Zabibu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Zabibu langu li tamu,
Pekee lanipa hamu,
Ni tamu tunda adhimu,
La kale kama ya Shamu!


Linaendelea...
 
Zabibu lako halizidi langu
Utamu wake washika hatamu
Kwa mbali lafanana na zambarau
Lapatikana kule Lamu

Kwingineko ni adimu
Wengine wasema ni haramu
Mimi na yeye latupa hamu
Na sasa tu damu damu

Nitarudi baadae........
 
Last edited:
Ni tamu hilo la kwangu,
Nafyonza kivyanguvyangu,
Ni tamu kuliko Changu
Nimelirundika chungu!

... litaendelea...
 
Ni tamu hilo la kwangu,
Nafyonza kivyanguvyangu,
Ni tamu kuliko Changu
Nimelirundika chungu!

Siyo tunda la kizungu,
La Uru siyo Marangu,
Nalamba vidole vyangu,
Naruka kama kulungu!

... litaendelea...
 
Si kwamba nawapa shua,
Ni kweli ilotukuka
Matunda tunayojua
Ni mengi yasiyolika

Toka kule misituni
Hadi hapo bustanini
Yanolika milimani
Au yale ya mwambaoni

Hata kama lamegeka
Si lazma lakuvundikwa
Dodo linalonyonyeka
Tayari l'meshikwashikwa

...Ha!...
 
Last edited:
Nimerudi nimerudi
Kama Nilivyoahidi
Wauliza toka wapi
Gulioni mchikichini

Kufanya nini nilienda
Kutafuta tunda nalolipenda
Tunda lile lenye kulika
Wengine hukataa kulila

Ni chachu kama ukwaju
Utamu wake kama changu
Ni kama umenyweshwa sumu
Ulionjapo japo kiduchu
 
Last edited:
Suki nimekusikia
Na Nyani nakubalia,
Tungo zilizotulia
Matunda mnayosifia!

Bado hamjafikia,
Zabibu ninalosifia,
La kwangu lilivyotulia,
Jinsi linaning'inia!

Jekundu lililoivia,
Utamu najisikia,
Ulimi najing'atia,
Jinsi ninalibugia!

Kicheko najiachia
Mguno najisikia
Raha ninajipatia,
Zabibu namumunyia!

... litaendelea...
 
hahahaahh auwiiiiiiiii! you all people are killing me with mashairi yenu for god sake sikujua kama cupcake wangu yupo so creative na yeye kwenye mambo ya mashairi..dang cuzin upo hapo so far?....
 
hahahaahh auwiiiiiiiii! you all people are killing me with mashairi yenu for god sake sikujua kama cupcake wangu yupo so creative na yeye kwenye mambo ya mashairi..dang cuzin upo hapo so far?....

Nimeona vitu vyake si utani anajitutumua.. we have to keep him if for no other reason..
 
Zabibu kweli ni tamu
kulisifia muhimu
ni tunda la humu humu
hata mimi nalijua

ila sikutarajia
kilingeni kuingia
mzee kulisifia
usijute kumegewa

kizuri kina gharama
tena huwa nicha ngama
utakuja kulalama
tutapojinyofolea

ni angalizo nakupa
ndugu yangu tupatupa
huna haja ya kufupa
kwanini watuzingua?

fyonza hadi katikati
ninakupa mkakati
hatuta kushika shati
kimya kimya ukilila

nyani ngabu ni hatari
vya watu hujivinjari
ili kuepusha shari
usirudie makeke.
 
Nimeona vitu vyake si utani anajitutumua.. we have to keep him if for no other reason..

Ni kweli kabisa we sure do!...inabidi you two muandike lyrics mtauza sana me i will be yur manager...maana i am good kwenye hiyo industry....Cuzin naona Suki yupo naye kwenye line uh.....unamtrain taratibu siyo mchedho.

Heheheheee....ndio bana imenibidi na mimi nitunishe kidogo vimisuli vyangu....lol


Naona mambo yako pumkin siyo mabaya kabisa wee i am impressed kwa kweli! haya mbona hujawahi kuniimbia miye live kihivyo?....you need to do that tonite.
 
Ni kweli kabisa we sure do!...inabidi you two muandike lyrics mtauza sana me i will be yur manager...maana i am good kwenye hiyo industry....Cuzin naona Suki yupo naye kwenye line uh.....unamtrain taratibu siyo mchedho.

cuz.. mchokozi.. Suki mtaalamu kivyake vyake, miye kwake styudenti!

Ila Mundu naye yumo, si unaona vitu vyake hapo juu!
 
cuz.. mchokozi.. Suki mtaalamu kivyake vyake, miye kwake styudenti!

Ila Mundu naye yumo, si unaona vitu vyake hapo juu!

I see kuna watu wana talent cuzin kumbe uh!.... ila i am proud of my cupcake! maana sijawahi kumsikia kabisa akiimba hayo mashairi hahahah!...

Alafu hivi what happend unakumbuka back in 2002 tulikuwa tutengeneze ile single yetu what happen>?...
 
Strike two!

I know... didn't I say I'm a first learner too?

Zabibu ukijapewa
Hilo utalichukuwa
La bure ukimegewa
Utalila kama muwa?

Vipi kama bado bichi,
Tena kijani kibichi,
Utasusa kuwa mbichi
Au hata hivyo huliachi?

Vipi ukilingishiwa,
Kinywani kupitishiwa
Ulimini kuonyeshwa
Kisha likaondolewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom