Yona atoswe baharini ili merikebu isizame

The end justify the, ... Ninawi ambayo ndiyo Uspain ya leo tunayoishudia ilipona, na ndicho tunachokiona Tanzania itapona ukiwemo wewe na mimi, hilo tu.
Kwa kupitia Yona huyuhuyu ambaye jina lake lilitokana na kupigiwa ramli chonganishi kwa kutumia mizimu ya makafri ambayo haijawahi kuwa na huruma na mtu au ni Yona mwingine?.
 
The end justify the, ... Ninawi ambayo ndiyo Uspain ya leo tunayoishudia ilipona, na ndicho tunachokiona Tanzania itapona ukiwemo wewe na mimi, hilo tu.
kwani huyu wetu ametumwa Tanzania akitokea wapi?ungeanzia hapo tungeweza kupima hiyo The end justify the .....
 
Nani wa kulitupa wakati wapambe kila mmoja anashangilia ujinga tu!
 
Mtoa mada na mtoa comment wote wanaweza wakawa sahihi kwa kulenga jambo lilelile moja, japo kuwa kuna mmoja anamuona Yona kama mtetezi na mkombozi.

Lakini hapa inaonekana kuwa jina la Yona lilipatikana kwa njia ya kupiga ramli jambo ambalo ni chukizo kwa Mungu,lakini hapohapo pamoja na Yona kutupwa bahari bado Mungu alitumia njia nyingine ya kumuwezesha Yona kufikisha ujumbe wake Ninawi.

Baada ya Mungu kumuokoa Yona asizame baharini kwa kumtuma samaki ammeze na kumtapikia kwenye ufukwe wa Ninawi na kufanikiwa kufikisha ujumbe aliotumwa na Mungu kwa wahusika ambao walitubu na kumugeukia Mungu.

Kitendo ambacho hakikumpendeza Yona kwa kuwa lengo lake alitaka watu wa Ninawi waangamie.

Kwa Yona wetu huyu jina lake litakuwa lilipatikana kwa njia ileile ya kupiga ramli na kwa ajili ya kuiokoa rangi ya kijani ambayo ilikuwa inaelekea kufutika na si kwa ajili ya kupeleka ujumbe wa Mungu kuwaponya watu wa Ninawi.

Kwani hata yeye mwenyewe hajui kama ujumbe aliopewa kupeleka Ninawi kama alipewa na Mungu, bali anachokijua yeye ni kwamba yeye alibipu akasukumiziwa.

Akasukumiziwa na nani, na wale wa rangi ya kijani ambao ua garagaza ilikuwa lazima rangi yao ya kijani iliokuwa inaelekea kufutika iokolewe.
Na kwa sababu huyu si Yona hallisi hata akili ya kujua kuwa hilo kundi la kijani analolipigania kwa expense ya nchi yetu ,ndiyo adui namba moja wa nchi hana.yeye an anaendeshwa tu kama robot
 
Kwa kupitia Yona huyuhuyu ambaye jina lake lilitokana na kupigiwa ramli chonganishi kwa kutumia mizimu ya makafri ambayo haijawahi kuwa na huruma na mtu au ni Yona mwingine?.

Ndio Yona huyuhuyu ambaye alipata neema na kibali cha Mungu. Na muujiza wake ndio unajadiliwa hadi leo duniani kote. Mungu alimnyanyua kutoka huko alikomtoa kwa mapenzi yake ambayo akili za mwanadamu haziwezi kuyachunguza. Vita vya panzi ikawa furaha ya kungunguru. Na panzi mmoja bado anahangaika hakusoma alama za nyakati, kipofu wa akili.
 
Yona mwenyewe ndo alipendekeza atoswe baharini maana aliamini kabisa yeye ndo alikuwa sehemu ya tatizo lililoikumba merikebu, sasa nyinyi mnataka sisi tumtose Yona baharini kabla ya yeye kutambua tatizo lake na kupendekeza kwa hiari yake mwenyewe atoswe baharini
 
Ndio Yona huyuhuyu ambaye alipata neema na kibali cha Mungu. Na muujiza wake ndio unajadiliwa hadi leo duniani kote. Mungu alimnyanyua kutoka huko alikomtoa kwa mapenzi yake ambayo akili za mwanadamu haziwezi kuyachunguza. Vita vya panzi ikawa furaha ya kungunguru. Na panzi mmoja bado anahangaika hakusoma alama za nyakati, kipofu wa akili.
Unahabari kuwa Yona huyuhuyu unayejaribu kumtetea kwa upole na unyenyekevu ndiye aliyesababisha upepo mkuu uliotaka kukivunja chombo walichokuwa wanasafiria na mwisho wake ilikuwa ni kifo kwa wasafiri?.

Unahabari kuwa waliotuliza upepo ule mkuu kwa kumtosa Yona baharini usiweze kuvunja chombo walichokuwa wanasafiria na kujiepusha na kifo kilichokuwa kinatokea kama wasingefanya hivyo ni wale waliokuwa ndani ya chombo?.

Una habari kuwa baada ya Yona kutoswa baharini waliokuwa ndani ya chombo walisafiri salama na kufika salama walikokuwa wanakwenda?.

Na mwisho,unahabari kuwa waliokuwa ndani ya chombo mambo ya Ninawi kama walipona au hawakupona hayawahusu,wao walikuwa wanahusika na safari ya kwenda Tarishishi na walifanikiwa kufika?.
 
Yona mwenyewe ndo alipendekeza atoswe baharini maana aliamini kabisa yeye ndo alikuwa sehemu ya tatizo lililoikumba merikebu, sasa nyinyi mnataka sisi tumtose Yona baharini kabla ya yeye kutambua tatizo lake na kupendekeza kwa hiari yake mwenyewe atoswe baharini
Ndio tumeshapiga kura sasa na kumtambua,kinachofuata ni kumuuliza tufanyenini ili dhoruba itulie.
 
yona ana pambana na matajiri. Wafanya biashara wote kwaiyo apo yona alifanya maksudi... Yona wa wanyoge
 
Mwandishi hakujua wale wote waliokuwa kwenye chombo na Yona walikuwa wa abudu shwetwani ndio maana walipiga ramli kujua chanzo cha tatizo ni nini? Na kuhakishia angekuwa na hayo maaono asingekuja na huu mfano maana hata yeye kawa exposed kuwa ni wafungu gani. Nimemsaidia kujua upande wa pili wa shilingi.
Hujaelewa dhima nzima ya bandiko hili...
 
🤣🤣🤣🤣.. safi sana. Yona aende tu bhana.. vinginevyo watazama ambao hawana hatia. Yona arushwe baharini haraka iwezekanavyo
 
The end justify the, ... Ninawi ambayo ndiyo Uspain ya leo tunayoishudia ilipona, na ndicho tunachokiona Tanzania itapona ukiwemo wewe na mimi, hilo tu.


Mkuu Spain Sio Ninawi. Ninawi ni moja ya miji ipatikanayo nchi ya Syria na Kuingia Irag huko Mosul.

Ninawi ni moja ya majiji makubwa katika zama hizo ambapo dola iliyokuwa inatawala dunia ilikuwa dola la Ashuru(Syria) ambapo waliishi Waashuru na Wakaldayo.

Kusema Spain ni Ninawi ni kuupotosha umma ima kwa makusudi au kwa ufinyu wa Historia.

Spain haijawahi kuwa dola la dunia.
 
Kwa wasioelewa, na ili wakiielewe vizuri kisa hiki na uhusiano wa Yona wetu wa leo waende kwenye Biblia takatifu wasome.....

Kitabu cha YONA kipo katikati ya vitabu vya manabii wengine wadogo wawili OBADIAna MIKA ktk Agano la kale.....

Kitabu hiki ni kifupi sana maana kina sura (chapters) NNE tu na zote zinasimulia kisa cha huyu nabii kutotii maagizo ya Bwana Mungu.....

Lakini mwisho wa siku alinyoosha maneno, kwani kila alipojaribu kumkwepa Mungu kufanya kazi yake, Mungu hakumwacha kwani ilikuwa ni lazima aifanye kazi hiyo.....yaani aende akawahubiri Habari Njema ya Injili watu wa Tarshishi ili waache maovu yao na kumrudia muumba wao.....

Kwa sbb angalia tu, hata alipotoswa baharini lengo lake likiwa kuwa afe tu kwa maji (eti ili ajiepushe na uso wa Mungu muumba wake), lakini wapi bwana, Mungu alituma samaki (nyangumi) ammeze na kumhifadhi tumboni mwake na kumsafirisha hadi ufukweni mwa bahari na kumtapika huko....

Baada ya hapo alitambua mara moja kuwa, kumbe hata afanyeje hawezi kuikimbia uso wa Mungu wala kukataa kufanya kazi yake!!

Alielekea Tarshishi na kuhubiri Injili na mji ule ukaponywa....!!

Sasa Yona wetu wa leo, naye anafanya yaleyale. Anafanya kazi asiyoagizwa na Mungu kuifanya. Lakini Mungu hatachoka kumkumbusha na kumrejesha kwenye mstari......

Lakini akiendelea kukaidi, hukumu ya Mungu ipo na siku zote HUKUMU yake ni ya HAKI......hapendelei wala haonei MTU awaye yeyote.....kila mtu hupokea ujira wake anaostahili kwa kadiri ya fikra na matendo yake!!
 
Back
Top Bottom