu.

Sina wakati mrefu kwa sababu nipo hapa Philipines tukitoa msaaada wa kibinadamu.
MV spice Islander ilipomezwa ulikuwepo kutoa huo msaada wa kibinadamu!!!!!!!!!!!!!!!!!mjinga mpe mda
 
Yes, nilikuwa nina maana hiyo na nimebadilisha. Thanks kwa dokezo.


Ninakubaliana na point yako lakini huoni kuwa kuna matatizo mbele kwa sababu kama wameishasema hawawezi hata kulipia 10% ya mchango wa muungano ina maana hakuna faida ya kuwa na muungano kwa Tanganyika.

Kama anasema ili kutetea kisiasa hoja ya Serikali mbili basi hajui kuwa angalizo lake linatufanya tuhoji mchango wa Zanzibar katika muungano huu uliopo na faida ya Tanganyika kuwepo ndani ya huu muungano ambao bila hata kuchunguza kwa undani ni ukweli kuwa Tanganyika inabeba gharama za Tanganyika na pia muungano achilia mbali utumishi ambao unawanufaisha Wazanzibar kwenye 50-50 wakati idadi yao yote ni kama mkoa mmoja wa Tanganyika.

Mimi nilishasema muda mrefu kuwa hatuhitaji Muungano kwa sasa. Ni bora kila nchi ibebe mzigo wake na tukutane kwenye mashirikisho kama SADC, EAC, COMESA, AU n.k.
Ikiwa hawawezi kugharamia muungano wataweza kweli kuchangia gharama za mashirikisho hayo? Mimi bado naunga mkono muungano lakini kwa uwazi ili Kila upande ufaidike lakini pia uwajibike. Masimango hatutaki, maana kuna kauli kuwa tunawaziba, tunawaibia, tunawanyima nafasi za ubalozi n.k.
 
Ikiwa hawawezi kugharamia muungano wataweza kweli kuchangia gharama za mashirikisho hayo? Mimi bado naunga mkono muungano lakini kwa uwazi ili Kila upande ufaidike lakini pia uwajibike. Masimango hatutaki, maana kuna kauli kuwa tunawaziba, tunawaibia, tunawanyima nafasi za ubalozi n.k.
Znz hawataki kuwajibika kwa lolote lile. Wanachotaka ni vyeo, nafasi za kazi, kuruhusiwa kuingiza bidhaa zo bila kodi na kila aina ya ubwanyenye na umwinyi. Hawana kitu kinaitwa gharama katika misamiati yao.

Hao waliokwenda Dodoma wamegharamiwa na ofisi ya makamu wa rais amabyo inagharamiwa na Tanganyika.
Hawagomi kwenda kwenye pesa, tatizo wakishapewa pesa midomo na maneno machafu kuliko maliwato.

Hivi nani anaweza kwenda kumdhulumu mtu mwenye uchumi kama wa znz. Lakini soma watu wao wanavyodai, eti wanadhulumiwa!

Huyo jamaa yao amesema ukweli kabisa nasi tunasema Tanganyika itakuwa kwa watanganyika.
Niliwahi kusema hawa watu hawajui wanatafuta nini. Nikawashauri waondoke katika muungano maana wao hawana muungano, wamebebwa tu. Bilioni 240 ni pesa za kuendesha wizara moja kwa mwezi sasa watoe nini.

Hizo hesabu alizosema jamaa tuliwahi kuziweka hapa na kusema serikali 3 bado ni zigo kwa Mtanganyika maana hiyo ya tatu atahudumia nani? Wamekimbia kimbia hoja lakini mwisho ukweli unajitokeza.

Tanganyika watakuwa wajinga kama wataendelea kuumiza watoto wao na raia wao kwa kodi kisa kuhudumia wapiga kelele. Acheni waende zao! tunawahitaji kwa lipi hasa! hakuna !
 
Mwiba, gombesugu,

..Zanzibar ni ndogo kieneo na kiuchumi.

..kuitia ktk muungano na Tanganyika ni kutafutana ubaya na lawama.

..haya mambo tumekuwa tukiyasema kwa muda mrefu sana hapa JF.

..tunaposema hayo wengine mnafikiria tumeamua kuwavunjia heshima lakini huyo mwakilishi kasema ukweli.

