Yona na Mramba: Mashtaka na yatokanayo

Yona na Mramba: Mashtaka na yatokanayo

Mkuu FMES: nimeonyesha sehemu ninazokubaliana na wewe 100% na ni maswali niliyoyauliza mapema kabisa. Kuhusu hii kuwa cabinet decision nimeishikia sana bango kwa sababu kuna sababu cabinet decisions zinafanyika hii ni ku-create collective responsibility, na kuhakikisha kuna mwafaka ili baadaye wasirukane kama sasa hivi. Na kama cabinet inastahili kushtakiwa basi wote washtakiwe akiwemo JK mwenyewe!
Sorry I am not bought on these charges na ninaona ni usanii mtupu na si kwamba Mramba na Yona wamekubalikuwa kafara bali ni kwamba wanatumika kama pawn in a chess game of powerful parties.

Mkulu Susuviri,

Yakhe hata mimi hizi habari ndio kwanza nimezipata leo katika kupekua pekua, nimefanikiwa kuongea na mkulu mmoja anayesubiri kukamatwa ndiye aliyenipa hizi zote leo.

Ninasema hivi wananchi tunahitaji kua macho sana na kinachoendelea, yaani kuchambua wka makini kesi za hawa watuhumiwa ili tusije lishwa sumu, leo nime-raise hii ishu sana na Mkulu mmoja wa serikali kwamba mbona kesi hakuna kwa kina Mramba na Yona? Wakanijia juu sana kwamba nina haraka sana na hukumu, kwamba nisubiri wote wanakwenda na maji haponi mtu, nikawaahidi kwamba tunafuatilia hili kwa makini na macho mawili kwa hiyo mkuu tupo ukurasa mmoja, nataka kuona wengine zaidi wakishikwa.

Ya rais kuhusika yamesemwa sana, sasa tunataka kuona walioshikwa, wakijitetea na kusema ukweli kwenye kujitetea, anyways ninasubiri kukutana uso kwa uso na mama k ambaye nitakua naye for the next one week in three days, ninaamini ukweli mwingi utakua wazi after!
 
Wakuu, tunauhakika cabinet ilijadili na kupitisha hayo yote(esp. in blue), au tuna speculate?...maana isije cabinet ikawa imemruhusu kwenda mwisho kibaha, yeye akapitiliza mpaka morogoro.

Mkuu Sober,

Hizi ni habari tunapewa na wanaohusika na hili deal, ndio walionipa leo kua cabinet ilihusika na muungwana akiwa waziri alihusika, na b akiwa rais.
 
1
3. Dataz zaidi nilizizopita leo ni kwamba Tanesco mpaka leo wanailipa Kiwira shillingi millioni 300 kwa mwezi kwa miaka 2 zaidi ijayo, sasa hapa hasara kubwa ni ya kina Mramba na yona, au hii pia? Je kweli hapa kuna kujaribu kusimamia sheria au kulipiza visasi kwa waliowapinga Mtandao?
Thanxs!



-A tale of two powerful families and their intertwining interests

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

FORMER cabinet minister Daniel Yona, who held the energy and minerals portfolio in the final years of the third phase government under Benjamin Mkapa, has been identified as a major shareholder in the $271.8m (approx. 340bn/-) Kiwira coal-fired power project along with the ex-president and his family.

Latest findings by THISDAY now indicate that both Yona and his son, Danny Yona, are also prominent shareholders of Kiwira Coal and Power Limited under the umbrella of Tanpower Resources Company Limited.

They are represented in the little-known but apparently high-powered Tanpower Resources through a private company called DEVCONSULT Limited, in which Yona senior owns 90 per cent of the shares while Yona junior holds the remaining 10 per cent.

THISDAY investigations have already established that Mr Mkapa and the former first lady, Mrs Anna Mkapa, have shares in the Kiwira company through their own private company ANBEM Limited, which was registered in 1999 with the couple as sole shareholders while they were still at State House.

Before being appointed minister for energy and minerals, Yona held a number of other key portfolios in the Mkapa government from 1995, including minister of state in the president’s office (planning), and minister of finance.

Apart from the shares held by ANBEM Limited, it has also been established that Mr and Mrs Mkapa’s son Nicholas Mkapa also has his own shares in the same Kiwira company through another company going by the name of Fosnik Enterprises Limited.

It is understood that Mkapa junior owns Fosnik Enterprises on a 50-50 basis with his wife, Ms Foster (Mbuna) Mkapa.

