Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,669
- 860,990
Hakuna kazi inayokosa changamoto, hata uwe mwerevu na mahiri vipi lakini lazima tu utakutana na kisiki
Waganga wa kienyeji nao hawajapona kwenye hili wengi walishapitia na majanga makubwa tu
Ukiacha yale ya kitapeli wa na wateja au kuua wa live au kupokea kichapo lakini vile vile kuna majanga kama haya
-kumchinja kuku kisha asife bali asimane bila kichwa
-kumchinja kuku kisha asitoke tone la damu
-kupasua nazi ikatae kabisa kupasuk
-kupika nyama isiive kabisa nk nk
Kuna baadhi ya waganga huwakataa wateja...kwakuwa wanajua huu ni mtego, kwenye ulimwengu wa roho ulimwengu wa giza kuna kujaribiana na kuoneshana nani zaidi
Zipo njia nyingi tu za mapambano ya aina hiyo na hii hutokea zaidi mmoja akiwa mahiri zaidi ya wengine au mmoja akijifanya mjuzi sana na kutambia wengine
Unaposikia mganga kafa kaugua au kapatwa na dhahama yoyote mara nyingi huyo kajaribiwa na wenzake.
Akipambana akashinda cheo huongezeka akipambana akashindwa lakini akaokoka na kifo aidha huacha kabisa uganga na kumrudia Mungu au hurudi kujipanga upya...sio wote wanaoacha uganga na kuokoka hufanya hivyo kwa ridhaa