..labda nikupeni mfano mdogo: kabla ya mapinduzi Znz majimbo ya uchaguzi yalikuwa hayazidi 30. sasa hebu angalia wakati huu tuna muungano Znz ina majimbo mangapi ya uchaguzi? majimbo yameongezwa Znz ifanane-fanane na Tanganyika.

cc Nguruvi3, Barubaru

yapo 50 tu
 
Last edited by a moderator:
hizi sarakasi za kina Jussa & co. lengo lao ni kuvunja muungano wala sio serikali tatu!

mkiti wa kamati kauli zake zinachefua na wachangiaji wanatoa hoja kama wapo kijiweni. Hakuna cha kujifunza hakuna kufaidika. Poor jamii forums
 
Tulieni! kasemea mwenzenu kuwa bajeti ya ulinzi na usalama ni trilion 1.3 ninyi bajeti ni 240bilioni. Lini Tanganyika itaitegemea znz. Leo tuna ushahidi kuwa kwa miaka 50 tumekuwa tunawalipia gharama halafu mnadai vyeo na nafasi za kazi.

Tume ya warioba znz 0 haikutoa hata senti tano. Mchango wa znz ni kukimbilia wajumbe sawa. Aly Salehe kapata ajira kimya. Bunge la katiba gharama zake hamuwezi kuchangia hata 1/8, mchango wenu vyeo na nafasi za ajira.

Hatuwahitaji, msije katika bunge la katiba,period. Tumechaoka kuwabeba mkicheza mdumange.



Nguruvi3

Mkuu huyo hajasema kwa wazanzibar kasemea CCM na pia Tanganyika bajeti yake haijulikani na wala Tanganyika haipo ama unataka kunambia Tanzania ndio Tanganyika halafu mijitu mwengine bwana unatulipia gharama zipi na mshirika mwenza hayupo (Tanganyika) sisi tutajua nyinyi munachangia ngapi halafu TANZANIA NI LINI NA MWAKA GANI ILOTOA BAJETI YAKE YENYEWE BILA YA MSAADA KUTOKA KWA WAFADHILI mwenye ushahidi alete kujisifu kwingi sisi tunawasaidia tunawasaidia munatusaidia nini na walipa kodi wengi karibu ya wote ni sisi nyinyi wauzaji karanga na shanga barabarani na elimu na vyeti vyenu vya kuunga nyambaff kabisa.

Kuwa sawa katika wajumbe ni haki yetu si ombi musitugeuza yatima haki yetu mukaona kama munatugaia.


Fufueni Tanganyika halafu twambie tusije katika bunge sasa utakua huna adabu kutwambia tusije wakati mshirika mwenza kafa lakini marupurupu anachukua.


Tuwachieni Tupumue mtajua kama sisi kidogo bajeti ndogo ama sehemu ndogo ZNZ ILISTAARABIKA KABLA YA TANGANYIKA NA UWEZO WA KUFANYA HIVYO TENA TUNAO.
 
Hakuna pesa Tanganyika inadaiwa.
Ninyi hamjui kuhusu mgao mnaoupata kila mwezi. Hamjui huduma ambazo mumezipata kwa miaka 50 na leo watu wenu wanaweka wazi kabisa kuwa muungano uliendeshwa na kodi za Watanganyika.

Vunjeni muungano mdai machodhani kama hamtajikuta mnauza kisiwa chote.

Tumewaambi siku nyingi kuhusu gharama za muungano. Leo maji yamewafika shingoni mnalalamika kuhusu udogo.

By the way ninyi vijana wa Tanganyika mliokosa mikopo iulizeni serikali yenu kwanini mkose mikopo ili hali pesa za kodi za baba zenu zinakwenda ZNZ kwa mikopo ya wananfunzi wa 1) Kusoma bila kurudisha mikopo 2) Kupewa hata nafasi zenu kwasababu tu ya uzanzibar..
Eto hawataki muungano wakati wapo Dodoma! thubutu nani asiyependa sh ya Tanganyika!

Wanajiandaa kuongeza wajumbe waje kwenye bunge la katiba badala ya kuwakataza, huku uvunguni mwa vitanda wanapiga domo hawataki muungano.

Tumechoka kusikia kelele zenu tuna mambo mengi ya muhimu. Hatuwezi kuishi kwa kuwabeba mkicheza msewe halafu mnataka vyeo na ajira. This time around pasu pasu kama hamtaki njiaa nyeupee bandarini rudini mkaijenge znz ya pembe za ndovu na watumwa. Znz iliyokuwa inagawa sambusa barabarani na mapilau katika vituo vya mabasi, znz yenye neema.

