Zabibu!

Tunda zabibu silifagilii
Utamu wake haunivutii
Hata ufanye bidii
Kunishawishi sintokutii


Tunda nilipendalo asilani
Ni Embe dodo la kijijini
Lina utamu uso kifani
Hasa likiivia mtini


Zuri likiivia mtini
Zabibu haioni ndani
Saba mara sabini
Daima lawa namba wani

Wewe Mzee wa kijijini
Kula zabibu umeanza lini
Waachie watu wa mjini
Zabibu iwe mwao akilini

Embe dodo la thamani
Likianguka toka mtini
Linalala mchangani
Kisha najiokotea kiualini

Ninalimenya kwa mbwembwe
Mithili ya Mwanamazingaombwe
Daima nalila kwa mbwembwe
Na umakini kama Zitto Kabwe
 
Wewe Mzee wa kijijini
Kula zabibu umeanza lini
Waachie watu wa mjini
Zabibu iwe mwao akilini

Balantanda usimzalau mzee wa kijijini ooh! shauri yako

anyways i am otu for the day!....see you all manyana...i got go cook for my cupcake.you know how it is inabidi na mimi nipalilie shamba langu maana mimi ni tunda uwii!...

xoxo
 
Balantanda usimzalau mzee wa kijijini ooh! shauri yako

anyways i am otu for the day!....see you all manyana...i got go cook for my cupcake.you know how it is inabidi na mimi nipalilie shamba langu maana mimi ni tunda uwii!...

xoxo

Yeah,always bradha awe first bwana...Thank God he found you 'embe dodo'
 
I know... didn't I say I'm a first learner too?

Zabibu ukijapewa
Hilo utalichukuwa
La bure ukimegewa
Utalila kama muwa?

Vipi kama bado bichi,
Tena kijani kibichi,
Utatusa kuwa mbichi
Au hata hivyo huliachi?

Vipi ukilingishiwa,
Kinywani kupitishiwa
Ulimini kuonyeshwa
Kisha likaondolewa?

Langu mie si zabibu
Nasema bila aibu
Ndizi iso mahasibu
Sebenzwayo taratibu

Lako katu sitamani
Hata kwa kisu shingoni
Tunda hilo la ugoni
Halifiki kisogoni
 
kwi kwi kwi kwi kwi............JF is soooo funny.... I Love JF wallah
 
jamani tunda nanasi
kula uwe na nafasi
unapojaa ukwasi
hautajifaidia

kwa chakula cha mchana
mezani kimejazana
juisi yake mwanana
hakika utasifia

nanasi liwe shinani
wachuma kiulaini
hakuna purukushani
mkononi wachukua

Embe dodo kule juu
hadi lidondoke puu!
kweli kwa mtaji huu
hupaswi kulisifia

jamani hizo zabibu
hasa alolima babu
sana sana kwa ulabu
kama wataka kulewa

nakukaribisha kwangu
leo maulidi yangu
ule nanasi mwanangu
ni tamu tena murua
 
Haiba yake machoni
Furaha tele moyoni
Toka ganda hadi ndani
Livutie utamani

Hizo ndogo mdomoni
Zaishilia kooni
Hilo nalo na shinani
Sitamani muwashani

Langu laja kwa mafungu
Uchaguzi ni wa kwangu
Nabeba wote mkungu
Hadi kunako uvungu

Sijali zielemee
Siziachi zilegee
Watu,ndege hata mee
Siwachi wakodolee

...kimya kimya...
 
Last edited:
Haiba yake machoni
Furaha tele moyoni
Toka ganda hadi ndani
Livutie utamani

Hizo ndogo mdomoni
Zaishilia kooni
Hilo nalo na shinani
Sitamani muwashani

Langu laja kwa mafungu
Uchaguzi ni wa kwangu
Nabeba wote mkungu
Hadi kunako uvungu

Sijali zielemee
Siziachi zilegee
Watu,ndege hata mee
Siwachi wasodolee

...kimya kimya...


Wewe kula hizo ndizi,
Wengine wala andazi,
Hata ule tangawizi,
Zabibu tunda la kazi!

Hadi umenye maganda,
yale yalogandaganda,
Ndiyo ule lako tunda,
Hilo unalolipenda.

Uzuri wake zabibu,
Kula kwake siyo tabu,
Mdomoni taratibu,
Nafyonza kama tabibu.

Ndizi ina ukakasi,
Ulimini kama pasi,
Zabibu ladha halisi,
Mwenyewe najinafasi!

Mundu kasema nanasi,
Kwangu halina nafasi,
Zabibu siwezi asi,
Nisije jipa mkosi!

Zabibu ninalo hamu,
Mengine siyo matamu,
Nitalila kitaalamu,
Kama nilivyo mwalimu!
 
jamani tunda nanasi
kula uwe na nafasi
unapojaa ukwasi
hautajifaidia

kwa chakula cha mchana
mezani kimejazana
juisi yake mwanana
hakika utasifia

nanasi liwe shinani
wachuma kiulaini
hakuna purukushani
mkononi wachukua

Embe dodo kule juu
hadi lidondoke puu!
kweli kwa mtaji huu
hupaswi kulisifia

jamani hizo zabibu
hasa alolima babu
sana sana kwa ulabu
kama wataka kulewa

nakukaribisha kwangu
leo maulidi yangu
ule nanasi mwanangu
ni tamu tena murua

Taja matunda yako yote
Yapatikanayo kotekote
Nanasi na mengine yote
Dodo tamu kuliko yote

Nanasi lina ukakasi
Kulila lataka nafasi
Nikila nina wasiwasi
Meno kupata ukakasi

Embe dodo nalipenda
Siliachi hata ukiponda
Mjini kijijini ukienda
Watu wengi walipenda

Hakika Dodo namba wani
Kuliko hata dafu la Pwani
Ukija kwangu ewe mgeni
Dodo daima lipo mezani.


Litaendelea……
 
Wewe kula hizo ndizi,
Wengine wala andazi,
Hata ule tangawizi,
Zabibu tunda la kazi!

Hadi umenye maganda,
yale yalogandaganda,
Ndiyo ule lako tunda,
Hilo unalolipenda.

Uzuri wake zabibu,
Kula kwake siyo tabu,
Mdomoni taratibu,
Nafyonza kama tabibu.

Ndizi ina ukakasi,
Ulimini kama pasi,
Zabibu ladha halisi,
Mwenyewe najinafasi!

Mundu kasema nanasi,
Kwangu halina nafasi,
Zabibu siwezi asi,
Nisije jipa mkosi!

Zabibu ninalo hamu,
Mengine siyo matamu,
Nitalila kitaalamu,
Kama nilivyo mwalimu!

Njoo uje huku kwa energy needs bana.
Tusiishie tunda tunda...huku mabazazi wanakata mti.
 
Mimi nina swali moja
Mara kichwani huja
Sitegemei vioja
Bali jibu lenye hoja

Mimi nataka kujua
Linahisije kuliwa
Tunda linalosifiwa
Au halina hisia?

Zabibu, nanasi, embe
Hivyo vyote ni viumbe
Vipi navyo visitambe
Atambe mshika jembe?

Mwenye ujuzi fumbua
Linahisije kuliwa
Tunda mnalochukua
Ganda lake kulivua?
 
Mimi nina swali moja
Mara kichwani huja
Sitegemei vioja
Bali jibu lenye hoja

Mimi nataka kujua
Linahisije kuliwa
Tunda linalosifiwa
Au halina hisia?

Zabibu, nanasi, embe
Hivyo vyote ni viumbe
Vipi navyo visitambe
Atambe mshika jembe?

Mwenye ujuzi fumbua
Linahisije kuliwa
Tunda mnalochukua
Ganda lake kulivua?


Swali lako ni makini
Ila ndani ni mtego
Umetegwa kilaini
kunasa wenye magego!

Siri nitaifichua
Hisia zake matunda,
Hili ukishalijua
Na mti utaupanda!

Tunda lapenda kuliwa,
Linapenda kutafunwa,
Langoja kutunguliwa,
Pole pole likamenywa!

Kisu kikapenya kati,
Mchuzi ukamwagika,
Bila hata varangati,
Meza tukaziandika.

Ndiyo maana yaiva,
Ili baadaye yaliwe,
Mengine yasiyoiva,
Kwanini yatunguliwe?

Raha yake ni kung'atwa
Au kisu kuchomekwa,
Na kisha hata kupikwa,
Jikoni yakabandikwa!

Yanajitoa mhanga,
Matunda nayasifia
Na yale yanayoringa,
Watu wanayachukia!

Raha ya tunda kuliwa
Mbinguni wameandika
Na mbegu zapunjuliwa
Wa kijiji naandika.

Kalamu naweka chini,
Tunda langu limeiva,
Kisu kiko mkononi
Tunda kalileta Eva!!
 
Wewe kula hizo ndizi,
Wengine wala andazi,
Hata ule tangawizi,
Zabibu tunda la kazi!

Hadi umenye maganda,
yale yalogandaganda,
Ndiyo ule lako tunda,
Hilo unalolipenda.

Uzuri wake zabibu,
Kula kwake siyo tabu,
Mdomoni taratibu,
Nafyonza kama tabibu.

Ndizi ina ukakasi,
Ulimini kama pasi,
Zabibu ladha halisi,
Mwenyewe najinafasi!

Mundu kasema nanasi,
Kwangu halina nafasi,
Zabibu siwezi asi,
Nisije jipa mkosi!

Zabibu ninalo hamu,
Mengine siyo matamu,
Nitalila kitaalamu,
Kama nilivyo mwalimu!


We upendaye zabibu,
Hueanda ushakuwa Babu,
Kulima kwako ghadhabu,
sifia tunda zabibu.

Kula dodo na nanasi,
Kunahitaji nafasi,
Hasira kama Mkisi,
Hazipatiwi nafasi.

Dodo nanasi na ndizi,
Ule kama mwizi,
Ukiwakimbia inzi,
Na usifanye ajizi.
 
Hodi hodi wahenga,
Mwanakijiji malenga,
Tenzi ujapozipanga,
Kumbe kuna zabibu!

Kumbe kuna zabibu,
Na kazijua Nyani_Ngabu
Huyo atazisulubu!
Maganda kukuachia


Maganda takuachia,
Utashindwa kusifia,
Utabaki kulilia,
Na nyani keshakimbia!

Zabibu usizipende,
Bora halua na tende,
Wazila kiupandeupande!
Na huku wagugumia!
 
Ni tamu hilo la kwangu,
Nafyonza kivyanguvyangu,
Ni tamu kuliko Changu

Nimelirundika chungu!

Siyo tunda la kizungu,
La Uru siyo Marangu,
Nalamba vidole vyangu
,
Naruka kama kulungu!

... litaendelea...

Mkuu MMK respect nimependa sana hapo kwenye Bold.
 
Zabibu langu si tamu,
Lanipa Uchungu Mkuu,
Nahaha HUku na Huku,
Nilapo Hili Zabibu,
Napata Ladha ya Nyongo Chungu.

ITAENDELEA
 
Swali lako ni makini
Ila ndani ni mtego
Umetegwa kilaini
kunasa wenye magego!

Siri nitaifichua
Hisia zake matunda,
Hili ukishalijua
Na mti utaupanda!

Tunda lapenda kuliwa,
Linapenda kutafunwa,
Langoja kutunguliwa,
Pole pole likamenywa!

Kisu kikapenya kati,
Mchuzi ukamwagika,
Bila hata varangati,
Meza tukaziandika.

Ndiyo maana yaiva,
Ili baadaye yaliwe,
Mengine yasiyoiva,
Kwanini yatunguliwe?

Raha yake ni kung'atwa
Au kisu kuchomekwa,
Na kisha hata kupikwa,
Jikoni yakabandikwa!

Yanajitoa mhanga,
Matunda nayasifia
Na yale yanayoringa,
Watu wanayachukia!

Raha ya tunda kuliwa
Mbinguni wameandika
Na mbegu zapunjuliwa
Wa kijiji naandika.

Kalamu naweka chini,
Tunda langu limeiva,
Kisu kiko mkononi
Tunda kalileta Eva!!

Mzee wewe mkali
Lakini sijakubali
Mbona meliweka mbali
Swali langu la awali?

Kupenda sio hisia
Bado hujaniambia
Vipi linajisikia
Kisu kinapoingia?

Kupenda sio kuhisi
Ni tendo lenye kiasi
Lizukalo kwa wepesi
Kati ya wenye nafasi

Doriani lapendeza
Machoni linaliwaza
Hebu puani sogeza
Harufuye taiweza?

Moyoni utalipenda
Na mti utaupanda
Mwenyewe utajipinda
Hisia zitakushinda

Mwenye kula hujilamba
Sasa jibu naliomba
Mwenye kuliwa ni rumba
Au ni ngoma ya Pemba?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom