kaisar19
JF-Expert Member
- May 24, 2021
- 228
- 391
Je! aliibiwa?: wakubwa shkamoni wadogo abari zenu mabinti mambo zenu.
Nakusogezea kisa hiki cha kusisimua kuhusu Mzimu wa Ziwa Tanganyika. Moja ya sababu ya maji kujaa na kuharibu mali za watu ni ukumbusho kutoka kwa Mzimu huu kwasababu wahusika waliacha kuutambika mzimu wa Ziwa Tanganyika.
Mzimu wa ziwa Tanganyika unaitwa 'Mwanzalulu' kwa kimanyema, kwa kiha unaitwa 'Mganzaruguru' na kwa kibembe huitwa 'mkangialukulu'. Huu ndio mzimu pekee ambao makabila yanayopatikana ziwa Tanganyika yanaweza kutambikia kupitia mfalme huyu wa maji ya Ziwa Tanganyika, Lualaba, Lukuti, na Luiche.
Mvua nyingi zilizoendelea mfululizo zimepelekea kujaa kwa maji ya Ziwa Tanganyika katika maeneo ya Ardhi ya Ujiji na viunga vyake vya mwambao. Ng'ambo ya Kongo Uvira pia mafuriko ya maji ya mvua yamevunja majumba na baadhi ya Wazee wa mji wamedai viongozi wa kimila wamesahau asili na kutotambikia Mwanzalulu.
Makabila mengi ya mwambao yameacha kwa kiasi kikubwa kutambikia mizimu ya wahenga na vijana wengi hawajui hata majina ya Mizimu na sifa zilizohusishwa nayo.
Kiasili Mzimu wa Mwanzalulu wa Ziwani hutokea Unyakarambani. Wanyakaramba, pia huitwa Wakwalumona, hili ni koo la Kimanyema lugha yao ni kibwari cha Kinyakaramba.
Unaweza usielewe vizuri, nakupa mfano wa watu wanaotoka koo ya Kinyakaramba ili twende sambamba: Mfano wao ni Sheikh Amri Abeid Karuta, Sheikh Khalfan Kiumbe, Sheikh Yahya Hussein (mnajimu) na Sheikh Kitama wa Ujiji.
Sasa huyu Mzimu wa Mwanzalulu kiasili hutokea Unyakaramba, ambapo kuna safu ya Milima inaitwa Milima ya Mwanzalulu, Misozi, Kalomba, Kabubili, Kibwe, Kabogo na Nkungwe.
Mwanzalulu yupo katika kundi la Mizimu ya Mazingira. Hii huwa ndiyo mizimu mikubwa zaidi. Mizimu hii hujivisha tashihisi "personification" ya mazingira yake mf. Milima, Mito, Aruta, Ziwa, Misitu n.k mf. Mwanzalulu, Lungwe, Kabogo, Rutale n.k. Mizimu hii ndiyo kwa jamii za wenzetu huiita Miungu (Jambo ambalo ni makosa kiimani).
Mizimu ya mazingira "nature spirits", hii kama ilivyo kwa tamaduni za kipagani za ulaya na asia ni hali za kimazingira zikivishwa roho au tashihisi yenye uhai na umaada wa kujitegemea wenye nguvu fulani. Kundi hili ni kubwa na huingia Visigo, Mwanzalulu, Kabogo, Nkungwe, Mtambala, Ashibo, Nkongolo Mwamba, Rutale, Kwibe n.k
Katika utamaduni wa kuamini uwepo wa viumbe hivyo pia upo utamaduni wa kale wa kuamini uwepo wa Mzimu korofi unaoishi kwenye lindi la Ziwa Tanganyika.
Mzimu huo zamani ukisadikiwa kuonekana usiku ukisoza na mtumbwi hasa kwa kutokea Kaskazini maeneo ya Karamba (Unyakaramba) ukitambaza Ziwa kuja kusini.
Mzimu huo wa jinsi ya kiume, uliokuwa na sifa ya kujipigia ngoma ya mbiu wenyewe kabla ya kuanza kutarai Ziwani. Wamanyema huuita MWANZALULU, Waha huuita MGANZARUGURU na Wabembe huuita MKANGIALUKULU.
Mwanzalulu ni baba wa familia kubwa ya mke na watoto wengi mno. Chakula chake hupendelea Samaki na dagaa sanasana maana yeye kiasili ni mvuvi.
Katika ulingano wa kimaumbile Kwenye milango ya kiruhani ya Ujinini Mwanzalulu hufanana zaidi na Subiani.
Kwa sasa kutokana na mabadiliko ya kimazingira huwa hauonekani tena, ila katika vilinge vya kimanyema kuna watumishi wengi wa Mzimu wa Mwanzalulu.