Tuwabebe halafu mtukane! ebo! leo mnasema bila haya hamjiwezi! mkiondoka hapo mumechukua posho mnaelekea bandarini na matusi. Posho za Mtanganyika! tumechoka kelele na midomo yenu.
Tatizo leni si muungano ni jingine linalohitaji kampeni ya Lowasa.



Mkuu


Naona ufahamu wako uko mbaali sana na sijui ulikua unapata ngapi form six ama form four HAKUNA KITU KINAITWA TANGANYIKA UNLESS UNAMBIE TANGANYIKA NDIO TANZANIA halafu me nataka kujua munatubeba wapi wakati bajeti ni ya msaada kwa tanzania siwafahamu ujuwe halafu sisi tunajulikana tunatoa ngapi jeee Tanganyika ilojificha inatoa ngapi
 
Nguruvi3

Mkuu huyo hajasema kwa wazanzibar kasemea CCM na pia Tanganyika bajeti yake haijulikani na wala Tanganyika haipo ama unataka kunambia Tanzania ndio Tanganyika halafu mijitu mwengine bwana unatulipia gharama zipi na mshirika mwenza hayupo (Tanganyika) sisi tutajua nyinyi munachangia ngapi halafu TANZANIA NI LINI NA MWAKA GANI ILOTOA BAJETI YAKE YENYEWE BILA YA MSAADA KUTOKA KWA WAFADHILI mwenye ushahidi alete kujisifu kwingi sisi tunawasaidia tunawasaidia munatusaidia nini na walipa kodi wengi karibu ya wote ni sisi nyinyi wauzaji karanga na shanga barabarani na elimu na vyeti vyenu vya kuunga nyambaff kabisa.

Kuwa sawa katika wajumbe ni haki yetu si ombi musitugeuza yatima haki yetu mukaona kama munatugaia.


Fufueni Tanganyika halafu twambie tusije katika bunge sasa utakua huna adabu kutwambia tusije wakati mshirika mwenza kafa lakini marupurupu anachukua.


Tuwachieni Tupumue mtajua kama sisi kidogo bajeti ndogo ama sehemu ndogo ZNZ ILISTAARABIKA KABLA YA TANGANYIKA NA UWEZO WA KUFANYA HIVYO TENA TUNAO.

kiduchu angalau na kwa mbali naona mwangaza kutokana na mchango wako
 
Mkuu


Naona ufahamu wako uko mbaali sana na sijui ulikua unapata ngapi form six ama form four HAKUNA KITU KINAITWA TANGANYIKA UNLESS UNAMBIE TANGANYIKA NDIO TANZANIA halafu me nataka kujua munatubeba wapi wakati bajeti ni ya msaada kwa tanzania siwafahamu ujuwe halafu sisi tunajulikana tunatoa ngapi jeee Tanganyika ilojificha inatoa ngapi

siyo six wala 4 hiyo ni udom anayoitolea masimbulizi.
 
Kweli Zanzibar ni ndogo kieneo ila kiuchumi sidhani kama ilikuwa hivyo ila baada ya huu Muungano ndio mmetutilia ufukara na kutufanya tuwe watu duni sana ,mnataka tuwe tunategemea kila kitu kutoka huko Tanganyika na ndio kama inavyoonekana katika hoja zenu ,nyie nchi ndogo sijui uchumi wenu mdogo ,hebu ulizia na katafute historia ya Zanzibar ,Zanzibar wakati kabla ya Muungano ilikuwa vipi na ilitoa msaada kumsaidia nani ? Yakhe huu Muungano ukifa leo basi nakuhakikishieni machogo ,hautapita muda mrefu tutawasaidia tena tutawasaidia kwa ari na mori na moyo wa jeuri ,huko Tanganyika hamna kitu mmekalia kuti kavu. lazima mtapigana mapanga tu !

"machogo" ni akina nai hao!
 
Mkuu


Naona ufahamu wako uko mbaali sana na sijui ulikua unapata ngapi form six ama form four HAKUNA KITU KINAITWA TANGANYIKA UNLESS UNAMBIE TANGANYIKA NDIO TANZANIA halafu me nataka kujua munatubeba wapi wakati bajeti ni ya msaada kwa tanzania siwafahamu ujuwe halafu sisi tunajulikana tunatoa ngapi jeee Tanganyika ilojificha inatoa ngapi
Mwenyekiti wa kamati yako kasema hamtaweza kwasababu mapato yenu ni bilioni 240.

Hapo hakuna bajeti ya ulinzi, mambo ya ndani, elimu ya juu achilia mbali mishahara na mambo mengine

Jiulize kwa bajeti ya znz ya bilioni 700 na mapato ya bilioni 240 pengo linazibwa na nani.

Nikuulize tume ya warioba mumechangia kiasi gani?
Bunge la katiba mtachangia kiasi gani.

Kelele kila siku mnanyonywa wakati ni kupe wakubwa.!
 
Ukweli umetimia sasa wanahangaika. Uongo wa kusema Tanagnyika inawanyonya sasa hadharani.

Kitu cha ajabu sana ni hao hao wanataka tume iwe asilimia 50, wanataka bunge la katiba liwe asilimia 50. Wanataka viongozi wa muungano na wafanyakazi wa serikali ya muungano wawe nusu kwa nusu.

Tumewahi kuwaeleza mara nyingi sana wazanzibar akiwemo Jusa na Ahmed Rajab kuwa Tanganyika haihitaji znz kwa lolote. Hatuhitaji znz ila znz inatuhitaji sana.period.

Ona sasa imefika wakati wa gharama wanajichafua nguo hovyo. Wale wanaosema Tanganyika inawanyonya znz wajiulize kama mwenyekiti wa kamati anasema hawana uwezo, Tanganyika inawanyonya wapi.

Hawa watu wamefundishwa ujinga wa kuamini maneno ya mitaani bila ushahidi wa kiuchumi.
Tunasema hivi serikali ni tatu na kila mmoja achangie sawa.
Muda wa kubeba watu migongoni wakitukana hovyo iumekwisha.

Hiki ni kijimkoa tu lakini kelele tu wamejaaliwa. Tutakomaa hadi mtaomba radhi kwa maneno yenu machafu.
Wananyanyua pua eti muungano ni nchi mbili wabia sawa. Thubutu, wabia sawa wakati wewe unachangia maneno na kelele ! usawa wa ubia upo wapi.

Wewe unavia kodi za Mtanganyika halafu unasema ubia sawa. Hawa watu waajabu sana.
Leo wanasema hawana uwezo na wakati wa kujadili muungano hali ya uchumi iangaliwe.
Ni hawa hawa walikomaa tume iwe na wajumbe sawa. By the way hawajui gharama za tume wala za bunge la katiba.Kelele zitawatokea puani this time

fungeni midomo na muwe na adabu. Shikeni adabu, muungano uchumi si mipasho na taarabu.
Leteni kitu mezani si kuvizia nafasi za urais wa zamu na uwaziri. Kupe wakubwa mninyi.

Mkome kusema mnanyonywa, nani anyoinye mnasikini wa mapato kama yenu.
Mkome kudai vyeo msivyojua gharama zake. Matabaki chini ya kivuli cha Tanganyika kwasababu hamna uwezo.period

GHIBUU takashi Jusa Jasusi JokaKuu Kakke Jasusi Nonda gombesugu Zinedine FJM

Link Warioba: Serikali ya Muungano haitakopa fedha - Kitaifa - mwananchi.co.tz
 
mwenyekiti wa hio kamati hebu na itafutwe hio cv yake ipimwe na kiwango cha elimu hasa kwenye uchumi. Kelele hizi zishakuwa nyingi na zishajibiwa na wengi tu, kuanzia general ulimwengu, warioba na wengi tu. hawa wengine kujikomba tu kwa faida zao wenyewe, wanashindwa kulipa hata umeme kwa wahusika wakati Zanzibar hakuna asielipishwa umeme, unaishia kwenye mifuko yao ya kampeni za ccm. unategemea aseme nini? Nchi ya watu milioni moja iungane na milioni arubaini halafu tuchangie sawa lakini wakati wa ruzuku kwa nini basi tusigawane sawa. formular za ccm hazina mashiko, kila kitu kinaendeshwa kwa nguvu theory.. Ikiwa tutagawana mgao wa nusu kwa nusu kwa nini tushindwe kuchangia gharama sawa? na ikiwa hatuwezi kugawana ruzuku kwa nusu kwa nusu kwa sababu ya population kwa nini tuchangie nusu kwa nusu pia? Ati mwenyekiti wa kamati ya uchumi, elimu darasa la saba ulitegemea nini?
 
I am not a prophet of doom, but I have said before, this relationship is in the rocks and we will witness its end in few years!
Though it has persevered for 50 odd years, it was not built on firm socio economic and political foundation. Its survival depended on political will of its founders.
ila na sema, majuto ni mjukuu, waswahili walinena. Tukumbuke kila alichosema Mwalimu Nyerere huwa kina kuja tokea. Unfortunately watakaokuja kujuta ni generatiin ijayo na ambao itatulaani sisi kwa kutokuona matokeo ya maamuzi yetu AMA Yale ya jazba ( bara) au ya kitumwa ( visiwani)


Ni mtazamo tu
 
mwenyekiti wa hio kamati hebu na itafutwe hio cv yake ipimwe na kiwango cha elimu hasa kwenye uchumi. Kelele hizi zishakuwa nyingi na zishajibiwa na wengi tu, kuanzia general ulimwengu, warioba na wengi tu.

hawa wengine kujikomba tu kwa faida zao wenyewe, wanashindwa kulipa hata umeme kwa wahusika wakati Zanzibar hakuna asielipishwa umeme, unaishia kwenye mifuko yao ya kampeni za ccm. unategemea aseme nini?

Nchi ya watu milioni moja iungane na milioni arubaini halafu tuchangie sawa lakini wakati wa ruzuku kwa nini basi tusigawane sawa. formular za ccm hazina mashiko, kila kitu kinaendeshwa kwa nguvu theory.. Ikiwa tutagawana mgao wa nusu kwa nusu kwa nini tushindwe kuchangia gharama sawa? na ikiwa hatuwezi kugawana ruzuku kwa nusu kwa nusu kwa sababu ya population kwa nini tuchangie nusu kwa nusu pia? Ati mwenyekiti wa kamati ya uchumi, elimu darasa la saba ulitegemea nini?
Kwani Warioba, Jenerali walisema nini?

Pili, umeme ni wa bure znz haijawahi kulipa. Kama kuna matatizo ni yenu sisi tunajua hiyo ni ruzuku mnayopata.
Wala si umeme, hata vijana wenu wanapata mikopo hata kama wana div 5 kwasababu tu ni wazanzibar.
Hawarudhidhi mikopo hiyo na wanapewa nafasi za Mtanganyika kwa vile tu ni raia bora za znz hata kama ni kwa gharama za kodi zetu na za watoto wetu.

Kijana wa Kitanganyika anasaga lami, hili si kosa lenu ni letu na tumeshalifanyia kazi.
Ndio maana tunawaeleza vijana wa kitanzania angalieni baba zenu wanalipia kodi kusomesha vijana wa nchi jirani yenye bendera, wimbo wa taifa na kila kitu isiyoweza kusomesha watu wake. Hamlioni hilo?

Tatu, wakati mnadai tume ya Warioba hamkuangalia population.
Mlisema ni nchi mbili huru zikae meza moja. Mkapewa wajumbe 15 bila nyongeza ama kupunguzwa.
Bunge la katiba mumetaka wajumbe sawa kwasababu ni wabia na hilo mumefanikiwa pia.

Mnataka rais wa Muungano awe kwa zamu, nafasi za ajira na utawala ziwe sawa. Hayo ni madai yenu.
Linapokuja suala la gharama mnaruka kimanga na kurudi katika population na eneo!
Hapo hakuna akili kwasababu unapodai haki unaidai jumla. Huwezi kudaia mafao usiyochangia huo ni ukupe na unyonyaji, mtaacha lini enyi wznz? Hivi nani alikuambieni mnatakiwa mpewe tu bila kuchangia!

Tunasema hivi muda wa kupitisha bakuli sasa basi, lazima mchangie si kudai nafasi za kazi na vyeo. Akili hiyo haifai katika karne hii. Kama humuwezi rudini katika znz ya ndovu na utumwa, manukato, kashata na piala za sultani. Miaka 50 sasa mnatakiwa mkue. Wekeni kitu mezani si kelele mipasho na majungu! aa !

Huwezi kutaka upewe kila kitu kwa mteremeko wakati wa kupanda unataka kudandia mgongoni.
Hakuna hata siku moja viongozi wanaofikiria kwa niaba ya wazanzibar wanongelea gharama. Hakuna!
Wanajua kuwa likija suala la gharama ni mwiba kwao. Mnachokiweza ni kuvizia ajira,vyeo baasi

Niambie lini umemsikia Maalim, Jusa au Ahmed akikokotoa namba za gharama.
Hilo hawalioni hata kwa bahati mbaya na ndio maana wznz hawaoni pia.

Ni ukweli kuwa mapato yenu hayawezi kuendesha wizara hata moja ya muungano.
Mfano aliotoa huyo mwenyekiti tumeshauweka JF siku nyingi.

Gharama za ulinzi na mambo ya ndani ni takribani 1.3 trillion. Mapato yenu ambayo hayatetegemea msaada wa Tanganyika hayafiki hata robo. Ukitaka kuchangia ni lazima znz itoe kila senti. Huo ni ukweli msiotaka kuusikia lakini ni ukweli.

Hatuwezi kuendelea kubeba watu migongoni wakicheza msewe na kunywa toga kisha kuporomosha mitusi.
This time around tumewaonyesha uongo wenu wa kufundishwa kuhusu kunyonywa halafu tutakaza uzi.
Hakuna msamaha kwasababu serikali 2 hazikubaliki tena. Tumechoka kubeba mizigo tunataka tupumue.

Mna hiari ya kwenda Dodoma au kukataa muungano ufikie hatima.
Mkienda Dodoma makao makuu yatakuwa hapo si michenzani na Tanganyika itakuwa Tanganyika wala haitalingana na znz kwa lolote kwa chochote. Tanganyika haiwahitaji, kwa lipi?

Mapato yenu ni bilioni 240 kasema mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLW. Hizo ni pesa za wizara hya elimu ya juu ambayo haipo katika mambo ya muungano lakini inatoa kwa SMZ tena kwa gharama za vijana wa Tanganyika.

TUACHENI TUPUMUE

 
I am not a prophet of doom, but I have said before, this relationship is in the rocks and we will witness its end in few years!
Though it has persevered for 50 odd years, it was not built on firm socio economic and political foundation. Its survival depended on political will of its founders.
ila na sema, majuto ni mjukuu, waswahili walinena. Tukumbuke kila alichosema Mwalimu Nyerere huwa kina kuja tokea. Unfortunately watakaokuja kujuta ni generatiin ijayo na ambao itatulaani sisi kwa kutokuona matokeo ya maamuzi yetu AMA Yale ya jazba ( bara) au ya kitumwa ( visiwani) Ni mtazamo tu
Ni kweli unachokisema lakini pia tuangalie pande zote kwa undani. Tanganyika hawajawahi kuzungumzia kuhusu muungano ingawa wao ndio wameubeba na mzigo wake.

Ulimwengu umeanishwa kuwa Tanganyika yenye bajeti ya trillion zaidi ya 10 inaiba kutoka bilioni 240.
Tumesikia kelele za kutaka vyeo sawa, kila jambo wenzetu wanataka usawa. Ukisema gharama wanasema hizo ni za Mtanganyika, sasa hapo kuna muungano au kunyonyana tu.

Sisi tumewaeleza siku nyingi njia nyeupee wakitaka. Wamekimbia fursa zaidi ya 10 za kuvunja muungano. Na ya mwisho ni bunge la katiba. Utashangaa walikuwa Dodoma katika semina ya muungano ule ule wasioutaka.
Hatuwezi kuishi na watu wasiokuwa tayari kutoa bali kufikiria ajira na veyo.

Let it be, hatuna cha kupoteza na laana ya mzee itawatafuna maana sisi tumevumilia hadi tumechoka.
Hivi bilioni 240 unaenda kuiba nini, hilo si tusi kweli.

Waache waende znz ya ndovu na utumwa, znz iliyokuwa na umeme wa meli na TV za rangi. Znz ilitokuwa na makaimati barabarani na chupa za chai kila baada ya nyumba 10 nje. Waacheni wakaifuate neema.

Tuacheni tupumue, kha! eti tuibe biioni 240! tena si zote kha! huku si kumuibia mgonjwa! dhambi ya nini hiyo.
Let them go!
 
Hivi Tanzania tuliyonayo sasa hivi ndiyo Tanganyika naombeni kufahamishwa naona watu wanaitaja kwa bashasha Tanganyika.
 
Back
Top Bottom