Zamu ya Zanzibar Urais 2015?

Hicho kipengele kilifutwa mwaka 1992 wakati tunaanzisha mfumo wa vyama vingi.
Hata mswala ya makamu wa rais kutoka zbar kwa sasa siyo lazima just wanafanya hivyo ili kuupa muungano nguvu.

Mkuu,

Kutokana na maelezo uliyoyatoa...

Kwa hiyo ni kusema muungano haupo tena, kinachoendelea ni usanii tu
 
Mkuu,

Kutokana na maelezo uliyoyatoa...

Kwa hiyo ni kusema muungano haupo tena, kinachoendelea ni usanii tu
Muungano upo mkuu ....Ila tumeungana kwenye baadhi ya mambo kama sikosei ni ardhi na resources zake, Idara za mambo ya nje and lastly kwenye swala la majeshi mkuu.
Mambo mengine zbar wanajitegemea kila kitu ndo maana kule kwao wana wizara zao pamoja na source ya mapato kupitia zanzibar revenue board ZRB.
 
Hicho kipengele kilifutwa mwaka 1992 wakati tunaanzisha mfumo wa vyama vingi.
Hata mswala ya makamu wa rais kutoka zbar kwa sasa siyo lazima just wanafanya hivyo ili kuupa muungano nguvu.

Mkuu ,
kama haya usemayo ni hivyo basi tumejitengenezea mazingira ya kuuvunja Muungano.
kama tunawaingiza kwa hisani tu lakini hakuna ulazima kuna siku tutaamua kuwa tusiwangize ..ndio maana yake au vipi?
sasa ndio ujanja huu??...kweli viongozi wetu hawako makini. hawafikri mbali.
 
Muungano daima, wenye ndoto za kuuvunja wataona utakavyo shamiri miaka si mingi ijayo..
 
Muungano daima, wenye ndoto za kuuvunja wataona utakavyo shamiri miaka si mingi ijayo..

Muungano hauna ridhaa/nguvu ya watu ni udongo wa zenj na Tanganyika tu ulio wekwa kwenye kwenye kibuyu tu na kukorogwa kwenye kikapo inawezekana kile kikapo walicho korogea huo udongo ni cha ushirikina Mungu utunusuru! Kumbe basi isipo tafutwa ridhaa ya wananchi wa pande zote mbili tena haraka basi huu muungano wa kisanii kwisha kwisha kabisa mbende mbendeee! na naomba dua Mungu akuweke hai uone kwa macho yako muungano ukifa sema INSHAALAH;!
 
Si kweli, hiyo thread yako imekosa data. Kwanza hakuna kitu kama article of association badala yake kuna article of union.

Na article hiyo imekuwa ikiongezewa vipengele kadhaa mara kwa mara. Kwa mfano, Aticle ya kwanza kbs ya mwaka 1964 iliainisha mambo 11 tu kama UNION MATTERs. Lakini kwa sasa mambo hayo yameongezwa na kufikia 33.

Cha msingi unachopaswa kujua ni kuwa Article of union halisi ya mwaka 1964 ni siri sana na haijawahi kuonekana hadharani.

Na hii inatokana na mambo makubwa mawili. Kwanza haijaainisha kimsingi masuala ya muungano, pili ambalo ni kubwa zaidi iliweka ukomo wa muunganno ni mwaka 1974.

Kwa mujibu wa makubaliano ya Mwalimu na Karume, ni kuwa muungano uwe wa miaka kumi na baada ya miaka hiyo kumi kama kila upande utaridhia basi waongeze mingine kumi.

Hivyohivyo waendelee kurenew kulingana na makubaliano ya vioogozi wetu na maridhiano ya wananchi wa pande znte.

Lakini ilipofika mwaka 1972 mzee Karume alionekana kuchoshwa na muungano hali iliyomfanya aonekane kuwa ikifika mwaka 74 hatakubali kurenew mkataba.

So inadaiwa zikapikwa njama za kumuua. Ndio maana hadi leo kifo chake ni utata mtupu.
mkuu,
hiyo document halisi inapatikana wapi? au japo kivuli cha hiyo doc. halisi.tudokeze ili tuifatilie. au kama unayo mdondoshee invinsible atufanyie kweli.
Itasaidia sana katika ku/solve some of the Union mysteries.
 
Kuna tetesi kwamba kwakuwa ccm maji yamekuwa ya shingo kisiasa, na kufukuzwa kwenye uongozi magwiji wa ufisadi kunategemewa mpasuko zaidi kwenye chama, Jk ataandaa mswada wa uchaguzi wa Urais mwaka 2015 Rais atoke Zanzibar ili Chama cha Democrasia na Maendelo (CDM) kisiweze kuiua CCM.

Wasiwasi mwingine ni kwamba, baada ya kuvunja CC na kuunda mpya, bado wananchi wanaona hakuna kilicho badilika kwani mtoto wa nyoka ni nyoka, kujivua gamba nyoka anabaki ni yule yule na tabia yake na udhaifu unabaki kama ulivyo na kwamba safari hii CCM imeibua siasa za kifamilia za kurithishana kwenye uongozi,
mfano
  • Mnauye alikuwa kwenye siasa na mwana sasa yuko ccm,
  • Mwinyi alikuwa Rais na sasa mwanae anaandaliwa kuwa Rais Zanzibar,
  • Karume alikuwa Rais mwanae naye kawa Rais
  • Makamba alikuwa kiongozi wa ngazi za juu na sasa mwanae naye kamfagilia njia kuwa kiongozi hivi sasa.
  • JK naye anapalilia Rizi kuwa kwenye uongozi wa juu wa ccm.
  • Kwakutaja hayo ni machache wako wengine wengi nikiandika kila mmoja nitawachosha.

Kwa hofu ya huu upuuzi wa siasa za ki-falme na za kifamilia, wana hofu ya CDM kuwapokonya utawala, hivo wanataka kumanuva ili Rais 2015 kutoka Zanzibar kama ilivyokuwa kwa baba wa taifa enzi zake hivo kudhoofisha chadema.

Wadau hili mnalionaje? Kweli nchi hii itasalimika? Mi Siu-mind Muungano hata kidogo! Nawasilisha
 
Muswaada wa aina hiyo hauwezi pelekwa bungeni. Lakini ktk rafu wanazofanyiana ndani ya chama chao. hizo tetesi kwamba anataka kuwabeba wazanzibari kwamba ni zamu yao kutoa mgombea wa urais wa JMT kwa tiketi ya CCM zipo! Maoni yangu ni kwamba CCM hata imlete mgombea wa aina gani 2015 uhakika wa kushinda kama walivyokua wamezoea hakuna!
 
Naona ya egypt na tunisia yanachelewa sana hapa kwetu................
 
  • Thanks
Reactions: JGG
Thubutu, rais ajaye lazima awe Mkatoliki na atokee bara chama kitakachopinga hili kitaisikia ikulu kwenye video
 
Kumaintain family tree inawaweka pazuri kwa kuendelea kutumbua utajiri waliojilimbikizia wakiwa watawala bila hofu ya kuface mkono wa sheria.
 
Kumaintain family tree inawaweka pazuri kwa kuendelea kutumbua utajiri waliojilimbikizia wakiwa watawala bila hofu ya kuface mkono wa sheria.

Hii isikupe shida sana rais ajaye hayumo katika list of shame so ushamjua mkuu
 
Kumaintain family tree inawaweka pazuri kwa kuendelea kutumbua utajiri waliojilimbikizia wakiwa watawala bila hofu ya kuface mkono wa sheria.

CDM hilo walitambue, wasije jikuta wanatafuta mgombea zanzibar bila mafanikio.
 
Nimekuwa nikihangaika sana kuuliza dhambi na makosa yaliyomfanya Salim A.Salim kushindwa kupata nafasi ya kuongoza nchi hii eti tu kwa mizengwe ya CCM ooooHizbu na kadhalika. Sasa nadhani magamba wameelewa walikosea kumchafua Salim na sasa wanataka mgombea atoke Zanzibar ili Salim aweze kuongoza na kufuta record chafu ya CCM ktk kipindi chote cha JK.

Watanzania tunasikitika tumepiga maktaimu sana kwa kukosa uongozi bora miaka hii kumi sasa bora Salim arudi na tunamuomba asikatae (huenda akasusa kwa vile walimkataa na kumuaibisha).

Ni mawazo tu, kama unadhani mwingine pia ataweza kutuongoza 2015 basi usisite kumtaja vinginevyo CCM uozo hawa watatuletea tena kiongozi mwenye kichwa cha nazi atuongoze.
 
Usishangae ukimuona Butilda buriani, Philip Marmo au Masha kusimikwa kama wagombea. Hii serikali nimeizalau kuliko kitu kingine chochote. Kwa sasa nikiwa CCM nikiteuliwa na JK nitaanza kujistukia kuhusu uwezo wangu, maana kama nina uwezo mzuri nitajiuliza kwanini sasa kanichagua?
 
Back
Top Bottom