....................
Sasa tunaingia katika ujio wa wazungu kunako ufahamu wao juu ya Mzimu huyu wa Ziwa Tanganyika'
Mzimu wa ziwani ulitajwa kwa mara ya kwanza na wazungu mwaka wa 1893, wakati Joseph Augustus Moloney aliporipoti kwamba mmishonari wa 'Mpala' alidai kuwa aliona 'Nyoka mkubwa sana Ziwani' mara mbili mara moja ziwani na mara moja ufuoni.
Mnamo mwaka wa 1907, wakati wa majadiliano ya 'Rothschild, mwanasayansi wa mambo ya asili 'Bwana Walter Rothschild' aliripoti kwamba afisa Mwingereza wa polisi alimwona mnyama mfano wa Nyoka mwenye pembe au mwenye manyoya kusini mwa Ziwa Tanganyika.
Kulingana na ripoti za Ujerumani kutoka Juni 1928, "Mwanzalulu" wakati mwingine alionekana akipita kama meli kwenye Ziwa Tanganyika, vijiji vingi vya mwambao wa Ziwa Tanganyika walikuwa wakiona Meli nyakati za usiku ikipita Ziwani ilihali kiuhalisia haikuwa meli bali alikuwa ni Mwanzalulu'
Ripoti hiyo ilidai kuwa nyimbo zisizotambulika zilikuwa zikisikika kwenye ufuo wa ziwa Tanganyika, na "kucha mbili kama za ndege mkubwa, kucha hizo ni kubwa zaidi kuliko tembo mzee.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari Lawrence Green, ambaye alidai kuwa uvumi wa uwepo wa Mzimu katika Ziwa Tanganyika ulikuwa wa kawaida, wakati wa ukoloni serikali ya Ujerumani ya Tanganyika ilitoa zawadi kwa kukamatwa kwa "Nyoka huyo mkubwa' aliyeonekana katika ziwa hilo, ambaye aliwahi kumeza mtumbwi uliokuwa na wasafiri ishirini.
Mwanzalulu aliripotiwa kutoka sehemu ya Burundi ya Ziwa Tanganyika mwanzoni mwa 1914 na kuelekea kusini mwa ziwa. Daktari Mjerumani M. V. Thierfelder, ambaye alikuwa akifanya kazi Tanganyika alishuhudia hali hiyo wakati wa janga la ugonjwa wa usingizi, alikuwa ameenda kuwinda karibu na ziwa akiwa yeye na mwalimu wake 'Ilsgensmeier, na mvulana mmoja wa kiafrika, walishuhudia hilo walipokuwa wakitembea karibu na fukwe ya ziwa iliyozungukwa na miamba.
Ghafla, nikaona, kitu ambacho sikuwahi kuona. Alikuwa ni kiumbe aliyefanana na nyoka wa kutisha. Hata hivyo, hakuogelea kama nyoka katika harakati za mlalo, lakini pete zake nilizihesabu zilikuwa sita, zilipanda wima juu ya maji. Mnyama huyo alifika kwenye ghuba kwa mwendo wa kasi, na akaenda moja kwa moja hadi karibu na ufuo wa mawe, ambapo tulikuwa tumelala. ' M. V. Thierfelder'.
Mnyama huyo alikuwa na urefu karibu mita hamsini na alikuwa na mafundo kadhaa katika mwili wake, kila fundo lilikuwa na urefu wa mita nne na nusu na kipenyo cha mita tatu. Kipenyo cha mnyama mzima kilikuwa sawa kutoka kwa kichwa chake hadi theluthi yake ya mwisho kuelekea mkia. ' M. V. Thierfelder'.
Mnyama huyo hakuwa na miguu, hata hivyo, kulikuwa na miundo myembamba kila upande. Rangi ya mnyama ilikuwa kahawia angavu; haikuwa na magamba, bali ilikuwa imefunikwa na ngozi nene. Kichwa kilikuwa kigumu kukitambua kwa sababu kilionekana kwa muda mfupi tu juu ya maji, lakini hakikuwa kipana zaidi ya mwili. Haikuwa kama kichwa cha nyoka, kwa mfano. Mdomo, ulionekana mwembamba na mrefu.
Mwalimu Ilsgensmeier pia alimwona mnyama huyo, na uchunguzi wake ulikubaliana kikamilifu na ule wa Thierfelder. Wafanyakazi wa Kiafrika, ambao hawakuwa wenyeji wa eneo hilo, hawakumtambua mnyama huyo, lakini walidai kuwa watu wa eneo hilo walimtaja kuwa ni mzimu wa Mwanzalulu' huwa anatokea mara moja kila baada ya miaka mitano. Thierfelder alichapisha alitoa makala ya mzimu huyu mwaka wa 1948.