At the same time, Nicholas Mkapa’s father-in-law Joseph Mbuna has also been discovered to be one of the shareholders and major figures in Kiwira Coal and Power Limited, which is based in Mbeya Region.

Mbuna, whose stake in the company is under the name of Choice Industries Limited company in which he is the majority shareholder, currently serves as chairman of the Kiwira Coal and Power Limited board of directors, whereby Nicholas Mkapa is one of the directors.

Like ANBEM Limited, DEVCONSULT Limited and Fosnik Enterprises Limited, Choice Industries Limited also falls under the umbrella of Tanpower Resources.

To put it in a nutshell, it has now been verified that Nicholas Mkapa and his father-in-law both sit on the Kiwira Coal and Power Limited board of directors, while former president Benjamin Mkapa and his wife are also among the company’s listed shareholders through ANBEM Limited.

Other shareholders of the Kiwira company have been identified as Evans Mapundi and Wilfred Malekia through the Universal Technologies Limited company, which is also under the Tanpower Resources umbrella. Mapundi and Malekia also sit on the six-member Kiwira board of directors.

Tanpower Resources is now understood to own up to 85 per cent of shares in Kiwira Coal and Power Limited, with the remaining 15 per cent of shares being formally held by the government of the day.

The government is currently represented on the Kiwira company’s board of directors by the Deputy Permanent Secretary in the Ministry of Infrastructure Development, Omari Chambo, while the Mbeya Regional Administrative Secretary, Ms Asumpta Ndimbo, also sits on the Kiwira board.

Serious questions have begun to be raised within government circles about the multi-billion shilling contract signed between Kiwira Coal and Power Limited and the Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) in March last year for the supply of 200 megawatts of electricity into the national power grid.

Impeccable sources privy to the contract details are now hinting at the growing possibility that the deal could eventually turn out to be another expensive trap for the national economy, along the same lines as the infamous 1995 IPTL affair.

According to THISDAY’s sources, the signs of potentially disastrous discrepancies in the contract have started to emerge as delays continue to hamper the still-pending launch of the project ? more than 16 months since the signing.

The sources have already revealed that at least one ’big hand’ in the Mkapa administration was responsible for exerting undue pressure on TANESCO officials to sign the contract with the Kiwira investors, and strongly hinted that the pressure came via the ministry of energy and minerals.

The controversial, 20-year power purchase agreement (PPA) which, among other things, gives the owners of Kiwira Coal and Power Limited enough discretion to calculate future power tariffs at will, was signed between the government, TANESCO and the private investor company.

Our sources now say TANESCO could end up being liable to pay Kiwira Coal and Power Limited a staggering $6m (approx. 8bn/-) each month once the firm starts delivering on the agreed 200MW of electricity.

This would bring TANESCO?s monthly obligations to three independent power producers (IPTL, Songas and Kiwira) to a figure exceeding $20m (approx. 26bn/-), which is well beyond the estimated $19.35m (around 25bn/-) per month that TANESCO currently earns from its revenues.
 
Hivi Mkapa hakutumia madaraka na ofisi ya raisi vibaya?

Mkuu wanaohusika wanasema hivi, alikuwa mjanaja sana kutumia jina la rais ambalo ndilo alilosaini kwenye makaratasi yote muhimu ya biashara zake, kwani alijua kua kama former pres. hataguswa kwa anything alichofanya kama rais,

ila wanasema alikosea one thing, kwenye makaratasi ya Kiwira hakusaini kama rais, bali alijiweka kama mjasiriamali, sasa ni hapo ndipo wanapomtafutia nasikia hii marathon yote ni tisa kumi wanaelekea hukooooooo!
 
Mkuu wanaohusika wanasema hivi, alikuwa mjanaja sana kutumia jina la rais ambalo ndilo alilosaini kwenye makaratasi yote muhimu ya biashara zake, kwani alijua kua kama former pres. hataguswa kwa anything alichofanya kama rais,

ila wanasema alikosea one thing, kwenye makaratasi ya Kiwira hakusaini kama rais, bali alijiweka kama mjasiriamali, sasa ni hapo ndipo wanapomtafutia nasikia hii marathon yote ni tisa kumi wanaelekea hukooooooo!

Won't that be sweet.....? Really, if that were to materialize, I will have a renewed and a new found faith in our govt. But until then, the arrest of these former ministers remains to be a charade in my eyes.
 
Last edited:
Kuna tetesi kuwa mawaziri wengine wako mbioni kupelekwa mahakamani na DPP au Takukuru. Kuna wasiwasi kuwa hizi kesi zinaharakishwa bila kulenga ufanisi kwenye uendeshwaji wake na hatimaye hukumu zitakazotolewa kwa haki...Tanzania ni mara ya kwanza kufikisha viongozi wa juu mahakamani kwa tuhuma za rushwa, kutumia madaraka vibaya n.k. Uzoefu huu katika vyombo vyetu vya sheria haupo na sio ajabu wengi wanaendeleza mjadala wa kuwa Raisi mstaafu anaweza kushitakiwa kwa kutumia madaraka vibaya au la. Wiki mbili zilizopita Mahakimu wa Kisutu waliandamana mpaka Mahakama Kuu kwenda kudai ulinzi baada ya kesi ya EPA kuanza kusikilizwa. Ni mpaka pale jaji Ferdinandi Wambali alipowahakikishia madi yao yatasikilizwa ndio wakapoa na kurudi kuendelea na kazi. Inaonyesha ni kwa kiasi gani hata Mahakimu wanashikwa na kwi kwi kwenye kuendesha hizi kesi.

Ingalikuwa busara kama kesi hizi nzito na zenye mengi ya kujifunza zingeenda kwa utaratibu wenye umakini zaidi kuliko tetesi zinavyoelekea kuwa na ukweli zinavyoonyesha. Mfano mmoja wapo ambao unaleta wasiwasi ni matamko ya mara kwa mara yanayotoka kwa DPP...matamko yake unaweza kufikiri DPP amekuwa Mbunge au cheo chake na maamuzi yake ni ya kisiasa. Lingine ni lile la Waziri wa Mambo ya Ndani bila aibu kwenda keko kuwatembelea Mahabusu. Mahakimu wetu wakisikia mtuhumiwa alitembelewa na Waziri mahabusu, anaweza kutoa haki kwa mujibu wa sheria bila woga wowote?? Hizi ni dalili za kutosha kuwa hatuna uzoefu na kesi za uzito wa aina hii; hivyo DPP na Takukuru wanahitaji kila darasa watakaloweza kupata kufanisha kesi hizi [ziwe huru na zitoe haki].

Wanasheria wanajua ukweli kuwa kesi mara nyingi huendeshwa kwa kuangalia pamoja na vigezo vingine lakini pia mienendo ya kesi za nyuma na maamuzi/ hukumu zilizofikiwa. Sasa hapa leo tumeona Yona na Mramba wamefunguliwa mashitaka, hata wiki haijapita tunasikia Karamagi atafikishwa kizimbani muda wowote, bila shaka naye mashitaka yake yatakuwa yale yale; kutumia madaraka vibaya n.k. Ili kuepuka kesi kuanguka kwa sababu zinazoweza kuzuilika kwa nini wasisubiri kuona kesi moja ikisogea na zingine zikiendelea kurekebishwa kabla ya kuziharakisha Mahakamani kadiri uzoefu wa ofisi ya DPP na Waendesha mashitaka unavyoongezeka.

Mbona kuna haraka, hii imetoka wapi au na nani aliwaambia DPP na hao Takukuru kuwa Watanzania wanataka hawa watu wawe wamefikishwa mahakamani kabla Krismasi..??!!

Hiyo ni dalili inayopelekea imani ya kuwa kesi hizi zimendaliwa kushindwa na watuhumiwa kuibuka kidedea. Inakuwa kama vile walipelekwa Mahakamani kusafisha majina yao badala ya kulipa haki kwa maovu waliyowatendea Watanzania. Au ni vita vya kisiasa ndani ya CCM kuelekea 2010..??
 
Yebo Yebo,

Hizi ni kesi zinazotokana na shutuma za siku nyingi. Hazikuharakishwa. Watanzania wamesubiri na kujadili muda mrefu sana. Sasa wanataka matendo, sio maneno tu.

Wewe ungewashika wezi wawili ungesema mwache mmoja akae tu kwanza, umpeleke mahakamani mwingine uone kesi inaendeleaje kwanza?

Si kweli kwamba hatujawahi kuwa na kesi za wakubwa kama hizi. Naamini utakumbuka kushtakiwa kwa kina Nalaila Kiula na George Mlingwa. Utakumbuka kesi za nyuma za kihaini zilizowahusu Michael Kamaliza na Bibi Titi Mohammed vile vile. Zilikuwa kubwa kuliko hizi za wizi wa kalamu.

Nakumbuka kuna wakati Mramba alionyesha kudhamini sana kila mtu kulipa kodi. Alisema “Kulipa kodi ni kama kifo. Ni kitu kisichoepukika” Alikuwa anadanganya? Mbona inaonekana kasamehe kodi kinyemela!

Haya mafaili mbona hayajumuishi vipengele vyote? La Yona limeacha wapi uuzaji wa NBC? Takukuru wameshindwa kuona mazingira ya rushwa yaliyokuwepo kwenye huo uuzaji? Mbona kuna faili la Buzwagi lakini hatusikii kuhusu shutuma za bandarini? Au watamaliza kifungo cha kesi moja ndio wakamatwe tena?

Justice delayed is justice denied.
 
Mhhhhh... the emerging facts zinaonyesha kuwa mambo yanaweza kuwa magumu kwa hawa ndugu zetu na wakaitumia weekend wakiwa lupango.
Habari kutoka Mahakama Kuu zinapasha kuwa kesi yao imepangwa kesho kwa ajili ya first mention na si hering. Kwa maana hiyo, itatajwa tu halafu itapangiwa tarehe (iwapo mahakama haitapindisha taratibu zake).
Kesi itakuwa chini ya Jaji Njengafibili Mwaikugile.
Na kuna marekebisho makubwa yamefanywa kwenye masharti ya dhamana, mahakama ya Ksutu imepunguza kiwango cha fedha kutoka bil 3.9 hadi Bil 2.9

Mambo mazito! Labda kama mawakili waliwasilisha maombi under certificate of emergency ndio itaweza kusikilizwa haraka..leo...na sababu za hiyo emergency haziwezi kuwa " kuhudhuria harusi!"
 
Mambo mazito! Labda kama mawakili waliwasilisha maombi under certificate of emergency ndio itaweza kusikilizwa haraka..leo...na sababu za hiyo emergency haziwezi kuwa " kuhudhuria harusi!"

Hii game ni tough sana kiasi kwamba sitamani kuachia computer yangu hata kwa sekunde, Ahsante sana FMES na wengine woote kwa kutuletea yanayojiri huko, hakika ni burudaaaani

Mungu ibariki JF
 


Mwanakijiji alionmya sana mwaka huu mwanzoni kuhsu suala la kuzungwa,Mie wakati mwingine huwa namuoina mwanakijiji kama nabii

hunipendi ndugu yangu; kasome mwisho wa manabii unakuwaje.. nina maadui wa kutosha tu so bora nibakie hivi hivi mtu wa porini, mshamba mshamba fulani hivi. Haya ya manabii yananiogofyesha.
 
hunipendi ndugu yangu; kasome mwisho wa manabii unakuwaje.. nina maadui wa kutosha tu so bora nibakie hivi hivi mtu wa porini, mshamba mshamba fulani hivi. Haya ya manabii yananiogofyesha.

Ili mie Yangu macho tu...Basi wewe ni Mwenye Heri..

Mwanakijiji hivi wewe unaonaje nchi ilivyo hivi sasa,Mie naogopa sana sababu imekuwa na usanii na uzugaji usio na mipaka.Najiuliza mbunifu wa mbinu hii ya sasa hivi ni nani..The master Planner?


Nasikia Wakina Mramba wameletwa high court huko?kuna mtu ana taarifa?Hivi nani aliplan dili ya IPTL?
 
hunipendi ndugu yangu; kasome mwisho wa manabii unakuwaje.. nina maadui wa kutosha tu so bora nibakie hivi hivi mtu wa porini, mshamba mshamba fulani hivi. Haya ya manabii yananiogofyesha.

Ngoja GT aamke, kwa post yako hii naona leo atapata kwa kuanzia lol....
 
Yebo Yebo,

Hizi ni kesi zinazotokana na shutuma za siku nyingi. Hazikuharakishwa. Watanzania wamesubiri na kujadili muda mrefu sana. Sasa wanataka matendo, sio maneno tu.

Wewe ungewashika wezi wawili ungesema mwache mmoja akae tu kwanza, umpeleke mahakamani mwingine uone kesi inaendeleaje kwanza?

Si kweli kwamba hatujawahi kuwa na kesi za wakubwa kama hizi. Naamini utakumbuka kushtakiwa kwa kina Nalaila Kiula na George Mlingwa. Utakumbuka kesi za nyuma za kihaini zilizowahusu Michael Kamaliza na Bibi Titi Mohammed vile vile. Zilikuwa kubwa kuliko hizi za wizi wa kalamu.

Nakumbuka kuna wakati Mramba alionyesha kudhamini sana kila mtu kulipa kodi. Alisema "Kulipa kodi ni kama kifo. Ni kitu kisichoepukika" Alikuwa anadanganya? Mbona inaonekana kasamehe kodi kinyemela!

Haya mafaili mbona hayajumuishi vipengele vyote? La Yona limeacha wapi uuzaji wa NBC? Takukuru wameshindwa kuona mazingira ya rushwa yaliyokuwepo kwenye huo uuzaji? Mbona kuna faili la Buzwagi lakini hatusikii kuhusu shutuma za bandarini? Au watamaliza kifungo cha kesi moja ndio wakamatwe tena?

Justice delayed is justice denied.


Mkuu Augustine

Dhumuni la maoni yangu linalenga kukata kiu niliyokuwa nayo ya kuona hawa Watuhumiwa wanatiwa hatiani kwa mujibu wa sheria [sababu sote tunajua; japo sio rasmi, hayo wanayoshitakiwa nayo ni sehemu tu ya ujangili waliufanya wakiwa viongozi Serikalini.]

Wananchi wengi wenye uelewa hawapendi kampeni za zima moto kama ambavyo hizi kesi zinaelekea kuwa na mtazamo wa hivyo. Wapo wanaona ni kheri kukawia lakini kesi ikienda Mahakamani basi kunakuwa na kesi yenye ushahidi wa kutosha.

Kesi ulizozianisha zilitokea enzi ambazo hata JF haikuwepo achilia mbali uhuru vyomba vya habari lukuki na wa maoni walionao Watanzania leo hii [hata msafara wa Raisi unapigwa mawe siku hizi..!!]. Nalaila Kiula alishitakiwa kwa "Rushwa" kesi ambayo kwa mtazamo wa nje ni kubwa na nyepesi kuthibitisha kuliko hizi za "kutumia madaraka vibaya". Hata hivyo kesi kama ile ya Nalaila Kiula ilimalizika kwa mshitakiwa kupata ushindi kwenye mahakama ya rufaa.

Hayo ndiyo ninayohofia kwenye kesi hizi za leo. Kiu ya wananchi kuona sheria zinasimamiwa ipasavyo na Mahakama ni kubwa. Kwa utaratibu huu unaoendelea sasa wa DPP, Takukuru na Serikali [Masha] inakuwa kama wanawasadia watuhumiwa kujisafisha machoni mwa Jamii.
 
natakiwa nifanye nini nitetemeke? maisha yangu na mawazo yangu hayazunguki JF...

Hehehe ninachofurahia ni kwamba kwa kiasi kikubwa umeweza kudhibiti nafsi yako kwa kutomjibu chochote GT ingawa yeye ameendelea kukurushia maneno ya hapa na pale, kimsingi watu wengi sana hapa Jf tunakuheshimu na tunaheshimu mawazo na mchango wako mkubwa katika mapambano ya kutaka kuiweka nchi yetu katika mstari ulioonyooka lakini kwa mtazamo wa watu wachache wakiongozwa na GT naona wanafeel vibaya sana kuona kuwa kuna watu hapa wanakuheshimu na heshima hii inatokana na ukweli ambao haujafichika kuwa Mzee mwana kijiji ni mtu unayejua kujibu hoja na unatoa hoja zenye muelekeo na zisizo na muonekano wa uchonganishi hata kidogo, kwa hili wapo watu waliodiriki hata kusema kuwa tunakuabaudu hapa JF, wamediriki hata kusema unampango wa kuiua JF kwa kuanzisha forum yako. Ni mengi yamesemwa lakini kiukweli ni kwamba hapa Jf tunakuheshimu na tunaendelea kuhitaji mchango wako kwa kiasi kikubwa sana hasa wakati huu ambapo nchi inamtiokisiko wa ufisadi. Ni hayo tu niliyoamua kuyasema leo hii sikutaka kudhulumu nafsi yangu na nimesema yes nimesema na weekens yangu itakuwa saaafi
God bless Jf na members wake wote wanaoitakia mema nchi yetu
 
Huyu bwana ni lazima ahudhurie harusi ya mwanawe kesho, Period!... Kivipi,? hio sio headache yake.... ni headache ya mawakili, wahakimu, wanasheria na wakulu wenzake walioko nje...bila hivyo, ule MPASUKO wa visiwani utavuka bahari.
 
Back
Top Bottom