Itaendelea......
Nakusogezea kisa hiki cha kusisimua kuhusu Mzimu wa Ziwa Tanganyika. Moja ya sababu ya maji kujaa na kuharibu mali za watu ni ukumbusho kutoka kwa Mzimu huu kwasababu wahusika waliacha kuutambika mzimu wa Ziwa Tanganyika.
Mzimu wa ziwa Tanganyika unaitwa 'Mwanzalulu' kwa kimanyema, kwa kiha unaitwa 'Mganzaruguru' na kwa kibembe huitwa 'mkangialukulu'. Huu ndio mzimu pekee ambao makabila yanayopatikana ziwa Tanganyika yanaweza kutambikia kupitia mfalme huyu wa maji ya Ziwa Tanganyika, Lualaba, Lukuti, na Luiche.
Mvua nyingi zilizoendelea mfululizo zimepelekea kujaa kwa maji ya Ziwa Tanganyika katika maeneo ya Ardhi ya Ujiji na viunga vyake vya mwambao. Ng'ambo ya Kongo Uvira pia mafuriko ya maji ya mvua yamevunja majumba na baadhi ya Wazee wa mji wamedai viongozi wa kimila wamesahau asili na kutotambikia Mwanzalulu.
Makabila mengi ya mwambao yameacha kwa kiasi kikubwa kutambikia mizimu ya wahenga na vijana wengi hawajui hata majina ya Mizimu na sifa zilizohusishwa nayo.
Kiasili Mzimu wa Mwanzalulu wa Ziwani hutokea Unyakarambani. Wanyakaramba, pia huitwa Wakwalumona, hili ni koo la Kimanyema lugha yao ni kibwari cha Kinyakaramba.
Unaweza usielewe vizuri, nakupa mfano wa watu wanaotoka koo ya Kinyakaramba ili twende sambamba: Mfano wao ni Sheikh Amri Abeid Karuta, Sheikh Khalfan Kiumbe, Sheikh Yahya Hussein (mnajimu) na Sheikh Kitama wa Ujiji.
Sasa huyu Mzimu wa Mwanzalulu kiasili hutokea Unyakaramba, ambapo kuna safu ya Milima inaitwa Milima ya Mwanzalulu, Misozi, Kalomba, Kabubili, Kibwe, Kabogo na Nkungwe.
Mwanzalulu yupo katika kundi la Mizimu ya Mazingira. Hii huwa ndiyo mizimu mikubwa zaidi. Mizimu hii hujivisha tashihisi "personification" ya mazingira yake mf. Milima, Mito, Aruta, Ziwa, Misitu n.k mf. Mwanzalulu, Lungwe, Kabogo, Rutale n.k. Mizimu hii ndiyo kwa jamii za wenzetu huiita Miungu (Jambo ambalo ni makosa kiimani).
Mizimu ya mazingira "nature spirits", hii kama ilivyo kwa tamaduni za kipagani za ulaya na asia ni hali za kimazingira zikivishwa roho au tashihisi yenye uhai na umaada wa kujitegemea wenye nguvu fulani. Kundi hili ni kubwa na huingia Visigo, Mwanzalulu, Kabogo, Nkungwe, Mtambala, Ashibo, Nkongolo Mwamba, Rutale, Kwibe n.k
Katika utamaduni wa kuamini uwepo wa viumbe hivyo pia upo utamaduni wa kale wa kuamini uwepo wa Mzimu korofi unaoishi kwenye lindi la Ziwa Tanganyika.
Mzimu huo zamani ukisadikiwa kuonekana usiku ukisoza na mtumbwi hasa kwa kutokea Kaskazini maeneo ya Karamba (Unyakaramba) ukitambaza Ziwa kuja kusini.
Mzimu huo wa jinsi ya kiume, uliokuwa na sifa ya kujipigia ngoma ya mbiu wenyewe kabla ya kuanza kutarai Ziwani. Wamanyema huuita MWANZALULU, Waha huuita MGANZARUGURU na Wabembe huuita MKANGIALUKULU.
Mwanzalulu ni baba wa familia kubwa ya mke na watoto wengi mno. Chakula chake hupendelea Samaki na dagaa sanasana maana yeye kiasili ni mvuvi.
Katika ulingano wa kimaumbile Kwenye milango ya kiruhani ya Ujinini Mwanzalulu hufanana zaidi na Subiani.
Kwa sasa kutokana na mabadiliko ya kimazingira huwa hauonekani tena, ila katika vilinge vya kimanyema kuna watumishi wengi wa Mzimu wa Mwanzalulu.
....................
Sasa tunaingia katika ujio wa wazungu kunako ufahamu wao juu ya Mzimu huyu wa Ziwa Tanganyika'
Mzimu wa ziwani ulitajwa kwa mara ya kwanza na wazungu mwaka wa 1893, wakati Joseph Augustus Moloney aliporipoti kwamba mmishonari wa 'Mpala' alidai kuwa aliona 'Nyoka mkubwa sana Ziwani' mara mbili mara moja ziwani na mara moja ufuoni.
Mnamo mwaka wa 1907, wakati wa majadiliano ya 'Rothschild, mwanasayansi wa mambo ya asili 'Bwana Walter Rothschild' aliripoti kwamba afisa Mwingereza wa polisi alimwona mnyama mfano wa Nyoka mwenye pembe au mwenye manyoya kusini mwa Ziwa Tanganyika.
Kulingana na ripoti za Ujerumani kutoka Juni 1928, "Mwanzalulu" wakati mwingine alionekana akipita kama meli kwenye Ziwa Tanganyika, vijiji vingi vya mwambao wa Ziwa Tanganyika walikuwa wakiona Meli nyakati za usiku ikipita Ziwani ilihali kiuhalisia haikuwa meli bali alikuwa ni Mwanzalulu'
Ripoti hiyo ilidai kuwa nyimbo zisizotambulika zilikuwa zikisikika kwenye ufuo wa ziwa Tanganyika, na "kucha mbili kama za ndege mkubwa, kucha hizo ni kubwa zaidi kuliko tembo mzee.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari Lawrence Green, ambaye alidai kuwa uvumi wa uwepo wa Mzimu katika Ziwa Tanganyika ulikuwa wa kawaida, wakati wa ukoloni serikali ya Ujerumani ya Tanganyika ilitoa zawadi kwa kukamatwa kwa "Nyoka huyo mkubwa' aliyeonekana katika ziwa hilo, ambaye aliwahi kumeza mtumbwi uliokuwa na wasafiri ishirini.
Mwanzalulu aliripotiwa kutoka sehemu ya Burundi ya Ziwa Tanganyika mwanzoni mwa 1914 na kuelekea kusini mwa ziwa. Daktari Mjerumani M. V. Thierfelder, ambaye alikuwa akifanya kazi Tanganyika alishuhudia hali hiyo wakati wa janga la ugonjwa wa usingizi, alikuwa ameenda kuwinda karibu na ziwa akiwa yeye na mwalimu wake 'Ilsgensmeier, na mvulana mmoja wa kiafrika, walishuhudia hilo walipokuwa wakitembea karibu na fukwe ya ziwa iliyozungukwa na miamba.
Ghafla, nikaona, kitu ambacho sikuwahi kuona. Alikuwa ni kiumbe aliyefanana na nyoka wa kutisha. Hata hivyo, hakuogelea kama nyoka katika harakati za mlalo, lakini pete zake nilizihesabu zilikuwa sita, zilipanda wima juu ya maji. Mnyama huyo alifika kwenye ghuba kwa mwendo wa kasi, na akaenda moja kwa moja hadi karibu na ufuo wa mawe, ambapo tulikuwa tumelala. ' M. V. Thierfelder'.
Mnyama huyo alikuwa na urefu karibu mita hamsini na alikuwa na mafundo kadhaa katika mwili wake, kila fundo lilikuwa na urefu wa mita nne na nusu na kipenyo cha mita tatu. Kipenyo cha mnyama mzima kilikuwa sawa kutoka kwa kichwa chake hadi theluthi yake ya mwisho kuelekea mkia. ' M. V. Thierfelder'.
Mnyama huyo hakuwa na miguu, hata hivyo, kulikuwa na miundo myembamba kila upande. Rangi ya mnyama ilikuwa kahawia angavu; haikuwa na magamba, bali ilikuwa imefunikwa na ngozi nene. Kichwa kilikuwa kigumu kukitambua kwa sababu kilionekana kwa muda mfupi tu juu ya maji, lakini hakikuwa kipana zaidi ya mwili. Haikuwa kama kichwa cha nyoka, kwa mfano. Mdomo, ulionekana mwembamba na mrefu.
Mwalimu Ilsgensmeier pia alimwona mnyama huyo, na uchunguzi wake ulikubaliana kikamilifu na ule wa Thierfelder. Wafanyakazi wa Kiafrika, ambao hawakuwa wenyeji wa eneo hilo, hawakumtambua mnyama huyo, lakini walidai kuwa watu wa eneo hilo walimtaja kuwa ni mzimu wa Mwanzalulu' huwa anatokea mara moja kila baada ya miaka mitano. Thierfelder alichapisha alitoa makala ya mzimu huyu mwaka wa 1948.
Itaendelea......